<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><?xml-stylesheet href="http://www.blogger.com/styles/atom.css" type="text/css"?><feed xmlns='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' xmlns:georss='http://www.georss.org/georss' xmlns:gd='http://schemas.google.com/g/2005' xmlns:thr='http://purl.org/syndication/thread/1.0'><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487</id><updated>2012-02-03T02:58:22.577-08:00</updated><category term='Tume ya Uchaguzi'/><category term='Muundo'/><category term='Uboreshaji'/><category term='Daftari'/><category term='Wagombea'/><category term='Vyombo Vya Habari'/><category term='Uteuzi'/><category term='Mafunzo'/><category term='Mnyika'/><category term='Makala'/><category term='Kura'/><category term='Sheria'/><category term='Elimu ya Uraia'/><category term='John Mnyika'/><category term='Matokeo'/><category term='Ubungo'/><category term='Uchaguzi'/><category term='Hotuba'/><category term='Wapiga Kura'/><category term='John'/><title type='text'>JOHN MNYIKA</title><subtitle type='html'></subtitle><link rel='http://schemas.google.com/g/2005#feed' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/posts/default'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default?max-results=100'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/'/><link rel='hub' href='http://pubsubhubbub.appspot.com/'/><link rel='next' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default?start-index=101&amp;max-results=100'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><generator version='7.00' uri='http://www.blogger.com'>Blogger</generator><openSearch:totalResults>269</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>100</openSearch:itemsPerPage><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-4031189334346199607</id><published>2012-02-02T05:15:00.000-08:00</published><updated>2012-02-02T05:15:38.627-08:00</updated><title type='text'>BUNGENI LEO: Mgomo wa madaktari na Sheria ya Bodi ya Mikopo</title><content type='html'>Asubuhi ya leo Naibu Spika Job Ndugai alitumia kanuni vibaya kuzuia hoja ya dharura bungeni kuhusu mgomo wa madaktari. Kimsingi, sikuwasilisha hoja ila niliomba muongozo wa Spika ili niweze kupatiwa nafasi ya kuwasilisha hoja ya dharura. Kwa kuwa hoja kama hiyo iliwasilishwa juzi na ikaungwa mkono lakini Spika akasema ameshakubaliana na serikali kuwa ingewasilisha kauli. Hata hivyo, jana hakukuwa na kauli ya serikali huku wananchi wakiendelea kupata madhara ya mgomo. Hivyo nikata muongozo kwa kuwa Spika alitumia kanuni ya 49 (2) ambayo kimsingi inatoa mwanya kwa kauli ya serikali kuwasilishwa kwenye wakati atakaoona yeye kuwa na unafaa juu ya jambo linaihusu serikali na lisilozua mjadala. Nilitaka kanuni hiyo isitumike badala yake wabunge tutimize wajibu wa kuisimamia serikali kwa kutumia kanuni ya 47 kuhusu hoja ya dharura. Kwa kuwa ilikuwa muongozo hakukuwa na hitaji la kikanuni la wabunge wengine kuunga mkono lakini akaamua kuilinda serikali kwa kuwa hawakuwa wamejiandaa. Lakini mwishoni ameahidi kuwa kauli ya serikali itatolewa kesho. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jioni ya leo bunge litajadili Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali na.2 wa mwaka 2011 ambao kwa sehemu kubwa ukiondoa sheria nyingine unahusu marekebisho ya kimsingi katika sheria ya bodi ya mikopo. Ni kwa bahati mbaya kwamba muswada huu umeletwa na hoja ya kusomwa kwa hatua zake zote tatu katika mkutano mmoja hivyo hakutakuwa na muda wa kukusanya maoni ya wadau kwa upana wake. Ni sehemu ndogo sana ya vifungu vya muswada huu ndio inapaswa kukubalika lakini kwa ujumla muswada huu unakwenda kuingiza mambo ambayo tuliyapinga kwa makongamano, migomo na maandamano yakaondolewa wakati sheria husika inatungwa mwaka 2004. Maudhui ya muswada huu yamenifanya nikumbuke makala ambayo niliandika mwezi kama huu lakini mwaka 2007: http://www.chadema.or.tz/makala/makala.php?id=43 Marekebisho haya yanaenda kuweka mazingira mengine ya migogoro katika elimu ya juu nchini kutokana na masuala ya mikopo kwa wanafunzi. Muswada huu ulipaswa kuja bungeni baada ya ripoti ya Tume ya Rais iliyoundwa tarehe 14 Februari 2011 na kukabidhi taarifa yake tarehe 29 Aprili yenye mapendekezo ya jinsi ya kuboresha utaratibu wa sasa wa ugharamiaji, utoaji na urejeshaji wa mikopo ya elimu ya juu kuwekwa wazi kwa bunge na kwa umma ili kufanya marekebisho mapana zaidi ya kimfumo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-4031189334346199607?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/4031189334346199607/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=4031189334346199607' title='7 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4031189334346199607'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4031189334346199607'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/02/bungeni-leo-mgomo-wa-madaktari-na.html' title='BUNGENI LEO: Mgomo wa madaktari na Sheria ya Bodi ya Mikopo'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>7</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-3003788521073127373</id><published>2012-01-31T19:52:00.000-08:00</published><updated>2012-01-31T19:52:09.342-08:00</updated><title type='text'>Hatimaye mkataba wa vijana wa Afrika waletwa bungeni kuridhiwa</title><content type='html'>&lt;br /&gt;Kwa Vijana wenzangu kwa nafasi na wote wenye nafsi za ujana, leo ule mkataba wetu wa Afrika (African Youth Charter) hatimaye unaingia bungeni kuridhiwa. Ni matokeo ya harakati zetu za miaka mingi kabla na hata baada ya Rais Kikwete kuusaini Gambia mwaka 2006 lakini ukaishia makabatini. Baada ya kunituma bungeni kuwatumikia mkataba huu ni kati ya mambo niliyohoji mara kwa mara kutaka uletwe bungeni kuridhiwa ili utekelezaji wake uweze kuanza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawashukuru wote tuliounganisha nguvu kwenye harakati za vijana kwa nyakati mbalimbali kuanzia NYF, TYVA, YUNA, TSNP, UDSM, BAVICHA, asasi zingine na mwisho lakini kwa umuhimu mkubwa vijana wote tuliokesha pamoja kulinda kura Loyola. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kurejea nyuma katika historia, nawaletea moja ya ujumbe nilioandika kwenu na kwa vijana wa Afrika mwaka 2008: http://mnyika.blogspot.com/2008/10/vijana-tufikiri-na-kuungana-kukomboa.html Kila kizazi lazima kiitambue dira na dhima yake; ama kisaliti au kitimize. Tuendelee kuwajibika; kwa pamoja tunaweza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika&lt;br /&gt;Bungeni, Dodoma-01/02/2012&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-3003788521073127373?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/3003788521073127373/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=3003788521073127373' title='4 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3003788521073127373'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3003788521073127373'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/hatimaye-mkataba-wa-vijana-wa-afrika.html' title='Hatimaye mkataba wa vijana wa Afrika waletwa bungeni kuridhiwa'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>4</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-2260095731534058088</id><published>2012-01-28T21:21:00.000-08:00</published><updated>2012-01-29T09:28:31.094-08:00</updated><title type='text'>Taarifa ya Hoja kuhusu utekelezaji wa maazimio juu ya Richmond</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Tarehe 25 Januari 2012 nimewasilisha kwa Katibu wa Bunge taarifa ya hoja kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la 2007 Kanuni 54 (4) na 55 (1) kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge juu ya mkataba baina ya TANESCO na Kampuni ya Richmond Development Company LLC.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hoja hiyo ikipewa nafasi ya kuwasilishwa na kujadiliwa itaongeza msukumo wa utekelezaji wa maazimio ya bunge na hivyo kuchangia katika mapitio ya mikataba yenye kuongeza bei ya umeme; kuweka mfumo wa kulihusisha bunge katika maandalizi ya mikataba yenye maslahi ya taifa ikiwemo katika mafuta, gesi asilia na ujenzi na kuwezesha uwajibikaji na hatua kamili kuchukuliwa kwa waliohusika na ufisadi na uzembe uliolisababishia hasara taifa. &lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Taaarifa hii ya hoja niliiwasilisha awali tarehe 13 Aprili 2011 na kupatiwa majibu; hata hivyo niliijibu ofisi ya bunge kupatiwa taarifa ya utekelezaji uliofanywa na serikali baada ya Februari 2010 bila kupatiwa majibu hivyo nimeiwasilisha tena ili hoja husika ijadiliwe.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Lengo la Hoja Binafsi nitakayoiwasilisha kufuatia taarifa hiyo ni kutaka uamuzi wa Bunge uliofanyika katika Bunge la Tisa Mkutano wa 18 mwezi Februari 2010 kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge juu ya mkataba baina ya TANESCO na kampuni ya Richmond Development Company LLC; UBADILISHWE.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;/div&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika muktadha huo, hoja binafsi husika itawezesha mjadala kuhusu uamuzi husika kufunguliwa na kutoa fursa kwa jambo hilo kufikiriwa tena ili kuwezesha hatua kamili kuchukuliwa juu ya maazimio 23 ya Bunge yaliyopitishwa tarehe 15 Februari 2008 katika Mkutano wa 10 wa Bunge la Tisa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Taarifa ya tatu ya Serikali Februari 2010 ilitanguliwa na Taarifa mbili zilizowasilishwa Bungeni na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo Pinda, tarehe 28 Agosti, 2008, tarehe 11 Februari, 2009 na Taarifa moja iliyokabidhiwa na kujadiliwa na Kamati, ambazo zililitaarifu Bunge kuwa utekelezaji wa Maazimio 10 kati ya 23 yaliyotolewa na Bunge, yamefanyiwa kazi hadi mwezi Februari, 2009 na Maazimio 13 bado yalikuwa hayajakamilika. Maazimio hayo 13 ni: Nambari 1,2,3,5,7,8,9,10,11,13,14,15 na 18. Hoja binafsi itakapojadiliwa bungeni itawezesha Bunge na wananchi kwa ujumla kupata taarifa ya utekelezaji wa maazimio hayo 13.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kati ya maazimio hayo 13, baadhi ya maazimio ambayo utekelezaji wake haujakamilika ni pamoja:&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Azimio Na. 3, ambalo liliagiza kwamba “Mkataba kati ya TANESCO na Richmond Development Company LLC (uliorithiwa na Dowans Holdings S.A.) na ile kati ya TANESCO na IPTL, SONGAS, AGGREKO na Alstom Power Rentals, ipitiwe upya mapema iwezekanavyo kama ambavyo Mikataba ya Madini ilivyopitiwa upya na Serikali”. Iwapo Azimio hili lingetekelezwa kwa ukamilifu wake, gharama za uzalishaji TANESCO zingepungua na hivyo bei ya umeme isingepandishwa kwa kiwango kikubwa kama ilivyo sasa, ambapo Januari 2011 ilipandishwa kwa wastani wa 18.5% na Januari 2012 imepandishwa tena kwa wastani wa 40.29 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mzigo mkubwa wa ufisadi na ubovu wa mikataba.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Azimio Na. 8 na 14, maudhui ya maazimio hayo yanafanana kwa sababu yaliitaka “Serikali iwawajibishe Viongozi wenye dhamana ya kisiasa waliokuwa Mawaziri wa Wizara ya Nishati na Madini ambao wakati ule alikuwa ni Mheshimiwa Dkt. Ibrahim Msabaha na Mheshimiwa Nazir Karamagi.” Bunge lilielezwa kwamba vyombo vya Dola vimekamilisha uchunguzi wake wa ndani ya Nchi kuhusu suala hili. Hata hivyo zoezi lililoendelea toka Februari 2010 ni kufanya uchunguzi wa nje ya Nchi kwa kushirikiana na Vyombo vya Dola vya Kimataifa ambapo mwaka mmoja umemalizika bila hatua zozote kuchukuliwa kwa wahusika katika kashfa ambayo maazimio ya bunge yalipitishwa zaidi ya miaka mitatu iliyopita hali ambayo inaweza kusababisha hata mashahidi na ushahidi kupotea.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Azimio Na. 13, “Serikali izihusishe Kamati za Kudumu za Bunge kwenye hatua za awali za maandalizi ya Mikataba mikubwa ya muda mrefu ya kibiashara ili kuondokana na utaratibu uliopitwa na wakati kwamba Mikataba ya Kibiashara ni siri hata kwa walipa kodi wenyewe. Aidha, Serikali ihakikishe kuwa, Kamati zote za Bunge zinapitia Mikataba mikubwa ya muda mrefu ya kibiashara chini ya sekta zao ili kuliondolea Taifa mizigo isiyo ya lazima”. Azimio hili halijaanza kutekelezwa kwa ukamilifu wake matokeo yake ni kwamba serikali katika kipindi cha kati ya mwaka 2008 mpaka 2011 imeendelea kuwa siri katika hatua za awali za maandalizi na pia mikataba mingi haijafanyiwa mapitio. Hoja binafsi itawezesha mjadala kuhusu suala hili kufunguliwa na utaratibu thabiti kuwekwa katika kipindi hiki ambacho taifa linaingia katika mikataba mingi ya ujenzi na miundombinu na pia mikataba ya utafutaji na uchimbaji wa madini, mafuta na gesi asilia ambayo ina umuhimu wa pekee kwa uchumi na usalama wa nchi. Aidha, azimio hili lingetekelezwa kwa ukamilifu lingesaidia kuwa na mfumo mzuri zaidi wa maandalizi ya mikataba wakati huu ambapo serikali inaingia mikataba mingi ya gharama kubwa ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme hali ambayo imeongeza mzigo mwingine wa gharama za maisha kwa wananchi.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Azimio Na. 10, “Gavana wa Benki Kuu pamoja na Bodi ya Wakurugenzi, wachunguze kwa makini uhalali wa malipo ya ziada (US$ 4,865,000) yaliyofanywa kwa Dowans Holdings S.A iliyorithi majukumu ya Richmond Development Company LLC na kuwachukulia hatua waliohusika na uzembe huo.” Hoja Binafsi itawezesha mjadala kufunguliwa na mambo zaidi yaliyojiri kuhusu suala hili na mengine kuweza kujulikana na hatua kuchukuliwa kwa wote waliozembea ili kuimarisha misingi ya uwajibikaji katika taifa. &lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Masuala zaidi kuhusu maazimio mengine nitayaweka katika Maelezo ya Hoja na Hoja Husika ili niwasilishe katika Mkutano wa Sita wa Bunge la 10 uliopangwa kuanza tarehe 31 Januari 2011 kwa kadiri itakavyoelekezwa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Imetolewa tarehe 27 Januari 2012 na:&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mbunge wa Ubungo&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-2260095731534058088?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/2260095731534058088/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=2260095731534058088' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2260095731534058088'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2260095731534058088'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/taarifa-ya-hoja-kuhusu-utekelezaji-wa.html' title='Taarifa ya Hoja kuhusu utekelezaji wa maazimio juu ya Richmond'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-1955178049284529592</id><published>2012-01-27T21:40:00.000-08:00</published><updated>2012-01-29T09:27:46.682-08:00</updated><title type='text'>Kuhusu Msongamano wa Magari DSM na Ziara Kwembe</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nashukuru kwamba jana Serikali ilituma ujumbe wa kuonana ana kwa ana madaktari; hata hivyo ni muhimu ikayafanyia kazi yaliyowasilishwa jana ili leo kuwa na ujumbe mzito zaidi majadiliano yakamilike kwa haraka ili madaktari warejee kazini. Leo naendelea na kazi za kijimbo:&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mosi, nitashiriki mkutano wa wadau kuhusu tatizo la msongamano wa magari katika mkoa wa Dar es salaam. Serikali imeleta kwa dharura mwaliko wa mkutano huo jana hivyo sijapata wasaa wa kuomba maoni yenu kuhusu utekelezaji, mnaweza kuendelea kuyatoa hapa na tutayaunganisha pamoja na kuyawasilisha kwa mamlaka husika. Nimekosa pia fursa ya kuandika uchambuzi wangu kwa ajili ya kuchochea mjadala hivyo hoja zangu nitakwenda kuzitoa moja kwa moja kwenye mkutano papo kwa papo. Kwa ujumla, huu si wakati wa maneno bali matendo; mikutano kuhusu foleni katika jiji la Dar es salaam imeshafanyika kadhaa kati ya mwaka 2005-2010, maoni yametolewa na mipango imeandaliwa. Kinachotakiwa hivi sasa ni kuunganisha nguvu ya wadau katika kuhamasisha na kuharakisha utekelezaji. Na katika kufanya hivyo, kunahitajika nyongeza ya bajeti kwa kuwa kiwango kilichotengwa kwa ajili ya kupunguza msongamano katika jiji la Dar es salaam kwa mwaka wa fedha 2011/2012 ni kidogo ukilinganisha na ukubwa wa tatizo, kiasi cha mahitaji na hasara ambayo wananchi na nchi inapata kila siku kutokana na msongamano katika Jiji la Dar es salaam.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kuitishwa kwa mkutano wa leo kumefanya nikumbuke ujumbe wangu ambao niliuandika kwenye mtandao wa Wanabidii tarehe 14 Disemba mwaka 2011 nikichangia mjadala na kujibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa. Takribani mwezi mmoja na nusu umepita toka niandike ujumbe huo, ambapo yapo ambayo tayari nimeshayafuatilia mwezi huu wa Januari kupitia vikao vya bodi ya barabara, RCC, Jiji na Manispaa na hatua zimeanza kuchukuliwa kama sehemu ya kuchangia katika kupunguza foleni katika jiji la Dar es salaam hususani Jimboni Ubungo. Hata hivyo, nanukuu mchango wangu huo kwa kuwa kuna mambo bado ambayo niliyasema wakati huo lakini yanaweza kuendelea kujadiliwa na wadau katika mkutano wa leo:&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;“ Nitachangia tu kwa ujumla bila kutenganisha hatua kati ya za dharura, muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;/div&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kuhusu masoko ya jioni, chanzo ni kikubwa zaidi. Kiwango cha magari ni kikubwa ukianzia yanayosafirisha mizigo nje ya nchi, ya wananchi wanaotoka makaz ini na daladala kwa ujumla. hivyo, ni lazima suluhisho lihusishe ama kupunguza uwingi wa magari kwa wakati mmoja au kupanua ukubwa wa eneo la magari kupitia. Kwa sasa mpango uliokubaliwa na serikali ni wa kupanua njia kwa kujenga njia ya kupishana (fly over), hata hivyo kwa kiwango kikubwa ni kauli lakini kwenye bajeti ya 2011/2012 hakujatengwa fedha za ujenzi kwa hiyo ya Ubungo, isipokuwa kidogo kwa Tazara. Hii inafanya kwa mwaka huu mzima kubaki na hatua za kupunguza, nazo ni kuwa na ratiba tofauti baina ya magari ya mizigo ya nje ya nchi na muda ambao wananchi wanakwenda au wanatoka makazini, hili linapaswa kushughulikiwa kwa ushirikiano baina ya wizara ya uchukuzi, mambo ya ndani nk. Aidha, tunaweza pia kwa kuwa Tanroads wameshatangaza kuwa jengo lao liko ndani ya barabara pale Ubungo mataa linaweza kuvunjwa kupata njia ya mkato ya kufika kwenye kituo cha daladala ili kupunguza msongamano kwenye mataa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wakati barabara za hewani (fly overs) zikisubiriwa ni muhimu kuharakisha ujenzi wa barabara za mzunguko na mchujo (ring and feeder roads ). Mathalani hakuna sababu ya mtu anayetaka kwenda Mbezi beach ya kawe akitoka Mbezi luis ya Ubungo kwenda mpaka Ubungo mataa wakati ambapo anaweza kupitia njia ya Goba au ya Msakuzi /Mpiji Magohe. Au mtu anayetaka kwenda airport/ukonga toka Kibamba si lazima aende Ubungo Mataa anaweza akapita tu Malambamawili mpaka Kinyerezi. Hii iko hivyo vile vile kwa njia nyingine za mkato kama Msewe, Bonyokwa, Kilungule nk. Barabara zote hizi tayari zimeshafanyiwa upembezi yakinifu, hata hivyo hakuna hatua ya ujenzi iliyoanza zaidi ya ukarabati. Kwenye vikao vya bodi ya barabara nimetaka sana twenda hatua ya ziada kuhusu barabara hizi kwa kuharakisha kufanya tathmini ya fidia. Kwa bahati mbaya kwenye bajeti ya mwaka 2011/12 jumla ya fedha kwa barabara za aina hii ni bilioni tano tu ambazo ni fedha kidogo. Tunapoelekea kufanya mid term budget review mwezi Februari ni muhimu zikaongezwa. Kutakuwa na foleni mbaya zaidi Dsm ujenzi wa barabara za DART utakapoanza kama hatua hizi za dharura&amp;nbsp;hazitachukuliwa. Walau tumeunganisha nguvu za pamoja daraja la Msewe limejengwa na sasa linapitika. Changamoto kubwa ni kwamba sehemu kubwa ya barabara hizi za pembezoni pamoja na umuhimu wake zipo chini ya Manispaa wakati fedha ziko kwenye vyombo vya serikali kuu. Tumeomba kwenye vikao kwamba barabara hizi zipandishwe hadhi kutokana na umuhimu wake katika kupunguza foleni. Hata hivyo, vigezo vya sasa vya upandishaji wa hadhi za barabara vimejikita katika barabara kuu, ndefu na kubwa hivyo ni vigumu kutumika.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nimeiomba&amp;nbsp;Wizara na Tanroads kuweka vigezo maalum kwa Dsm kutokana na suala la foleni. Pia, kama katibu wa wabunge wa Dsm niwaeleze kwamba tulikwisha omba bungeni kukutana na Waziri Mkuu kuhusu masuala ya ardhi na barabara. Hivyo, mjadala huu ni muhimu kwa mamlaka zinazohusika kupata mambo ya ziada ya kuzingatia kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kuhusu kituo kikuu cha mabasi ya Ubungo, wazo la njia mbili linatekelezeka kwa kuwa upo uwezekano wa kuwa na njia ya nyuma. Changamoto ni kuwa bado kuna kiwingu kuhusu mwelekeo wa kituo husika. Yapo mapendekezo ya kuwa sehemu ya mabasi iwe na kituo cha nje ya mji, pengine hata Bagamoyo baada ya kukamilika kwa upanuzi wa Barabara husika ili kupunguza msongamano Ubungo. Pia, sehemu kubwa ya kituo kikuu cha mabasi cha Ubungo itakatwa kwa ajili ya miundombinu na kituo cha mabasi ya Haraka (DART). Hivyo, maamuzi yoyote lazima yatazame picha pana na mpango wa muda mrefu. Kuna mambo mengi bado tunaendelea kutofautiana kuhusu hili ambayo nisingependa kuyatolea maoni hadharani katika hatua ya sasa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa ujumla, hatua za kupunguza foleni, na hapa nijikite zaidi katika muktadha wa barabara ya Morogoro zinahitaji kushughulikia mfumo mzima.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kuwe na usafiri wa umma ( mass transit) wa abiria kwa njia ya barabara na kwa njia pia ya treni/reli kwa Dsm. Utekelezaji wa mradi wa DART unaelekea kusuasua hivyo wananchi na wadau kwa ujumla tunahitaji kuunganisha nguvu za pamoja kufuatilia. Aidha, wakati wa mkutano wa nne wa bunge nilisisitiza haja ya ongezeko la bajeti ya uchukuzi kuzingatia pia kuwa na mabehewa kwa ajili ya safari za Dsm.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Barabara hizi za pembezoni zipewe uzito kutokana na matatizo ya foleni. Tubadili mifumo ya ujenzi na ukarabati wake; kama tunazibakiza kwa halmashauri basi bajeti za barabara kwa manispaa zetu toka serikali kuu ziongezwe kwa&amp;nbsp; sababu ya mahitaji lakini na kuzingatia pia Dsm inachangia kwa kiwango kikubwa mapato yanayotokana na kodi za barabarani na za mafuta. Mathalani sasa hivi kipande kidogo cha barabara toka ubungo maziwa mpaka makuburi external kupitia daraja la Ubungo Kisiwani kinahitaji ujenzi wa daraja kubwa zaidi na upanuzi, lakini ni rahisi kwa Tanroads kutoa jibu jepesi kuwa barabara hiyo iko chini ya Manispaa ya Kinondoni wakati ambapo pamoja na ufupi wake ina umuhimu katika kupunguza foleni. Au barabara ya Kijitonyama mpaka Manzese Chakula bora. Au ujenzi wa madaraja kama ya Golani, Msigani nk. Ni lazima ama serikali kuu iongeze fedha kwa Manispaa au miundombinu husika ijengwe na serikali kuu kupitia Tanroads.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pia, lazima kupunguza idadi ya malori kwenye barabara ya Morogoro ili kupunguza foleni na ajali kwa kuharakisha matengenezo ya reli nchini ili mizigo mikubwa ibebwe kwa treni. Pia, kuharakisha upanuzi wa barabara ya Bagamoyo ili baadhi ya malori yapitie njia ya Msata badala ya Kibaha. Kwa miaka ijayo hatuwezi pia kuepuka kuipanua barabara ya Morogoro yenyewe. &lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hatua za sasa zitasaidia kupunguza tatizo la wakati huu, lakini halitaleta suluhisho la kudumu bila kutazama masuala mapana zaidi ya mipango ya muda mrefu yanayohusu ukuaji wa jij la Dsm. Ni lazima jiji lipanuliwe kwa kuelekea pembezoni kuhakikisha kwamba msongamano unapungua katikati. Hii ni pamoja na kuhakikisha kwamba maeneo ya pembezoni yanapimwa na watu kupewa hati ili wakati wote kuhakikisha kwamba ujenzi wetu wa nyumba unaacha barabara za kutosha kwa ajili ya kupunguza mzigo kwa barabara kuu. Aidha, miji ya pembeni yenye huduma za msingi (sattellitte towns) kama ile ya Luguruni Kibamba inabidi ifuatiliwe. Wengine tunaifuatilia, lakini ni jukumu la wadau wote kuunganisha nguvu za pamoja. Katika vikao nimehoji sana kuhusu uboreshaji wa master plan ya Dsm, tutaendelea kupeana taarifa kuhusu hatua ambayo imefikia.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kujenga miundombinu pekee, bila kupunguza kiwango cha mfumuko wa wananchi wa maeneo mengine ya nchi kuja DSM hakutaweza kuleta suluhisho la muda mrefu. Hivyo, ni lazima sisi kama viongozi na wananchi wa Dsm tuhakikishe tunachangia katika maendeleo ya maeneo mengine ya nchi ili kupunguza msongamano Dsm,; tushiriki katika kukuza miji mingine nchini. Ukiangalia eneo la Dsm na idadi ya watu, sio mji wenye msongamano ukilinganisha na miji mingine duniani. hata hivyo, kutokana na udhaifu wa muda mrefu katika mipango na miundombinu, gharama ya kulibadili jiji la Dsm ni kubwa sana. Ni muhimu kuweka uwiano baina ya kulibadili Jiji na kujenga majiji mengine.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wakati hatua hizi za muda mrefu, kuna hatua za haraka zinaweza kuchukuliwa kwa kuboresha utendaji tu wa vyombo vyetu iwe ni serikali za mitaa au serikali kuu ili kwa rasilimali zinazotumika sasa miundombinu iendelezwe na isimamiwe vizuri. Mathalani, jambo dogo tu kama ukarabati wa barabara ya Sinza mpaka Tandale linasababisha sasa hivi foleni inaongezeka; naamini TANROADS wataharakisha zaidi walau hili. Au foleni ya Mbezi Mwisho, wakati ambapo kituo cha mabasi mbezi luis kilichojengwa kwenye eneo la barabara kinachelewa kufunguliwa kwa sababu ya kutokuwa na choo au maofisini. Au malori ya nafaka yanaendelea kuja mjini na kuongeza foleni, badala jiji kuharakisha kukamilisha ujenzi wa kituo na soko la nafaka pale Mbezi ambao umeanza muda mrefu. Tunaendelea kuyafuatilia haya, tunahitaji kuendelea kuyajadili ili kuwez a kuunganisha nguvu za pamoja."&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pili; baada ya mjadala huo nitakuwa na ziara ya kichama katika kata ya Kwembe Jimboni Ubungo. Nitakuwa na kazi ya uzinduzi wa ofisi za chama za matawi mbalimbali pamoja na kuzungumza na wananchi na wanachama katika mikutano ya ndani. Mitaa nitayotembelea ni Kwembe Kati, Kwembe Mpakani, Kwembe Luguruni, Kwembe Kati. Katika mikutano hiyo pamoja na kueleza kazi ambazo tumezifanya katika mwaka 2011 katika kusimamia utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo, nitawajulisha pia wananchi na wanachama shughuli ambazo zinatarajiwa kufanyika katika mkutano wa Bunge unaonza tarehe 31 Januari 2012 ikiwemo miswada inayokusudiwa kujadiliwa ikiwa ni sehemu ya kutimiza wajibu wa kufanya mikutano kabla ya kila mkutano wa bunge. Hii ni ziara ya pili kabla ya mkutano huu wa sita wa bunge, ziara ya kwanza niliifanya tarehe 12 Januari 2012 kuhusu miundombinu ambayo niliifanya katika kata za Mbezi, Saranga, Kimara na Ubungo. &lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nawaomba tuendelee kushirikiana katika kutimiza wajibu wa kibunge kwa mujibu wa ibara ya 63 wa kuwakilisha wananchi, kutunga sheria na kuisimamia serikali ili kuwezesha maendeleo. Maslahi ya Umma KWANZA.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;John Mnyika(Mb)&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-1955178049284529592?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/1955178049284529592/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=1955178049284529592' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1955178049284529592'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1955178049284529592'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/kuhusu-msongamano-wa-magari-dsm-na.html' title='Kuhusu Msongamano wa Magari DSM na Ziara Kwembe'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-4712240358499304880</id><published>2012-01-27T01:03:00.001-08:00</published><updated>2012-01-29T09:24:42.249-08:00</updated><title type='text'>KUHUSU MGOMO WA MADAKTARI</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mgomo wa madaktari unaoendelea hivi sasa umedhihirisha kwamba tuna serikali dhaifu yenye ombwe la uongozi. Haiwezekani wananchi wakawa wanakufa kwa kukosa matibabu stahiki na wengine wakipata madhara kutokana na kuchelewa kupata matibabu sababu ya mgomo wa madaktari halafu viongozi wenye dhamana hawachukui hatua sahihi.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye mwenye dhamana kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 33 ndiye kiongozi wa shughuli za serikali na ibara ya 35 shughuli zote za utendaji wa serikali zinatekelezwa na watumishi wa serikali kwa niaba ya Rais; ameondoka kwenda nje ya nchi mgomo ulipoanza na hakuna kauli yoyote mpaka sasa toka kwa Makamu wa Rais wala kwa Ikulu.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Mkuu Mizengo Pinda badala ya kwenda kwenye eneo la mgomo na kuzungumza na madaktari naye ameishia kuzungumza na vyombo vya habari. Waziri wa Afya Dk. Haji Mponda na Naibu Waziri Dk. Lucy Nkya nao jana wamezungumza na waandishi wa habari badala ya kwenda kukutana na madaktari na kuzungumza nao kuhusu madai yao ya msingi.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa upande wetu CHADEMA tulitoa kauli tarehe 25 Januari 2012 ya kutaka serikali ichukue hatua na tuliona tuipe serikali nafasi ifanye kazi yake hata hivyo serikali haionyeshi kuupa uzito unaostahili mgogoro huu wenye kuathiri hali za wagonjwa na maisha ya wananchi katika maeneo mbalimbali ya nchi.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;/div&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Tuliacha kwenda katika eneo la mgomo kukutana na madaktari katika siku za awali kuepusha suala hili kutafsiriwa kuwa ni la kisiasa. Hata hivyo, kuchelewa kwa serikali kukutana na madaktari kunahitaji hatua za pamoja. Dhamira yangu kama mwananchi, mbunge katika mkoa wa Dar es salaam na kiongozi wa chama cha siasa naumizwa na hali inayoendelea. Ni vigumu kuweza kuendelea na majukumu ya kibunge na ya kichama katika masuala mengine wakati serikali iko legelege katika suala ambalo linahusu uhai wa wananchi wenzangu uko mashakani. &lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hivyo nawajibika siku ya leo kuelekeza nguvu katika kuungana mkono na madaktari katika madai yao ili kuishinikiza serikali kuweza kutuma ujumbe mkubwa kukutana na madaktari leo au kesho. Na iwapo serikali haitakutana nao katika muda huo, itabidi uongozi wa kambi ya upinzani bungeni ukiwa ni serikali kivuli na uongozi mkuu wa CHADEMA ukiwa ni chama mbadala kuweza kukutana nao.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Natambua kwamba uzembe na ufisadi katika serikali kwenye sekta ya afya unaligharimu taifa na maisha ya wananchi. Hivyo, CHADEMA inaitaka serikali kukamilisha kwa haraka majadiliano na madaktari na kutimiza madai yao ili kuepusha madhara zaidi kwa umma.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nawapa pole wananchi ambao wameathirika na migomo inayoendelea na kuzingatia kwamba mgomo huo umesababishwa na udhaifu katika serikali.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Natoa mwito kwa umma wa watanzania kuwaunga mkono madaktari na watumishi wengine wa sekta ya afya katika hospitali na zahanati za umma kama sehemu ya kuboresha huduma katika maeneo husika.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Madai ya madaktari na watumishi wengine wa sekta ya afya nchini yasiposhughulikiwa kwa wakati na kwa ukamilifu watumishi husika wanaweza wasiwe kwenye mgomo wa wazi kama ilivyo kwa baadhi ya hospitali na zahanati nchini lakini wataendelea na migomo baridi kwa kutoa huduma mbovu au kuacha kazi kwenye maeneo ya umma na wengine kwenda kufanya kazi nje ya nchi wakati kukiwa na uhaba wa watumishi nchini.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Aidha, pamoja na migomo inayoendelea, naendelea kutoa rai kwa madaktari na watumishi wengine wa umma kuhakikisha maisha ya wagonjwa walio katika hali ya hatari yanaokolewa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nimezungumza na viongozi wetu wakuu kuhusu suala hili na natoa mwito kwa wadau wote kuunganisha nguvu katika kuisimamia serikali kushughulikia madai ya madaktari na wafanyakazi wengine wa sekta ya afya kwa haraka ili kuepusha madhara zaidi kwa umma.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wananchi wenzangu wa Jimbo la Ubungo na umma kwa ujumla uzingatie kwamba tangu Mwalimu Nyerere aondoke madarakani mwaka 1985, Serikali ya CCM imeongeza wingi wa majengo mbalimbali kwenye sekta ya afya hata hivyo imeshindwa kusimamia utoaji bora wa huduma za afya katika zahanati, hospitali na vituo vya afya. Kutokana na mfumo mbaya wa usimamizi wa sekta ya afya, misingi imara ya kuimarisha sekta ya afya iliyowekwa baada ya uhuru imevunjwa na kubomolewa ikiwemo katika masuala yanayohusu kujali maslahi ya watumishi wa umma katika sekta hii muhimu.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hali hii imefanya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuwa na nakisi ya watumishi asilimia 48% na takwimu zinaonesha kuwa 18% ya wafamasia, 15% ya madaktari, 13% ya madaktari wasaidizi waliacha vituo vyao vya kazi na kwenda kutafuta kazi kwenye mashirika ambayo yanalipa mishahara mikubwa na mizuri. Nakisi hii itaongezeka zaidi iwapo madai ya msingi ya madaktari na watumishi wengine hayatashughulikiwa na serikali itaendelea kuchelewa kushughulikia migogoro na migomo mingine inayoendelea.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Ni imani yangu kwamba serikali ikiwa na dhamira inaweza kuongeza mishahara kwa watumishi wa sekta ya afya ili kuweza kuwavutia wataalamu kubakia nchini badala ya kwenda kugoma au kwenda kutafuta kazi nje ya nchi kutokana na malipo mazuri huko. Hii ni pamoja kuwezesha malipo ya mazingira magumu kutolewa kwa watumishi wa afya wanaofanya kazi katika maeneo na kada maalum.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa sababu hii, leo sitashiriki kikao cha Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kinachoendelea ili kupata wasaa wa kufuatilia kwa karibu suala hili na kuwasiliana na viongozi wenzangu kwa ajili ya hatua zaidi za pamoja. &lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;27/01/2012&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-4712240358499304880?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/4712240358499304880/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=4712240358499304880' title='9 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4712240358499304880'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4712240358499304880'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/kuhusu-mgomo-wa-madaktari.html' title='KUHUSU MGOMO WA MADAKTARI'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>9</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-8979421317547111134</id><published>2012-01-17T08:51:00.000-08:00</published><updated>2012-01-17T08:51:47.842-08:00</updated><title type='text'>Picha za Msiba wa Regia Mtema - Muhimbili mpaka Karimjee</title><content type='html'>&lt;div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/-PXeiequqlNE/TxWj5c7zv5I/AAAAAAAAAnw/nORSqSIDlUI/s1600/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee+2.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"&gt;&lt;img border="0" height="265" src="http://1.bp.blogspot.com/-PXeiequqlNE/TxWj5c7zv5I/AAAAAAAAAnw/nORSqSIDlUI/s400/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee+2.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/-pHR6tlTy9Yw/TxWj6-pcwRI/AAAAAAAAAn4/Sniuid9U0Hc/s1600/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee+3.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"&gt;&lt;img border="0" height="265" src="http://2.bp.blogspot.com/-pHR6tlTy9Yw/TxWj6-pcwRI/AAAAAAAAAn4/Sniuid9U0Hc/s400/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee+3.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/-twYrYxp9Lfw/TxWj8ETtpbI/AAAAAAAAAoA/Ux1UsGSf2u4/s1600/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee+4.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"&gt;&lt;img border="0" height="266" src="http://4.bp.blogspot.com/-twYrYxp9Lfw/TxWj8ETtpbI/AAAAAAAAAoA/Ux1UsGSf2u4/s400/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee+4.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/-xydJdv2lDAU/TxWj9ASI6xI/AAAAAAAAAoI/036ZVZgU4YI/s1600/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"&gt;&lt;img border="0" height="266" src="http://3.bp.blogspot.com/-xydJdv2lDAU/TxWj9ASI6xI/AAAAAAAAAoI/036ZVZgU4YI/s400/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-8979421317547111134?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/8979421317547111134/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=8979421317547111134' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8979421317547111134'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8979421317547111134'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/picha-za-msiba-wa-regia-mtema-muhimbili.html' title='Picha za Msiba wa Regia Mtema - Muhimbili mpaka Karimjee'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/-PXeiequqlNE/TxWj5c7zv5I/AAAAAAAAAnw/nORSqSIDlUI/s72-c/Regia+kutoka+Muhimbili-Karimjee+2.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-2707883074540700762</id><published>2012-01-17T08:49:00.000-08:00</published><updated>2012-01-17T08:52:26.868-08:00</updated><title type='text'>Picha za Msiba wa Regia Mtema - Misa Tabata</title><content type='html'>&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/-RkLWTnGYBhg/TxWk2fntuiI/AAAAAAAAAoQ/PWjbdCzkYT8/s1600/Akifukiziwa+ubani.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="225" src="http://2.bp.blogspot.com/-RkLWTnGYBhg/TxWk2fntuiI/AAAAAAAAAoQ/PWjbdCzkYT8/s400/Akifukiziwa+ubani.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Akifukiziwa Ubani&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://2.bp.blogspot.com/-wK4HGsIY95c/TxWk3fVwfAI/AAAAAAAAAoY/W-pEw7ZKm24/s1600/cheyo-makinda-1.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="260" src="http://2.bp.blogspot.com/-wK4HGsIY95c/TxWk3fVwfAI/AAAAAAAAAoY/W-pEw7ZKm24/s400/cheyo-makinda-1.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Mh. Spika Makinda&amp;nbsp;na&amp;nbsp;Mh. Cheyo&amp;nbsp;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/-xKCmCus1-RU/TxWk4pP6e2I/AAAAAAAAAog/mqvrlPCsZqw/s1600/jeneza.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="225" src="http://1.bp.blogspot.com/-xKCmCus1-RU/TxWk4pP6e2I/AAAAAAAAAog/mqvrlPCsZqw/s400/jeneza.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Jeneza&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/-sS7tTksFdpo/TxWk5_N8JtI/AAAAAAAAAoo/YUfawpA8PTI/s1600/mapadre-askofu.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="282" src="http://3.bp.blogspot.com/-sS7tTksFdpo/TxWk5_N8JtI/AAAAAAAAAoo/YUfawpA8PTI/s400/mapadre-askofu.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Mapadre na Askofu&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/-KNH_8F2KJLQ/TxWk6xidL_I/AAAAAAAAAow/BopYeJLB2qA/s1600/Mbowe+na+Lilian.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="225" src="http://3.bp.blogspot.com/-KNH_8F2KJLQ/TxWk6xidL_I/AAAAAAAAAow/BopYeJLB2qA/s400/Mbowe+na+Lilian.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Mh. Freeman na Lilian Mbowe&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://3.bp.blogspot.com/-86nJqE_EeZc/TxWk8QEo23I/AAAAAAAAAo4/81O0qMr8zhM/s1600/Remija-pacha+wa+Regia.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="236" src="http://3.bp.blogspot.com/-86nJqE_EeZc/TxWk8QEo23I/AAAAAAAAAo4/81O0qMr8zhM/s400/Remija-pacha+wa+Regia.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Remija, pacha wake Regia&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/-vePPP-Df5dY/TxWk9p4Rp-I/AAAAAAAAApA/O0BhT-MARxc/s1600/slaa-josephine.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="253" src="http://4.bp.blogspot.com/-vePPP-Df5dY/TxWk9p4Rp-I/AAAAAAAAApA/O0BhT-MARxc/s400/slaa-josephine.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Dr. Wilbrod Slaa&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;table align="center" cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="margin-left: auto; margin-right: auto; text-align: center;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/-nZY1YBVLHBQ/TxWk_HHt3fI/AAAAAAAAApI/AXJSrdFvcXM/s1600/Waumini.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="225" src="http://4.bp.blogspot.com/-nZY1YBVLHBQ/TxWk_HHt3fI/AAAAAAAAApI/AXJSrdFvcXM/s400/Waumini.jpg" width="400" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption" style="text-align: center;"&gt;Waumini&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-2707883074540700762?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/2707883074540700762/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=2707883074540700762' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2707883074540700762'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2707883074540700762'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/picha-za-msiba-wa-regia-mtema-misa.html' title='Picha za Msiba wa Regia Mtema - Misa Tabata'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/-RkLWTnGYBhg/TxWk2fntuiI/AAAAAAAAAoQ/PWjbdCzkYT8/s72-c/Akifukiziwa+ubani.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-1606962740583324147</id><published>2012-01-14T08:25:00.000-08:00</published><updated>2012-01-14T08:25:37.288-08:00</updated><title type='text'>TANZIA</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;table cellpadding="0" cellspacing="0" class="tr-caption-container" style="float: left; margin-right: 1em; text-align: left;"&gt;&lt;tbody&gt;&lt;tr&gt;&lt;td style="text-align: center;"&gt;&lt;a href="http://4.bp.blogspot.com/-RQZtT7LEafk/TxGsEoupEUI/AAAAAAAAAno/c6QALv76_VE/s1600/Regia.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; margin-bottom: 1em; margin-left: auto; margin-right: auto;"&gt;&lt;img border="0" height="231" src="http://4.bp.blogspot.com/-RQZtT7LEafk/TxGsEoupEUI/AAAAAAAAAno/c6QALv76_VE/s320/Regia.jpg" width="320" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;tr&gt;&lt;td class="tr-caption"&gt;&lt;div style="text-align: center;"&gt;&lt;i&gt;Mh.  Regia Mtema; Mbunge wa Viti Maalum na&amp;nbsp;&lt;/i&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: center;"&gt;&lt;i&gt;Waziri Kivuli wa Kazi na Ajira&lt;/i&gt;  &amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;/td&gt;&lt;/tr&gt;&lt;/tbody&gt;&lt;/table&gt;Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepatwa na majonzi makubwa na kinasikitika sana kwa kifo cha Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Taifa, Mheshimiwa Regia Mtema ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum na Waziri Kivuli wa Kazi na Ajira. Mheshimiwa Regia Mtema amefariki leo tarehe 14 Januari 2011 kwa ajali ya gari katika eneo la Ruvu darajani.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika uhai wake marehemu Regia Mtema amefanya kazi mbalimbali za kisiasa na kijamii katika taifa. Marehemu Regia Mtema amezaliwa tarehe 21 mwezi Aprili mwaka 1980 na kusoma shule za sekondari kidato cha kwanza mpaka cha sita katika shule ya sekondari ya Forodhani na Shule ya Wasichana ya Sekondari ya Machame. Marehemu Regia Mtema alipata shahada yake ya kwanza (Bsc Home Economics and Human Nutrition) katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mara baada ya kuhitimu masomo yake marehemu Regia Mtema alifanya kazi katika taasisi mbalimbali kabla ya kujiunga na CHADEMA na kuteuliwa kuwa Afisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Vijana ya CHADEMA na baadaye kuteuliwa kuwa Afisa Mwandamizi katika Kurugenzi ya Mafunzo ya CHADEMA nafasi ambayo aliishikilia hadi mwaka 2010 alipoteuliwa kuwa mbunge wa viti maalum.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Viongozi wakuu wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, Katibu Mkuu Dr. Wilbroad Slaa, wajumbe wa kamati kuu, wakurugenzi wa chama makao makuu na wabunge wamejumuika hivi sasa na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;CHADEMA inatoa pole kwa familia ya marehemu Regia Mtema, wanachama wote na wananchi wa Mkoa wa Morogoro hususani wa Jimbo la Kilombero kutokana na msiba huu wa ghafla katika wakati ambapo mchango wake ukihitajika kwa chama na kwa taifa.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Taarifa zaidi kuhusu taratibu za maziko, itatolewa mara baada ya kukamilisha majadiliano baina ya familia ya marehemu, chama na Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mipango ya mazishi ya marehemu inapangwa nyumbani kwa Baba wa Marehemu Regia Mtema, Ndugu Estelatus Mtema, Tabata Chang'ombe. Ratiba ya maziko itatolewa baada ya kukamilika kwa taratibu zinazopangwa na familia ya marehemu, Ofisi ya Bunge na chama.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mungu ailaze roho ya Marehemu Regia Mtema, mahali pema peponi. Amina.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Imetolewa na:&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;b&gt;&lt;/b&gt;&lt;br /&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;&lt;b&gt;John Mnyika(Mb)&lt;/b&gt;&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;b&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;Mkurugenzi wa Habari na Uenezi&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;/b&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-1606962740583324147?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/1606962740583324147/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=1606962740583324147' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1606962740583324147'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1606962740583324147'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/tanzia.html' title='TANZIA'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/-RQZtT7LEafk/TxGsEoupEUI/AAAAAAAAAno/c6QALv76_VE/s72-c/Regia.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-7907490948299913457</id><published>2012-01-09T05:34:00.000-08:00</published><updated>2012-01-09T05:34:39.419-08:00</updated><title type='text'>Magufuli hajasema kweli; Anaficha Udhaifu wa Serikali na Wizara yake</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: center;"&gt;&lt;b&gt;TAARIFA KWA UMMA&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;&lt;br /&gt;&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;UTANGULIZI&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Tarehe 4 na 5 Januari 2011 Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa John Magufuli alinukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari akitoa madai mbalimbali juu yangu wakati akijibu kauli za Wabunge wa Dar es salaam juu ya ongezeko la nauli katika vivuko vya Kigamboni na maeneo mengine nchini.Toka Waziri Magufuli atoe kauli zisizokuwa za kweli dhidi yangu badala ya kujibu hoja za msingi nilizotaka maelezo toka wizara yake na serikali kwa ujumla sikutoa tamko kwa kuwa nilikuwa katikati ya kazi mbalimbali jimboni Ubungo na majukumu mengine ya kitaifa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hata hivyo, kuna msemo kwamba ‘uongo ukiachwa ukarudiwa rudiwa unaweza kuaminika kuwa ndio ukweli’; hivyo naomba kutoa taarifa kwa umma kujibu madai hayo kwa lengo la kuweka rekodi sahihi.Namheshimu Waziri Magufuli, hata hivyo kauli alizozitoa dhidi yangu zinadhirisha kuwa ameanza kulewa sifa kwa kiwango cha kuwa mpotoshaji na mzushi. Ni vyema umma ukachukua tahadhari kwamba imani ya wananchi juu yake ameanza kuitumia vibaya kulinda uzembe, ubabe na ufisadi.Aidha, ni muhimu akawa anajielekeza kujibu madai ya msingi ya wananchi badala ya kuibua masuala mengine kwa lengo la kuhamisha mjadala; hivyo nitarudia tena masuala ambayo nilitaka ayatolee maelezo na vielezo kwa maslahi ya umma.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;&lt;br /&gt;&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU KIINGILIO KATIKA KITUO KIKUU CHA MABASI UBUNGO (UBT)&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Magufuli amezusha na kupotosha kwamba sijawahi kuhoji kupandishwa kwa kiingilio katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo (UBT) cha 200. Ukweli ni kwamba kama ambavyo napinga ongezeko holela la nauli za vivuko nchini, nilipinga ongezeko la kiingilio katika Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo kwa maslahi ya wananchi wa jimbo letu na ya wasafiri wote nchini wanaotumia kituo hicho. Ukweli zaidi ni kwamba viingilio vya Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo pamoja na ongezeko lake vilipitishwa kwa kutungiwa sheria ndogo (by law) na jiji kabla ya mimi kuchaguliwa kuwa mbunge.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hata hivyo, pamoja na kuwa sikuwa mbunge wakati kiingilio kinawekwa mara baada ya kuwa mbunge niliendelea na harakati nilizozianza kabla ya kuwa mbunge za kupinga ufisadi wa mapato katika kituo hicho. Tarehe 28 Januari 2011 nilifanya ziara ya kituoni hapo kama sehemu ya kutimiza wajibu wa kibunge ambapo pamoja na mambo mengine nilikutana na mawakala wa kituo kusikiliza malalamiko yao ikiwemo kuhusu kiingilio. Kufuatia kupinga huko Tarehe 11 Mei 2011 Kamati ya Fedha na Uongozi ya Jiji la Dar es salaam ilipitisha azimio la kupendekeza kwamba utekelezaji wa sheria ndogo iliyoongeza kiingilio usitishwe.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa kuwa sheria ndogo imetungwa na baraza la madiwani, nilikwenda mbele zaidi kupinga kiwango cha kiingilio na ufisadi katika Kituo cha Mabasi Ubungo kwa kuwasilisha hoja binafsi Tarehe 15 Mei 2011. Kutokana na ukubwa wa hoja ya ufisadi katika kituo hicho kwa mujibu wa vyanzo vyetu na ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali suala hilo limekuwa likichukua muda kushughulikiwa na nimeendelea kupinga na kuhoji kwenye vikao vya jiji, kupitia vyombo vya habari na hata bungeni Waziri Magufuli akisikia.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa sasa tayari jiji limekubaliana na hoja hiyo kinachofuata ni baraza la madiwani kupitisha azimio la kufanya mabadiliko husika. Hivyo, Waziri Magufuli hakusema ukweli alipodai kwamba sijawahi kupinga ongezeko la kiingilio katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo. Jaribio lake dhaifu la kutaka kuonyesha kwamba nimeacha ya kwetu nakwenda kushughulikia ya wengine hatimaye litashindwa ukweli utakapotamalaki.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU MADAI KWAMBA SIJAWAHI KUPENDEKEZA BARABARA ZA KUPANDISHWA HADHI NA KUFANYIWA KAZI KWA AJILI YA KUPUNGUZA FOLENI&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Magufuli amezusha na kupotosha kwamba sijawahi kupendekeza barabara za kupandishwa hadhi ili zishughulikiwe na serikali kuu kwa ajili ya kupunguza foleni katika jimbo la Ubungo na Dar es salaam kwa ujumla. Ukweli ni kwamba mara baada ya kuchaguliwa katika kikao changu cha kwanza kabisa kushiriki cha Bodi ya Barabara ya Mkoa mwezi Februari 2011 ambacho chombo cha Wizara yake cha utendaji cha Wakala wa Barabara (TANROADS) kikiwepo nilitoa mapendekezo ya barabara husika na hatua ambazo serikali ilipaswa kuchukua katika maandalizi ya kupandisha hadhi na pia katika bajeti, hatimaye orodha ya barabara husika za kupandishwa hadhi ziliwasilishwa na kupitishwa katika vikao vilivyofuatia.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pia, nimeandika barua rasmi mbili zenye mapendekezo mahususi kwa TANROADS na Waziri wa Ujenzi barabara za kushughulikiwa kupunguza foleni (Aprili na Mei 2011); lakini Waziri Magufuli hajawahi kujibu barua hata moja huku miezi zaidi ya sita ikiwa imepita. Baada ya ukimya kwa kutokutekelezwa kwa mapendekezo ya kikao cha bodi ya barabara na kutokujibiwa kwa barua nilichukua hatua za kuwasilisha mapendekezo bungeni ya barabara muhimu kwa ajili ya kupunguza foleni na kutaka majibu ya kuzipandisha hadhi barabara husika wakati nachangia kwenye mjadala wa Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano Tarehe 14 Juni 2011.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nikaeleza zaidi hatua zinazopaswa kuchukuliwa na serikali kupunguza foleni jimbo la Ubungo na Dar es salaam kwa ujumla Tarehe 2 Agosti 2011 wakati nachangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ikiwemo kuhusu kupandisha hadhi barabara husika na kuongeza kiwango cha bajeti. Waziri Magufuli kuzusha na kupotosha kwamba sijawahi kupendekeza kupandishwa hadhi kwa barabara inadhirisha kwamba amekuwa msahaulifu na amefanya jaribio dhaifu la kunichonganisha na wananchi wa jimbo letu kuwa sifuatilii masuala yetu. Ukweli ni kwamba foleni inaendelea kuwepo kwa sababu ya uzembe wa Wizara ya Ujenzi na serikali kwa ujumla kushindwa kutenga Fedha za kutosha kwa ajili ya kulimaliza tatizo pamoja na kupata hasara ya mabilioni kila siku, kiwango ambacho kimetengwa kwa ajili ya barabara za pembezoni za kupunguza msongamano ikiwemo za Ubungo na Dar es salaam nzima kwa mwaka wa Fedha 2011/2012 ni bilioni tano tu; hivyo suala la msingi ambalo Waziri Magufuli anapaswa kulijibu ni iwapo serikali imekubaliana na ushauri wangu wa kufanya mapitio ya bajeti na kuongeza Fedha kwenye mkutano ujao wa bunge kwa ajili ya mkakati wa kuondoa foleni Dar es salaam.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU MADAI YA KUSHINDWA KUJA NA WAZO LA KUSHIRIKISHA WAKALA WA NYUMBA (TBA) KWENYE KUTAFUTA SULUHISHO LA MALAZI KWA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU:&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Magufuli amezusha suala tofauti la madai ya kushindwa kuja na wazo la kushirikisha Wakala wa Nyumba (TBA) kwenye kutafuta suluhisho la malazi kama sehemu ya nyingine ya jaribio lake dhaifu la kuhamisha mjadala na kujaribu kutafuta huruma ya kuungwa mkono na wanafunzi wa vyuo vikuu jimboni Ubungo. Ukweli ni kwamba kazi kubwa ya TBA ambayo iko chini ya Wizara ya Ujenzi na kujenga nyumba za watumishi wa umma, na katika mwaka wa Fedha 2011/2012 ina rasilimali chache za kumalizia miradi iliyopo na kutafuta viwanja vya kujenga nyumba za serikali.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa hiyo, katika kufanya kazi za kibunge kuhusu TBA ninachofuatilia kwa sasa ni nyumba za watumishi wa umma na masuala ya malazi ya wanafunzi nayafuatilia kwa vyombo na mamlaka nyingine. Ingekuwa TBA ina fursa hiyo anayodai Waziri Magufuli angeiwezesha kuwepo katika harambee iliyofanywa na Rais Jakaya Kikwete jimboni Ubungo kwa ajili ya Kituo cha Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) ambao taasisi na watu mbalimbali tulichangia kwa ajili ya ustawi wa wanafunzi. Katika hali ya sasa, TBA haina uwezo wa kuanza kujenga maeneo ya malazi ya wanafunzi wakati haijaweza hata kuziba pengo la nyumba za serikali zilizouzwa kinyemela kwa uratibu wa Waziri Magufuli.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wanafunzi wa Vyuo Vikuu hawawezi kupotoshwa na Waziri Ujenzi kwamba ana dhamira ya kuwajengea maeneo ya malazi wakati ambapo amesababisha mpaka mawaziri na watumishi wenzake wa umma kukaa mahotelini au kupanga kwa gharama kubwa kwa sababu ya watangulizi wao akiwemo Magufuli kujiuzia nyumba za serikali kwa upendeleo. Waziri Magufuli anapaswa kuwaeleza wanafunzi wa vyuo vikuu na watanzania kwa ujumla kiwango cha ubadhirifu na madeni kwa taifa kinachopunguza uwezo wa serikali kuwapatia mikopo ya elimu ya juu, kuwajengea maeneo ya malazi na kutekeleza miradi mingine ya msingi ya maendeleo na athari ambazo TBA imepata kutokana na kuuzwa kiholela kwa nyumba za serikali.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU KUKUTANA KUZUNGUMZIA MAAFA YA MAFURIKO YALIYOLIKUMBA JIJI LA DAR ES SALAAM&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Magufuli amezusha na kupotosha kwamba hatujawahi kukutana kwa ajili ya kuzungumzia maafa ya mafuriko. Ukweli ni kuwa kauli kuhusu suala la kivuko tulizitoa tukiwa tunajiandaa kuingia kwenye kikao cha kamati ya maafa ya mkoa kujadili masuala ya mafuriko, na kabla ya siku hiyo wabunge tumejumuika kwenye vikao vingine vya maafa katika Mkoa wetu. Aidha, toka maafa ya mafuriko yatokee Tarehe 20 Disemba 2011 nimeshiriki kwa hali na mali katika hatua zote ikiwemo hatua aliyoitaja Waziri Magufuli ya kupendekeza njia bora za kuwasaidia wanaoishi mabondeni. Hivyo, kauli hii ni jaribio linguine dhaifu la kujaribu kujenga hisia kuwa hatujali matatizo ya msingi ya wananchi ya wakati huu ili kuhamisha mjadala.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU MADAI KWAMBA NILIPASWA KUSHUGHULIKIA MAMBO YA UBUNGO NA SI YA KIGAMBONI&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Magufuli amejaribu kujenga dhana potofu kwamba nilipaswa kushughulikia masuala ya jimbo letu la Ubungo na si kujiingiza kwenye kero za jimbo linguine. Ukweli ni kuwa kero zote tatu alizodai kuwa nimeziacha jimboni bila kuzifuatilia za kiingilio cha Ubungo, kupandisha hadhi barabara za kupunguza foleni na suala la kutumia TBA katika kupata suluhisho la malazi ya wanafunzi wa vyuo vikuu nimezitolea maelezo yenye kuonyesha kwamba nimetimiza wajibu husika wa kibunge.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Maelezo hayo yanayonyesha kwamba ili tuweze kushughulikia kwa haraka zaidi kero za msingi za wananchi mabadiliko ya mfumo wa utendaji kazi yanahitajika kufanya serikali na viongozi wake waweze kuwajibika ipasavyo. Hii inahitaji kuunganisha nguvu ya wengine na mamlaka zingine katika kuisimamia serikali suala ambalo haliwezi kutimia kwa kazi za ndani ya jimbo pekee. Ukweli ni kwamba mbunge pamoja na kuwakilisha wananchi wa jimbo waliomtuma, anawajibika vile vile kwa nchi, kwa chama na kwa nafasi yake. Hivyo, katika kutimiza majukumu ya kibunge yanatokana mamlaka ya bunge ya kuisimamia serikali kwa mujibu wa Ibara ya 63; mbunge anapaswa kuwasimamia mawaziri na serikali kwa ujumla.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Matokeo ya kuwezesha mabadiliko ya kiutendaji na uwajibikaji yanatija kwa wananchi wote ikiwemo wa jimbo la Ubungo. Aidha, kama katibu wa wabunge wa Mkoa wa Dar es salaam nina wajibu wa kushughulikia suala lolote linalomgusa mbunge yoyote wa Mkoa wetu iwapo linahitaji nguvu ya pamoja kwa maslahi ya umma. Izingatiwe pia, mwingiliano wa Dar es salaam wapo wananchi wa Ubungo wanaofanya kazi ama kufanya biashara Kigamboni ambao nao wametaka niwawakilishe kwenye suala hili kama ninavyofanya kwa mengine. Pia, ifahamike kwamba kilichotukutanisha wabunge siku tuliyotoa kauli ni kikao na kamati ya maafa ya mkoa tofauti na madai potofu aliyotoa kwamba wabunge hatujawahi kukutana kwa ajili ya masuala ya maafuriko yaliyoukumbuka mkoa wa Dar es salaam.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU KIWANGO CHA UPANDISHWAJI WA NAULI KATIKA KIVUKO CHA KIGAMBONI NA VIVUKO VINGINE NCHINI&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Magufuli ameamua kupotosha kwamba nilichompinga na kupanda kwa nauli kutoka shilingi 100 mpaka 200, na kuacha kujibu hoja kuu ambazo nilitaka azitolee maelezo na vielelezo. Ukweli ni kuwa nilichotaka kisitishwe ni utekelezaji wa agizo kupitia gazeti la serikali (GN 367) ya tarehe 4 Novemba 2011 na kuanza kutumika kwa nauli mpya kwa ujumla wake kutokana na kukiukwa kwa misingi ya utawala bora na pia baadhi ya viwango kutokuzingatia hali halisi. Kwa upande wa kupanda kwa nauli nilisisitiza kuwa kero kuu sio kupanda nauli ya mtu mzima toka shilingi 100 mpaka 200 bali kupandishwa kupindukia kwa nauli za vyombo vya usafiri na usafirishaji hali ambayo itasababisha kupanda kwa bei ya bidhaa katika eneo la Kigamboni na kuathiri watu wengi zaidi.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mathalani, Baskeli za matairi matatu (Guta) toka Tsh 200 hadi Tsh 1800 (Asilimia 800); bei ambayo ni kubwa kuliko ya gari ndogo; bajaj zimepanda toka Tsh 300 hadi Tsh 1300 (Asilimia 333); mikokoteni imeongezeka toka Tsh 200 hadi Tsh 1500 (Asilimia 650) na mizigo nayo inatozwa kati ya shilingi 200 mpaka 500. Sasa kwa kuwa utekelezaji wa agizo unafanyika kwa ujumla, nikataka viwango vipya kwa ujumla wake visitishwe mpaka kwanza serikali itoe maelezo na vielezo vya msingi wa kufanya ongezeko kubwa la kiwango hicho. Nilitaka serikali itoe maelezo ikizingatia kwamba vivuko ni huduma sio biashara kwa kuwa maeneo mengi yenye vivuko yalipaswa kuwa na madaraja kwa ajili ya vyombo hivyo vya usafiri na wananchi kuweza kupita.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nilieleza wazi kwamba kazi ya msingi ya Wizara ya Ujenzi ni kujenga barabara, madaraja na miundombinu mingine sio kufanya biashara ya vivuko hivyo, ongezeko la kuangalia soko linaweza kushawishi ucheleweshaji wa ujenzi wa madaraja. Ieleweke kwamba kazi kuu ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) sio kuendesha vivuko na kama tunataka suala hili kuwa ndio kipaumbele tunayo Wizara ya Uchukuzi ambayo inahusika pia na uchukuzi majini na inashirika la meli. Kumekuwepo na kukosekana na uwazi na udhibiti wa kutosha wa mapato na matumizi ya kivuko hivyo tulitaka serikali ieleze kwa mchanguo badala ya kauli za ujumla kuhusu suala hili ili kujenga uhalali wa kupandisha nauli husika kwa hoja ya kupanda kwa gharama za uendeshaji. Nilipinga ongezeko kubwa la bei ya umeme kwa kisingizio hicho hicho, kwa kuwa mchakato ulikuwa shirikishi naamini kutokana na maoni ya wadau yako ambayo yatarekebishwa na TANESCO tofauti na mapendekezo yao ya awali.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Haiwezekani suluhisho la kupanda kwa gharama za maisha kwa wabunge ikawa kujiongezea posho za vikao na suluhisho kwa taasisi za umma kama Wizara ya Ujenzi na TEMESA ikiwa ni kijiongeza mapato kwa kuongeza nauli bila kuzingatia kubana matumizi na kumjali mtanzania wa kipato cha chini ambaye anabeba mzigo mkubwa wa kupandwa kwa gharama za maisha na sasa anapindishiwa hata na serikali yake nauli za vyombo vya usafiri kuvuka tu kwenye kivuko. Hivyo, Wizara ya Ujenzi kupitia vyombo vyake inapaswa kuhusisha mapato yanayokusanywa kwenye barabara na ujenzi wa miundombinu na uendeshaji wa vivuko vya muda wakati miundombinu inasubiriwa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pia, pamoja na nauli, msingi wa uendeshaji wa vivuko unapaswa pia kuwa mapato kutoka kwenye barabara na vyanzo vingine. Badala ya kujibu hoja ya msingi, Waziri Magufuli amejikita katika ongezeko la shilingi 100 mpaka 200 na kulinganisha pia na mazingira yasiyoendana baina ya kivuko cha Kigamboni na vivuko vingine nchini ambavyo vinatofautiana umbali, muda na gharama za uendeshaji.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU SHERIA NA UTARATIBU AMBAO UMETUMIKA KUPANDISHA VIWANGO HUSIKA&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Magufuli amezusha na kupotosha kwamba nilisema amekiuka sheria ya uendeshaji wa vivuko. Ukweli ni kwamba katika kauli yangu nilisema wazi kwamba Waziri Magufuli amepandisha viwango vya kivuko hicho kwa mamlaka aliyopewa na sheria mbovu ya vivuko (Ferries Act), hata hivyo nilisisitiza kwamba mamlaka hayo ameyatumia kibabe na kwa kutozingatia misingi ya utawala bora. Nilisema kwamba Waziri Magufuli anapaswa kuzingatia kwamba nchi haiongozwi kwa sheria moja, na ikiwa anataka kutumia sheria moja basi sheria mama ni katiba ya nchi.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nilisema kwamba kwa mujibu wa ibara ya 8 ya katiba ya taifa letu wananchi ndio msingi wa mamlaka, ibara ya 18 inataka wananchi wapewe taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali kwa maisha na shughuli zao na ibara ya 21 inatoa haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi ama moja kwa moja au kupitia wawakilishi. Hivyo, katika kutekeleza sheria ya vivuko na kanuni zake badala ya kutumia ubabe Waziri Magufuli alipaswa kuzingatia misingi hiyo muhimu lakini hakufanya hivyo kwa sababu nauli zimepandishwa bila kuwa na uwazi wala ushirikishwaji. Wananchi na wadau hawakushirikishwa katika kutoa maoni kuhusu suala linalowahusu kama ambavyo mamlaka zingine za kiserikali zinafanya wakati wa michakato ya kupandisha bei, mathalani mashirika ya umma ya umeme, mafuta na gesi hufanya michakato hiyo kupitia EWURA.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nikasema kwamba pamoja na kuwa sheria hailekezi kwa kina jambo hili, Waziri Magufuli na Wakala wa Serikali wa Ufundi na Umeme (TAMESA) walipaswa kuonyesha mfano hasa kwa kuwa walishaombwa kufanya hivyo kwa barua ya mwaka 2011 mwanzoni ambayo wizara yake haikutimiza wajibu hata wa walau kujibu. Nikaeleza kwamba Serikali imeweka mfumo kama huu kwa usafiri wa nchi kavu na majina kupitia SUMATRA kwa upande wa watoe huduma wengine, hivyo ilipaswa na yenyewe kuonyesha mfano. Ndio msingi wa kusema kwamba kwa kuwa suala hili limelalamikiwa na wananchi na wabunge ni vizuri agizo likasitishwa na taratibu shirikishi zikatumika kwa kushauriana na SUMATRA.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nilieleza kwamba suala hili linatokana na udhaifu wa mifumo yetu ya utendaji na uendeshaji ambapo taasisi za kiserikali zinahodhi michakato muhimu ya kitaifa na linakuwa zito zaidi kwa kuwa halikuelezwa bayana hata wakati bunge linajadili makadirio ya mapato na matumizi ya serikali bungeni ya Wizara ya Ujenzi Tarehe 1 na 2 Agosti 2011. Nikaeleza kwamba mjadala huu ni muhimu kwa taifa kwa ajili ya kubadili sheria na taratibu husika pamoja na kuweka mfumo mzuri zaidi wa utendaji na uwajibikaji bila kuwa na mivutano kwenye masuala ambayo kama yangekuwepo mawasiliano na mashauriano yasingefikia hatua ya kuwa malumbano. Hivyo, tukiachia hali hii ikiendelea bila uwazi, ushirikishaji na uwajibikaji itaendelea kwenye masuala yanayowagusa wananchi wa maeneo mengine nchini ikiwemo wa jimbo letu la Ubungo. Kwa hiyo, kuunga kwangu mkono suala hili ilikuwa ni sehemu ya kutekeleza ahadi ambayo niliwaahidi wananchi wa Ubungo wakati wa uchaguzi kwamba nitasimamia vyombo vyote vinavyohusika na masuala ya usafiri na mengine ya huduma za msingi wa umma.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;b&gt;KUHUSU KAULI ZISIZOZINGATIA MISINGI YA UONGOZI NA UTAWALA BORA&lt;/b&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nilipinga kauli za Waziri Magufuli zisizozingatia uongozi na utawala bora mathalani kuwaambia wananchi wapige mbizi au kumshambulia mbunge katika jambo ambalo kama Waziri Magufuli na TEMESA wangezingatia misingi ya utendaji bora kwa kujibu barua lisingefikia kuwa na malumbano hadharani. Waziri Magufuli angeweza kabisa kujenga hoja bila kuzusha vioja visivyo vya lazima, kisingizio cha kauli ya watendaji wa Wizara yake kwamba alifanya hivyo baada ya kuzomewa na wananchi hakiwezi kuhalalisha misingi muhimu ya uongozi wa busara na unyenyekuvu badala ya ubabe na uropokaji. Jambo hili lisingekuwa na uzito kama ingekuwa ni makosa ya mara ya kwanza, hata hivyo nililazimika kutoa kauli ya kumtaka aombe radhi nikikumbuka pia kauli zake ambazo mpaka sasa hajawahi kuomba radhi kwa umma wakati akijibu wananchi na viongozi waliokuwa wakilalamikia uuzwaji holela wa nyumba za serikali kwamba ‘nyie mwaona wivu’ ama ‘mlie tu’. Hivyo, ameendeleza tu hulka yake na sitarajii kwamba itabadilika hata baada ya taarifa hii kwa umma kuhusu masuala ambayo amezusha na kupotosha juu yangu. Kwa heshima niliyonayo kwake natarajia kwamba atabadilika, na natarajia utakubali ndani ya wiki moja kunijibu kukubali kupokea changamoto hizi na kuzifanyia kazi. Asipofanya hivyo, tutakutana bungeni na nitafuatilia mabadiliko ya kisheria, kikanuni, kimfumo na kiutendaji katika Wizara yake kwa karibu zaidi kwa ajili ya maendeleo ya miundombinu ya wananchi wa Jimbo la Ubungo na Taifa kwa ujumla.Wenu katika utumishi wa umma,&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;08/01/2012&lt;/div&gt;&lt;/div&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-7907490948299913457?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/7907490948299913457/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=7907490948299913457' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7907490948299913457'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7907490948299913457'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/magufuli-hajasema-kweli-anaficha.html' title='Magufuli hajasema kweli; Anaficha Udhaifu wa Serikali na Wizara yake'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-1683587930290525779</id><published>2012-01-05T04:16:00.000-08:00</published><updated>2012-01-05T05:38:29.551-08:00</updated><title type='text'>Kuhusu kauli za Waziri Magufuli</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa wote mliotaka maoni yangu juu kuhusu kauli za Waziri Magufuli  vyombo vya habari kuhusu mbunge wa Ubungo na Jimbo letu. Katika siku hizi tatu sina muda wa malumbano, niko katikati ya kazi ya kuwatumikia wananchi jimboni na kutekeleza wajibu mwingine wa kitaifa. Wananchi na wadau wengine mnaweza kumwambia ukweli mnaoufahamu kuhusu aliyoyasema mkipenda, kwa kuwa matendo yanazungumza zaidi ya maneno. Mjadala huu na mingine ni muhimu pia kubadilisha mifumo na kurejesha utamaduni wa uwajibikaji katika taifa letu.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mambo ambayo amesema kwamba siyashughulikii ukweli ni kwamba nilishachukua hatua kwa nyakati mbalimbali kwenye mwaka 2011 ndani ya bunge, kwenye halmashauri na pia nje ya bunge, na matokeo yameanza kuonekana. Baadhi ya hatua hizo nilimhoji yeye mwenyewe au mamlaka za Wizara yake kama sehemu ya kutimiza wajibu wa kibunge wa kuwakilisha wananchi, kutunga sheria na kuisimamia serikali.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa bahati mbaya amekuwa msahaulifu hata wa kauli zake mwenyewe kuhusu masuala niliyoyaibua, amelewa sifa kwa kiwango cha kusema maneno yasiyokuwa ya kweli, imani juu yake imempa upofu wa kupindisha mambo mbalimbali na kugeuzia watu wengine mambo ambayo yeye mwenyewe au wenzake katika serikali wamefanya uzembe wa kutochukua hatua kwa wakati.  Kwa bahati nzuri, ukweli una sifa moja, huwa unadumu milele; nitamjibu hoja kwa hoja nikipata wasaa kwa sasa naendelea na utumishi, maslahi ya UMMA kwanza.&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-1683587930290525779?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/1683587930290525779/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=1683587930290525779' title='5 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1683587930290525779'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1683587930290525779'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/kuhusu-kauli-za-waziri-magufuli.html' title='Kuhusu kauli za Waziri Magufuli'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>5</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-7484534843560311300</id><published>2012-01-04T10:33:00.001-08:00</published><updated>2012-01-05T05:38:56.690-08:00</updated><title type='text'>Kazi za leo jimboni Ubungo</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Leo nimeendelea na kazi za kibunge jimboni katika kata ya Kwembe nimefanya ziara na kukutana na wananchi, wameniuliza maswali kuhusu maji, barabara ya kwenda Mpiji Magohe, Luguruni Satellite town, mgogoro wa ardhi katika eneo la Msakuzi na uharibifu wa daraja katika mto Mdidimua/Kibwegere (Mji Mpya). Nimewajibu hatua ambazo nimechukua kwa kila jambo.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pia nimekabidhi Jengo la Kituo cha Afya na Mama na Mtoto Kata ya Kwembe Jimboni Ubungo, tulichojenga kwa fedha za Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo (CDCF). Habari zaidi zitafuata; Maslahi ya Umma KWANZA.&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-7484534843560311300?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/7484534843560311300/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=7484534843560311300' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7484534843560311300'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7484534843560311300'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2012/01/kazi-za-leo-jimboni-ubungo.html' title='Kazi za leo jimboni Ubungo'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-1381640536807246013</id><published>2011-12-29T22:26:00.000-08:00</published><updated>2011-12-30T12:33:29.112-08:00</updated><title type='text'>Kuhusu matatizo ya maji kata ya Goba; uvumilivu unakaribia kikomo</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Matatizo ya maji kata ya Goba ni matokeo ya udhaifu wa watendaji katika ngazi mbalimbali na natoa mwito kwa mamlaka zinazowasimamia watendaji hao kuchukua hatua stahiki na kutoa taarifa kwa wananchi katika kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kazi ya mbunge kwa mujibu wa katiba na sheria ni kuwakilisha wananchi, kuisimamia serikali na kutunga sheria. Utekelezaji ni jukumu la mamlaka, vyombo na ngazi mbalimbali za kiserikali.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Matatizo ya maji kata ya Goba yanafahamika kwa mamlaka zote husika kuanzia Wizara ya Maji, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Manispaa ya Kinondoni na vyombo vya dola kuanzia mwaka 2007 mpaka mwaka 2011 lakini hatua kamili hazijachukuliwa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wananchi wamepoteza uvumilivu na kama hatua hazitachukuliwa kwa haraka viongozi wa kuchaguliwa hatutakuwa na sababu ya kuendelea kuwaambia wavute subira; tutaungana nao katika kushinikiza uwajibikaji.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika kipindi cha wiki mbili huduma ya maji isiporudishwa kwenye kata ya Goba nitatangaza mgogoro na Manispaa ya Kinondoni pamoja na mamlaka zingine husika na kuwaunganisha wananchi kuchukua hatua watakazoona zinafaa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nimefikia hatua ya kutoa kauli hii nzito kwa sababu njia zote za kawaida kupitia vikao na mawasiliano ya kiofisi zinaelekea kukwamishwa na uzembe, hujuma na urasimu na udhaifu wa kiutendaji katika ngazi mbalimbali.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kufuatia DAWASCO kutokutoa majibu kwa suala hili na mengine tarehe 5 Septemba 2011 niliwaunganisha wananchi kwa pamoja tukaandamana kwenda ofisi ya DAWASCO makao makuu ambapo tulikutana na mtendaji mkuu wa kampuni husika na kufanya mazungumzo ambayo yamesaidia baadhi ya hatua za msingi kuchukuliwa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kufuatia maandamano na mazungumzo hayo DAWASCO wametekeleza wajibu wao kwa hatimaye kukubali kurejesha maji kwenye kata ya Goba na kupanga utaratibu wa deni kulipwa kwa awamu.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika kuchangia kuwezesha hatua hiyo kuchukuliwa kwa wakati nilishawishi kiwango cha milioni tatu kutolewa kwa ajili ya mradi wa maji Goba kutoka katika Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo (CDCF).&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hata hivyo, pamoja na kutengwa kwa fedha hizo kikwazo cha huduma ya maji kurejeshwa katika vituo vya kutoa huduma ya maji katika kata ya Goba ni matatizo katika kamati ya maji kwa upande mmoja na udhaifu mkubwa wa watendaji wa manispaa ya Kinondoni idara ya maji mpaka ngazi ya kata.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kisingizio wakati wote kimekuwa ni zoezi la kufukua mabomba kwa ajili ya uhakiki; hali ambayo imefanya matatizo ya maji yadumu Goba kwa zaidi ya miezi minne na kufanya watanzania wa kipato cha chini wanunue maji kwa bei ya juu au kuyapata kwa umbali mrefu.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Tarehe 24 Oktoba 2011 niliandika barua kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni kutoa mwito wa hatua za dharura kuchukuliwa ili kuhakikisha uhakiki unafanyika wakati huo huo wananchi wengine wanaendelea kupata huduma ya maji; lakini udhaifu wa kiutendaji umefanya hatua ziwe za kusuasua.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika kushughulikia masuala la maji kwenye kata ya Goba, narudia kusisitiza hatua zifuatazo kuendelea kuchukuliwa kwa haraka na mamlaka zifuatazo:&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mosi; Mamlaka za Manispaa ya Kinondoni zikiongozwa na Meya na Mkurugenzi zinapaswa kufuatilia kwa haraka kuhakikisha maji yanarejeshwa Goba. Hatua hii iende sambamba na kupanua wigo wa maji Goba kwa kutekeleza kwa haraka upatikanaji wa maji kutoka pia mradi wa maji toka Madale Kisauke. Manispaa izingatie matatizo yaliyopo kwenye miradi ya maji inayoendeshwa na manispaa pamoja na kamati za wananchi au vyama vya watumia maji katika maeneo mbalimbali. Hivyo, pamoja na kuchukua hatua kuhusu mradi wa maji wa Goba, Manispaa ichukue hatua juu ya miradi iliyokwamba ukiwemo wa Msewe Golani. Pia, Manispaa ya Kinondoni inapaswa kufanya mabadiliko kwenye idara ya maji kwa kuwa ina udhaifu mkubwa wa kiutendaji.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pili; Wizara ya Maji, Mamlaka ya maji safi na maji taka (DAWASA) na Kampuni ya maji safi na maji taka (DAWASCO) zizingatie kwamba maeneo ya pembezoni ya Dar es salaam ambayo awali yalikuwa vijiji sasa ni mitaa yenye wakazi wengi. Hivyo, maeneo kama kata ya Goba na mengine ya pembezoni yanapaswa kuunganishwa moja kwa moja na mtandao wa maji chini ya mamlaka husika kwa mujibu wa sheria iliyounda DAWASA badala ya mfumo uliopo ambalo haulingani na mahitaji.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Tatu; vyombo vya ulinzi na usalama vinapaswa kushughulikia vyanzo vya migogoro badala ya kusubiri mpaka matatizo yanapoibuka kwa kushughulikia kwa wakati malalamiko yanayotolewa. Mathalani, Jeshi la Polisi (Ofisi ya DCI) na TAKUKURU wanapaswa kutoa kauli kuhusu hatua zilizochukuliwa juu ya tuhuma za ufisadi na ukiukwaji wa sheria katika mradi wa maji Goba ambazo zimetolewa na wananchi kwa mamlaka husika kuanzia mwa 2007.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mamlaka husika zizingatie kuwa tarehe 27 Februari 2011 na 6 Machi 2011 nilifanya mikutano na wananchi katika kata ya Goba ambapo risala ya wananchi pamoja na ripoti ya ukaguzi wa mradi wa mradi wa maji Goba ya mwaka 2007 zilizosomwa ambazo zilieleza bayana matatizo yaliyokuwepo kwenye kamati ya maji pamoja na mradi kwa ujumla ikiwemo yaliyohusu upotevu wa fedha ambayo vyombo vya dola vilipatiwa taarifa lakini hatua hazikuchukuliwa kwa wakati.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Itakumbukwa kwamba tarehe 1 Septemba 2011 nilitoa taarifa ya awali kuhusu ufuatiliaji ambao nilifanya na hatua ambazo nilikusudia kuzichukua kuhusu maji kukatwa katika kata ya Goba na tuhuma juu ya kamati mpya ya maji.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika taarifa hiyo nilieleza kwamba , iwapo DAWASCO isingetoa majibu kabla tarehe 3 Septemba 2011 kuhusu masuala mbalimbali ya maji katika Jimbo la Ubungo ikiwemo kuhusu malalamiko juu ya deni la maji katika kata ya Goba nitawaongoza wananchi wa kata mbalimbali kwenda makao makuu ya DAWASCO wiki ijayo ili kuunganisha nguvu ya umma hatua za haraka zaidi ziweze kuchukuliwa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Aidha, nilitoa mwito kwa Manispaa kuitisha na kuijadili ripoti ya mkaguzi wa ndani kuhusu mradi husika pamoja na taarifa ya kamati ya kufuatilia mfumo mzima wa uendeshaji wa mradi.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika taarifa hiyo nilieleza pamoja na mambo mengine kuwa katika ufuatiliaji wangu nimebaini kwamba Matatizo ya Maji katika Kata ya Goba kama ilivyo katika kata zingine katika Jimbo la Ubungo na Mkoa wa Dar es salaam kwa ujumla yanatokana na matatizo ya kimfumo, kiuongozi, kifedha na kiutendaji yanayosababishwa na Kamati ya mradi wa Maji Goba, DAWASCO, DAWASA, Halmashauri za Jiji la Dar es salaam na Wizara ya Maji ambayo nimekuwa nikiipa taarifa na kutaka iingilie kati kwa nyakati mbalimbali.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;30/12/2011&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-1381640536807246013?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/1381640536807246013/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=1381640536807246013' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1381640536807246013'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1381640536807246013'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/kuhusu-matatizo-ya-maji-kata-ya-goba.html' title='Kuhusu matatizo ya maji kata ya Goba; uvumilivu unakaribia kikomo'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-118789818273320712</id><published>2011-12-29T01:15:00.000-08:00</published><updated>2011-12-29T11:45:52.187-08:00</updated><title type='text'>Serikali itoe taarifa uchunguzi wa kashfa ya UDA</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Serikali inapaswa kutoa taarifa kuhusu hatua iliyofikiwa juu ya ukaguzi na uchunguzi wa tuhuma za ufisadi, ukiukwaji wa sheria, kanuni na maslahi ya wananchi katika mchakato wa ubinafsishaji wa Shirika la Usafiri Dar es salaam (UDA).&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Taarifa hiyo inapaswa kutolewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, vyombo vya dola na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa umma umeanza kupoteza matumaini juu ya hatma ya ukaguzi na uchunguzi huo ambao serikali iliahidi ungefanyika katika kipindi cha mwezi mmoja lakini mpaka sasa miezi minne imepita huku ukimya na usiri ukitawala.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Mkuu Mizengo Pinda anapaswa kutoa taarifa kwa kuwa alitoa agizo bungeni tarehe 4 Agosti 2011 wakati wa kipindi cha maswali kwa mujibu wa Kanuni za Bunge kifungu cha 38 (4) ya kuelekeza vyombo vya dola hususan Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) , Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) na Ofisi ya Upepelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma husika.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Toka agizo hilo litolewe umma wala wabunge hatujawahi kuelezwa hatua ambayo vyombo vya dola hususani TAKUKURU na ofisi ya DCI imefikia katika uchunguzi wa tuhuma za ufisadi, ukiukwaji wa sheria, kanuni na maslahi ya wananchi katika mchakato wa ubinafsishaji wa Shirika la Usafiri Dar es salaam (UDA).&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Taarifa pekee ambayo imetolewa mpaka sasa na ofisi ya Waziri Mkuu ni kuwa tarehe 13 Agosti 2011 Waziri wa Nchi (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa) George Mkuchika alikabidhi barua kwa CAG ya kutaka ufanyike ukaguzi maalum katika kipindi cha mwezi mmoja. Hata hivyo, miezi miwili ilipita bila ukaguzi husika kukamilika na hatimaye mwezi Oktoba CAG akatangaza kwa umma kwamba ameshindwa kumalizia ukaguzi husika kutokana na kutingwa na majukumu mengine.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kutokana na hali hiyo CAG alieleza kwamba ofisi yake imeiteua kampuni binafsi ya KPMG kufanya ukaguzi husika katika kipindi cha mwezi mmoja. Hatahivyo, takribani miezi miwili imepita bila ukaguzi huo kukamilika hivyo; CAG Ludovick Utouh anapaswa kutoa taarifa kwa umma kuhusu hatua iliyofikiwa juu ya ukaguzi huo na kuhakikisha kwamba ukaguzi unakamilika kwa haraka.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Ni muhimu umma ukafahamu kwamba uchunguzi uliokuwa ufanywe na Kamati iliyoundwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) bado haujaanza kutokana na uongozi wa Bunge kuelekeza kwamba uchunguzi huo unapaswa kusubiri ukaguzi wa CAG.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Aidha, ieleweke kwamba madiwani wa jiji la Dar es salaam nao ni vigumu kuchukua hatua kamili kutokana na suala hilo kuwa katika uchunguzi wa maelekezo ya ofisi ya Waziri Mkuu.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hivyo vyombo vya uwakilishi wa wananchi yaani bunge na baraza la madiwani vimebanwa kiufundi kuchukua hatua vikisubiri uchunguzi huo wakati ambapo ukaguzi haujakamilika na kampuni ya Simon Group imeshaingizwa katika umiliki na uendeshaji wa kampuni ya UDA.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pia, wakati ukaguzi huo ukiendelea kuchelewa maofisa waliohusika katika jiji, kampuni ya UDA, wizara mbalimbali na taasisi za serikali wanaendelea na utumishi kama kawaida katika mazingira ambayo yanaacha mianya ya hujuma kwa mali za kampuni na vielelezo mbalimbali.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Pamoja na kuhimiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi, narudia kutoa  mwito kwa Serikali kuagiza kusitishwa mara moja kwa mkataba batili na maamuzi  haramu yaliyofanyika ya kukabidhi hisa, mali na uendeshaji wa kampuni ya UDA kwa Kampuni ya Simon Group Limited ili katika kipindi hiki cha uchunguzi masuala yote ya kampuni hiyo yaratibiwe na bodi huru itayoundwa na kusimamiwa kwa mujibu wa sheria.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Izingatiwe kwamba tarehe 4 Agosti 2011 wabunge wa Dar es salaam tulitoa tamko kwamba tuko tayari kutoa ushahidi kwa vyombo hivyo pamoja na kushirikiana na serikali kwa ujumla wake ili kuwezesha hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa haraka kuhusu tuhuma hizo. Hata hivyo, mpaka sasa kama katibu wa wabunge sijaitwa na chombo chochote cha serikali kuhusu suala la UDA na sijapokea taarifa toka kwa mbunge yoyote mwingine iwapo maelezo yametakiwa toka kwa wabunge juu ya ukaguzi unaoendelea.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Ni vizuri umma wa wakazi wa mkoa wa Dar es salaam  na watanzania kwa ujumla ukakumbuka kwamba maamuzi yote yaliyofanywa na Mstahiki Meya Didas Massaburi kuhusu kampuni ya UDA yanayotajwa kuridhiwa na vikao vya jiji ni batili kwa kuwa yalifanyika kwenye vikao visivyokuwa halali bila kuzingatia sheria, kanuni na maslahi ya wananchi wa Dar es salaam; bila ridhaa ya wabunge ambao ni Wajumbe wa Baraza la Halmashauri ya Jiji.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Maamuzi hayo yalifanyika bila kuheshimu maelekezo ya barua ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya tarehe 28 Februari 2011 yenye kumbu. Na CAB. 185/295/01/27 ambayo iliagiza kusitisha mara moja mchakato wa kuuza hisa ambazo hazijagawiwa barua ambayo nakala yake iliwasilishwa kwa mkurugenzi wa Jiji na Meneja Mkuu wa UDA pamoja na Wizara zingine zinazohusika.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Katika kufanya ukaguzi na uchunguzi ni muhimu kwa serikali kuzingatia  kwamba pamoja na udhaifu kwenye uongozi wa Jiji la Dar es salaam matatizo ya UDA yamechangiwa pia na Ofisi ya Msajili wa Hazina kutokuwa makini katika hatua zote kwa kushirikiana na CHC katika masuala ya ubinafsisaji wa UDA. Pia, CHC katika hatua ya sasa nayo ina udhaifu wa kushindwa kushughulikia masuala husika kutokana na migogoro ya kiutawala inayosababishwa pia na Waziri wa Fedha. Hivyo, pamoja na kutaka taarifa za taasisi husika ni muhimu Waziri Mkuu Pinda kutoa kauli kuhusu utekelezaji wa agizo alilolitoa bungeni kuhusu kashfa ya UDA.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Nahitaji kauli ya serikali kuhusu suala hili kama sehemu ya kutimiza wajibu wa kibunge wa uwakilishi na usimamizi ili kulinda mali za umma na pia kutetea maslahi ya wakazi wa Jimbo la Ubungo na Jiji la Dar es salaam kwa ujumla wanaohangaika na adha ya usafiri.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;29/12/2011.&lt;/div&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-118789818273320712?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/118789818273320712/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=118789818273320712' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/118789818273320712'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/118789818273320712'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/serikali-itoe-taarifa-uchunguzi-wa.html' title='Serikali itoe taarifa uchunguzi wa kashfa ya UDA'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-8627255391804476791</id><published>2011-12-28T00:10:00.001-08:00</published><updated>2011-12-28T07:33:37.463-08:00</updated><title type='text'>Serikali itake Israel waombe radhi; tukijiheshimu, tutaheshimiwa</title><content type='html'>&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa  ya CHADEMA  inaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa tamko juu ya kauli ya Waziri wa Ulinzi wa Israel ya kwamba nchi yetu si ya muhimu wala ya maana.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Waziri Barak alifanya mahojiano na Radio Israel na kutoa kauli ambayo imenukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari vya nchi hiyo wiki iliyopita kuwa “ Germany, France and England are not Tanzania, Mauritania or Tripolitania…..these are very important, very relevant countries and we don’t have an interest in increasing tensions with them or making them bitter enemies”.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kwa kauli hii serikali ya Israel inaiona Tanzania sio nchi ya muhimu wala ya maana hata kufikia hatua ya kuilinganisha na eneo tu ndani ya Libya linaloitwa Tripolitania.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Tunamtaka Waziri wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa, Benard Membe kuitaka serikali ya Israel kuomba radhi kufuatia kauli hiyo au kueleza wazi iwapo mazungumzo hayo ya Waziri Barak ni msimamo wa nchi hiyo kuhusu uhusiano wa kidiplomasia wa mataifa yetu.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Barua pekee ya balozi wa heshima wa Tanzania nchini Israel,  Kasbian Nuriel Chirich kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Avigdor Lieberman ya kulaani matamshi hayo ya Waziri Barak na kumkaribisha mwakilishi wa Israel kutembelea Tanzania haitoshi kuifanya serikali ya nchi hiyo kutambua athari za kidiplomasia za kauli iliyotolewa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Aidha kwa kuwa serikali imekuwa ikieleza kwamba Tanzania ina mahusiano mazuri ya kiulinzi na Israel, ni muhimu pia Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,  Dr Hussein Mwinyi akaeleza umma iwapo kauli hiyo ya Waziri Barak ndio msingi wa mahusiano yaliyopo kati ya nchi zetu kuhusu ulinzi na usalama.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa inachukua fursa hii kurudia kuwakumbusha watanzania kwamba kupuuzwa huku kwa nchi yetu katika medani ya kimataifa kunatokana na sera mbovu ya mambo ya nje chini ya utawala wa sasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Tanzania imepoteza heshima katika siasa za dunia kutokana na diplomasia yetu kujikita katika kuomba omba kimataifa; pamoja na kuwa kimaneno na maandishi serikali inazungumza kuhusu diplomasia ya kiuchumi, kivitendo mahusiano yetu yamejengeka katika misingi ya utegemezi, kupungua kwa urari wa kibiashara na kuachia mianya ya uporwaji wa rasilimali.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa inatambua kwamba wakati wa uongozi wa awamu ya kwanza wa hayati Mwalimu Julius Nyerere, Tanzania ilikuwa na heshima  na sauti kimataifa sio tu katika jitihada za ukombozi kusini mwa Afrika bali pia katika mahusiano ya kisiasa, kiuchumi na kijamii baina ya nchi za kusini na mataifa mengine duniani.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hali ya Tanzania kupoteza sauti katika medani ya kimataifa imedhihirika pia hivi karibuni katika mkutano kuhusu mabadiliko ya tabia nchi (COP 17) uliomalizika hivi karibuni nchini Afrika Kusini; wakati nchi yetu ikiwa ni miongoni mwa waathirika wakubwa zaidi wa mabadiliko ya tabia nchi. Iwapo hatua hazitachukuliwa kurejesha heshima na sauti ya Tanzania kimataifa maamuzi mengi yatafanyika yenye athari kwa wananchi wengi bila ushiriki wao thabiti kama yanayoendelea hivi sasa kuhusu Mikataba ya Kiuchumi na Nchi za Jumuia ya Ulaya (EPA) yenye madhara kwa wakulima na wenye viwanda nchini.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kurugenzi ya Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa inatoa mwito kwa watanzania kuendelea kuunganisha nguvu ya umma kusimamia uwajibikaji na  kufanya mabadiliko ya kimsingi ya kiuongozi, kisera na kimfumo  ya kitaifa ili kuweza kurejesha nafasi na heshima ya Tanzania kimataifa katika mazingira ya sasa ya ushindani wa kiuchumi, kiulinzi, kijamii na kisiasa.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Kauli ya Waziri Barak nimuendelezo tu wa mataifa mbalimbali kuifanya Tanzania na baadhi ya nchi nyingine za Afrika kuwa hazina heshima wala sauti katika siasa za kimataifa kama ambavyo Serikali za Uingereza na Marekani zimeweka masharti yenye mwelekeo wa ukoloni mamboleo kuhusu masuala ya ushoga na usagaji.&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Hatua za kupinga kauli za kudharauliwa na kulazimishwa mambo tusiyoyataka ziende  sambamba na kudhibiti mianya yote ya ufisadi wa kimataifa, uwekezaji uchwara  na kutetereka kwa misingi wa utawala wa kisheria masuala ambayo yanasababisha migogoro na pia rasilimali za nchi kutokutumika kwa manufaa ya wananchi walio wengi; tukijiheshimu, tutaheshimiwa.&amp;nbsp;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Wenu katika Demokrasia na Maendeleo,&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div style="text-align: justify;"&gt;Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Mahusiano ya Kimataifa (CHADEMA)&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-8627255391804476791?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/8627255391804476791/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=8627255391804476791' title='15 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8627255391804476791'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8627255391804476791'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/serikali-itake-israel-waombe-radhi.html' title='Serikali itake Israel waombe radhi; tukijiheshimu, tutaheshimiwa'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>15</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-2442114418936593191</id><published>2011-12-26T01:43:00.000-08:00</published><updated>2011-12-27T15:15:07.016-08:00</updated><title type='text'>Waraka wa Pili wa Mbunge kwa Wananchi wa Jimbo la Ubungo</title><content type='html'>&lt;a href="http://1.bp.blogspot.com/-x985TeGqNLY/TvhGkt9YLUI/AAAAAAAAAk8/2xPxFk3mfaE/s1600/MNYIKA.jpg"&gt;&lt;img alt="" border="0" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5690375725808889154" src="http://1.bp.blogspot.com/-x985TeGqNLY/TvhGkt9YLUI/AAAAAAAAAk8/2xPxFk3mfaE/s320/MNYIKA.jpg" style="cursor: hand; cursor: pointer; display: block; height: 320px; margin: 0px auto 10px; text-align: center; width: 234px;" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight: bold;"&gt;Uhuru na Kazi:&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;Nimekuja kuwatembelea kuona hali halisi ya uharibifu wa makazi yenu, mali zenu na miundombinu yetu kutokana na maafa ya maafuriko katika mitaa hii ya kata ya mabibo. Kuanzia maafa yatokee tarehe 20 Disemba mpaka tarehe 24 Disemba nimekuwa pamoja na wananchi wenzangu wa jimbo la Ubungo bega kwa bega katika jitihada za uokoaji na utoaji wa huduma za kijamii katika maeneo mbalimbali mathalani Msewe, Ubungo, Kisiwani, Kibo, Mburahati, Sinza D, Sinza E, Uzuri, Manzese Chakula Bora, Mburahati Kisiwani, Msigani, Mbezi Kibanda cha Mkaa, Kimara B. Na pia, nimeenda kutoa misaada kwa majimbo jirani ya Kinondoni (Magomeni Sunna na Kigogo), Kawe (Msasani Bonde la Mpunga na Bunju) na Ilala (Mchikichini). Kutokufika Mabibo, katika hizo siku chache, kunadhihirisha ukubwa wa maafa yenyewe na ilikuwa vigumu kuwepo mahali pote wakati wote. Hata hivyo, katika wakati huo wote nilikuwa na mawasiliano na wananchi na viongozi kuhakikisha kwamba mamlaka zinazohusika na uokoaji zinafika katika maeneo haya. Nawashukuru wote mliotoa ushirikiano wakati wa uokoaji na nawashukuru pia mliotoa msaada wa hali na mali kwa majirani zenu katika kipindi hiki kigumu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimekuja kwenu leo katika sikukuu ya kufungua zawadi (boxing day) kutoa michango yangu ya chakula na mavazi kwa waathirika wa maafa wasio na uwezo; hata hivyo zawadi yangu kubwa kwenu leo; sio vitu hivi tulivyotoa, ni waraka ninaoutoa kwenu wananchi wenzangu wa jimbo la Ubungo. Waraka huu naamini utakuwa ‘chakula’ cha fikra kwenu leo na kesho kwa ajili ya mabadiliko katika maisha yetu na taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika waraka wangu wa kwanza kwenu niliwapa mrejesho kuhusu uwakilishi wa Mbunge katika mkutano wa pili wa Bunge. Nawaandikia waraka huu “Uhuru na Mabadiliko” katika mwaka 2011 wa  kumbukumbu ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika ambayo sasa inaitwa Tanzania bara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lengo la waraka huu ni kuungana nanyi katika mwaka huu kutafakari kila mmoja wetu kuhusu taifa letu lilipotoka, lilipo na tunapotaka liende katika kipindi cha miaka 50 toka Uhuru na kutumia fursa hiyo pia kutafakari kuhusu jimbo letu katika kipindi cha mwaka mmoja toka uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na kuwatakia heri ya mwaka mpya wa 2012.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waraka huu wote, isipokuwa aya ya kwanza na aya hii ya tatu, niliuandika tarehe 9 Disemba 2011; hata hivyo sikuutoa siku hiyo kutokana na ‘macho na masikio’ ya wengi kuelekezwa katika ‘sherehe’ za siku hiyo pamoja na matarajio kuhusu hotuba ya Mkuu wa Nchi kugusa masuala mapana kuhusu mwelekeo wa taifa. Nimeona niutoe waraka huu katika kipindi cha kuelekea mwisho wa mwaka, na ni wakati muafaka wa kutafakari zaidi baada ya ‘sherehe’ kwa kuwa mpaka sasa Rais Jakaya Kikwete hajatoa hotuba nyingine ndefu kama alivyoahidi tarehe 9 Disemba na pia taifa linamaliza majonzi yaliyotokana na maafuriko yaliyoleta maafa katika mkoa wa Dar es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hali hii ni wakati muafaka wa kurudi nyuma na kutafakari kiwango cha fedha tulichotumia kwenye ‘sherehe’ za uhuru; huku taifa likiwa halina hata vifaa vya msingi vya uokoaji wakati wa maafa. Ni wakati muafaka wa kutafakari, ‘mafanikio’ ya miaka 50 ya uhuru, tukiwa na matatizo ya mipango miji na kutetereka kwa misingi ya utawala wa sheria katika mkoa wa Dar es Salaam ambao ulitangazwa kuwa jiji mwaka huo huo wa uhuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nashukuru kwamba waraka huu nautoa kwa mara ya kwanza hadharani kwenye kata ya Mabibo jirani kabisa na eneo la Loyola ambalo linabeba kumbukumbu ya kihistoria kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kwa Jimbo la Ubungo. Hivyo Nitatumia vile vile waraka huu na fursa hii kuwadokeza baadhi ya wajibu wa msingi ambao mbunge ameutekeleza katika Jimbo la Ubungo katika kipindi cha mwaka mmoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naelewa kwamba wapo wengine ambao walitumia mwaka huu wa 2011 wa maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru kufanya ‘sherehe’ ama kufanya ‘maonyesho ya kijeshi’, lakini binafsi nimeona pamoja na yote niwaandikie tutumie kutafakari. Ni wakati wa kila mmoja wetu kujiuliza ameifanyia nini nchi na pia kujiuliza nchi na wananchi wenzake wamemfanyia nini katika miaka 50 ya uhuru wetu. Tafakari hii haiwezi kuwa ya siku moja ya tarehe 9 Disemba bali ni mchakato endelevu wa kujimbua na kuchukua hatua. Tuna kila sababu ya kukumbuka na kuadhimisha siku ya uhuru, lakini hatuna sababu nyingi za kusherehekea tena kwa gharama kubwa tukilinganisha baina ya umri, rasilimali na mafanikio tuliyoyapata. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunaelezwa kwamba Tanganyika ilipata uhuru bila kupigana vita hivyo maonyesho ya kijeshi ni ishara tu ya kujipanga kwetu katika kulinda uhuru wa mipaka yetu; lakini ilipaswa sikukuu ya leo iwe ni ya kuonyesha matunda ya miaka 50 ya uhuru.&lt;br /&gt;Mwaka 1958 wakati Mwalimu Julius Nyerere akihutubia Umoja wa Mataifa (UN) kutaka Uhuru wa Tanganyika dhidi ya mkoloni alieleza kwamba tunapodai uhuru kutoka kwa Waingereza sio kwamba tunataka ili watupe tu utawala, bali ni kwa sababu wameshindwa kuondoa umaskini, wameshindwa kuelimisha Watanganyika na pia wameshindwa kutoa huduma za afya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tarehe 9 Disemba 1961 kupitia hotuba zake mbili kwa nyakati na matukio tofauti Nyerere akarudia kuwatangaza maadui watatu wa taifa- umaskini, ujinga na maradhi na akataka kila mmoja awapige vita. Siku hiyo hiyo, Nyerere akatangaza kuwa adui mkubwa ni umaskini!  Miaka michache baada ya uhuru akarejea kumtaja adui mwingine mkubwa zaidi ambaye aliwahi kumweleza hata wakati wa kudai uhuru; naye ni ufisadi. Kwa hiyo vita yetu kwa sasa ni ya maadui wanne; ufisadi, umaskini, ujinga na maradhi. Katika kutathmini tulipotoka, tulipo na kupanga tunapotaka kwenda ni muhimu tukawatazama maadui hawa miongoni mwetu wananchi na katika nchi yetu kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawashukuru tena kwa kunipa heshima ya kunituma kuwawakilisha na kuwatumikia kwa kadiri nilivyowaomba kupitia uchaguzi ili kuunganisha nguvu za pamoja katika masuala ya kitaifa bungeni lakini pia tukiweka mkazo katika utekelezaji wa ahadi jimboni kwa kuweka kipaumbele kwenye; Akili, Ajira, Miundombinu, Maji, Uwajibikaji, Usalama, Ardhi na Afya (AMUA). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi kazi tatu kuu za mbunge ambazo zinatokana na mamlaka ya bunge kwa mujibu wa ibara ya 63 ya katiba ni; Mosi kuwakilisha (representation) wananchi, pili ni kutunga sheria (legislative) na tatu ni kuisimamia serikali (oversight) kuweka mazingira bora ya maendeleo kwa mwananchi mmoja mmoja na nchi kwa ujumla. &lt;br /&gt;Kama sehemu ya uwakilishi na usimamizi mbunge ana wajibu pia wa kuunganisha nguvu ya umma jimboni kuhamasisha maendeleo kupitia mfuko wa maendeleo ya jimbo na wadau wengine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwishoni mwa mwaka tutatoa Jimboni Ubungo taarifa ya kina ya utekelezaji ya kata kwa kata lakini katika waraka huu nitaeleza baadhi katika muktadha wa kutafakari mabadiliko ya nchi yetu kiuchumi, kisiasa na kijamii miaka 50 baada ya Uhuru wa Tanganyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa uhuru taifa hili lilikuwa na watu chini ya milioni 10; sasa Dar es salaam pekee ina wananchi takribani milioni nne, karibu nusu ya Tanzania ya wakati huo ikiwa Tanganyika. Miaka 50 ya Uhuru sasa taifa lina watu wanaokaribia milioni 50; hivyo taifa letu watu wake zaidi ya robo tatu ni kizazi cha baada ya uhuru. Maanake katika kila watu kumi tunaopishana nao barabarani, zaidi ya saba ni kizazi cha baada ya uhuru. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuwa harakati za uhuru zilifanyika kona zote za nchi wakazi wa Jiji la Dar es salaam lenye umri wa miaka 50 tunabeba historia ya pekee ya harakati hizo ziliratibiwa kwa busara za wazee wenye imani kuwa vijana ni nguvu ya mabadiliko. Baadhi ya vijana hao kama Chifu Patrick Kunambi waliweka makazi yao katika Jimbo la Ubungo wakati huo kwa sehemu kubwa likiwa mapori. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazee wa Dar es salaam ndio waliomuita Mwalimu Nyerere toka Pugu, kwa mchango wao wa hali na mali, kijana wao, akawa mwenyekiti wa taifa wa chama cha wakati huo cha TANU akiwa na miaka 32, akaongoza harakati za uhuru, mpaka nchi ikapata uhuru. Akaongoza nchi hii vizuri katika miaka ya kwanza ya uhuru, akiweka misingi ya muda mrefu ya taifa yenye kutazama mbele kwa miaka mingi kiuchumi, kisiasa na kijamii; misingi ambayo wenzake wameitupilia mbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waraka huu ni kwa ajili ya wote wenye kuamini kwamba uhuru wa kweli, si uhuru wa bendera bali ni uhuru dhidi ya umasikini, ujinga, maradhi na ufisadi. Uhuru wa kweli, ni uhuru wenye kuleta maendeleo kisiasa, kijamii na kiuchumi. Uhuru huu ni wenye mabadiliko ya kweli, yenye kuhimili misukosuko ya ukoloni mamboleo; na kujenga taifa lenye kutumia vizuri rasilimali katika kutoa fursa kwa raia wake. Uhuru na Kazi, Uhuru na Mabadiliko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight: bold;"&gt;Uhuru na Mabadiliko ya Uchumi:&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;Katika kufakari tulipotoka, tulipo na tunapotaka uchumi wetu ufike miaka 50 baada ya uhuru tunapaswa kukumbuka kwamba dhamira ya kudai uhuru ilikuwa ni nchi kujitegemea kiuchumi na kuweka mazingira ya mabadiliko katika maisha ya wananchi kiuchumi. Katika hotuba zake mbili za tarehe 9 Disemba 1961, Nyerere alisisiza kwamba tukiweza kupambana na umaskini tutaweza kupata silaha ya kupambana na ujinga na maradhi. &lt;br /&gt;Katika kutimiza azma hiyo taifa lilihamasishwa kufanya kazi , kujitegemea na pia kutumia vizuri rasilimali za taifa. Katika kufanya hivi Nyerere alitambua ‘utajiri wa Tanganyika bado uko ardhini’ na kusisitiza ‘ni juu yetu tuijenge Tanganyika sisi wenyewe zaidi kwa kutumia utajiri tulionao na kwa juhudi zetu wenyewe’ . Miaka 50 ya uhuru tumeruhusu utajiri huo utoke ardhini lakini hatujaweza kuutumia vizuri kukuza uchumi wa nchi na kubadili maisha ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukitumia kipimo cha umaskini cha wastani wa pato kwa mwananchi, miaka michache baada ya uhuru wastani wa pato lilikuwa dola nne; lakini miaka 50 baada ya uhuru sehemu kubwa ya watanzania wanaishi chini ya dola moja kwa siku hali ambayo inaonyesha kuwa umaskini umeongezeka huku gharama za maisha zikizidi kupanda. Nyerere aliwahi kuhimiza kwamba maendeleo ya kweli ni ya watu sio ya vitu; hivyo miaka 50 baada ya uhuru vitu vinaweza kuwa vimeongezeka lakini ukilinganisha maisha ya watu taifa lina changamoto kubwa ya kushughulikia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kutekeleza wajibu wa uwakilishi na usimamizi nimefuatilia bungeni na jimboni kwa njia mbalimbali kuhusu kupanda kwa gharama za maisha kunakochangiwa na mfumuko wa bei pamoja kuporomoka kwa thamani ya shilingi. Jambo ambalo limenisukuma kutoa mwito kwa serikali kuandaa mpango wa dharura wa kunusuru uchumi na kupunguza gharama za maisha kwa wananchi. Hatimaye serikali imetoa kauli ya kuandaa mpango wa haraka wa kushughulikia suala hili. Nitaendelea kufuatilia kwa karibu ili mpango huu uwasilishwe bungeni na utekelezaji uanze. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba katika mkutano wa bunge la bajeti nilipinga ongezeko la kodi kwenye mafuta ya taa na kuwasilisha jedwali la marekebisho kwenye muswada wa Sheria ya Fedha ili kupunguza kodi ya petroli na dizeli kwa ajili ya kupunguza bei kwa mteja. Hata hivyo, uwingi wa wabunge wa CCM ulitumika kupinga mapendekezo haya ambayo nitaendelea na hatua ya kuyasukuma kufuatia pia maamuzi ya vikao vya juu vya chama hicho kuendana na misingi ya marekebisho niliyoyapendekeza awali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine, nitaendelea na hatua niliyoianza ya kuwakilisha bungeni muswada binafsi wa sheria kwa ajili ya kudhibiti bei ya bidhaa muhimu. Aidha, nitaendelea kushirikiana na wadau wengine wenye kutaka nchi iongeze uzalishaji kwa kupitia mpango maalumu kwa wazalishaji wadogo katika kilimo na viwanda ili kuchangia katika mauzo ya nje ya kuboresha urari wa biashara na wakati huo huo kupanua wigo wa ajira hususani kwa vijana. Kadhalika, nitaendelea kuunganisha nguvu na wote wanaotaka serikali ibane matumizi na kushughulikia ubadhirifu ili kuokoa uchumi na kupunguza athari za gharama za maisha kwa wananchi. Kupinga posho za vikao na kukataa aina zote za ufisadi ni sehemu ya kuchangia katika jitihada hizo kwa maendeleo ya wananchi wa Ubungo na taifa kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka ya mwanzo ya Uhuru nchi ilikuwa katika mkondo sahihi wa kiuchumi wa kuweka msukumo katika uzalishaji na manunuzi ya ndani. Kasoro pekee ya Nyerere lilikuwa ni kuweka mkazo sana kwa dola kwa maana ya serikali kumiliki njia za uzalishaji; badala ya uchumi kimilikiwa na umma. Kosa hili lilifanya serikali ishindwe kubeba mzigo mkubwa wa kusimamia sera kisiasa wakati huo huo kufanya utekelezaji kwa kuendesha njia za uzalishaji mali za kiuchumi wakati huo huo ikiwa inatoa huduma za kijamii. &lt;br /&gt;Kwa ujumla pamoja na kuimba haja ya kujitegemea, dola ikazalisha raia wategemezi kifikra, ambao chini ya mfumo wa chama kimoja na mwelekeo dhaifu wa kiuchumi; walipoteza ujasiri wote wa ushindani. Ni hali hii ndio ilifanya wengine kuanzisha vyama mbadala yenye kuamini katika mfumo wa soko la kijamii; lenye kuhakikisha kwamba uchumi unamilikiwa na wananchi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ni mfumo wa kiuongozi wa kisera na kirasilimali ambao unahakikisha kuwa rasilimali za nchi zinatumika kwa manufaa ya maisha ya wananchi wake; kwa kujenga taifa lenye kutoa fursa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini afadhali kosa la Nyerere linaweza kusameheka miaka 50 baada ya uhuru, lakini makosa ya warithi wake, baada ya kung’atuka kwake na baadaye kufa kwake yameacha majeraha makubwa yanayohitaji taifa hili likombolewe upya miaka mingi ijayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Awamu zilizofuata za utawala zikaruhusu kusukumwa fikra za kifisadi na utupu wa kiitikadi, kuindoa nchi katika ujamaa wa dola na kuitumbukiza katika soko holela badala ya soko la kijamii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chini ya sera dhaifu na ubinafsi wa viongozi wake, njia za uzalishaji mali zikauzwa kwa bei chee; toka kwa dola kwenda kwa wageni, na kwa tabaka la wachache linalojifunika kwa kivuli cha mabepari uchwara wa ndani; wengi wao wakiwa kwenye korido za chama tawala  na serikali yake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa Uhuru tarehe 9 Disemba 1961 pamoja na kuwa nchi ilikuwa na vyama vingi vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi katika hotuba zake zote mbili Mwalimu Nyerere alitambua umuhimu wa chama kilicho madarakani katika kuongoza nchi, na kueleza wajibu wa TANU baada ya uhuru. Ukitathmini miaka 50 baada ya uhuru utabaini kwamba miaka 50 baada ya Uhuru chama kilikabidhiwa wajibu huo cha CCM kimeutelekeza badala ya kuutekeleza jambo ambalo linapaswa kuunganisha watanzania wote bila kujali vyama kufanya mabadiliko ya kimfumo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mathalani miaka 50 baada ya uhuru, watanzania wanaendelea kupotoshwa kwamba Taifa letu linafuata siasa ya ujamaa na kujitegemea suala ambalo linatajwa pia katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni wazi chama kilichopo madarakani kinapotawala huku kikiwa na ombwe na kiitikadi na kufilisika kimaadili ni lazima taifa litakuwa na uongozi dhaifu na kuathirika kiuchumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kwa kweli si maneno yangu, ni ukweli uliosemwa na Muasisi wa TANU na CCM, mwandishi wa Azimio la Arusha, Hayati baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambaye aliandika katika kitabu cha Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania, namnukuu: “Halmashauri Kuu ya Taifa iliketi Unguja ikabadili Azimio la Arusha bila kwanza kutafuta maoni ya wananchi. Na walikuwa na haki ya kufanya hivyo, maana sera ni yao, ubaya wao ni kwamba jambo lenyewe walilifanya kwa hila na janja janja, na hadi sasa wanaendelea kuwadanganya wananchi kwamba sera ya CCM bado ni Ujamaa na Kujitegemea”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Udhaifu huo wa kifikra ukachanganyika na uozo wa kimaadili na kufanya miaka 50 baada ya uhuru tushuhudie viwanda vikiuzwa kwa bei ya kutupa na vingine kugeuzwa magofu baada ya kuuzwa kwake hali ambayo imechangia katika kuingia kwenye ukoloni mamboleo wa kiuchumi; wa kutegemea kuwa bidhaa za nje na kutegemea kusafirisha bidhaa ghafi kwenda nje ya nchi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jimboni Ubungo viwanda mbalimbali ambavyo vilianzishwa na Nyerere mara baada ya uhuru mathalani kiwanda cha Zana za Kilimo (UFI), Kiwanda ca Ubungo Maziwa, Kiwanda cha Nguo Urafiki na viwanda vingine vimeuzwa kinyemela na kubadilishwa matumizi ama kuanza kufilisiwa hali ambayo imeathiri uchumi wa nchi hususani kupunguza mapato ya serikali, kuongeza bidhaa za kutoka nje katika soko letu la ndani na pia kupunguza fursa za ajira. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara baada ya kuchaguliwa nimetembelea katika kiwanda cha Nguo cha Urafiki na kufanya mazungumzo na wafanyakazi na kubaini kwamba kiwanda kinazidi kudidimia; nyumba za wafanyakazi ziliuzwa kinyemela kwa kivuli cha ubinafsishaji, mpaka mitambo mingine imeuzwa kama chuma chakavu; pamoja na wafanyakazi kulipwa mishahara duni hata maghorofa ya wafanyakazi yanaendeshwa kibiashara badala ya kuwa huduma ya msingi kwa wafanyakazi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia hali hiyo katika kipindi cha mwaka mmoja nimefanya kazi ya uwakilishi na usimamizi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa njia mbalimbali za kibunge na mawasiliano na serikali. Suala la malipo pungufu ya wafanyakazi kufuatia likizo ya lazima kutokana na ukosefu wa pamba nililifuatilia na hatimaye wakapata nyongeza. Kufuatia hatua hizo, kamati ya bunge ya viwanda na biashara nayo imetembelea kiwanda na kuthibitisha masuala ambayo tumeyasema bungeni wakati wa bunge la bajeti na kamati hiyo imetangaza kuunda kamati ndogo kwa ajili ya kufanya uchunguzi zaidi na kuisimamia serikali kuchukua hatua zaidi. Aidha, nitaendelea kuifuatilia serikali kuchukua hatua husususani kupitia Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) pamoja na Wizara zote husika kuhusu viwanda vilivyopo Jimboni Ubungo vilivyobinafishwa kiholela ili kushughulikia matatizo ya muda mrefu ya wafanyakazi, kupanua wigo wa ajira hususani kwa vijana na kuongeza uzalishaji wa bidhaa na mapato kwa serikali.&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru viwanda vyetu vinaendelea kufa huku tukilazimishwa kisera kujibidiisha kuwa watafutaji wa malighafi na kuzisafirisha kwenda viwanda vya nje zikiwa ghafi na hivyo kushindwa kuwa na uwiano wa kimalipo (Balance of Payment). Wakati tukiua viwanda vya ndani na kupunguza uzalishaji; tunafungua mipaka yetu kwa kiwango cha ajabu na kuingiza bidhaa za nje zikiwemo zisizokuwa na kiwango. Taratibu tunajenga uchumi wa kuwa wachuuzi wa bidhaa kutoka nje. Huo sio uhuru wa kiuchumi ambao waasisi wa taifa hili waliupigania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumehadithiwa na wazee wetu, kwamba wakoloni walitutawala ili kupata nguvu kazi ya bei chee; kupata malighafi kwa ajili ya viwanda vyao na kupata masoko kwa ajili ya bidhaa zao. Tulipotafuta uhuru, ilikuwa ni dhamira yetu kuondoa udhalili huu. Hali imeanza kurejea kwa ari, nguvu na kasi zaidi na kutia doa katika sherehe za miaka 50 ya Uhuru. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukoloni mamboleo ndani ya taifa lenye uhuru wa bendera; ndio unaofanya wafanyakazi kutoa nguvu kazi yao kwa bei chee kwa kulipwa mishahara midogo na kupata maslahi duni hususani katika makampuni makubwa ya kigeni ukilinganisha na wafanyakazi toka nje. Sasa utumwa huo unabisha hodi kwa wakulima, kupitia mikakati mipya ya kilimo inayoendelezwa hivi sasa yenye kupokonya ardhi (land grabbing) kwa watanzania wa kawaida kwa kisingizio cha kupanua mashamba kumbe mwishowe watanzania watakuja kuwa manamba. Kumiliki ardhi ni ishara kuu ya uhuru wa wananchi, hivyo tunapokwenda tunapaswa kurekebisha hali hii kwa haraka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa Jimboni Ubungo katika kipindi cha mwaka mmoja nimefanya kazi ya uwakilishi katika masuala yanayohusu migogoro na usimamizi wa ardhi kwa ujumla. Nimekuwa sambamba na wananchi wanaodai fidia ya ardhi zao ama wenye migogoro mbalimbali ya ardhi kwa kuwasilisha masuala yao kwenye mamlaka husika na wengine kuwawezesha kupata ushauri wa kisheria. Pamoja jitihada hizo bado migogoro ya ardhi katika kata za pembezoni ni mingi suala ambalo linahitaji kutazamwa kwa ukaribu zaidi. Nimeongeza nguvu zaidi katika kutaka viwanja vya umma vilivyovamiwa viweze kurejeshwa kupitia bungeni na kwenye manispaa kwa kutaka ripoti ya uchunguzi juu ya maeneo hayo iwekwe hadharani na hatua zichukuliwe. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na jitihada hizo tayari baadhi ya masuala yaliyofanywa siri awali ya ripoti hizo yamejadiliwa na baraza la madiwani na pia baadhi ya viwanja hivyo tayari vimewekewa mabango ya ilani kuonyesha kwamba ni maeneo yaliyovamiwa. Sasa hatua madhubuti zinazopaswa kuchukuliwa ni kuhakikisha viwanja hivyo vinarejeshwa na hatua stahiki zinachukuliwa kwa wahusika ili kuweka misingi ya uwajibikaji ya kulinda rasilimali za umma. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matumizi bora ya ardhi yanahitaji kuweka mkazo katika mipango miji pamoja na kuongeza kasi ya upimaji wa maeneo na utoaji wa hati za viwanja hali ambayo itawezesha pia kutoa fursa kwa wananchi kuweza kuzitumia nyaraka hizo kwa ajili ya kujiendeleza kiuchumi na kuongeza thamani ya mali zao. Kwa hali ilivyo sasa jiji la Dar es salaam lina maeneo mengi hatarishi katika mabonde, kingo za mito, karibu na mitambo na viwanda na kwa ujumla katika sehemu zisizopimwa. Hali hii inafanya jiji lisiwe salama panapotokea hatari ya moto, maafuriko na majanga ya aina nyingine. Tumefika hapa tulipo kutokana na udhaifu katika mipango miji na kutokusimamiwa kwa utawala wa sheria. Katika mwaka 2012 na kuendelea lazima tusukume utamaduni wa uwajibikaji. Ni muhimu maeneo yote hatarishi yakatambuliwa na serikali ikaweka utaratibu wa kuyakinga maeneo husika dhidi ya majanga na kwa maeneo ambayo ni vigumu kuyakinga kwa ujenzi wa miundombinu serikali ihakikishe wananchi husika wanakwenda kwenye makazi mbadala. Hatua hii ni muhimu sana katika wakati huu ambao jiji la Dar es salaam kama ilivyo nchi kwa ujumla inapaswa kubadilika kimipango katika kukabiliana pia na athari za mabadiliko ya tabia nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na kupungua kwa ajira katika viwanda na aina nyingine za uzalishaji, wapo wananchi ambao wamejiajiri katika kufanya biashara katika ngazi mbalimbali. Hata hivyo, kundi la wafanyabiashara ndogo ndogo hawana uhuru wa kufanya biashara kutokana na kukosa maeneo mazuri ya kufanyia biashara zao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha mwaka mmoja nimefanya kazi ya kuwawakilisha watengewe maeneo maalum ya biashara na kuwatetea wasihamishwe kwenye maeneo wanayofanyia biashara hivi sasa mpaka watakapotengewa maeneo muafaka ya kufanyia biashara zao. Tumefanikiwa kwa manispaa kutenga baadhi ya maeneo lakini kwa kuwa hayajitoshelezi nimewasilisha pendekezo kwa serikali bungeni kutenga kutoka maeneo ya viwanda yaliyotekelezwa ili tupate eneo la viwanda vidogo pamoja na biashara kupanua wigo wa ajira kwa wanawake na vijana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala la kuweka mkazo kwa wazalishaji wadogo nililipa mkazo pia wakati nikitimiza wajibu wa kibunge wa kutunga sheria kupitia marekebisho ya Sheria ya Maeneo Maalum ya kiuchumi na biashara sanjari na kutaka viwanda vinavyowekeza katika maeneo hayo kuanza kulipa kodi mapema zaidi na kupanua wigo wa ajira.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiondoa ongezeko la ujenzi wa barabara kuu miaka 50 baada ya Uhuru; miundombinu mingine imeachwa hohehahe. Hali ya usafiri wa reli inazidi kuwa mbaya usafirishaji wa abiria na mizigo kwa njia hii unazidi kupungua mwaka hadi mwaka. Serikali inazidi kuingiza fedha za walipa kodi katika uwekezaji wa kibadhirifu na kudhoofisha miundombinu iliyojengwa kwa jasho la umma katika Shirika la Reli (TRL). Nashukuru kwamba wabunge tuliungana pamoja bungeni miaka 50 ya Uhuru kutaka nyongeza ya fedha katika bajeti ya miundombinu; hata hivyo ongezeko hili halitakuwa na tija iwapo hatua stahiki dhidi ya ufisadi katika sekta husika. Katika nyongeza ya bajeti ya miundombinu, pamoja na masuala mengine ya kitaifa nilisisitiza umuhimu wa reli ya kutoka Ubungo mpaka Stesheni kuanza kufanya kazi kwa ajili ya kubeba abiria kama sehemu ya kupunguza msongamano na serikali imekubali kulipa kipaumbele suala hilo.&lt;br /&gt;Mikakati mipana ya kukabiliana na foleni bado inasuasua kwa kuwa katika mwaka wa fedha 2011/2012 fedha kidogo takribani bilioni tano pekee ndizo zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara za pembezeno za kupunguza foleni ambazo zingepunguza kiwango kiwango cha magari katika barabara ya Morogoro. Shughuli pekee ambayo imekamilika baada ya kuipa msukumo ni ujenzi wa daraja la Msewe ambalo limeanza kupunguza foleni kupitia barabara ya Chuo Kikuu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha muda mfupi ni lazima kuweka mkazo zaidi katika ujenzi wa barabara hizo za mzunguko (ring roads) kwa kiwango cha lami na Mfumo wa Usafiri wa Umma (DART). Kabla ya miradi mingine ya muda wa kati kama upanuzi wa barabara ya Morogoro na ujenzi wa njia za mpishano (fly over). Hata hivyo, mikakati yote hii haitawezesha suluhisho endelevu iwapo mipango miji ya Dar es salaam haitazingatia mwelekeo wa muda wa jiji lenyewe na hata taifa kutokana na kasi ya ongezeko la watu hususani kutoka vijijini. Katika kipindi cha mwaka mmoja kama sehemu ya uwakilishi na usimamizi nimehoji kuhusu Mpango Kabambe wa Jiji (Master Plan) na nitaendelea kufuatilia kwa karibu ili tupate msingi wa kuchukua hatua zaidi miaka 50 baada ya uhuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha katika kuwezesha hatua za muda mfupi, Mfuko wa Maendeleo wa Jimbo la Ubungo umeweza kutenga fedha za ukarabati wa baadhi ya barabara za mtaani pamoja na ujenzi wa madaraja ya watembea kwa miguu. Pia, manispaa imeweza kushawishiwa kutenga fedha kwenye bajeti 2011/2012 kuweza kutenga fedha zaidi za ujenzi wa madara katika kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru hali ya viwanja vyetu vya ndege na shirika la umma la ndege (ATCL) ni ya kuliaibisha. Taifa limeingia katika kugharamia shirika hili kwa maamuzi mabovu katika vipindi tofauti tofauti. Serikali imeshindwa kufanya upanuzi wa Bandari kubwa kwa wakati; badala yake wameingia mikataba mibovu ya upakuzi wa mizigo inayopelekea kupunguza hata kiasi cha shehena kinachohudumiwa katika bandari zetu. Wakati washindani wetu nchi za jirani; wanapanua bandari zao na kuwekeza katika miundombinu, sisi ambao tuko katika nafasi bora zaidi ya bandari zetu kupata soko kubwa la nchi za maziwa makuu tunabaki tumetahayari kutokana na sera legelege na uongozi mbovu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa kudai uhuru, ni vijana makuli wa pale bandarini ndio Dar es salaam waliokuwa mstari wa mbele kwenye kudai uhuru; hawakuigopa serikali dhalimu ya kikoloni kwa kuwa hawakuwa na cha kupoteza kama wenye kazi za kola nyeupe(white collar) waliokuwa kwenye serikali ya mkoloni. Ndio maana huwa nafarijika kila ninapoona vijana wasio na ajira na watanzania wa kawaida kwa ujumla wanapoendelea kuunga mkno mabadiliko ya kweli ili kupata uhuru wa kweli. Tabaka hili, halina cha kupoteza isipokuwa umasikini wao na malipo watakayopata ni kuishi kwenye taifa lenye kutoa fursa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika tumeendelea kuwa na upungufu wa umeme hali ambayo imeathiri uchumi kwa kupunguza uzalishaji na kuongeza gharama za maisha. Hali hii imetokana na utegemezi wa kiwango kikubwa wa vyanzo vya umeme wa maji vilivyoanzishwa wakati wa serikali ya awamu ya kwanza na kukithiri kwa ufisadi katika ununuzi na mikataba ya umeme wa dharura kwenye awamu zilizofuata za utawala.&lt;br /&gt;Katika kipindi cha mwaka mmoja nimeungana na wengine kuisimamia serikali kuwasilisha bungeni mpango wa dharura wa umeme. Pamoja na mpango husika kuwasilishwa nimeendelea kupinga gharama kubwa kwa mikopo ya kibiashara na utekelezaji wa kusuasua wa mpango wa dharura wa umeme. Hatua hii imeenda sambamba na kushawishi kufikishwa kwa umeme katika baadhi ya maeneo ya jimbo ambayo hayakuwa na umeme kabla. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala ya ‘sherehe’ za uhuru zenye kugharimu zaidi ya bilioni 50;  nilitarajia kwamba siku hiyo ingetumika kuzindua mitambo mipya ya umeme ya kununua sio ya kukodi ili kuacha alama ya kudumu miaka 50 baada ya uhuru. Kutokana na takribani MW 250 ambazo zilikuwa ziwe zimepatikana kati ya Septemba mpaka Disemba 2011 kutopatikana mpaka hivi sasa nitaendelea kuchukua hatua kuisimamia serikali kutekeleza ahadi ya kuondoa tatizo la mgawo wa umeme. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, nitaendelea kuwawakilisha wananchi kupinga ongezeko la bei ya umeme la wastani wa asilimia 185 na badala yake kuitaka serikali kuwa na mpango wa kulinusuru Shirika la Umeme (TANESCO) dhidi ya gharama kubwa zinazotokana na mitambo ya kukodi, ufisadi kwenye mikataba , madeni ya serikali na kuhakikisha gharama zinabebwa zaidi na watumiaji wakubwa badala ya watumiaji wadogo wa kipato cha chini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru serikali inajivunia kuboresha miundombinu kwa kutumia takwimu za kuongezeka kwa idadi ya wanaotumia simu za mkononi. Lakini ukitafakari kwa undani ukuaji wa sekta hii utabaini kwamba umetokana na  nguvu ya sekta yenyewe kwa sababu za nje ya sera za serikali na hivyo kufanya mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa taifa na hata kubadili kipato cha watanzania mmoja mmoja mwenye simu kuwa ni finyu. Tathmini ya hivi karibuni katika maeneo mbalimbali ya nchi inaonyesha kwamba katika kila watanzania kumi (10) wenye simu, ni watanzania wawili (2) ndio wanatumia simu zao kwa matumizi binafsi na biashara; hivyo asilimia kubwa ya watanzania watumia simu kwa matumizi binafsi pekee na si biashara ama shughuli za uzalishaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru tunakabiliwa na athari ya kiuchumi ya utegemezi ambao taifa letu limeingizwa kwa kutegemea misaada kutoka nje huku rasilimali za taifa zikifyozwa kibeberu. Hali hii inatuhitaji kwa pamoja tufanye mabadiliko tuwe na uhuru wa kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanafalsafa Frantz Fanon aliwahi kusema kwamba kila kizazi lazima nje ya uvungu uvungu kiutambue utume wake; ama kiutumize au kiusaliti. Kizazi cha wakati huo, kilidai uhuru, na kujenga misingi ya taifa (national building) ingawa misingi hiyo imekuja kuvurugwa na kutuingiza katika ukoloni mambo leo (neo colonialism). Ni wajibu wa kizazi chetu; kudai uhuru wa kweli, uhuru dhidi ya umasikini, ujinga, maradhi; hatuwezi kudai uhuru huo bila kumpiga vita adui ufisadi. Wajibu wa kizazi chetu ni kuweza kupambana katika mazingira ya ushindani wa ndani na nje ya nchi yetu; kujenga taifa tukitazama kizazi chetu na kijacho. Mabadiliko haya tuyafanye katika maeneo mbalimbali ya nchi yenye rasilimali ambayo yameporwa; iwe ni maeneo ya migodi, maeneo ya uwindaji, maeneo ya uwekezaji katika kilimo cha mashamba makubwa. &lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru naiona laana ya rasilimali (resource curse) kuwa ni moja ya visababishi vya kuvunjika kwa amani nchini. Tunaelekea kwenda kuchimba mafuta na madini ya urani; nchi hii iko mashakani kama hatutafanya mabadiliko kimfumo na kiuongozi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kuchangia mabadiliko kwenye sekta za nishati na madini kwa nafasi ya uwaziri kivuli tarehe 15 Julai 2011 niliwasilisha bajeti mbadala bungeni ambayo baadhi ya mapendekezo yake serikali imeanza kuyafanyia kazi. Hata hivyo, sehemu kubwa ya kasoro bado serikali haijachukua hatua hivyo tunapokwenda tutaongeza nguvu zaidi katika kuhakikisha usimamizi thabiti wa sekta hii ambayo ni mtaji kwa taifa.&lt;br /&gt;Katika kutimiza wajibu wa kibunge wa usimamizi na kutunga sheria zenye kuhakikisha mabadiliko ya kiuchumi nilikuwa mstari wa mbele katika kufanya marekebisho katika Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2011 ili kuweza kuongeza ufanisi na kudhibiti mianya ya ufisadi katika ununuzi wa umma kwenye serikali kuu, taasisi zake na katika serikali za mitaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight: bold;"&gt;Uhuru na Mabadiliko ya Jamii&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;Nchi hii imewekwa rehani kijamii; ndoto ya waasisi wa taifa hili la kujenga taifa lenye uhuru na umoja inaanza kufifishwa. Baadhi ya viongozi katika utawala wanatembea kifua mbele wakizusha mijadala ya ukabila na udini yenye kuligawa taifa. Katika hotuba zake mbili za tarehe 9 Disemba 1961 Nyerere alitabiri hali hii kwa kueleza kwamba msingi wa kufanikiwa kwa TANU ulikuwa ni umoja wake na kwamba wanachama wake wakigombana na kutengana mambo yao na mambo ya taifa zima yatakwenda tenge. Umoja kati CCM ya sasa na ndani ya Serikali umetoweka; chama legelege kimezaa serikali legelege.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 ya uhuru chini ya sera mbovu na utawala dhaifu matabaka yanazidi kumea katika taifa, pengo kati ya masikini na matajiri linaongezeka kila kukicha. Uchambuzi unaonyesha kwamba watanzania wameanza kupoteza matumaini ya kuwa na maisha bora; katika kila watanzania kumi, saba wamesema kwamba hali yao ya maisha haijawa bora. Na kati yao; asilimia hamsini hali yao imekuwa mbaya zaidi. Nyufa hizi ni tishio kwa mustakabali mwema wa taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru, huduma za kijamii zinazidi kudorora; kwa kiwango cha huduma hizo na hata upatikanaji hususani kwa watanzania masikini. Elimu ni sehemu ya uhuru wa kweli kwa vijana; kwa Tanzania ya leo mfumo mzima wa elimu ujenga matabaka. Katika kipindi cha mwaka mmoja wa utumishi wa umma nimetembelea shule za kata mbalimbali za jimbo la Ubungo na kubaini matabaka kuanzia chekechea mpaka sekondari; baina ya shule binafsi na za umma, utofauti wa mazingira ya kusomea na maslahi ya walimu ni kubwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilichobaini ni kwamba ruzuku ya bajeti ya elimu kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari (capitation grant) kwa kiwango cha kutosha na hata inayofika haifiki kwa wakati na pia hakuna uthibiti makini wa matumizi. Hili ni eneo ambalo nitalipa uzito wa pekee tuendako. Pamoja na kuongezeka kwa idadi ya madarasa katika shule za umma, bado kuna tatizo la ubora wa madarasa yenyewe yaliyojengwa kwa ukilinganisha na kiwango cha fedha za michango ya wananchi zilizotumika. Kwa kushirikiana na madiwani tumesimamia na kubaini ujenzi wa madarasa hewa na pia kiwango duni cha majengo ya kipindi kilichopita ikiwemo vyoo katika mashule na hatua mbalimbali zimeanza kuchukuliwa ikiwemo baadhi ya wakandarasi kulazimishwa kukamilisha kazi husika.&lt;br /&gt;Pia, baada ya kubaini hali hiyo tumejadiliana na madiwani kuweza kuwa na kampeni maalum ya kumaliza tatizo la madawati katika shule za msingi na sekondari katika jimbo na manispaa kwa ujumla. Kwa kushirikiana na meya maamuzi yalifanyika ya kuchukua fedha kutoka mafungu mengine ya halmashauri kwa ajili ya kutengeneza madawati kwa wingi na kusambaza katika shule mbalimbali. Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo la Ubungo nao umetoa sehemu ya madawati. Madawati hayo yameanza kusambazwa kwa awamu katika shule mbalimbali. Orodha ya madawati kwa shule zilizopatiwa itatolewa katika taarifa ya utendaji kwa kila kata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa elimu ya juu; vijana wa vyuo vikuu ni wajibu wao kuwa mstari mbele kuendelea kuunga mkono mabadiliko, kwani ni mashuhuda wa namna ambavyo serikali inavyofanya matumizi ya anasa, fedha za umma zikipotea kwa ufisadi. Hatima ya yote mzigo unarudi kwa mwanafunzi na wazazi wake kupitia sera za uchangiaji ambao wengine imewanyima fursa ya kusoma. Katika kipindi cha mwaka mmoja, nimefanya kazi ya kuwakilisha masuala mbalimbali ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa ajili ya kupata majibu ya serikali bungeni. Hata hivyo, majibu hayo pamoja na kuweza kutatua baadhi ya matatizo hayo hayajaweza kutoa suluhisho la kudumu hali ambayo imefanya migomo ya kudai haki miongoni mwa wanachuo ikiwemo wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuendelea. &lt;br /&gt;Pia, kuna udhaifu mkubwa katika mfumo wa bodi ya mikopo kwa kiwango ambacho wapo wanafunzi ambao katika mazingira ya kawaida wangepewa kipaumbele katika mikopo lakini hawajapata mikopo. Hivyo, tofauti na ahadi ya Rais kwamba hakuna mtoto wa maskini atayeshindwa kusoma kutokana na kukosa mikopo wapo watoto wa maskini ambao wameshindwa kuendelea na masoko. Tumeweza kuchangia baadhi yao kupitia Mfuko wa Elimu Ubungo unaochangiwa asilimia 20% ya mshahara wa mbunge kwa mwezi lakini maombi na mahitaji ni mengi zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii iko hivi wakati ambapo toka Januari mpaka Disemba 2011 kwa ajili ya ‘sherehe’ za uhuru serikali ikiwa imetumia fedha ambazo zingeweza kulipia mikopo wanachuo zaidi ya elfu hamsini na kubaki. Fedha hizi zimetumiwa kuanzia kwenye maonyesho ya Wizara na Taasisi zake huku matumizi yakijirudia rudia wakati wa maonyesho ya kila Wizara pekee, wakati wa Saba Saba na wakati wa maonyesho maalumu ya mwezi Desemba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapokwenda nitaendelea kuwakilisha na kuwasilisha masuala ya wanafunzi wa elimu ya juu ikiwemo kutaka ripoti ya tume ya Rais kuhusu mikopo iwekwe wazi hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kuboresha mfumo wa ugharamiaji wa elimu ya juu. Aidha, mwaka 2012 nitaunganisha nguvu ya wadau wengine ili kupanua wigo na ufanisi wa mfuko wa elimu Ubungo ili kuwa na uwezo wa kunufaisha wanafunzi wengi zaidi wa msingi, sekondari, vyuo pamoja na elimu ya mtaani kwa vijana na wanawake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kipindi cha miaka 50 katika Jiji la Dar es salaam uwezo wa kupata maji kutoka makampuni na taasisi za umma ambazo zimekuwa zikibadilika majina katika nyakati mbalimbali toka uhuru unapungua badala kuongezeka. Maelezo yanayotolewa ni kwamba kuna upotevu wa maji kutokana na mitambo michakavu kwa kuwa imejengwa mara baada ya uhuru na kwamba kasi ya ongezeko la watu hailingani na kiwango cha upanuzi wa miundombinu ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa maji. Ikiwa hali hii ipo katika jiji la Dar es salaam itachukua miaka mingapi ya uhuru kuweza kuhakikisha kila mtanzania anapata maji safi na salama na pia miundombinu ya maji taka inakuwepo katika miji yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili kuchangia kupata ufumbuzi mwezi Januari 2011 niliwaita pamoja wadau katika Kongamano la Maji Jimbo la Ubungo na maazimio ya kongamanao hilo ulikuwa msingi wa ufuatiliaji jimboni, bungeni na kwenye mamlaka mbalimbali kwa kipindi cha mwaka mmoja. Baada ya kuona utendaji kazi wa mamlaka husika una sua sua ilinibidi kama sehemu ya uwakilishi na usimamizi niunganishe nguvu ya umma kuweza kwenda Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) kuweza kupata majibu ya msingi ya hatua ambazo zimechukuliwa. Matokeo ya jitihada zote ni kufanyika kwa operesheni maalum ya kushughulikia biashara haramu ya maji pamoja na kuongeza mgawo wa maji ambayo imesaidia baadhi ya maeneo ambayo awali yalikuwa hayapati maji na sasa yanapata kwa vipindi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, yapo maeneo ambayo mpaka sasa hayajaweza kupata maji hivyo jitihada zaidi zinahitajika katika mwaka 2012; ikiwemo kukabiliana na ufisadi katika sekta ya maji, Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) kuongeza kasi katika uwekezaji kwenye uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa maji na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kuweza kudhibiti bei za maji. Katika kipindi husika tumefanya vile vile ufuatiliaji na kubaini udhaifu mkubwa zaidi katika usimamizi wa miradi ya maji ya jumuia hali ambayo imefanya wananchi kukosa maji; kama sehemu ya uwakilishi nimezisimamia mamlaka husika katika Manispaa kuchunguza miradi hiyo na hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa katika kata husika. Kwa upande mwingine miradi ya washirika wengine kwenye kata ambayo ilikwama kwa miaka mingi ya uchimbaji wa visima virefu na usambazaji wa mabomba ya maji imesimamiwa na iko kwenye hatua za mwisho za kuanza kufanya kazi katika kata mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 ya uhuru wananchi wanapoteza kwa wingi maisha yao kwa wingi kwa magonjwa yanayoweza kutibika kama malaria. Pamoja na sera ya uchangiaji kuwa mzigo wa watanzania walio wengi bado vifaa na madawa havipatikani hususani katika hospitali na zahanati za umma. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Familia za maskini ambazo zimepoteza wanawake wajawazito au watoto wakati wa kujifungua kutokana ubovu wa huduma za afya wanaweza kuelezea vizuri zaidi hali ya sekta ya afya nchini. Jitihada za Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo la Ubungo kujenga kituo cha Afya ya Mama na mtoto Jimboni ni sehemu tu ya mfano kwa serikali kuchukua hatua zaidi kuweka mazingira bora zaidi kwa wakina mama na watoto katika zahanati na vituo vya afya kwa kila kata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, baadhi ya athari za kiafya zimekuwa zikichangiwa na matatizo katika uchafuzi wa mazingira. Kwa upande mmoja kumekuwa na uchafuzi wa mazingira kutokana na udhaifu katika mfumo mzima wa maji taka katika jiji la Dar es salaam lakini kwa upande mwingine kutokana na uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na viwanda. Katika kipindi cha mwaka mmoja, niliweka mkazo katika uchafuzi wa mazingira unaotokana na utiririshaji wa maji taka toka kwenye Hosteli za Chuo Kikuu eneo la Mabibo kwenda kwenye Mto Kisiwani pamoja na uchafu katika mabwawa ya maji taka eneo la Mabibo. Nimetembelea maeneo husika na nimezisukuma mamlaka husika kuchukua hatua kwa nyakati na njia mbalimbali. Hatua hizo zimeweza kupunguza ukubwa wa matatizo kwa muda, hata hivyo katika mwaka 2012 nitaendelea kuzifuatilia mamlaka husika ili kuweza kuwa na suluhisho la kudumu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine, matatizo ya afya mazingira yameendelea kushamiri kutokana na kukithiri kwa uchafu katika jiji la Dar es salaam. Matatizo hayo yanachangiwa na udhaifu katika mfumo mzima wa uzoaji, ukusanyaji, usafirishaji, uhifadhi na utumiaji wa takataka. Mfumo mpya wa Manispaa kujitoa katika uzoaji wa moja kwa moja wa taka katika maeneo mengi na badala yake kubaki na jukumu la uratibu bila kufanya maandalizi ya kutosha kwa serikali za mitaa na wananchi wa maeneo husika umesababisha migogoro na uchafu katika maeneo mengi. Kutokana na hali hii, nilitoa pendekezo la tathmini kuweza kufanyika kwa mfumo mzima na hatua mbadala kuchukuliwa. Kufuatia pendekezo hilo manispaa ya Kinondoni tayari imekutana na wenyeviti na watendaji wa mitaa kufanya tathmini husika; hata hivyo, bado hatua za ziada zinahitajika katika mwaka 2012 kuweza kupunguza matatizo ya uchafu hatua ambazo zinapaswa pia kuhusisha kuongeza vifaa na kuboresha mfumo mzima ikiwemo wa ushirikishwaji wa wananchi. Kwa upande mwingine, kuna matatizo ya gharama kubwa ya uzoaji taka kutokana na umbali wa usafirishaji wa taka na pia changamoto katika madampo mbalimbali. Ili kupunguza matatizo haya, ni muhimu katika mwaka 2012 kuongeza kasi ya kuwa na dampo mbadala kwa ajili ya Manispaa ya Kinondoni ili liweze pia kuhudumia kata mbalimbali za jimbo la Ubungo kwa ukaribu zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ujumla huduma za kijamii iwe ni elimu, afya au maji zimegeuzwa kuwa bidhaa za ghali na adimu. Ni muhimu kuwa na mfumo wa uchumi wa jamii ya kwamba hata katika soko ni lazima kwa taifa kuwa na mifumo ya ulinzi wa kijamii (social security) inayogusa makundi mbalimbali katika maeneo mbalimbali ya huduma za kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru ahadi za kutoa fursa pana kwa makundi maalum mathalani wanawake, wazee, vijana na wenye ulemavu kuweza kujiendeleza zimekuwa ni maneno matupu bila vitendo. Sera zinazotekelezwa zinayatazama makundi haya kama watu tunaohitaji kusaidiwa badala ya kuwa wadau wa msingi wa kimaendeleo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kutambua hali hii katika michango yangu bungeni niliweka mkazo wa pekee katika masuala ya wanawake ikiwemo yanayohusu Benki ya Wanawake na kutaka pia pawepo na Benki ya Vijana wazo ambalo serikali imelikubali. Hata hivyo, uwepo wa benki hizi unapaswa uongezewe nguvu kwa mabadiliko ya kimfumo na kiutaratibu katika taasisi mbalimbali za fedha kuweza kupanua wigo kwa makundi haya ya kijamii kujikwamua kiuchumi na kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wangu, katika kipindi cha mwaka mmoja nimeendelea kushirikiana na wanawake na vijana katika kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo jimboni. Kutokana na hali hii pamoja na michango toka fedha binafsi za mbunge kwa ajili ya vikundi mbalimbali vya vijana na wanawake nimeweza kutenga fedha toka kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo kwa ajili ya Muungano wa VICOBA 100 vya Jimbo la Ubungo kwa ajili ya kukopeshana. Aidha, nimedhamini mashindano mbalimbali ya michezo kwa wanawake na kwa vijana katika maadhimisho mbalimbali jimboni Ubungo. Hatua hizi zote hazijitoshelezi ukilinganisha na idadi ya wanawake na vijana jimboni pamoja na ukubwa wa matatizo ya ukosefu wa ajira na fursa za kujiendeleza miongoni mwa wanawake na vijana jimboni hivyo katika mwaka 2012 nitaweka mkazo maalumu kwa ajili ya mabadiliko ya kimfumo lakini pia katika kuunganisha nguvu za wadau wengine zaidi ili kuchangia katika maendeleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapokwenda tuweke pia mipango ya kuhakikisha badala ya wazee wetu kuonekana kuwa kundi linalopaswa tu kubebwa na kuhudumiwa, sera mbadala zitaboresha kiwango na mifumo ya malipo ya wastaafu na kupanua wigo wa mifuko ya kijamii kujumuisha ajira ambazo haziko kwenye mkondo rasmi ikiwemo kilimo ili kutoa pensheni kwa wazee wote. Katika kipindi cha mwaka mmoja  nimeshiriki kuwakilisha hitaji la uboreshaji wa mifumo ya wastaafu ili kuwezesha wazee wetu kuwa na fursa ya kupata huduma za msingi na kuwa na kipato stahili cha kuwakimu hata baada ya kumaliza utumishi wao kwa taifa&lt;br /&gt;Miaka 50 ya Uhuru, vyombo vya ulinzi na usalama vimeweza kulinda mipaka ya nchi yetu ilipovamiwa na Iddi Amin wa Uganda katika vita ya Kagera. Hata hivyo, nafasi ya vyombo vyetu katika kulinda maslahi ya nchi na kudhibiti masuala yenye kulihujumu taifa inaanza kuporomoka. Ni muhimu kwa vyombo vya ulinzi na usalama kujitafakari na kuweka mstari wa mbele kulinda maslahi ya umma badala ya matakwa ya mafisadi. Vyombo vya dola ambavyo vinapaswa kutimiza wajibu huu kwa ukaribu zaidi ni Usalama wa Taifa (TISS), TAKUKURU na Jeshi la Polisi kwa kuweka mkazo masuala ya kiuchumi na kijamii katika kazi zao ndani na nje ya mipaka yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha mwaka mmoja wa utumishi wa umma, nimekuwa nikivikumbusha vyombo husika bungeni na kwa njia nyingine mbalimbali za uwakilishi kuweza kuchukua hatua stahiki kuhusu masuala mbalimbali. Aidha, nimechangia jitihada za kuimarisha ulinzi jimboni dhidi ya vitendo vya ujambazi na uhalifu wa aina nyingine kwa kushiriki katika harambee za ujenzi wa vituo vya polisi pamoja na ulinzi shirikishi. Pia, nimeweka mkazo katika kuunga mkono jitihada za kuboresha maslahi ya askari ikiwemo kushughulikia malalamiko ya madai ya malipo pungufu ya posho na malimbikizo ya madeni mbalimbali. Tuendako ni muhimu pia kuweka mkazo katika ujenzi wa kituo cha kisasa cha polisi cha ngazi ya wilaya jimboni Ubungo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru pigo lingine kwa mwelekeo wa taifa letu, na utumwa wa kiutamaduni unaoendelea kumea. Vijana wanaweza kubebeshwa mzigo wa lawama wa kuiga tamaduni za kigeni kwa kiwango chenye kupoteza utaifa wetu; ukweli ni kuwa chanzo cha yote haya ni uongozi usio na maono. Unapokuwa na utawala wenye sera ambazo hata vyombo vya habari vya umma vinakuwa kinara wa kuwa vioo vya tamaduni za nchi zingine; usitegemee vijana kubeba urithi wa nchi yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tuendako viongozi wetu wanapaswa kuelewa kwamba nchi zilizofanya mapinduzi ya kiuchumi; muhimili thabiti wa mwelekeo wao ni tamaduni zao. Kinyume chake, nchi zenye viongozi wabinafsi; viongozi wasiojiamini, viongozi wasiowajibika ambayo ni matokeo ya utamaduni wa ufisadi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni muhimu tukaungana kuendelea kufanya mabadiliko ili kuweka mkazo katika kujikwamua kifikra; kuanzia katika desturi zetu; fasihi zetu; muziki wetu; michezo yetu; familia zetu: vyote vituelekeze katika kujenga taifa lenye kukumbuka tulipotoka na kutengeneza mweleko mwafaka wa vizazi vijavyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight: bold;"&gt;Uhuru na Mabadiliko ya Siasa:&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;Tarehe 9 Disemba 1961 bendera ya wananchi wa Tanganyika yenye rangi tatu za kijani kibichi, nyeusi na dhahabu kama ishara ya uhuru wa kisiasa wa kujitawala. &lt;br /&gt;Baada ya Uhuru, viongozi wa kwanza wakiongozwa na Mwalimu Nyerere walianza mikakati ya kujenga taifa (National Building) kwa kuchukua maamuzi muhimu ya kuleta umoja. Maamuzi hayo yaliongozwa na dhana kama  ‘uhuru na umoja’, ‘uhuru na kazi’ na hata baadaye ‘uhuru na maendeleo’; huku kauli mbiu kama ‘siasa ni kilimo’ zikitumika kusukuma ajenda husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya maamuzi makubwa ya kisiasa ni pamoja na: Muungano katika ya Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964; kufutwa kwa Mfumo wa Vyama vingi mwaka 1965; kutangazwa kwa Azimio la Arusha mwaka 1967 kulikofuatiwa na utaifishaji (nationalization) wa njia kuu za kiuchumi- kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea; kufutwa kwa dhana ya serikali za mitaa mwaka 1972 na kuanzishwa kwa madaraka mikoani nk. Kwa ujumla kati ya kipindi cha mwaka 1961 mpaka 1985 taifa lilioongozwa kufanya maamuzi mengi ya kisiasa yenye taathira kubwa ya kiuchumi na kijamii ambayo inaonekana hadi leo. Si lengo la waraka huu kuchambua kila uamuzi na faida na hasara zake; katika kipindi husika ambacho Urais wa taifa letu uliongozwa na Mwalimu Julius Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru kwa ujumla maamuzi mengi yaliyofanyika wakati huo yaliwezesha kujengwa kwa taifa lenye umoja, amani na mshikamano; hata hivyo maamuzi hayo hayo yamedumaza utamaduni wa ushindani katika taifa letu iwe ni kwenye sekta za kiuchumi na hata siasa yenyewe. Mathalani, uamuzi wa kufanya chama kishike hatamu, ulifanya moja kwa moja taasisi ambazo zinapawa kuwa huru kugeuzwa kuwa mihimili ya chama kinachotawala; kuanzia vyama vya wafanyakazi, asasi za kiraia na hata jeshi ambalo baada ya maasi (mutiny) ya mwaka 1964, jeshi mpya la wazalendo (JWTZ) liliundwa na askari kutoka umoja wa vijana wa TANU (TYL). Uhuru wa fikra uliminywa kiitikadi, kisheria na kimatendo kwa kutumia kivuli cha kutaka kujenga umoja wa kitaifa. Wakati huo huo, katika kipindi husika kuliendelezwa kwa kiasi kikubwa sheria na mfumo wa utawala tuliorithi kutoka kwa mkoloni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Awamu ya Pili ya Utawala Tanzania kati ya mwaka 1985 mpaka mwaka 1995 chini ya Rais wa wakati huo- Ali Hassan Mwinyi; nao ulikuwa na maamuzi yake ambayo ni muhimu kukumbukwa kihistoria. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kiasi kikubwa maamuzi hayo ya kisiasa yakifanyika kwa shinikizo kutoka nje, ambapo maamuzi ya kiuchumi ndiyo kwa kiwango kikubwa yaliyokuwa yakiamua hatma ya mwelekeo wa kisiasa. Kwa masharti ya Benki ya Dunia (WB) na Taasisi ya Fedha ya Kimataifa (IMF), Tanzania ikafanya ‘geuka nyuma’ ya kisiasa, kwa maelezo ya kufuata sera za ubinafsishaji na soko huria. Lakini mageuzi hayo yalikuwa ni barakoa (mask) ya kutupeleka kwenye utamaduni wa ubinafsi na soko holela. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kati ya matukio ya kukumbukwa wakati huo ni pamoja na: Maamuzi ya Zanzibar ya mwaka 1991 ambayo yalifuta misingi muhimu ya Azimio la Arusha, hususani iliyohusu maadili ya uongozi na nchi kuingia katika mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Hata hivyo, mageuzi yote hayakuendena na kuandikwa kwa katiba mpya, na matokeo yake ni sheria na hata utamaduni wa kisiasa kuendeleza misingi ya chama tawala kuwa chama dola; mithili ya nchi kuendelea kuwa katika mfumo wa chama kimoja. Ripoti za Tume ya Nyalali na Tume ya Kisanga zinaweza kutupa picha ya ziada ya hali ya kisiasa katika kipindi husika na maamuzi ambayo yalipaswa kufanyika miaka 50 baada ya uhuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Awamu ya tatu ya utawala chini ya urais wa Benjamin Mkapa kati ya mwaka 1995 mpaka mwaka 2005 ulitaasisisha misingi ya soko holela na ubinafsi na hivyo kuliondoa taifa katika misingi ya uwajibikaji na kulitumbikiza katika utamaduni wa ufisadi. Ukiweka katika mizani, mafanikio ya Mkapa katika kuweka misingi ya kiuchumi iliyojikita zaidi katika utandawazi, uwekezaji wa kigeni na unyonyaji wa kodi toka kwa wananchi masikini hayawezi kulingana na hasara ya ufisadi na uuzaji wa rasilimali ambao ulifanyika katika awamu yake ya utawala. Ni katika kipindi hicho hicho ambacho maamuzi ya siasa zetu katika uchaguzi, yameanza kuwekwa katika nguvu zilizo nje ya nguvu ya umma wa watanzania miaka 50 baada ya uhuru wa Tanganyika. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Awamu ya nne imeingia mwaka 2005 chini ya Rais Jakaya Kikwete na kuahidi kuendeleza yale yaliyoachwa na awamu ya tatu kwa ari, nguvu na kasi mpya; na mwaka 2010 kuendeleza zaidi pale ambapo utawala wake umefikia. Tarehe 9 Disemba 1961, Nyerere aliiasa TANU dhidi ya kupoteza wakati katika kugombania vyeo na fahari ya nafsi; hali ambayo sasa imeikumba CCM na kuathiri mwelekeo wa chama tawala katika kuisimamia serikali iliyo madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka 50 baada ya uhuru wa Tanganyika nchi yetu inakabiliwa na changamoto nyingi za kisiasa na kiutawala zenye taathira kubwa katika maendeleo ya taifa letu na watu wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bado taasisi muhimu katika nchi yetu hazijaweza kutoa uongozi wa kisiasa  na hivyo kufanya taifa kudumbukia katika siasa chafu na utawala mbovu katika ngazi mbalimbali. Ombwe hili la uongozi, lenye ishara zote za kushindwa kufanya maamuzi bora katika masuala ya msingi yanayolikabili taifa; limesababisha misingi ya haki na utawala wa sheria inazidi kutetereka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Toka orodha ya mafisadi (list of shame) isomwe mnamo Septemba 15, 2007; mafisadi wameendelea kuachwa wakitamba na kuliteteresha taifa. Mtiririko wa matukio unaonyesha kwamba vikao vya juu vya chama kinachotawala vimetekwa mafisadi hali ambayo inaelekea kujipenyeza mpaka kwenye mihimili mingine ya dola. Kuachwa kwa hali hii miaka 50 baada ya uhuru kumefanya mazoea ya ufisadi kusambaa kwenye ngazi mbalimbali za serikali na taasisi nyingine badala ya taifa kuwa na utamaduni wa uwajibikaji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha mwaka mmoja ya utumishi wa umma nimehoji kwa njia mbalimbali hatua za serikali kuhusu ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia kampuni ya Kagoda, Kampuni ya Meremeta, uuzwaji kinyemela wa Shirika la Usafiri Dar es salaam (UDA), mikataba mibovu kwenye kituo cha Mabasi cha Ubungo (UBT), Richmond/Dowans, upotevu wa mapato katka gesi asilia hususani kuhusu kampuni ya Pan African Energy, malipo kwa Twiga Chemicals nk. Tunapokwenda nitaendelea kushirikiana na wote wenye kupinga ufisadi ili kuhakikisha hatua za msingi zinachukuliwa kwa ajili ya kuwezesha wimbi la uwajibikaji katika ngazi mbalimbali za utumishi wa umma.&lt;br /&gt;Miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika katika kutafuta uhuru wa kweli wa kisiasa tuendelee kusimamia mabadiliko ya katiba ili tuweze kubadili sheria na mazingira ya kisiasa. Hii ihusishe mabadiliko ya mfumo wa kiutawala kuondokana na misingi iliyorithiwa kwa mkoloni wa kuwapa madaraka makubwa viongozi wa kuteuliwa kama wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa; hodhi ya utawala ikiwa kwa serikali kuu badala ya kuongozwa kwa nguvu ya umma kupitia viongozi waliochaguliwa na umma kidemokrasia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kipindi cha mwaka mmoja nimeshiriki katika kusukuma suala la mabadiliko ya kimfumo kwa kutaka kuanzishwa kwa mchakato wa katiba mpya wenye kuwahusisha wananchi. Wakati serikali ilipotaka kuanza mchakato moja kwa moja kwa mamlaka ya Rais bila kuwa na sheria wala kuhusisha vyombo vingine vya uwakilishi nilipinga kwa nguvu suala hili na kueleza kusudio la kuwasilisha hoja binafsi bungeni. Hatua hii ilifungua mjadala mpana na hatimaye serikali ikakubali suala husika kuanzia bungeni kwa kutungiwa sheria. Pamoja na kasoro zote zilizojitokeza baadae muswada wa sheria husika kupelekwa bungeni ni suala ambalo limesaidia katika kupanua wigo wa mjadala, kuwezesha utaratibu kuwekewa mfumo wa kisheria na pia kufanya dhamira ya serikali kutaka kuhodhi mchakato kuonekana bayana kwa watanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tarehe 5 Novemba 2011 kabla ya kwenda kwenye mkutano wa tano wa Bunge uliojadili Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba nilifanya Mkutano wa Wananchi jimboni kuweza kupata maoni kuhusu muswada huo. Mkutano huo ulivamiwa na polisi ambao walikamata viongozi waandaji, wakakata nyaya za vipaza sauti na kuondoka pamoja na gari la matangazo pamoja na nyaraka za katiba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Licha ya hali hiyo nilipofika kwenye eneo la mkutano niliendelea kuhutubia wananchi bila kipaza sauti na kupata maoni yao ambao kwa ujumla wao walipinga muswada huo na kunitaka nisusie kwenda kuujadili mpaka pale umma utakapopata muda wa kutoa maoni ya kuuboresha. Ni msimamo huo ndio niliokwenda nao bungeni ambapo muswada ulipitishwa bila kuwa na mjadala wenye tija na Rais akasaini sheria husika hata baada ya kupokea ushauri wa kamati ambayo mimi nilishiriki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 ina vifungu vyenye kukinzana na haki za msingi za binadamu kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa na katiba ya nchi yetu na haijengi muafaka wa kitaifa wa kupata katiba mpya.  Pia, muundo na uwakilishi katika Tume na Bunge Maalum ya katiba ulivyo katika sheria husika hautawezesha maandalizi ya rasimu na hatimaye utungaji wa katiba bora ya nchi yetu. Hatimaye kura ya maoni ya kuhalalisha katiba husika itasimamiwa na tume ya sasa ya uchaguzi bila kuwa na muundo na mfumo huru na wa haki wa kitaasisi na kisheria wa kura husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni muhimu kwa maslahi ya umma tuungane pamoja kutaka kwanza mabadiliko ya msingi ya sheria husika kwa kuwashirikisha wananchi kabla ya mchakato wa katiba kuanza ili taifa lisiingie katika hasara ya kugharamia mchakato ambao utaleta katiba mbovu na migogoro katika nchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight: bold;"&gt;Uhuru na Mabadiliko:&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;Ili uhuru wetu uweze kuwa wenye matokeo kwenye maisha yetu na ya taifa letu tunahitaji kuungana kufanya mabadiliko ya kweli. Changamoto kubwa ambayo nimeiona ni kwamba kuna udhaifu katika mifumo yetu ya kiserikali kwenye ngazi mbalimbali hali ambayo inakwaza hatua za haraka za kuleta mabadiliko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa pamoja tunapaswa kuendelea kulitoa taifa letu katika kufilisika kimaadili na kiitikadi na kukubaliana tunu za kitaifa zenye kuwezesha misingi ya uwajibikaji. Uhuru wa kweli wa kisiasa utakuja kwa kuwa na uongozi wenye maono (vision) na maadili (values) na kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika kipindi cha kuanzia sasa na kuendelea kutuwezesha kunufaika na rasilimali zetu: iwe ni vipaji vyetu, kodi zetu au maliasili za nchi yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Binafsi, jambo kubwa ambalo nimelifanya katika kipindi cha mwaka mmoja ni kutimiza majukumu ya kibunge ya uwakilishi, usimamizi na kutunga sheria kwa kuwa na utaratibu wa kufanya mikutano na wananchi, kuwa na ofisi ya mbunge inayohudumia umma na kuwasilisha masuala husika kwa kwa mamlaka mbalimbali bungeni, maofisini, manispaa na kwa njia nyingine mbalimbali. Ni dhamira yangu kuendeleza uwajibikaji tunapokwenda ili kuunganisha nguvu ya umma kila mmoja aweze kutimiza wajibu kwa nafasi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nihitimishe kwa maneno ya Nyerere kwa taifa siku ya uhuru wa Tanganyika tarehe 9 Disemba 1961 akiwaeleza wananchi kuhusu utendaji kazi wa baraza lake dogo la mawaziri 11 tu: “..mimi na wenzangu ni watumishi wenu ninyi mnaonisikiliza. Tunajua kuwa mnatuamini, nanyi tunawaamini. Na ni ninyi mnaotupa nguvu zetu tunazozihitaji kwa kazi kubwa iliyo mbele yetu…Na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu tutajitahidi kuwatumikieni bila kujitafutia faida zetu wenyewe au fahari ya cheo”.  Uhuru na Kazi, Uhuru na Mabadiliko.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawatakia heri ya mwaka mpya wenye upendo, furaha na mafanikio tukiweka mstari wa mbele ukweli, uadilifu, na uwajibikaji katika maisha yetu.&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight: bold;"&gt;John MNYIKA (Mb)&lt;br /&gt;26/12/2011&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-2442114418936593191?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/2442114418936593191/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=2442114418936593191' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2442114418936593191'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2442114418936593191'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/waraka-wa-pili-wa-mbunge-kwa-wananchi.html' title='Waraka wa Pili wa Mbunge kwa Wananchi wa Jimbo la Ubungo'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/-x985TeGqNLY/TvhGkt9YLUI/AAAAAAAAAk8/2xPxFk3mfaE/s72-c/MNYIKA.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-3860622547219863457</id><published>2011-12-24T23:28:00.000-08:00</published><updated>2011-12-27T15:15:59.908-08:00</updated><title type='text'>Majina mapya bila mfumo mpya hauwezi kutuhakikisha ufanisi wa tume wala kuwa na chaguzi huru na za haki</title><content type='html'>Kufuatia Rais Jakaya Kikwete kufanya uteuzi wa Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wadau mbalimbali wametaka maoni yangu kuhusu watu walioteuliwa. Kwa maoni yangu hatupaswi kutoa maoni kuhusu watu walioteuliwa kwa sababu matatizo ya tume yetu ya uchaguzi ni ya mfumo mzima. Hivyo, uteuzi wa mwenyekiti na mkurugenzi mpya wa tume ya uchaguzi hauwezi kuleta mabadiliko yoyote ya maana katika utendaji wa tume ya uchaguzi wala hauwezi kuisaidia tume hiyo kuweza kuaminika na umma.  Majina mapya bila mfumo mpya hauwezi kutuhakikisha ufanisi wa tume wala kuwa na chaguzi huru na za haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uteuzi huu mpya hauwezi kuhakikisha watanzania kuwa na chaguzi huru na haki katika chaguzi za marudio zinazotarajiwa kufanyika, wala hauwezi kuleta uchaguzi huru na haki wakati wa kura za maoni za kufanya maamuzi ya kuhalalisha katiba mpya wakati wa mchakato wa mabadiliko ya katiba kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2011. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia, uteuzi wa mwenyekiti na mkurugenzi mpya wa tume ya uchaguzi hautaweza kuhakikisha Tanzania inakuwa na uchaguzi huru na wa haki kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Hivyo, wananchi na wadau wote badala ya kupongeza uteuzi uliofanyika tunapaswa kuunganisha nguvu ya umma kuendelea kudai mabadiliko ya mfumo mzima wa uchaguzi ikiwemo utaratibu mzima unaoongoza uteuzi. Kwa sasa Rais Kikwete amepewa mamlaka makubwa ya uteuzi kwa mujibu wa katiba na mamlaka hayo ameyakuwa akiyatumia vibaya kufanya teuzi mbalimbali bila kuzingatia ridhaa ya umma na maslahi ya taifa kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uteuzi huu umedhihirisha mashaka ambayo wadau mbalimbali wamekuwa nayo juu ya mamlaka makubwa ya Rais katika mchakato wa mabadiliko ya katiba na pia katika masuala ya uchaguzi. Chini ya tume hii ya uchaguzi pamoja na uteuzi mpya uliofanyika maoni yatakusanywa na tume iliyoteuliwa na rais na katiba ikishatungwa na bunge la katiba itapitishwa kwa kupigiwa kura ambazo zitasimamiwa na tume hii hii ya uchaguzi ambayo imeteuliwa na Rais. Hivyo, tukiacha mfumo huu ukaendelea kama ulivyo tutapata katiba mpya kwa jina lakini katiba mbovu isiyokuwa na muafaka wa kitaifa kwa kuwa watanzania wengi hatuna imani na mfumo mzima wa sasa wa tume ya uchaguzi. Aidha, tume hii iliyoteuliwa na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM bila mapendekezo kutoka kwenye chombo chochote na bila uteuzi wake kuidhinishwa na chombo chochote itakwenda kusimamia uchaguzi katika mazingira yasiyokuwa huru na haki na hivyo kufanya uchakachuaji wa kura kama ilivyokuwa kwenye uchaguzi wa mwaka 2010. Katika mazingira haya, badala ya kutoa maoni kuhusu majina ya watu walioteuliwa tuitake serikali ifanye mabadiliko ya kikatiba na pia ifanye mabadiliko ya sheria ya uchaguzi ili mfumo mpya uwepo ambao utafanya uteuzi uweze kuwa wa kuamininiwa na wenye tija.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni muhimu tuijadili mifumo ya kisheria na kiuchaguzi kwa ajili ya uchaguzi na Muundo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Pamoja na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sheria mbalimbali zimekuwa zikisimamia uchaguzi hususani: Sheria ya Uchaguzi na. 1 ya mwaka 1985; Sheria ya Vyama vya siasa na. 5 ya mwaka 1992 na Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambazo zimetoa mamlaka kwa tume kusimamia na kuratibu uchaguzi ikiwemo kutoa maelekezo na taratibu mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muundo wa Tume unatokana na Katiba Kifungu 74(1) kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria na. 4 ya 1992 na Sheria na. 7 ya mwaka 1993; Tume inateuliwa na Rais(Katiba na Sheria husika zimeeleza sifa za wanaoweza kuteuliwa). Mkurugenzi wa Uchaguzi naye anateuliwa na Rais kwa mapendekezo ya Tume. Katiba kifungu 74 imebainisha majukumu ya Tume ya Uchaguzi. Wadau mbalimbali kwa nyakati tofauti wamekuwa wakidai tume huru ya uchaguzi wakati wa marekebisho ya 14 ya katiba yaliyofanyika karibu na uchaguzi mkuu wa 2005. Hata hivyo suala la muundo wa tume huru ya uchaguzi halikujadiliwa wala kuingizwa kama sehemu ya marekebisho hayo. Matokeo yake maandalizi ya chaguzi za 2005 na 2010 yalifanywa na tume ile ile ambayo ilisemwa kipindi chote kwamba haiko huru. Kamati mbalimbali ziliundwa na kufanya kazi kipindi cha uchaguzi pekee. Uteuzi huu wa Rais umeendeleza hali hiyo ambayo imekuwa ikilindwa kwa muda mrefu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Marekebisho ya sheria ya uchaguzi yaliyofanyika mwaka 2010 hayakubadili misingi ya muundo wa tume ya uchaguzi badala yake yalitoa tu mamlaka ya kuteua wasimamizi wa uchaguzi kutokana na ofisi au sifa zao tofauti na ilivyo ambapo tume huteua wasimamizi wa uchaguzi kutokana na ofisi pekee. Upenyo wa tume kuachiwa kuamua kati ya vyeo na sifa unatoa mianya ya kuruhusu hujuma. Mathalani, katika uchaguzi wa serikali ya mitaa wa mwaka 2009 pamoja na kuwa haukusimamiwa na tume; kanuni za uchaguzi huo zilitaja kwamba wasimamizi wa uchaguzi wangeteuliwa kwa cheo au kwa sifa; matokeo yake idadi kubwa iliteuliwa kutokana na vyeo ndio maana uchaguzi husika kwa sehemu kubwa ulisimamiwa na watendaji wa serikali kwa nafasi zao. Hali hii ilidhihirika pia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambapo chaguzi tume iliangalia vyeo na kuteua wakurugenzi na maafisa watendaji wa kata kusimamia uchaguzi badala ya uteuzi kuegemea zaidi katika sifa na kuepuka kuwateua watendaji wa serikali. Matokeo yake ilikuwa na uchakachuaji katika maeneo kadhaa na mivutano katika maeneo mbalimbali ya nchi wakati wa ujumlishaji wa kura na utangazaji wa matokeo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, badala ya kujadili majina ya watu walioteuliwa tuitake serikali kufanya mabadiliko ya kimfumo katika katiba na sheria kwa kuzingatia yafuatatayo: Pawepo na Sheria ya Tume ya Uchaguzi ili kuipa uhuru na mamlaka zaidi tume ya uchaguzi kama ilivyo katika nchi kadhaa za Kusini mwa Afrika.(Pendekezo hili limetolewa pia na Tume ya Uchaguzi na Vyombo mbalimbali vya Ufuatiliaji/Uangalizi wa uchaguzi).&lt;br /&gt;Katiba na Sheria vifanyiwe mabadiliko/marekebisho ili kutoa uhuru na mamlaka ya Tume ya Uchaguzi wa Kuzingatia vigezo vya Kanuni/Matamko na Misingi mbalimbali ya Uchaguzi ya Kimataifa ambayo taifa letu limeridhia. Baadhi ya masuala mahususi ni pamoja na: Tume iwe nje ya mfumo wa kiutendaji wa kiserikali(Watendaji wa Serikali kama Wakurugenzi na Watendaji wa Kata wasiwe watumishi wa Tume ya uchaguzi hata wakati wa uchaguzi); Wajumbe wa Tume wachaguliwe kwa mashauriano na Wadau wengine vikiwemo vyama vya siasa na baadaye wathibitishwe na Bunge; mwenyekiti achaguliwe na wajumbe hao miongoni mwao badala ya kuteuliwa na Rais kama ilivyo sasa; Utumishi wa Wajumbe waandamizi wa Tume wa ulindwe(durability and security of tenure) kisheria na kikatiba kama walivyo majaji; Uwakilishi wa Tume uzingatie jinsia, uwakilishi wa kijamii na makundi rika; Tume ya Uchaguzi iwajibike kwa Bunge badala ya Kuwajibika kwa Serikali; Tume ya Uchaguzi iwe na Bajeti inayojitegemea itakayopitishwa moja kwa moja na Bunge. Kamati za Tume ziwe ni za kudumu; ziendelee na kazi hata baada ya uchaguzi. Vitengo vya TEKNOHAMA (ICT) na Elimu ya Uraia viwe sehemu ya vitengo vya kudumu vya Tume. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tume ya Uchaguzi iwe na watendaji wa Kudumu katika ngazi mbalimbali; utaratibu wa kuwatumia maofisa wa serikali kama wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi usitishwe. Hii ihusishe kuwezesha bajeti ya Tume ya uchaguzi iwekewe fungu pekee kutoka katika mfuko mkuu wa fedha za umma(consolidated fund) badala ya kuwa sehemu ya bajeti za kawaida za wizara.Hivyo mjadala utakaowezesha kuunganisha nguvu za kidemokrasia na kimaadili ili kudai na kushawishi mabadiliko ya sheria za uchaguzi na mazingira ya kisiasa ikiwemo wenye kuboresha usimamizi wa uchaguzi ni muhimu uendelezwe hata baada ya Rais kuteua mwenyekiti na mkurugenzi mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-3860622547219863457?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/3860622547219863457/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=3860622547219863457' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3860622547219863457'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3860622547219863457'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/majina-mapya-bila-mfumo-mpya-hauwezi.html' title='Majina mapya bila mfumo mpya hauwezi kutuhakikisha ufanisi wa tume wala kuwa na chaguzi huru na za haki'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-7988075780965989286</id><published>2011-12-24T02:26:00.000-08:00</published><updated>2011-12-27T15:16:16.806-08:00</updated><title type='text'>Heri ya Xmas, Tamasha la Injili na kutoa zawadi</title><content type='html'>Nachukua fursa hii kuwatakia heri katika sikukuu ya noeli.  Kwa waumini siku hii ni kumbukumbu ya kwa mkombozi hivyo inapaswa kuleta mabadiliko ya kuzaliwa upya kiroho na kimaisha. Aidha nawahimiza kutumia siku hiyo kujumuika na waliokumbwa na matatizo mbalimbali katika jamii wakiwemo waathirika wa maafa ya maafuriko yaliyotokea Dar es salaam na maeneo mengine ya nchi yetu. Nawaalika kujumuika nami kwa hali na mali katika matukio ya tarehe 25 na 26 Disemba ambayo nitashiriki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kuadhimisha sikukuu ya mwaka huu pamoja na kujumuika na familia, tarehe 25 Disemba 2011 nitashiriki katika katika Tamasha la Muziki wa Injili na tarehe 26 nitatembelea nyumba za waathirika wa mafuriko eneo la Mabibo kutoa zawadi mbalimbali za sikikuu pamoja na kujumuika nao kwa chakula.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kuadhimisha sikukuu hii nimealikwa kuwa Mgeni Rasmi katika tamasha la muziki wa Injili litakalofanyika katika Ukumbi wa Landmark Hotel-Ubungo siku ya Krismas kuanzia saa 8:30 mchana ambalo limeandaliwa na RudishaMusic ikishirikiana na WAPO Radio FM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lengo kuu la tamasha hili ni kusherehekea sikuku ya Noel-(Krismas) na kuendeleza jitihada za kukuza tasnia ya muziki wa Injili hapa nchini. Tamasha litahusisha vikundi mbalimbali vya muziki wa injli wa moja kwa moja (live performance) ambapo vikundi vitakavyoshiriki ni pamoja na Host of Praise, Glorious Celebration, Holy of Holies, Jackson Benty, Rachel Marlon na Mwanamapinduzi Band. (Maelezo zaidi kuhusu tamasha husika yanapatikana kupitia: www.XmasExtravaganza.co.tz.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kuadhimisha sikukuu ya kufungua zawadi (Boxing Day) tarehe 26 Disemba 2011 nitatembelea kaya mbalimbali za kata ya Mabibo ambazo zimeathiriwa kwa kiwango kikubwa na mafuriko kutoa zawadi mbalimbali za noeli na kula chakula cha mchana pamoja na waathirika wakubwa wa maafa. Nitatumia vile vile fursa hiyo kutoa ujumbe wangu wa kuwatakia wananchi wote wa Ubungo na watanzania kwa ujumla heri ya mwaka mpya 2012.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-7988075780965989286?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/7988075780965989286/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=7988075780965989286' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7988075780965989286'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7988075780965989286'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/heri-ya-xmas-tamasha-la-injili-na-kutoa.html' title='Heri ya Xmas, Tamasha la Injili na kutoa zawadi'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-2728301515585173040</id><published>2011-12-22T01:47:00.000-08:00</published><updated>2011-12-27T15:16:42.559-08:00</updated><title type='text'>Hatua kuhusu maafa katika Jimbo la Ubungo</title><content type='html'>Jana na leo nimeshiriki katika jitihada za uokoaji na nimetembelea maeneo mbalimbali katika Jimbo la Ubungo kwa ajili ya kuchukua hatua za kibunge kufuatia maafa ambayo yamejitokeza kutokana na mvua na mafuriko yanayoendelea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama sehemu ya kazi ya mbunge ya uwakilishi na kuisimamia  serikali nimekuwa nikiwasiliana mara kwa mara na mamlaka zinazohusika na naomba kitengo cha maafa kuongeza nguvu zaidi katika kushughulikia matatizo yaliyojitokeza. Ingawa kuna udhaifu mkubwa katika mfumo wetu mzima wa kukabiliana na maafa na dharura kwa ujumla, hata hivyo huu si wakati wa kulaumiana bali kuunganisha nguvu katika kuchukua hatua za haraka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, natoa pole kwa wananchi wote waliofiwa au kuathirika kutokana na maafa yanayoendelea na kuwasihi waishi kwa tahadhari lakini wawe na utulivu katika kipindi hiki kigumu. Pia, natoa mwito kwa wadau wengine wote ikiwemo mashirika ya misaada ya kinadamu kutembelea katika maeneo ya maafa kuona hali halisi na kuchukua hatua zinazostahili kuunga mkono jitihada ambazo tunaendelea nazo hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maeneo ambayo nimetembelea nyumba za wananchi na miundombinu ni pamoja na kata ya Ubungo (maeneo ya Ubungo Kisiwani na Msewe), Kata ya Sinza (Maeneo ya Sinza D na Sinza E) kata ya Mabibo (Maeneo ya Mabibo farasi na Loyola) na Manzese (maeneo ya Uzuri na Chakula Bora).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha nimefuatilia kupitia kwa madiwani na watendaji wengine taarifa za maeneo mengine yaliyokumbwa na maafa ya kata za Kimara, Makuburi, Mbezi na Goba na wakati wote nimekuwa nikitoa taarifa kwa mamlaka zote zinazohusika na kuwezesha hatua mbalimbali hususani za uokoaji kuweza kuchukuliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Natoa taarifa hii nikiwa njiani nikiendelea kutembelea maeneo mengine ili maafa haya yanayoendelea yaweze kuchukuliwa kwa udharura na uzito unaostahili na wananchi na mamlaka zote zinazohusika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na maafa haya wapo wananchi ambao makazi yao yameharibiwa kabisa na wanahitaji maeneo ya dharura ya kuweza kuishi pamoja na kupata mahitaji ya kibinadamu hasa baadhi ya kaya za eneo la Ubungo Kisiwani (Nyuma ya Land Mark Hotel) na baadhi ya kaya za eneo la Manzese (Uzuri na Chakula Bora). Manispaa ya Kinondoni inapaswa kutangaza eneo maalum kwa ajili ya huduma husika kuweza kupatikana kwa wahanga kama jambo la dharura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, miundombinu ya maeneo mbalimbali imeharibiwa hali ambayo inahitaji njia mbadala za wananchi kuweza kuvuka mito na mikondo ya maji katika maeneo husika bila kuhatarisha maeneo yao. Baadhi ya madaraja yaliyoharibiwa ni pamoja na daraja la Msewe, madaraja ya Kilungule, daraja la Mabibo Farasi na daraja linalounganisha kata ya Mbezi Louis na Goba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuunga mkono agizo la mkuu wa mkoa kuwataka wanaoishi katika mabonde kuchukua tahadhari ya kukaa mbali na maeneo yao wakati huu wa mvua kubwa, nimebaini katika ziara niliyofanya kwamba maafa ya sasa yanagusa watu wengi zaidi ya waishio katika mabonde.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, ni vizuri serikali ikatambua kwa dharura maeneo yote ambayo yako hatarini kufikiwa na maafuriko hata kama yako mbali na mabonde na kuweza kutoa tahadhari mahususi kwa wananchi na kuwaeleza utaratibu mbadala wa makazi ya dharura.&lt;br /&gt;Pia, yapo maeneo ambayo uwezekano wa kukumbwa na mafuriko zaidi ni mkubwa pamoja na kuwa mbali na eneo la mto kutokana na kuziba kwa njia za mto kwa sababu mbalimbali ikiwemo matatizo katika ujenzi na mipango miji lakini pia kutokana na uchafu. Hivyo, hatua za dharura zinahitajika katika kusafisha, kupunguza kifusi na kuweka kingo ili kuwezesha maji kuweza kupita wakati huu wa dharura. Hatua hii ihusishe mito mbalimbali iliyoko jimbo la Ubungo ikiwemo mto ng’ombe katika kata na maeneo mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na matatizo ya mipango miji ya ujenzi holela, udhaifu katika usafishaji wa mito pamoja na uchafuzi wa mazingira inaelekea maafa ya sasa yamechangiwa pia na mvua kubwa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi. Hivyo, suala hili linapaswa kuchukuliwa kwa uzito wa kitaifa ili kukabiliana na athari za sasa na madhara makubwa zaidi yanayotarajiwa siku za usoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua zinazochukuliwa mpaka hivi sasa bado hazilingani na ukubwa wa tatizo kwa kuwa kwa sehemu kubwa zinahusisha serikali katika ngazi ya mkoa, wilaya na manispaa mbalimbali za jiji la Dar es salaam katika maafa yenye uzito wa kitaifa yanayohitaji vyombo vyote vinavyohusika na maafa na wananchi kwa ujumla kuweza kuunganisha nguvu katika kuchukua hatua stahiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimewahimiza madiwani, watendaji wa kata, wenyeviti wa mitaa na watendaji wa mitaa kuweza kufanya tathmini katika maeneo yao na kutoa taarifa za dharura kwa ajili ya kuwezesha hatua kuchukuliwa kwa wakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nitatoa taarifa kwa umma kuhusu masuala mengine yanayohusu misaada ya kibinadamu katika Jimbo la Ubungo baada ya kukutana na kamati ya maafa ya wilaya ya Kinondoni. Tumevitaarifu vyombo vya dola kuhusu vifo ambavyo vimetokea mpaka hivi sasa na naamini watatoa taarifa kwa umma. Aidha, mara baada ya kukamilisha kuchukua hatua za kushughulikia dharura ya maafa nitatoa taarifa ya kina zaidi ya athari za hali hii pamoja na madhara ya hatua kutokuchuliwa kwa wakati toka maamuzi yalipofanyika baada ya maafa yaliyotokana na mvua za El Nino miaka michache iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika-Mbunge wa Jimbo la Ubungo&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;PS: &lt;strong&gt;Taarifa hii niliitoa jana tarehe 21 Disemba 2011. Jana hiyo hiyo jioni tulikaa kikao cha Kamati ya Maafa ya Wilaya. Kutokana na kuwa na haraka ya kuelekea kwenye maeneo ya maafa sitaweza kuandika kwa kina maazimio tuliyoyafikia. Hata hivyo, tayari tumeshaanza utekelezaji wa kushirikiana na mamlaka mbalimbali kuhusu athari za kibinadamu na pia kuhusu miundombinu. Ofisi ya mbunge ubungo imeshawasiliana na madiwani, watendaji wa mitaa, wenyeviti na watendaji kwa ajili ya kuwajulisha hatua mbalimbali ambazo wanaendelea kuzichukua. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo ninashiriki katika kazi za maafa katika maeneo mbalimbali: Mosi, nitaungana na wenzetu wa jimbo la Kinondoni kwa ajili ya kutoa misaada ya kinadamu kwa wahanga wa maafa wa Hananasif, Magomeni Sunna, Tandale na Kigogo. Pili; nitakuwa na ziara ya jimbo la Ubungo kwa ajili ya kutoa misaada ya kibinadamu kwa wahanga wa Mbezi/Saranga (Kibanda cha Mkaa) na pia nitatembelea maeneo yaliyoathirika ya Kimara Kilungule na kwa Msuguri (eneo la Msingwa). Aidha, nitashiriki maziko ya mahanga waliofariki jana kutokana na maafa ya maafuriko katika kata ya Mburahati na pia walioangukiwa na ukuta kutokana na mvua katika eneo la Kilungule. Aidha, napenda kurudia tena kusisitiza kwamba huu si wakati wa kulaumiana bali kuunganisha nguvu katika kukabiliana na athari za maafuriko haya; hata hivyo baada ya maafa haya nitarejea katika kumbukumbu mbalimbali za kibunge na za vikao vya jiji na manispaa kuhoji sababu za hatua kutokuchukuliwa kwa wakati wa ukamilifu hata baada ya kutoa tahadhari mbalimbali na kutaka hatua kuchukuliwa kwa nyakati mbalimbali toka niingie katika utumishi wa umma ili hatua za uwajibikaji ziweze kufuata.&lt;/strong&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-2728301515585173040?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/2728301515585173040/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=2728301515585173040' title='6 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2728301515585173040'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2728301515585173040'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/hatua-kuhusu-maafa-katika-jimbo-la.html' title='Hatua kuhusu maafa katika Jimbo la Ubungo'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>6</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-1818687486126206398</id><published>2011-12-19T23:33:00.000-08:00</published><updated>2011-12-27T15:18:03.185-08:00</updated><title type='text'>Kuhusu Serikali kulinda Viwanda vya ndani</title><content type='html'>Leo tarehe 19 Disemba 2011 vyombo mbalimbali vya habari vimemnukuu Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwahakikishia wafanyabiashara kwamba Serikali inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete itaendelea kulinda viwanda vya ndani ili viweze kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa taifa na kuongeza ajira.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, kauli hiyo haipaswi kuleta matumaini ya kweli kwa wafanyabiashara na watanzania kwa ujumla katika kipindi hiki cha kuathirika kwa uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kutokana na mfumuko mkubwa wa bei na kuporomoka kwa kasi kwa shilingi ya Tanzania ukilinganisha na dola kunakochangiwa pamoja na sababu mbalimbali ikiwemo kupungua kwa uzalishaji nchini katika kilimo na viwanda pamoja na ongezeko kubwa la uingizaji wa bidhaa kutoka nje.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri Mkuu Pinda anapaswa kutoa kwa wafanyabiashara wenye viwanda na umma wa watanzania mpango wa haraka wa kukuza uchumi wa nchi na kupunguza gharama za maisha ambao pamoja na mambo mengine utajikita katika kuongeza uzalishaji nchini, kupanua wigo wa ajira, kupunguza kiwango cha uagizaji wa bidhaa kutoka nje ili kuboresha urari wa biashara na kudhibiti bei ya bidhaa muhimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a name='more'&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, Waziri Mkuu Pinda amewaeleza wafanyabiashara wenye viwanda kuwa kama sehemu kulinda viwanda vya ndani Rais Jakaya Kikwete ameweka msisitizo katika ujenzi wa kanda huru za kibiashara (EPZ/SEZ) ili wawekezaji wasipate shida ya ardhi na miundombinu mingine; bila kueleza umuhimu wa kuweka mkazo katika kufufua na kuokoa viwanda vya ndani ambavyo vingi vimeathirika kutokana na ubinafsishaji holela na vingine kutokana na kutowekewa mazingira mazuri ya kibiashara ya kuviwezesha kuchangia katika kukuza uchumi na kuongeza ajira.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, natoa mwito kwa Waziri Mkuu Pinda kama kiongozi wa shughuli za serikali bungeni  kuonyesha mfano kwa vitendo vya kulinda viwanda vya ndani kwa kushughulikia matatizo ya viwanda ambavyo serikali ina hisa kwa kupitia kumbukumbu za bunge na kufuatilia kuhakikisha ahadi mbalimbali ambazo serikali imezitoa bungeni zinatekelezwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kati ya hatua hizo mahususi ni muhimu kwa serikali kufanya uchunguzi wa dharura kuhusu Kiwanda cha Nguo cha Urafiki kilichopo katika jimbo la Ubungo ili hatua za haraka ziweze kuchukuliwa kunusuru kiwanda hiki ambacho kina hali mbaya ya uzalishaji, migogoro ya wafanyakazi na uuzwaji au ukodishwaji wa mali za kampuni bila kuzingatia taratibu na maslahi ya umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, Rais Kikwete kwa nafasi yake ya kiongozi wa serikali na mwenyekiti wa baraza la mawaziri awaagize Waziri wa Fedha, Waziri wa Viwanda na Biashara na Waziri wa Kazi na Ajira kutekeleza mipango ya kulinda viwanda vya ndani hususani kiwanda cha Nguo cha Urafiki ambacho kina hali mbaya lakini kina fursa ya kuchangia katika kuongeza ajira na pato la serikali iwapo hatua za haraka zitachukuliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama inavyofahamika, moja ya viwanda vikubwa vya nguo hapa nchini vilivyojengwa wakati wa Awamu ya Kwanza  ya Utawala wa nchi yetu chini ya Rais Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni kiwanda cha Nguo cha Urafiki ambacho kilijengwa miaka michache baada ya uhuru kwa mkopo wa masharti nafuu kutoka nchi ya China.  Baadaye kiwanda kilibinafsishwa kiholela na sasa kinaendeshwa kwa ubia kuanzia mwaka 1997 ambapo serikali ya Tanzania inamiliki asilimia 49 ya hisa huku asilimia 51 zikiwa chini ya kampuni ya nchini China.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuwa mwenye hisa nyingi ndiye anawajibika zaidi katika uendeshaji wa kiwanda kiuendeshaji na maslahi ya wafanyakazi, serikali kwa kuwa na hisa 49% kwa niaba ya watanzania ina wajibu wa pekee wa kufuatilia kwa karibu hali ya kiwanda kama sehemu ya kulinda viwanda vya ndani, kudhibiti hasara kwa serikali na kuzuia upotevu wa mali za umma. Hata hivyo, kwa zaidi ya miaka kumi wajibu huu umekuwa hautekelezwi ipasavyo hali ambayo imedidimiza kiwanda kwa kiwango kikubwa na kuathiri uzalishaji pamoja na kupunguza ajira.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kubaini hali hiyo tarehe 4 Februari 2011 nilitembelea Kiwanda cha Nguo cha Urafiki Ubungo na kufanya mazungumzo na wafanyakazi pamoja na wawakilishi wa menejimenti. Kutokana na mkutano huo na vyanzo vingine nilipata maelezo ya kina kuhusu hali mbaya ya kiwanda ikiwemo kusimama kwa uzalishaji wa nguo na maslahi duni ya wafanyakazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia taarifa hizo nilichukua hatua ya kuziandikia mamlaka husika kuweza kuchukua hatua za haraka kunusuru hali ya kiwanda. Kutokana na mamlaka husika kuchelewa kuchukua hatua nilikwenda mbele zaidi kwa kutumia mamlaka ya kibunge kuhoji mawaziri husika wakati wa mkutano wa nne wa Bunge wakati wa kujadiliwa kwa bajeti za wizara mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya Wizara nilizozitaka kuchukua hatua ni pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Fedha hususani ofisi ya Msajili wa Hazina na Shirika Hodhi la Mali ya Mashirika ya Umma (CHC), Wizara ya Kazi na Ajira na mamlaka zingine. Hatua ambazo zimechukuliwa mpaka sasa zimekuwa za kususua na hazionyeshi kama serikali inayachukulia matatizo ya Kiwanda cha Nguo cha Urafiki kwa uzito unaostahili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuitaka serikali kuchukua hatua pia nilitoa mwito kwa kamati husika za bunge kuchukua hatua ambapo kamati ya Viwanda na Biashara iliitikia mwito huo na Novemba 2011 ilitembelea kiwanda na kushuhudia ukweli wa madai ambayo tumekuwa tukiyatoa kuhusu hali mbaya ya kiwanda. Kamati hiyo ilitoa kauli ya kutaka uchunguzi wa ziada ufanyike hatua ambayo haijatekelezwa mpaka hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Izingatiwe kuwa kabla ya Kuingia ubia, Serikali ilifanya ukarabati mkubwa wa mitambo kwa gharama za walipa kodi watanzania. Aidha, mara baada ya ubia serikali ya Tanzania iliingia mkataba mwingine na Serikali ya China wa mkopo wa dola milioni 27 (zaidi ya bilioni 30) kwa ajili ununuzi wa mitambo mipya badala yake kwa sehemu kubwa fedha hizo zikatumika kununua mitambo chakavu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo yake uzalishaji ukaanza kupungua na wafanyakazi wakaanza kupunguzwa na hivyo kusababisha kushuka kwa mapato ya serikali na kuongezeka kwa matatizo ya ajira. Pia, kutokana na matatizo hayo baadhi ya mitambo imeondolewa na kuuzwa kinyemela kama vyuma chakavu hali ambayo imesababisha wafanyakazi kupewa likizo wengi bila malipo na wengine kwa malipo pungufu kwa visingizio mbalimbali. Kutokana na hali hiyo nilizitaka Wizara na Mamlaka husika kuchunguza madai hayo na kuongeza ukaribu wa serikali katika uendeshaji wa kiwanda husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine maslahi ya wafanyakazi nayo yamezidi kuwa duni badala kuboreshwa baada ya ubia kuingiwa na hivyo kushusha  motisha ya ufanyaji wa kazi. Pia wafanyakazi hawalipwi mishahara kwa viwango vipya vilivyotangazwa na serikali katika hatua za awali. Hali hizi zimesababisha migogoro mbalimbali kati ya kampuni na serikali kwa upande mmoja na  wafanyakazi walioko kazini na walioachishwa kwa upande mwingine na hivyo kuongeza mizigo ya madeni kupitia hukumu za mahakama, mamlaka zingine na madai lukuki. Kufuatia hali hiyo kudumu kwa muda mrefu zaidi ya miaka kumi, nilitoa mwito kwa Wizara na Mamlaka husika kuchukua hatua za haraka kumaliza matatizo ya wafanyakazi katika Kiwanda cha Nguo cha Urafiki ili kuelekeza nguvu katika uzalishaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mikutano ya tatu na nne ya Bunge kwa nyakati na njia mbalimbali nilizieleza pia Wizara na mamlaka mbalimbali za serikali kuwa hali mbaya ya kiwanda inahusisha pia kukosekana kwa udhibiti katika mali za kampuni na pia kiwanda kuanza kufanya shughuli ambazo ziko nje ya kazi ya msingi ya ubia wa uzalishaji wa nguo. Niliitaka serikali kuchunguza na kuchukua hatua juu ya shughuli zinazoendelea kufanywa na Kiwanda cha Nguo cha Urafiki nje ya mikataba na misingi ya ubia mathalani: upangishaji wa Nyumba za wafanyakazi, upangishaji wa maeneo ya wazi, upangishaji wa maghala ya kiwanda, uuzaji wa nyumba za wafanyakazi, mfano mzuri ni nyumba 50 za THB eneo la Manzese, na ukodishaji wa maeneo kwa ajili ya kufanya biashara ya mafuta. Hali hii imeambatana na uingizaji wa bidhaa za nje kwa mgongo wa kampuni ya Urafiki na zingine tanzu kinyume na ubia wenye msingi wa kulinda na kuendeleza viwanda vya ndani hali ambayo imeleta athari katika uchumi wa taifa na kupunguza ajira za uzalishaji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na hali hiyo nilitoa mwito kwa Serikali kuingilia kati kupitia Wizara ya Fedha hususani Ofisi ya Msajili wa Hazina na Shirika Hodhi la Mali za Mashirika ya Umma (CHC) na Wizara ya Viwanda na Biashara kuchukua hatua zinazostahili juu ya kiwanda cha Urafiki. Aidha, kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda na Biashara kuchukua hatua za kuisimamia serikali ili kuharakisha hatua za kunusuru kiwanda hiki kama ili kuonyesha pia mfano wa hatua zinazopaswa kuchukuliwa kuhusu viwanda vingine. Hata hivyo, mpaka sasa hakuna hatua kamili zilizochukuliwa na Wizara na Mamlaka husika hivyo Waziri Mkuu Pinda anapaswa kuingilia kati kusukuma hatua kuchukuliwa baadala ya kutoa kauli za ujumla kwamba serikali inalinda viwanda vya ndani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, ili dhamira hiyo ya Rais Kikwete kuendeleza uwekezaji katika viwanda vya ndani iweze kudhihirika serikali iweke wazi kwa umma taarifa ya uchunguzi kuhusu hali ya viwanda vilivyobinafsishwa ambayo imebaini ufisadi na matatizo makubwa ya kiutawala katika uwekezaji ili kuweka msingi wa hatua kuchukuliwa kunusuru viwanda hivyo pamoja na kudhibiti hali kama hiyo isijitokeze katika uwekezaji katika maeneo maalum ya kiuchumi unaoendelea hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ps: Taarifa hii niliitoa jana 19/12/2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-1818687486126206398?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/1818687486126206398/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=1818687486126206398' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1818687486126206398'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/1818687486126206398'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/kuhusu-serikali-kulinda-viwanda-vya.html' title='Kuhusu Serikali kulinda Viwanda vya ndani'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-6782128458439564110</id><published>2011-12-16T04:18:00.000-08:00</published><updated>2011-12-16T04:20:58.193-08:00</updated><title type='text'>Taarifa ya Mkutano wa Kanda Maalum DSM</title><content type='html'>Taarifa inatolewa kwa viongozi, wanachama na wapenda demokrasia na maendeleo wa Jiji la Dar es salaam na Manispaa kuhusu Mkutano Mkuu wa CHADEMA wa Kanda Maalum Dar es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkutano huo utafanyika jumapili ya tarehe 18 Disemba 2011 kuanzia saa 4 kamili asubuhi katika Ukumbi wa Kilamuu ulioko Mbezi jijini Dar es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Washiriki wa mkutano huo ni viongozi wa chama wa Mikoa ya kichama ya Temeke, Ilala, Kinondoni na wajumbe wa mikutano mikuu ya majimbo yote ya jiji la Dar es salaam. Aidha, waalikwa katika mkutano huo ni pamoja na viongozi wa kuchaguliwa katika ngazi mbalimbali, viongozi wilaya, kata na wawakilishi wa matawi mbalimbali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa zaidi kuhusu ushiriki wa wanachama na wapenda demokrasia na maendeleo katika mkutano husika zinatolewa katika ofisi mbalimbali za chama katika ngazi za mikoa, wilaya/majimbo ya kanda maalum ya Dar es salaam. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ajenda za Mkutano huo ni waraka na. 1 na 2 wa chama wa mwaka 2011 kuhusu uchaguzi ndani ya chama  na waraka na. 3 wa mwaka 2011 kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011.  Mgeni rasmi katika Mkutano huo ni Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa ambaye pia atashiriki katika kutoa mada.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkutano huu ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya mpango mkakati wa CHADEMA wa mwaka 2011 mpaka 2016 ambapo umeweka mkazo kwa chama kufanya mikutano katika ngazi mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa chama pia kwa ajili ya kushughulikia masuala muhimu ya kitaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika ajenda ya waraka namba 1 na 2 Mkutano utapokea na kujadili maelezo na maelekezo mbalimbali kuhusu maandalizi ya uchaguzi wa ndani ya chama katika ngazi mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ajenda ya Waraka namba 3 ni sehemu ya utekelezaji wa azimio la Kamati Kuu la tarehe 20 Novemba 2011 ambayo iliwaagiza viongozi wote wa chama na wa kuchaguliwa wa ngazi zote nchi nzima kufanya mikutano ya ndani na ya hadhara kwa lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya sheria ya Mabadiliko ya Katiba na madhara yake kwa mchakato wa kupata katiba mpya na bora kwa nchi yetu ili kuunganisha umma wa watanzania kuweza kufanya mabadiliko ya msingi. Kamati Kuu ilizingatia  kwamba sheria husika ilisomwa na kujadiliwa kwa mara ya pili bila ya wananchi kushirikishwa kwa ukamilifu kutoa maoni yao na muswada kuboreshwa kwa kuzingatia makubaliano ya kitaifa kuhusu mchakato wa katiba mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha Kamati Kuu iliazimia kwamba CHADEMA itaendelea kutoa elimu kwa wanachama, wananchi na wadau wote juu ya ubovu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na juu ya haja ya kuwa na sheria itayoweka utaratibu bora zaidi wa kuunda Tume Shirikishi ya Katiba kwa lengo kukusanya maoni ya wananchi, kuandaa ripoti na rasimu ya katiba mpya, Bunge Maalum la Katiba na usimamizi wa kura ya maoni itayowezesha wananchi kufanya maamuzi kwa uhuru na kwa haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba kwa mujibu wa waraka na. 4 wa mwaka 2007 chama kilielekeza kwamba Hoja ya Mabadiliko ya Katiba ya Nchi kuwa ya kudumu katika vikao vya kikatiba vya chama pamoja na mikutano na wananchi mpaka pale taifa letu litakapokuwa na katiba mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maandalizi ya Mkutano huo ni matokeo ya kikao cha pamoja cha viongozi wa Mikoa ya kichama, wilaya za kichama, na majimbo ya kiuchaguzi ya Kanda Maalum ya kichama ya Dar es Salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Mikoa ya Kanda Maalu ya Dar es salaam&lt;br /&gt;Na Mwenyekiti wa Mkoa wa Kichama wa Kinondoni.&lt;br /&gt;16/12/2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-6782128458439564110?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/6782128458439564110/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=6782128458439564110' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6782128458439564110'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6782128458439564110'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/taarifa-ya-mkutano-wa-kanda-maalum-dsm.html' title='Taarifa ya Mkutano wa Kanda Maalum DSM'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-8307684967421650847</id><published>2011-12-15T06:30:00.000-08:00</published><updated>2011-12-15T06:34:54.942-08:00</updated><title type='text'>Mwigamba apata dhamana; tuepuke dola ya kipolisi</title><content type='html'>Hatimaye leo tarehe 15 Disemba 2011 Samson Mwigamba mmoja wa Waandishi wa Makala aliyefikishwa mahakamani tarehe 8 Disemba 2011 ametoka mahabusu kwa dhamana. Kuchelewa kutoka kwake kumesababishwa na ugumu wa dhamana iliyotokana na aina ya dhamana iliyotakiwa. Awali ilitarajiwa angeshtakiwa kwa kosa la uchochezi hivyo viongozi wa chama walijiandaa kwa dhamana husika. Hata hivyo, hata hivyo alifunguliwa kesi ya jinai namba 289 ya mwaka 2011 yenye mashtaka makubwa zaidi ya kudaiwa kushawishi askari na maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama kutoendelea kutii serikali inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete (kosa lenye mwelekeo wa uhaini).&lt;br /&gt;Mahakamani alidaiwa kutenda kosa hilo tarehe 30 Novemba 2011 kutokana na Makala yake kwenye gazeti la Tanzania Daima Toleo Na. 2553 ambayo inadaiwa kuwa maudhui yake yamekwenda kinyume na kifungu 46 (b), 55 (10)(a) na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na mashtaka hayo alitakiwa kati ya mdhamini mmoja wapo aweke hati ya nyumba yenye thamani iliyotajwa na mahakama. Kwa kuwa sharti hili lilitolewa tarehe 8 Novemba na kesho yake ilikuwa sikukuu ya uhuru tarehe 9 Disemba hakukuwa na fursa ya kutimiza masharti yote kwa wakati pamoja na jitihada zote zilizofanywa na viongozi husika wa chama. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni kwa sababu taratibu za dhamana ya hati yenye mali isiyohamishika zinahusisha mali hiyo kufanyiwa uthamini (valuation) na baadaye kufanyiwa tena tathmini ya uthibitisho (verification) hatua ambazo huchukua muda kutokana na urasimu katika mamlaka mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa heshima yake na kwa ajili ya kupanua wigo wa mjadala nimeona niwaletee ujumbe huu ambao nilichangia kwenye mtandao wa Wanabidii tarehe 7 Disemba 2011, siku moja kabla ya Mwigamba kufikishwa mahakamani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Nimesoma tena ujumbe ambao Mwigamba aliundika kwenu, najua wengine waliuchukulia kuwa ni mwito wa kawaida tu polisi kwa kuwa mhariri gazeti lililochapa makala yake hakuitwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, vyanzo vyangu ndani ya Jeshi la Polisi vimenieleza kuwa kesho asubuhi Mwigamba anatarajiwa kupelekwa mahakama ya Kisutu kushtakiwa kwa kosa la uchochezi. Taratibu Tanzania inaelekea kuwa dola ya kipolisi (police state), hali ambayo ikifikia itakuwa na athari kubwa kisiasa, kiuchumi na kijamii katika nchi yetu. &lt;br /&gt;Sina hakika kama wakuu wetu kwenye vyombo vya ulinzi na usalama wanayafanya haya kwa kwa maelekezo ya Rais kwa mujibu wa ibara ya 33 na 35 ya katiba au ni matakwa tu binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa vyovyote vile, Rais anapaswa kushauriwa: KAMATA KAMATA KWA ARI, NGUVU NA KASI ZAIDI (ANGUKA); Miaka 50 baada ya Uhuru, tumeanza kurudi katika zile zama za watu kukamatwa na kuwekwa kizuizini.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tofauti ya wakati huo na sasa ni kwamba sasa hukamatwi kwa kificho, wala huwekwi mafichoni; ni rahisi tu, polisi wanakukamata halafu wanakupeleka mahakamani. &lt;br /&gt;Wanajua baada ya hapo utakuwa tayari umepoteza sehemu ya uhuru wako, utapaswa kwenda mahakamani mara kwa mara. Kesi itachukua muda mrefu kwa polisi hao hao walikuona una kosa wakakupeleka mahakamani kutoa sababu kwamba ‘upelelezi haujakamilika’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kosa la Mwigamba linaelezwa kutokana na makala yake aliyoiandika “Waraka kwa Askari wa Tanzania”, anadaiwa kwamba kupitia makala hiyo amewachochea polisi kukaidi amri za viongozi wao na kuwachochea polisi kukataa kutimiza wajibu wao wa kisheria. Suala hili limenifanya noisome makala yake, na baada ya kuisoma naona sasa tunaelekea katika dola ya kipolisi (police state).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ari, Nguvu na Kasi hii ya Jeshi la Polisi kusoma, kufanya ufuatiliaji na kuchukua hatua dhidi ya ‘wahalifu’ ningeiunga mkono kama ingekuwepo toka wakati Orodha ya Mafisadi (List of Shame) iliposomwa 15 Septemba 2007 pale viwanja vya Mwembe Yanga na baadaye kusambazwa na vyombo vya habari na mitandao mbalimbali. Lakini mpaka leo Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Makosa ya Jinai (DCI) hakuna hatua za maana alizochukua lakini ana ari, nguvu na kasi zaidi ya kuwakamata na kuwahoji waandishi wa makala nyingine za magazetini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli ya kwamba si lazima kwa askari kufanya kile ambacho wakubwa wake wanamuamrisha kufanya hata kama anacholazimishwa ni kinyume cha sheria na kinyume cha maadili na haki na kwamba askari polisi watumie pia akili zao kufikiri Mwigamba sio wa kwanza kuiandika au kuisema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania inaelekea kuwa dola ya polisi, sio kwa baadhi ya wabunge na wapinzani tu bali hata kwa wananchi wengine na hata katika ya polisi wa juu dhidi ya polisi wa ngazi za chini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukio hili limenifanya nikumbuke mambo kadhaa dhidi ya jeshi letu ya polisi yaliyojiri katika mkutano wa nne wa Bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mosi; Wakati wa bunge la bajeti nilihoji kuhusu jeshi la polisi juu ya polisi kuwa na maslahi duni, Serikali ikasema bungeni kuwa posho zao (ration allowance) zimeongezwa mpaka laki unusu. Ukweli ni kwamba askari hawalipwi kiwango hicho cha posho, hata hivi sasa pamoja na ufafanuzi kuhusu mgawo wa posho za askari tulioomba bungeni tarehe 28 na 29 Julai 2011.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia kauli ya serikali bungeni askari wakaanza kuulizia kuhusu posho hizo na waliowaunganisha wenzao kuhoji wakaitwa ‘wachochezi’; wakuu wa vikosi na vituo wakapewa waraka wa ‘kufuta’ kauli hiyo ya serikali nje ya Bunge na kuchunguza askari wote wanaopandikiza ‘chuki’ kwa wenzao dhidi ya serikali kwa kutumia suala hilo la posho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Polisi maeneo mbalimbali nchini wakaelezwa kwamba vitendo vya kushawishi askari aliyekula kiapo cha utii kwa serikali kufanya hujuma kama hizo za kudai posho ambayo imeahidiwa bungeni ni hujuma kwa serikali hivyo ni UHAINI.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, kitabu kinachosambazwa na Jeshi la Polisi Mitaani na Vijijini cha “Utii wa Sheria bila Shuruti” ambacho kinaonyesha mwelekeo wa serikali kuanza kuandaa mazingira ya dola ya kipolisi (police state). Kitabu hicho chenye kueleza kuhusu “wajibu wa vyama na watu walioshindwa katika uchaguzi” kinawaasa watanzania dhidi ya wanasiasa na wanaharakati wenye kutumia ‘tabia ya kutumia shida na kero za wananchi kuchochea hasira, munkari na jazba dhidi ya viongozi halali’. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, kampeni ya “Utii wa Sheria bila Shuruti” inawakumbusha wananchi wajibu wa “Kuepuka kushiriki katika mikutano, maandamano na harakati za kuichokoza mamlaka ya dola, kwa uwasilishaji wa malalamiko au kero kwa njia ambazo zinasababisha bughudha na karaha kwa wengine”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitabu cha “Utii wa Sheria bila Shuruti” kinaeleza kwamba ‘Sheria inampa mamlaka afisa wa Polisi wa himaya inayohusika kusitisha maandamano, mkutano au mkusanyiko wowote endapo atabaini kwamba kuna habari au taarifa kwamba kuendelea kufanyika kwa mkutano kunaweza kusababisha uvunjaji wa amani na kuhatarisha usalama. Na kwamba endapo amri hiyo itaonekana kuupuuzwa kwa namna yoyote hata kama maandamano, mkutano au mkusanyiko ulikuwa ni halali utahesabika kuwa ni haramu. Hivyo hatua za kuwatawanya kwa njia ya shuruti itafuata ikiwemo kuwakamata waandaaji na washiriki na kuwafikisha mahakamani”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu hiki kilitumiwa kwenye Mkutano wangu na Wananchi tarehe 5 Novemba 2011 kwa kuvamia katika mkutano halali, kukata nyaya za vipaza sauti, kukamata viongozi waandaji na kuondoka nao pamoja na gari lenye nyaraka mbalimbali za katiba. Maelezo ambayo waliwaeleza awali viongozi hao ni kuwa mkutano haurusiwi kutokana na tishio la ugaidi wa Al Shabab. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipoelezwa nikawaambia viongozi waendelee na maandalizi ya mkutano kwa kuwa Rais hajatangaza hali ya hatari, kama kuna tishio la kawaida la vurugu polisi waje wamejiandaa kufanya kazi yao ya kulinda amani kama ambavyo walikuwa wamejiandaa kulinda mechi zingine za mpira zilizofanyika siku hiyo hiyo ya tarehe 5 Novemba na matembezi ya Mke wa Rais yaliyofanyika DSM wiki hiyo hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na viongozi kukamatwa na vipaza sauti kuchukuliwa kabla ya kufika uwanjani, nilipofika niliendelea kufanya mkutano wa kupata maoni ya wananchi kuhusu muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba na masuala mengine muhimu ya jimbo na taifa kwa ujumla kabla ya kwenda mkutano wa tano wa Bunge ulioanza tarehe 8 Novemba 2011. Nawashukuru askari walioacha kunikamata pamoja na maagizo waliyokuwa wamepewa ya kunikamata.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwanini nimeandika yote haya? Sababu ya Mwigamba kuitwa mchochezi ni kuwa amewaambia askari watumie akili zao wasikubali kutumwa kukamata na kupiga watanzania wenzao katika hatua za maandamano ya kupinga sheria ya mabadiliko ya katiba wakati njia za kidiplomasia kupitia mikutano za kutaka sheria hiyo ifanyiwe mabadiliko kabla ya kuanza kutumika zitakapopuuzwa na hatimaye kulazimika kuunganisha nguvu ya umma kupitia maandaamano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimeamua kutafakari kwa sauti wakina Mwigamba wengine mnisikie, kwamba tusipoungana kuwakanya viongozi wetu tunaelekea kuwa dola ya kipolisi na kwenye mchakato wa katiba dola hiyo (Mungu apishie mbali) inaweza kutumiwa na watawala kuvuruga utulivu wetu wa kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hiyo ni dola ya polisi wasiofikiri kabla ya kutenda; polisi wanaofikiri baada ya kutenda kwa kutumwa na watawala walioacha kufikiri na kujikita katika kutoa amri haramu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Akili zao zinadhihirika kwenye kauli zao na za wataalamu wao mathalani kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali bungeni wakati wa kuhalalisha kifungu kwenye sheria ya Mabadiliko ya Katiba chenye kutoa adhabu ya faini isiyopungua milioni tano na isiyozidi milioni kumi na tano au kifungo kwa muda usiopungua miaka mitatu na isiyozidi miaka saba au adhabu zote mbili kwa kwenda kinyume cha sheria hiyo.&lt;br /&gt;Makosa yenyewe ya hukumu hiyo ni pamoja na ‘kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi’ na ‘kuendesha elimu ya mabadiliko ya katiba kinyume na masharti ya sheria’ hiyo. Makosa ya kukusanya maoni na kutoa elimu sasa yametengewa hukumu kubwa kuliko ya mafisadi na ambao wameisababishia hasara serikali. Huo ndio “Utii wa Sheria bila Shuruti” wanaoutaka kwa watanzania. Kwa maneno ya Werema bungeni kuhalalisha kifungu husika “matatizo tuliyonayo sasa ambayo yanasababishwa na watu ambao hawataki kufuata utaratibu kwa mambo ya siasa, inatakiwa kutoa elimu ya kisiasa katika jambo hili la katiba kwamba wapewe adhabu kali; ndiyo maana yake”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawaandikia kuwaomba mjiandae iwe ni wanahabari, wanaharakati, wanasiasa, viongozi wa dini, wanataaluma au wananchi wa kawaida; kuwa mkiwa na mawazo tofauti kuhusu katiba na polisi hawa wa “Utii wa Sheria bila Shuruti” wakaagizwa kuwakamata kwa kutoa elimu ama kukusanya maoni kinyume cha sheria adhabu yenu itakuwa kifungo cha hadi miaka saba au faini ya hadi milioni 15 au vyote. Na polisi jiandae, huu ni wakati wa pekee katika historia taifa letu; miaka 50 baada ya Uhuru wa Tanganyika, muwafunge wananchi wenzenu wanaodai uhuru wa kweli dhidi ya ujinga, umasikini, maradhi na ufisadi kwa kudaiwa na serikali ya mkoloni kuwa ni wachochezi kama alivyofanyiwa Mwalimu Nyerere na TANU au msimame upande wa haki na ukweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na hili halihusu tu maslahi ya taifa ambayo tunawaomba askari myasimamie popte pale mlipo, inahusu pia kusimamia maslahi yenu wenyewe. Wakiitisha mabaraza ya askari, wakiwaambia polisi kwamba mnapaswa kuendelea kulipwa ration allowance ya laki moja tu, kwa mujibu wa waraka wa idara kuu ya utumishi wa tarehe 26 May 2009 wenye kumb. Na. C/AB.129/271/01/E41 waambieni waje watuambia sisi bungeni kwa kuwa walitoa kauli kuwa mnalipwa laki na hamsini; waje waje wafute kauli bungeni tujadili msingi wa wao kukataa kuwalipa haki yenu hiyo kwa mwezi, wakati ni pungufu ya posho iliyoongezwa kinyemela ya mbunge ya siku moja pekee ya kukaa kwenye kikao (sitting allowance).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkitumwa kwenye kufanya operesheni haramu na kulipwa viwango duni vya posho kwa kuwapiga watanzania wenzenu kwa maelezo kuwa waraka mwingine wa tarehe 27 Januari 2009 wenye kumb. Na. C/BC. 129/271/01/18 umewaongezea posho kwa 15% waulizeni mbona serikali imeongeza posho haramu kwa wabunge ya kukaa kwenye vikao kwa zaidi ya 150%.&lt;br /&gt;Wakiendelea kuwalipa mishahara midogo huku kima cha chini kikiwa kimeongezeka toka 219,170 mpaka 243,000 tu sawa na ongezeko la 10% huku bei za bidhaa na gharama za maisha zimeongezeka kwa zaidi ya 100% waulizeni uhuru na usawa tulioupigania miaka 50 uko wapi?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Najua wanaendelea kuwaeleza mkiwa kwenye maandalizi ya gwaride la sherehe za uhuru kuwa muendelee kuwa na ‘utii na uvumilivu kwa kuwa serikali haina uwezo’ na kwamba nyongeza hiyo ndogo kupitia waraka wa tarehe 13 Julai 2011 wenye kumbukumbu na. CAC/205/228/01/A/41 imetokana na hali halisi ya uchumi wetu. Muwakumbushe kiwango cha fedha ambacho kinakaribia kufika bilioni 50 kinachotumika kwenye ‘sherehe’ za miaka 50 ya uhuru toka maandalizi yake yaanze mpaka mwisho huku mkiidai serikali malimbikizo ya madeni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali yenu ni sawa na ya walimu, watumishi wa sekta ya afya na kada nyingine za chini katika utumishi wa umma ambapo mtajumuika kwa ‘utii wa bila shuruti’ katika halaiki ya 9 Disemba ‘kusherehekea uhuru’. Hampaswi kugoma kwa kuwa kazi yenu ni wito, lakini msiache kuwafikishia ujumbe watawala; msikubali kutumiwa kuminya haki zenu wenyewe na za wenzenu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tekelezeni amri zote halali za ulinzi na usalama wa taifa letu, wakatalieni amri zote haramu zenye kuvunja sheria, kuvuruga amani na kukiuka haki za msingi za binadamu. Tenganisheni kati ya kusimamia maslahi ya taifa na kulinda matakwa ya mafisadi; tambueni kuna amri za watawala kudumisha utawala wao na kuna amri za viongozi kusimamia mahitaji ya umma. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watawala wameapa kulinda katiba, ambayo ibara ya 8 (a) inatamka wananchi ndio msingi wa mamlaka yote na serikali itapata madaraka kwa wananchi; ibara ya 9 inawataka wao na serikali wanayoongoza kulinda haki za binadamu, kuendeleza utajiri wa taifa kwa manufaa ya wananchi wote, kuhakikisha serikali na vyombo vyake vyote vinatoa nafasi sawa kwa raia wote bila ubaguzi na kwamba aina zote za dhulma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini. Waambieni wakumbuke kiapo chao, na wasiwalazimishe nyinyi kutii amri zinazokiuka kiapo chao wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msiwaogope wao kuliko wananchi wanaowalipa mishahara yenu kwa kodi zao na ndugu zenu mnaishi nao katika mazingira yenu ya ugumu wa maisha. Kama hamuwaogopi wananchi wenzenu basi walau muogopeni Mwenyezi Mungu anayetaka muenende kwa upendo, haki na ukweli. Sheria kuu kuliko zote ya kuitii sio ya Tanzania; bali ya nafsi zenu na Mungu wetu. Msiwatii wanapowataka mtende dhambi. Kwa maneno ya Mahatma Ghandi, ‘kuweni mawakala wa mabadiliko mnayotaka kuyaona’”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama nilivyoandika miaka michache iliyopita wakati mwanahabari wa gazeti la Mwanahalisi Saed Kubenea aliposhambuliwa; shambulizi dhidi ya mwanahabari ni chambulizi dhidi ya ‘uhuru wa habari’. Hivyo, kamata kamata dhidi ya watoa maoni, ni kamata kamata juu ya ‘uhuru wa kutoa maoni’. Tukio hili lipaswa kuwa chachu ya kuendelea kutoa maoni na kudai uhuru wa kutoa maoni ikiwemo uliopokwa kwenye Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011. Kesi hii ni muhimu kwa taifa kuhusu haki ya msingi ya kibinadamu na kuwasiliana na kutoa maoni, hivyo tuifuatilie kwa karibu mwenendo wake. Aidha, ni wakati sasa wa kuunganisha nguvu ya umma kudhibiti nchi yetu kugeuzwa ‘dola ya kipolisi’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-8307684967421650847?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/8307684967421650847/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=8307684967421650847' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8307684967421650847'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8307684967421650847'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/mwigamba-apata-dhamana-tuepuke-dola-ya.html' title='Mwigamba apata dhamana; tuepuke dola ya kipolisi'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-3067147667937503171</id><published>2011-12-14T03:52:00.000-08:00</published><updated>2011-12-14T03:54:08.814-08:00</updated><title type='text'>Utekelezaji wa Mpango wa Dharura wa Umeme</title><content type='html'>Tarehe 8 Disemba 2011 Wizara ya Nishati na Madini imetoa Taarifa kwa Umma kuhusu Maendeleo ya Sekta ya Nishati na Madini. Tunaendelea kuipitia taarifa husika na tutatoa taarifa mbadala kwa umma kama sehemu ya wajibu wa kikatiba wa kuishauri na kuisamia serikali. Hata hivyo, nimeshangazwa na ukimya wa serikali mpaka hivi sasa kuhusu haja ya kutoa kwa taarifa kwa umma kuhusu utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme na maendeleo ya sekta ya nishati ambayo inakabiliwa na changamoto nyingi kwa sasa zenye kuathiri uchumi wa nchi na maisha ya wananchi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuanzia mkutano wa tano wa bunge ulionza tarehe 8 Novemba 2011 ilitarajiwa kwamba serikali ingetoa taarifa bungeni kwa mujibu wa ibara ya 63 (2) na (3) ya katiba kuhusu mpango wa dharura wa umeme na maendeleo ya sekta ya nishati; hata hivyo suala hilo halikuingizwa kwenye ratiba ya bunge. Baada ya taarifa kutokutolewa bungeni nilitarajia serikali ingetoa taarifa kwa umma lakini mpaka sasa Wizara ya Nishati na Madini haijatoa taarifa husika hivyo natoa mwito kwa Waziri husika kutoa taarifa kwa umma kuhusu hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mpango wa dharura wa umema na maendeleo ya sekta ya nishati kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mpango wa Dharura uliwasilishwa bungeni tarehe 13 Agosti 2011, ahadi ya serikali ilikuwa kuongeza MW 572 ifikapo mwezi Disemba 2011. Kati ya hizo, MW 150 ilikuwa zizalishwe kupitia makubaliano baina ya Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na TANESCO; ilitarajiwa kuzalishwe MW 50 Septemba, MW 50 Oktoba na MW 50 Novemba 2011.&lt;br /&gt;Kimsingi kauli iliyotolewa bungeni kuwa mitambo ilikuwa imepatikana haikuwa ya kweli hivyo ahadi ya kupata umeme huo ilikuwa hewa. Mpaka sasa hakuna hata MW moja ambayo imezalishwa kwa ushirikiano kati ya NSSF na TANESCO. Ujumbe ulipotumwa Marekani kwenda kuona mitambo iliyokuwa inaelezwa kwamba ipo haikukuta mitambo yoyote, walikuta kampuni ambayo haikuwa na uwezo kama ilivyokuwa kwa Richmond Development LLC; timu hiyo ya wataalamu ilibidi kwenda Ufaransa nako ikakosa mitambo ya dharura. Hivyo, fedha nyingi za umma zimetumika kufuatilia ahadi hewa na umeme mpaka sasa haujapatikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba mpango mwingine wa muda mfupi ulioelezwa bungeni tarehe 13 Agosti 2011 ni mradi wa kununua mitambo ya  MW 100 wa Jacobsen wa gesi asili ambao awali ulikuwa ukamilike 2009/2010 lakini kutokana uzembe ndani ya serikali mradi huo haukukamilika mpaka mwaka 2011. Kuchelewa kwa kununuliwa na kufungwa kwa mitambo hii ambayo ilikuwa ifungwe Ubungo ndiko kuliongeza makali ya mgawo wa umeme kuanzia mwishoni mwa 2010 mpaka mwanzoni mwa mwaka 2011. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kuchelewa kwa mradi huu serikali ikakubaliana na mkandarasi kuwa mradi huo ukamilike Juni 2012. Kutokana na ahadi ya MW 150 za dharura toka NSSF kuthibitika kuwa ni hewa, serikali ikarudi tena mezani kufanya majadiliano na mkandarasi wa mradi wa Jacobsen ili kuharakisha utekelezaji uzinduliwe mwezi Disemba 2011 wakati wa ‘sherehe’ za uhuru. Hata hivyo, wataalamu hawakumueleza tena ukweli Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa matarajio waliyompa ya kuzindua mradi huo wakati wa sherehe za uhuru nayo yamethibitika kuwa hewa kwa kuwa sherehe zimepita bila umeme wa nyongeza. Kutokana na hali hii, Rais Kikwete alilazimika kurudia mara kwa mara kwamba asingetoa hotuba ndefu uwanja wa taifa kwenye maadhimisho tarehe 9 Disemba katika siku ambayo wananchi walitarajia mkuu wa nchi azungumze masuala makubwa ya kitaifa ikiwemo suala la umeme na sekta ya nishati wa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine, udhaifu wa kutokutekeleza mipango ya uzalishaji wa gesi na makaa ya mawe kwa wakati umesababisha utegemezi mkubwa kwenye matumizi ya mafuta katika mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura. Zaidi ya nusu ya umeme unaozalishwa nchini hivi sasa ambao ni sawa na takribani MW 660 unazalishwa kwa kutumia dizeli, mafuta ya ndege na mafuta mazito hali ambayo imeongeza mahitaji makubwa ya uagizaji wa mafuta toka nje ya nchi. Hii imesababisha mahitaji makubwa ya fedha za kigeni kwa ajili ya kuagiza mafuta na hivyo kuchangia katika kuporomoka kwa thamani ya shilingi. Aidha, ongezeko kubwa la uagizaji toka nje limeathiri urari wa biashara na hivyo kuchangia katika mfumuko wa bei ambao hivi sasa umefikia zaidi ya asilimia 16. Hivyo, watanzania hivi sasa wanabeba mzigo wa kupanda kwa bei za bidhaa na gharama za maisha kwa ujumla kutokana na ufisadi kwenye mikataba, ubadhirifu katika matumizi, uzembe katika uongozi na upungufu katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya serikali kwenye sekta ya nishati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuwa ahadi za mpango wa dharura bado hazijatekelezwa kwa ukamilifu wake serikali inaendelea kutumia zaidi ya bilioni 2 kila siku kama gharama za mafuta ya kuzalishia umeme suala ambalo linahitaji kufanyiwa uchunguzi wa kina kuhusu vyanzo vya fedha hizo na uhalali wa matumizi ya miradi ya Aggreko International, Symbion Power LLC na IPTL.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilionya bungeni kuhusu gharama kubwa za mpango wa dharura wa umeme na kupendekeza vyanzo mbadala vya fedha ambavyo serikali ilivipuuza. Uamuzi wa kukopa katika mabenki ya biashara kwa ajili ya kugharamia mpango wa dharura wa umeme tayari umeshaanza kuathiri Shirika la Umeme (TANESCO), serikali na utaathiri maisha ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba tarehe 15 Julai 2011 nilieleza bungeni vyanzo mbadala vya kuongeza fedha katika bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini bila kuathiri kwa kiwango kikubwa maisha ya wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla. Tarehe 18 Julai 2011 Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikubaliana na mapendekezo yetu na hivyo wakati anatoa hoja ya kuahirisha majumuisho ya mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini akaahidi kwenda kukata fedha kwenye posho na matumizi mengine yasiyokuwa ya lazima katika bajeti ya serikali ili kuelekeza fedha kwenye mradi wa dharura wa umeme.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, tarehe 13 Agosti 2011 Serikali ikageuka na kuleta mpango wa dharura tofauti ambao ulijikita katika serikali kuidhamini TANESCO kwenda kukopa kwenye mabenki ya kibiashara zaidi ya bilioni 400. Siku hiyo nilirudia kumsomea Waziri Mkuu kumbukumbu ya Bunge (Hansard) ya ahadi yake ya tarehe 18 Julai 2011 ambayo haikuitimiza, inaelekea serikali ilitoa ahadi hewa ndio maana haikutaka kabisa kubadili msimamo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo ya hali hiyo ni hivi sasa serikali kutafuta namna ya kuinusuru TANESCO kwa kubebesha mzigo mkubwa wananchi kwa kuwa hivi karibuni imewasilisha ombi la kupandisha bei ya umeme kwa wastani wa 155% (zaidi ya mara tatu) ya bei ya sasa. Ombi hili likikubaliwa kwa ukamilifu wake litakuwa na athari kubwa sana katika uchumi wa nchi na maisha ya wananchi. Ikumbukwe kwamba Januari 2011 umeme ulipanda bei kwa 18.5% tu lakini kupanda huko kulisababisha mfumuko wa bei, sasa watanzania wajiulize itakuwaje ukipanda kwa 185%. Hata hivyo, ni vigumu kwa EWURA kukubali kupandisha bei kwa kiwango hicho kwa kuwa ikumbukwe kwamba Disemba 2010 TANESCO iliomba kupandisha bei kwa zaidi ya 30% lakini haikukabaliwa. Kukataliwa kupandisha kwa bei kubwa kutaiweka TANESCO njia panda kwa kuwa tayari imeshakopa kwa gharama kubwa katika mabenki ya biashara na pia gharama za uendeshaji wa TANESCO zipo juu kutokana na ufisadi katika mikataba mbalimbali na pia kutokana na madeni makubwa ambayo TANESCO inadai kwa serikali na wateja wengine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, upo uwezekano wa mikopo kushinda kulipwa kwa wakati na TANESCO na madeni kurudi kwa umma kupitia kwa dhamana za serikali. Katika hali hii hatua za haraka zinapaswa kuchukuliwa na Wizara ya Nishati na Madini kutoa taarifa ya kina ya hali halisi ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme na maendeleo ya sekta ya nishati ili kudhibiti mianya ya uchelewaji na ubadhirifu ambayo imeanza kujitokeza kwa kuzingatia pia mapendekezo ambayo tuliyatoa bungeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Waziri Kivuli wa Nishati na Madini&lt;br /&gt;14/12/2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-3067147667937503171?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/3067147667937503171/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=3067147667937503171' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3067147667937503171'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3067147667937503171'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/utekelezaji-wa-mpango-wa-dharura-wa.html' title='Utekelezaji wa Mpango wa Dharura wa Umeme'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-4869661114353417744</id><published>2011-12-13T02:02:00.000-08:00</published><updated>2011-12-13T02:05:53.668-08:00</updated><title type='text'>Kuhusu migogoro ya UDSM, UDOM na MUHAS</title><content type='html'>Kwa mujibu wa ibara ya 63 (2) na (3) mamlaka ya bunge ni kutunga sheria na kusimamia serikali. Kutokana na mamlaka hayo kazi za mbunge ni kuwakilisha wananchi, kushiriki katika kutunga sheria pamoja na kuisimamia serikali na viongozi wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr Shukuru Kawambwa aliahidi bungeni kwenye mkutano wa nne kwamba serikali imepata mkakati wa kumaliza migogoro na matatizo katika vyuo vikuu nchini na kwamba hatua za haraka zingechukuliwa kama sehemu ya utekelezaji wa bajeti ya serikali kwa mwaka 2012/12.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, badala ya migomo na migogoro kumalizika inaelekea kuongezeka. Katika siku za karibuni pamekuwepo na maandamano ya mara kwa mara katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS). Aidha, hali ya mambo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) haijatulia mpaka sasa, huku wanafunzi 567 wakiwa bado wamesimamishwa. Katika kipindi cha mwezi mmoja imekuwa ikijirudia rudia hali ya mvutano baina ya wanafunzi na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali katika vyuo vikuu hivi na vingine haiendani na ahadi ambayo Waziri Kawambwa alizitoa bungeni na kwa umma miezi kadhaa iliyopita. Leo nimeingia ofisini jimboni na kukatizwa kazi za kufuatilia masuala mengine ya wananchi na habari za mgomo katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam Mlimani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kuwa bado sijapokea taarifa rasmi ya toka kwa Utawala wa Chuo au kwa Serikali ya Wanafunzi (DARUSO); wakati nikifuatilia taarifa zaidi nimeona nichukue hatua za kiutendaji za kuwasiliana na wizara yenye dhamana ili waweze kuingilia kati kama sehemu ya kutimiza ahadi iliyotolewa bungeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kukabiliana  migomo na migogoro katika elimu ya juu serikali imekuwa ikichukua hatua dhidi ya matokeo badala ya kushughulikia vyanzo vya matatizo hivyo natarajia wakati huu Waziri husika atajielekeza katika madai ya msingi ya wanafunzi na wahadhiri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali izingatie kwamba chimbuko la mgogoro wa MUHAS ni tofauti katika utekelezaji wa agizo la serikali la tarehe 12 Juni 2009 (GN. 178)  ambayo limefanya mabadiliko ya makubwa kwenye uendeshaji wa serikali za wanafunzi katika vyuo vikuu na hivyo kuanzisha mivutano baina ya wanafunzi na utawala katika chuo hicho na vyuo vingine nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali irejee kwamba chanzo cha migomo UDOM ni madai ya wanafunzi kuhusu mafunzo kwa vitendo na malalamiko mengine kutoka kwa wahadhiri. Toka wanafunzi wasimamishwe mwezi Juni 2011 mpaka sasa ikiwa imepita karibu miezi sita wanafunzi 567 bado wamesimamishwa masomo huku zoezi la kumhoji mmoja mmoja likisuasua na kutarajiwa likiwa limepangwa kumalizika mwishoni mwa Mwezi Machi mwaka 2011. Serikali inaweza kabisa kwa kushirikiana na chuo kuharakisha taratibu za kinidhamu wakati huo huo kushughulikia madai ya msingi ya wanafunzi ili kuepusha mazingira ya mivutano kudumu kwa muda mrefu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali itambue kwamba chanzo cha migomo ya hivi karibuni UDSM ni kugeuzwa kwa taratibu za utoaji mikopo na hatimaye kuchelewa kwa malipo ya wanafunzi na wengine kupata pungufu au kukosa kabisa. Katika mazingira hayo ni muhimu kwa Waziri Kawambwa kuweka wazi kwa umma ripoti ya Tume ya Rais iliyoundwa tarehe 14 Februari 2011 na kukabidhi taarifa yake tarehe 29 Aprili yenye mapendekezo ya jinsi ya kuboresha utaratibu wa sasa wa ugharamiaji, utoaji na urejeshaji wa mikopo ya elimu ya juu.&lt;br /&gt;Kuwekwa wazi kwa taarifa hii kutawezesha wawakilishi wa wananchi, wanafunzi, wazazi, vyuo vikuu na wadau wengine wote kuunganisha nguvu katika kushughulikia matatizo yanayoendelea kujitokeza katika elimu ya juu hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba Rais Jakaya Kikwete aliahidi mwaka 2007 kuyapatia ufumbuzi matatizo ya wanafunzi wa elimu juu nchini ili kupunguza migomo na migogoro. Katika Mkutano wake na wanafunzi wa vyuo vikuu mwezi Februari 2007 alikwenda mbali zaidi kwa kuwaeleza kwamba hakuna mtoto wa maskini atayeshindwa kuendelea na masomo kutokana na masharti ya mikopo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka mitano imepita toka ahadi hizo zitolewe migomo katika vyuo vikuu inaendelea na pia wapo watoto wa walalahoi ambao wamefaulu kidato cha sita lakini wemeshindwa kuendelea na masomo kutokana na kukosa mikopo; hivyo Waziri asipochukua hatua za haraka itadhihirika kwamba ahadi za serikali zimekuwa za ‘kiini macho’.&lt;br /&gt;  &lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;13/12/2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-4869661114353417744?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/4869661114353417744/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=4869661114353417744' title='7 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4869661114353417744'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4869661114353417744'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/kuhusu-migogoro-ya-udsm-udom-na-muhas.html' title='Kuhusu migogoro ya UDSM, UDOM na MUHAS'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>7</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-103146719570186215</id><published>2011-12-11T02:20:00.000-08:00</published><updated>2011-12-11T02:23:27.993-08:00</updated><title type='text'>Waziri Mkuu aeleze ufujaji wa sherehe za Uhuru</title><content type='html'>Vyombo mbalimbali vya habari vya leo tarehe 11 Disemba 2011 vimeeleza kwamba kesho tarehe 12 Novemba 2011 Waziri Mkuu Mizengo atakuwa mgeni rasmi katika shughuli maalumu ya kufunga Wiki ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru itakayofanyika kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa Mkoani Dar es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa makadirio ya vyanzo mbalimbali kiwango cha fedha kilichotumiwa mwaka huu kwa ajili ya ‘sherehe’ za miaka 50 ya uhuru kinazidi bilioni 50; hivyo natarajia kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ndiye mwenyekiti wa maandalizi ya maadhimisho hayo atatumia shughuli hiyo ya kufunga kueleza pia kiwango halisi cha fedha ambacho kimetumiwa hivi sasa na Serikali kupitia Wizara na taasisi zake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Toka wakati wa bunge la bajeti nimekuwa nikisikitishwa na kiwango kikubwa cha fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya ‘sherehe’ za uhuru katika bajeti za Wizara mbalimbali huku kukiwa na upungufu wa fedha za miradi ya maendeleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gharama za maisha kwa wananchi ziko juu na uchumi wa nchi uko kwenye hali tete kwa sababu ya pamoja na mambo mengine mfumuko wa bei na kuporomoka kwa shilingi. Hali hii inachangiwa pia na ubadhirifu na matumizi ya anasa ya fedha za umma ambapo ‘sherehe’ hizi ni sehemu za matumizi hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa bunge la bajeti nilipiga kura ya HAPANA ya kukataa bajeti ambayo ilitenga fedha nyingi kwenye posho za vikao na matumizi mengine yasiyokuwa ya lazima huku mipango mingine muhimu ya maendeleo mathalani ya kuwezesha jiji la Dar es salaam kupata maji, ujenzi wa barabara za pembezoni kwa ajili ya kupunguza foleni, malipo ya madeni ya walimu, askari na watumishi wa umma pamoja na mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ikiwa haijatengewa fedha za kutosha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majibu ya serikali wakati wote yamekuwa ni kwamba hakuna fedha za kutosha sasa ni muhimu Waziri Mkuu Pinda  watanzania mabilioni ya ‘sherehe’ hizo yametoka wapi; kwa kuwa kiwango cha matumizi yaliyofanyika kinaonyesha kuwa juu hata ya kile ambacho kimekuwepo kwenye bajeti iliyopitishwa bungeni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiwango hicho cha fedha kingeweza kugharamia masuala yafuatayo ambayo yangefanyika katika kipindi cha mwaka mmoja maadhimisho ya uhuru yangekuwa na maana zaidi kwa sababu tarehe 9 Disemba 1961 Mwalimu Nyerere akihutubia taifa alieleza kuwa ‘uhuru ni kazi’ wala hakusema ‘uhuru ni sherehe’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru yangekuwa na maana kama yangeacha kumbukumbu ya mwaka 2011 kwa kulipa madeni yote ya walimu, askari na watumishi wengine wa umma; pamoja na kuelekeza fedha hizo kwenye miradi iliyotengewa fedha kidogo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mathalani ujenzi wa barabara za pembezoni za kupunguza foleni Dar es salaam umetengewa bilioni tano tu, ujenzi wa bwawa la maji la Kidunda umetengewa bilioni sita, na kuna watoto wa maskini ambao wamekosa mikopo na kushindwa kuendelea na elimu tofauti na ahadi ya Kikwete; fedha hizi zingetosha kufanya matumizi haya yote na mengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha katika kufunga maonyesho hayo Waziri Mkuu Pinda afafanue pia sababu za maonyeshoya Wizara na Taasisi mbalimbali kufanyika zaidi mkoani Dar es salaam kama vile miaka 50 ya Uhuru ilikuwa kwa ajili ya watu wa Dar es salaam pekee. Fedha hizi za umma zingekuwa na maana kama zingetumiwa kuzunguka nchi nzima kuhamasisha maendeleo mitaani na vijijini ili kusonga mbele kama taifa kwa kuwa mafanikio ya miaka 50 ya Uhuru yanapaswa kujionyesha yenyewe katika maisha ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati Wizara na Taasisi hizo zikiwa zinatumiwa fedha nyingi kufanya maonyesho kwa gharama za posho, machapisho na matumizi mengine yasiyokuwa na lazima; watumishi wa umma wako kwenye hali mbaya na mishahara katika taasisi zao imekuwa ikicheleweshwa. Hivyo, pamoja na kufunga maonyesho Waziri Mkuu Pinda anapaswa kufuatilia  kwa kina matumizi ya wizara zote na taasisi zote zinazowahusu ili kuwa na uwajibikaji kutokana na matumizi haya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Izingatiwe kwamba matumizi haya yamehusisha pia matumizi ya mara nyingi ya fedha za umma kwenye masuala yale yale ya maonyesho kwa kuwa toka mwaka huu uanze Wizara na Taasisi zimekuwa zikifanya maonyesho yao kila moja pekee na kutumia fedha za umma. Wizara na Taasisi hizo hizo nyingi zikashiriki tena maonyesho ya Saba Saba na Wizara na Taasisi hizo hizo zimerudia tena kushiriki maonyesho ya Uhuru katika viwanja hivyo hivyo; katika mkoa huu huu mmoja wa Dar es salaam. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haya yanafanyika wakati wakina mama wajawazito na wagonjwa wengine wanafariki katika Hospitali ya Mwananyamala, Temeke, Amana, Muhimbili na Ocean Road kwa ajili ya kukosa madawa na huduma nyingine za msingi miaka 50 baada ya uhuru; haya yanafanyika wakati bado kuna shule nyingi za msingi na sekondari katika Mkoa huu huu wa Dar es salaam ambazo hazina vifaa muhimu ikiwemo madawati miaka 50 ya Uhuru.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, ili kushughulikia mianya ya ufujaji na ubadhirifu kutokana na maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru ni kamati ya maandalizi iliyoongozwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda itoe taarifa ya mapato na matumizi. Aidha,  Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) aingize kipengele maalum cha matumizi ya fedha za ‘sherehe’ za uhuru katika ukaguzi wake wa kila Wizara, Taasisi za Umma , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa katika ukaguzi wa Matumizi ya fedha za mwaka wa fedha 2011/2012.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika  (Mb)&lt;br /&gt;11/12/2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-103146719570186215?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/103146719570186215/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=103146719570186215' title='4 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/103146719570186215'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/103146719570186215'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/waziri-mkuu-aeleze-ufujaji-wa-sherehe.html' title='Waziri Mkuu aeleze ufujaji wa sherehe za Uhuru'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>4</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-6204777735030847262</id><published>2011-12-07T03:29:00.000-08:00</published><updated>2011-12-07T03:37:25.507-08:00</updated><title type='text'>Msimamo wangu juu ya suala zima la Posho!</title><content type='html'>Kufuatia habari tarehe 28 Novemba kuhusu ‘kupanda kimya kimya kwa posho za wabunge kwa zaidi ya asilimia 150’ tarehe 29 Novemba 2011 nilitoa kauli yangu kama mbunge na katibu wa wabunge wa CHADEMA kuhusu suala husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kauli hiyo nilieleza kuwa: “ Wabunge wa CHADEMA hatujapokea taarifa rasmi kwamba masharti ya kazi ya ubunge yamebadilika na kwamba viwango vya posho vimeongezwa. Wala kamati ya wabunge wa CHADEMA haijawahi kuridhia ongezeko lolote la posho ya vikao (sitting allowance) kwa wabunge. Napenda kutumia fursa kusisitiza msimamo wetu wa kutaka posho za vikao (sitting allowance) ziweze kufutwa kwa wabunge na katika mfumo mzima wa malipo ya wakati wa kazi miongoni mwa watumishi wa umma”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, kama mbunge na katibu wa wabunge wa CHADEMA nilitoa  mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kwa niaba ya Serikali na Spika Anna Makinda kwa niaba ya Bunge kutoa kauli kuhusu suala hili ili kuondoa hisia zinazojengeka kwamba ‘wabunge wote tumekaa bungeni na kukubaliana kujiongezea posho ya vikao’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia Spika Makinda kutoa kauli na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari tarehe leo tarehe 7 Novemba 2011 naomba kutoa msimamo wangu kama ifuatavyo:&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;“ Ongezeko la posho ya vikao lilofanyika linapaswa kusitishwa kwa kuwa limefanyika kinyume na taratibu na pia halina uhalali wowote kimantiki na halijazingatia uhalisia wa maisha ya wananchi na uchumi wa nchi kwa ujumla; nyongeza hiyo ya posho ya vikao ni haramu (Illegitimate).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bado narudia kutoa mwito kwa Rais Kikwete kutoa kauli wake na wa Ikulu na Ofisi ya Rais kwa ujumla unaacha ombwe lenye athari kubwa kwa serikali na kwa bunge mbele ya wananchi ambao kwa mujibu wa katiba ibara ya nane ndio wenye mamlaka na madaraka.&lt;br /&gt;Aidha, kauli ya Spika Makinda kwamba nyongeza hiyo ya posho za vikao ni kwa sababu ya kupanda kwa gharama za maisha mkoani Dodoma haina ukweli, wala mantiki na ina mwelekeo wa upendeleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyongeza hiyo ya posho ya vikao ni matumizi mabaya ya madaraka na ni dharau kwa walipa kodi wanaohangaika na kupanda kwa gharama za maisha na athari za ubadhirifu wa fedha za umma. Ni udhaifu kufikiri kwamba suluhisho la kupanda kwa gharama za maisha ni kuongeza posho za kikao; tatizo la kupanda kwa gharama za maisha linapaswa kushughulikiwa kwa kuchukua hatua dhidi ya matatizo ya kiuchumi katika nchi ili kuweza kuwa na tija kwa wananchi wengi ambao ni waathirika zaidi wa kupanda kwa gharama za maisha kuliko wabunge. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia, utetezi wa Spika Makinda kuhalalisha upandishaji wa kinyemela wa posho za vikao kwa wabunge haina maana kuwa kama sababu ingekuwa chanzo ni kupanda kwa gharama maisha ingepandishwa posho ya kujikimu (subsistence allowance) ambayo imebaki pale pale 80,000 . &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha kufuatia kauli ya Spika Makinda, hatua za kinidhamu zinapaswa zichukuliwe na Rais Kikwete dhidi ya Katibu wa Bunge Dr Thomas Kashilillah ya kutoa taarifa potofu kwa umma kwa kukanusha kwamba ofisi ya bunge haijaongeza posho kwa wabunge na pia kwa kufanya malipo kinyume na taratibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kugongana kwa kauli baina ya Spika na Katibu wa Bunge ni ishara ya kuwepo kwa jambo ambalo linafichwa kuhusu suala hilo la nyongeza haramu ya posho za vikao kwa wabunge na pia ni ushahidi wa taratibu kukiukwa hali ambayo inahitaji kauli kutoka kwa mwenye mamlaka kwa mujibu wa sheria kuhusu masuala ya posho za wabunge ambaye ni Rais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia, katibu wa wabunge anapaswa kutuomba radhi wabunge kwa kauli yake kwamba mabadiliko ya posho za vikao yametokana na mkutano wa wabunge tarehe 8 Novemba 2011 kuiomba serikali ipandishe posho hizo za vikao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Binafsi nilikuwepo kwenye mkutano huo wa tarehe 8 Novemba 2011 na hakuna uamuzi wowote ambao ulifikiwa wa kuiomba serikali ipandishe posho za vikao. Kilichotokea ni kwamba katika kuchangia maelezo ya serikali na ya bunge kuhusu masuala mbalimbali ya bunge na serikali yaliyojiri baada ya mkutano wa nne wa Bunge na mpangilio wa mkutano wa tano wa bunge, wabunge walipewa fursa ya kujadili taarifa hizo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kujadili taarifa hizo wapo wabunge wachache waliotoka nje ya hoja za msingi na kuzungumzia kuhusu nyongeza ya posho ya vikao; hata hivyo mkutano huo wa wabunge haukufanya maamuzi yoyote na wala haukukamilika. Kabla ya majina yetu wengine kufikiwa kuweza kuchangia Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye kwa nafasi yake ya kiongozi wa shughuli za serikali bungeni ni mwenyekiti wa mikutano ya wabunge alieleza kwamba muda umemalizika hivyo mkutano na kwamba tarehe nyingine ingepangwa kwa ajili ya kuendelea kujadili masuala mbalimbali yaliyohojiwa na pia kuweza kutoa fursa kwa wabunge wengine kuweza kutoa maoni yao kuhusu masuala hayo.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Katika hatua hiyo Waziri Mkuu Pinda alisoma majina yetu na kueleza kwamba mkutano huo wa wabunge ungeendelea katika tarehe nyingine lakini haukufanyika mkutano mwingine; hivyo katika mkutano wa tano wa bunge uliomalizika wabunge ambao mimi nilishiriki wabunge wote hatujawahi kukaa na kujipangia nyongeza ya posho za vikao kama inavyoelezwa hivi sasa wala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia, wabunge hatujawahi kupatiwa nakala ya muktasari au kumbukumbu wa vikao vya kamati ya uongozi au vya tume ya bunge ambavyo vimekaa na kupitisha nyongeza ya posho ya vikao kutoka 70,000 mpaka 200,000 kama Spika alivyonukuliwa na vyombo vya habari. Ni muhimu watanzania wakazingatia kwamba mwenye mamlaka ya kupandisha posho za wabunge ni Rais na natoa mwito kwa Rais kukataa kupandisha posho za vikao kwa wabunge na badala yake azifute kabisa. Watumishi wote wa umma ikiwemo wabunge hatustahili kulipwa posho za kukaa kwenye vikao vyetu ambavyo mwisho wa mwezi tunalipwa mshahara kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia hali hii, kwa kuwa sasa imeshatoka kauli rasmi ya bunge yenye kudhihirisha kwamba posho za vikao zimepandishwa kinyemela badala ya kufutwa kama tulivyotaka awali; tutaitisha kikao cha wabunge wa CHADEMA ili kukabaliana hatua za ziada za kuchukua kwa kuwa ofisi ya bunge na serikali wanaendelea kuingiza posho za vikao kwenye akaunti za wabunge hata baada za kuzipinga.”&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kauli yangu ya tarehe 29 Novemba 2011 nilieleza kwamba ni vyema umma ukafahamu kwamba Sheria ya Utawala wa Bunge (National Assembly Administration Act) ya mwaka 2008 kifungu cha 19 kinataja aina ya posho ambazo zinaweza kutolewa kwa wabunge kama ambavyo Rais ataeleza kwa maandishi. Katika kipengele (d) sheria imetaja orodha (i) mpaka (iii) ya posho ambazo wabunge wanastahili kulipwa za usafiri, kujikimu na wasaidizi. Katika orodha hiyo hakuna Posho ya Kikao (Sitting Allowance) ambayo inalipwa hivi sasa kwa kuwekwa kwenye akaunti za wabunge moja kwa moja ambayo kamati ya wabunge wa CHADEMA tunataka ifutwe mara moja kama sehemu ya mchakato wa kubadili mfumo mzima wa malipo ya posho kwa watumishi wa umma.&lt;br /&gt;Kifungu 19 (d) (iv) kimempa mamlaka Rais ya kutoa posho zingine kwa wabunge kwa kadiri atakavyoelekeza; kifungu hiki kimetoa mwanya wa kutolewa kwa waraka wa Katibu Mkuu Kiongozi Ofisi ya Rais wa tarehe 25 Oktoba 2010 wenye kumbukumbu na. CAB111/338/01/83 masharti ya kazi ya mbunge ambao umeeleza viwango vya posho mbalimbali ikiwemo kutoa posho ya vikao (Sitting Allowance). &lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Hivyo, ofisi ya Rais na Ofisi ya Bunge zinapaswa kuwaeleza watanzania iwapo waraka huo umebadilishwa na sababu za wabunge kutojulishwa kuhusu mabadiliko hayo.&lt;br /&gt;Aidha tarehe 29 Novemba 2011 nilieleza kuwa, iwapo mabadiliko hayo yamefanyika ni muhimu yakasitishwa kwa kuwa zitakwamisha utekelezaji wa mpango wa kufuta posho za vikao (sitting allowance) na kupunguza matumizi ya serikali kama ilivyoelezwa katika Ilani ya CHADEMA ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 pamoja na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano uliopitishwa bungeni mwaka 2011.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Izingatiwe kwamba uchumi wa nchi hivi sasa unasuasua, serikali ina hali mbaya ya fedha kutokana na kupungua kwa kiwango cha fedha kinachopatikana katika kodi na washirika wa kimaendeleo ukilinganisha na mahitaji ya bajeti; na hivyo kukopa kibiashara kwa ajili ya kuziba nakisi iliyopo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupungua kwa uzalishaji, kiwango cha fedha pamoja na kuongezeka kwa ubadhirifu katika matumizi ya rasilimali za umma kunachangia katika mfumuko wa bei hali inayohitaji mpango wa dharura wa kunusuru uchumi wetu ukaohusisha pamoja na mambo mengine kubana matumizi ya serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“ Binafsi natarajia serikali ije kwetu wabunge na mpango wa kukabiliana na ongezeko la gharama za maisha kwa wananchi badala ya kutuletea mpango wa kutuongezea wabunge posho za vikao huku mwelekeo wa uchumi na utekelezaji wa mipango ya maendeleo ukiwa kwenye hali tete”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kamati ya wabunge wa CHADEMA ilikubaliana posho hizo zifutwe kwa kuwa Ilani ya CHADEMA ya mwaka 2010 imeeleza kwamba lengo la msingi ni kuondoa posho za vikao (sitting allowance ) hatua ambayo itaambatana na nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma kuendana na ujuzi, nafasi, wajibu ili wafanyakazi walipwe kwa haki kwa kile wanachofanya kwa haki. Uamuzi huu ungewezesha pia kuelekeza fedha zaidi katika miradi ya maendeleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ofisi ya Rais na Ofisi ya Bunge zizingatie kuwa Serikali ya CCM imeridhia msimamo huo na kuuingiza kwenye Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano 2011/2012-2015/2016 uliosainiwa na Rais Jakaya Kikwete tarehe 7 Juni 2011 ambao kwenye  ukarasa wa 17 unatamka bayana kwamba posho za vikao na nyinginezo zinapaswa kufutwa au kuwianishwa hivyo kuziongeza ni kupuuza mpango huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;07/12/2011&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-6204777735030847262?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/6204777735030847262/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=6204777735030847262' title='25 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6204777735030847262'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6204777735030847262'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/msimamo-wangu-juu-ya-suala-zima-la.html' title='Msimamo wangu juu ya suala zima la Posho!'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>25</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-9005687477364421237</id><published>2011-12-01T02:57:00.000-08:00</published><updated>2011-12-01T10:08:01.353-08:00</updated><title type='text'>Jitokeze kesho, 2nd Dec, 2011 Ukumbi wa Makumbusho Dar(mkabala na IFM) ktk Mkutano wa wadau ulioitishwa na TANESCO!Kukataa ongezeko la bei ya umeme</title><content type='html'>Kesho tarehe 2 Disemba 2011 katika Ukumbi wa Makumbusho Dar es salaam (mkabala na IFM) kuanzia saa 4 asubuhi EWURA imeitisha Mkutano wa Wadau kujadili ombi la TANESCO la kupandisha bei ya umeme kwa wastani wa 155% (zaidi ya mara tatu ya bei ya sasa).&lt;br /&gt;Nawaomba wanamtandao wote tuhamasishe  umma kwa kutumia TEHAMA (sms, facebook, twitter, email na njia nyingine) ili wananchi waweze kuhudhuria mkutano husika kwa wingi na kutoa maoni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtakumbuka kwamba tarehe 23 Novemba 2011 nilitoa taarifa kwa umma kwamba Serikali inapaswa kusitisha ombi la dharura la kupandisha bei ya umeme kwa kiwango kikubwa ili kuepusha athari katika usalama na uchumi kutokana na mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha. Aidha, serikali inapaswa kuchukua hatua za haraka kulinusuru Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) dhidi ya mzigo mkubwa wa gharama unaotokana na ufisadi wa muda mrefu katika mikataba ya gesi asilia na gharama za mitambo ya kufua umeme wa dharura badala ya kuweka mkazo katika kuongeza bei ya umeme kwa wananchi wa kawaida. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Izingatiwe kuwa tarehe 9 Novemba 2011 Mamlamka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ilipokea ombi la dharura toka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) la kuidhinisha ongezeko la bei za huduma ya umeme kwa wastani wa asilimia 155 ya bei ya sasa (zaidi ya mara tatu).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naomba umma wa watanzania uzingatie athari za maombi hayo katika uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa ujumla hivyo mjadala wa kitaifa unahitajika na natoa mwito kwa wananchi kuweza kutoa maoni yao kuanzia sasa. Aidha ni muhimu kwa wananchi kushiriki kwa wingi katika mkutano wa kukusanya maoni ya wadau ulioitishwa na EWURA tarehe 2 Disemba 2011.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umma wa watanzania ufahamu kwamba ongezeko hili sio ombi la TANESCO pekee bali ni agizo kutoka kwa serikali kwa kurejea maelezo ya Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja bungeni katika mkutano wa nne wa bunge na kusisitizwa na kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda mwezi Septemba 2011 akihutubia mkutano wa hadhara mkoani Mara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Namshangaa Rais Jakaya Kikwete katika hotuba yake kwa taifa tarehe 18 Novemba 2011 alipozungumzia utekelezaji wa mpango wa dharura wa umeme hakuwaeleza watanzania kwamba uwasilishaji wa ombi hilo ni sehemu ya mpango huo wa dharura ambao utawaongezea wananchi bei ya umeme na gharama na maisha na hivyo kuathiri utekelezaji wa ahadi ya maisha bora kwa kila mtanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wakumbuke kwamba hii ni mara ya pili katika kipindi cha takribani mwaka mmoja kwa TANESCO kupandisha bei ya umeme; mara ya kwanza ikiwa mwezi Januari 2011 ambapo umeme ulipanda kwa asilimia 18.5 na kuchangia katika kupanda kwa gharama za uzalishaji katika nchi na kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ombi la TANESCO la wakati huo la kupandisha umeme lilikuwa ni asilimia 34 likakataliwa na EWURA na kushushwa mpaka asilimia 18.5, sasa Rais Kikwete, Waziri Mkuu Pinda na Waziri Ngeleja wanapaswa kuwaeleza watanzania sababu za kufanya ombi hilo la dharura kuwa la wastani wa asilimia 155 ili wananchi waweze kutoa maoni kwa kuzingatia mzigo ambao umma unataka kubebeshwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na matatizo ya kifedha ya TANESCO ambayo serikali inapaswa kuyashughulikia kwa pamoja na mambo mengine kutoa ruzuku katika kipindi hiki cha mpito; gharama kubwa za uzalishaji zinazolikabili shirika zinachangiwa na ufisadi wa muda mrefu katika mikataba ikiwemo ya uzalishaji wa gesi na ukodishaji wa mitambo ya kufua na pia maamuzi ya kukopa kibiashara katika kutekeleza mpango wa dharura wa umeme.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kabla ya kuongeza bei ya umeme kwa watanzania wa kawaida, Serikali iwaeleze wananchi imewapunguzia mzigo kiasi gani kwa kupitia upya mikataba ya kifisadi inayolinyonya Shirika la Umeme Tanzania kama ilivyopendekezwa kwenye ripoti mbalimbali ikiwemo katika maazimio ya Bunge ya mwaka 2008 juu ya mkataba wa ukodishaji wa mitambo ya kufua umeme ya Kampuni ya Richmond Develepment Company LLC ambapo orodha ya mikataba na makampuni mengine ilitajwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, umma uelezwe pia ukweli iwapo uamuzi wa kuchukua mikopo ya kibiashara yenye riba kubwa umeongeza zaidi gharama za uzalishaji wa umeme na hivyo kuifanya TANESCO iongeze zaidi bei ya umeme kwa wateja ikizingatiwa kuwa tarehe 15 Julai 2011 na 13 Agosti 2011, nilisisitiza bungeni serikali ipunguze bajeti katika maeneo mengine yasiyokuwa ya lazima na kuelekeza rasilimali nyingi zaidi kwenye umeme bila kuongeza mzigo mkubwa wa riba utakaolipwa na wananchi kupitia ongezeko la bei.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi huu wa kupandisha kwa kiwango kikubwa bei ya umeme utasababisha ongezeko la ziada la mfumuko wa bei hali ambayo ni tishio wa usalama na uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa ujumla. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali izingatie kwamba mfumuko wa bei nchini hivi sasa umefikia asilimia 17.9 na bidhaa zinazochangia mfumuko huo kwa kiwango kikubwa ni vyakula, mafuta na umeme. Kupanda kwa bei kwenye sekta ya nishati pekee kumekuwa kwa asilimia 37.4 na kusababisha kupanda kwa gharama za maisha, sasa  viongozi wajiulize itakuwaje umeme ukapopanda kwa wastani wa asilimia 155.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wananchi wakumbuke kwamba katika hotuba yake kwa taifa tarehe 18 Novemba 2011 Rais Kikwete ameelezea kwamba mfumuko wa bei na kuporomoka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola kwa ujumla kumetokana na uchumi wa nchi mbalimbali duniani hususani za Ukanda wa Sarafu ya Ulaya (Eurozone) kuwa katika kipindi kigumu na cha mashaka na kueleza kwamba suluhisho la matatizo la uchumi wetu litategemea uchumi wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli hii imedhihirisha kwamba Serikali haina mpango wa haraka wa kukabiliana na mfumuko wa bei, kuporomoka kwa shilingi na kupanda kwa gharama za maisha. Hali itakuwa mbaya zaidi iwapo tutaruhusu pamoja na sababu za nje ya nchi yetu tukaongeza vyanzo vya ndani vya kuongezeka kwa gharama za uzalishaji na bei za bidhaa kwa kupandisha bei ya nishati ya umeme ambayo chanzo chake ni hapa hapa nchini. Hivyo, mpango huu wa kupandisha bei ya umeme kwa wastani wa asilimia 155 unapaswa kusitishwa ama kubadilishwa kwa kulinda maslahi ya makundi mbalimbali kwa kuzingatia aina za matumizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Waziri Kivuli wa Nishati na Madini&lt;br /&gt;1/12/2011&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-9005687477364421237?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/9005687477364421237/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=9005687477364421237' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/9005687477364421237'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/9005687477364421237'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/12/jitokeze-kesho-2nd-dec-2011-ukumbi-ifm.html' title='Jitokeze kesho, 2nd Dec, 2011 Ukumbi wa Makumbusho Dar(mkabala na IFM) ktk Mkutano wa wadau ulioitishwa na TANESCO!Kukataa ongezeko la bei ya umeme'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-8210440611427621429</id><published>2011-11-28T03:08:00.000-08:00</published><updated>2011-11-28T03:20:58.461-08:00</updated><title type='text'>Mkutano wa CHADEMA na Rais</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/-0NAAHC4HBaQ/TtNuZUhxxQI/AAAAAAAAAkw/MVhX4igHshU/s1600/JJ%2Bakisalimiana%2Bna%2BJK.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://4.bp.blogspot.com/-0NAAHC4HBaQ/TtNuZUhxxQI/AAAAAAAAAkw/MVhX4igHshU/s320/JJ%2Bakisalimiana%2Bna%2BJK.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680004936330495234" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/-XmhtaqMDRPE/TtNt7KGMPfI/AAAAAAAAAkk/8Vrq3I_Jq4g/s1600/JK%2Bna%2BMbowe.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://2.bp.blogspot.com/-XmhtaqMDRPE/TtNt7KGMPfI/AAAAAAAAAkk/8Vrq3I_Jq4g/s320/JK%2Bna%2BMbowe.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680004418134359538" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-j1gU1NyxnMc/TtNt6hRjAAI/AAAAAAAAAkY/rIIL3-PM-iA/s1600/nazidi%2Bkutafakari.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-j1gU1NyxnMc/TtNt6hRjAAI/AAAAAAAAAkY/rIIL3-PM-iA/s320/nazidi%2Bkutafakari.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680004407176134658" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-l7szYGOo-iQ/TtNt6b-AOPI/AAAAAAAAAkM/v0pYncmgxiY/s1600/Nikinukuu%2Bktk%2Bmkutano.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-l7szYGOo-iQ/TtNt6b-AOPI/AAAAAAAAAkM/v0pYncmgxiY/s320/Nikinukuu%2Bktk%2Bmkutano.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680004405751986418" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/-c_dTbiKMvm8/TtNt50a55EI/AAAAAAAAAkA/voGpilo_DWU/s1600/JK%2Bna%2Btimu%2Bzima.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://2.bp.blogspot.com/-c_dTbiKMvm8/TtNt50a55EI/AAAAAAAAAkA/voGpilo_DWU/s320/JK%2Bna%2Btimu%2Bzima.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680004395135788098" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-k6YnDac8_Eg/TtNt5v73FYI/AAAAAAAAAj0/CgNAaxHhb7c/s1600/natafakari.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-k6YnDac8_Eg/TtNt5v73FYI/AAAAAAAAAj0/CgNAaxHhb7c/s320/natafakari.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680004393931838850" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/-LkrGGQdNw_w/TtNtOwpdxII/AAAAAAAAAjo/R2BJ1CqBz5c/s1600/Prof%2BSafarri%2Bakisalimiana%2Bna%2BRais%2BJJ%2Bpembeni.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://2.bp.blogspot.com/-LkrGGQdNw_w/TtNtOwpdxII/AAAAAAAAAjo/R2BJ1CqBz5c/s320/Prof%2BSafarri%2Bakisalimiana%2Bna%2BRais%2BJJ%2Bpembeni.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680003655388742786" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/-Ybuy3dPj4eY/TtNtD83HWUI/AAAAAAAAAjc/Zt6Cg6vRy20/s1600/JJ%2Bna%2BKikwete%2Bwakiagana.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://4.bp.blogspot.com/-Ybuy3dPj4eY/TtNtD83HWUI/AAAAAAAAAjc/Zt6Cg6vRy20/s320/JJ%2Bna%2BKikwete%2Bwakiagana.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5680003469688658242" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-8210440611427621429?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/8210440611427621429/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=8210440611427621429' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8210440611427621429'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8210440611427621429'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/mkutano-wa-chadema-na-rais.html' title='Mkutano wa CHADEMA na Rais'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://4.bp.blogspot.com/-0NAAHC4HBaQ/TtNuZUhxxQI/AAAAAAAAAkw/MVhX4igHshU/s72-c/JJ%2Bakisalimiana%2Bna%2BJK.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-3136278456983545074</id><published>2011-11-25T04:54:00.001-08:00</published><updated>2011-11-25T04:55:52.320-08:00</updated><title type='text'>Juu ya hoja ya kutaka kupandishwa bei ya umeme!</title><content type='html'>Mnyika ataka bei ya umeme isipandishwe&lt;br /&gt;Wednesday, 23 November 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MBUNGE wa Ubungo,jijini Dar es Salaam, John Mnyika, ameitaka Serikali kusitisha ombi la Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 155, ili kuepusha athari katika usalama na uchumi wa nchi, utakaozidishwa na mfumuko wa bei.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Mbunge huyo alisema hayo jana kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari, kufuatia hatua ya Tanesco  kutaka kupandisha bei ya umeme kwa kiwango hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mnyika alisema Serikali inapaswa kuchukua hatua za haraka kuinusuru Tanesco dhidi ya mzigo mkubwa wa gharama unaoikabili, badala ya upandisha bei ya umeme kwa wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;"Itakumbukwa kwamba Novemba 9 mwaka huu Mamlamka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), ilipokea ombi la dharura kutoka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) la kuidhinisha ongezeko la bei za huduma ya umeme kwa wastani wa asilimia 155 ya bei ya sasa, bei ambayo ni zaidi ya mara tatu ya sasa" alisema Mnyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mnyika pia alisema ni muhimu kwa wananchi kushiriki kwa wingi katika mkutano wa kukusanya maoni ya wadau ulioitishwa na Ewura kuhusu  upandishaji bei ya umeme ili nao, wapate fursa ya kutoa maoni yao ipasavyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;"Wananchi wakumbuke kwamba hii ni mara ya pili katika kipindi cha takribani mwaka mmoja kwa Tanesco kupandisha bei ya umeme. Mara ya kwanza ilikuwa Januari mwaka huu ambapo umeme ulipanda kwa asilimia 18.5 na kuchangia katika kupanda kwa gharama za uzalishaji na kuongeza ugumu wa maisha kwa wananchi" alisema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mnyika alisema kabla ya kuongeza bei ya umeme kwa wananchi, Serikali inapaswa kwanza kuwaeleza namna ilivyowapunguzia mzigo kwa kupitia upya mikataba inayoinyonya Tanesco.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alisema uamuzi wa kupandisha bei ya umeme utasababisha ongezeko la mfumuko wa bei , jambo ambalo litatishia  usalama na uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kwa jumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“ Serikali izingatie kwamba mfumuko wa bei nchini hivi sasa umefikia asilimia 17.9 na bidhaa zinazochangia mfumuko huo kwa kiwango kikubwa ni vyakula, mafuta na umeme. Kupanda kwa ya nishati ya umeme pekee kumekuwa kwa asilimia 37.4 na kusababisha kupanda kwa gharama za maisha” alisema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alisema mpango huo wa kupandisha bei ya umeme kwa wastani wa asilimia 155 unapaswa kusitishwa ama kubadilishwa kwa kulinda maslahi ya makundi mbalimbali kwa kuzingatia aina za matumizi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/51-habari-nyingine/17784-mnyika-ataka-bei-ya-umeme-isipandishwe&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-3136278456983545074?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/3136278456983545074/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=3136278456983545074' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3136278456983545074'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/3136278456983545074'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/juu-ya-hoja-ya-kutaka-kupandishwa-bei.html' title='Juu ya hoja ya kutaka kupandishwa bei ya umeme!'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-5783133801757404883</id><published>2011-11-23T08:19:00.000-08:00</published><updated>2011-11-23T08:38:12.727-08:00</updated><title type='text'>Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Prof.Anna Tibaijuka katika Kata ya Sinza kukagua uuzwaji maeneo ya wazi</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-KLD4eMnpmJE/Ts0hBH5ZvVI/AAAAAAAAAjQ/oyMit1QK8hw/s1600/Sinza%2B1.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-KLD4eMnpmJE/Ts0hBH5ZvVI/AAAAAAAAAjQ/oyMit1QK8hw/s320/Sinza%2B1.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5678231008367459666" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka akiongea na mkazi wa Sinza Ndahani Yohana ambaye amenunua eneo la wazi kwa utapeli kwa shilingi milioni 500 wiki mbili zilizopita, ambapo ramani halisi inaonyesha eneo hilo ni la wazi.&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-vOsuIkluetA/Ts0f6QXutlI/AAAAAAAAAjE/9Bf3R_YgcaI/s1600/Sinza%2B2.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-vOsuIkluetA/Ts0f6QXutlI/AAAAAAAAAjE/9Bf3R_YgcaI/s320/Sinza%2B2.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5678229790871434834" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka akihakiki na kuonyesha kupitia ramani maeneo ya wazi yaliyouzwa na kuvamiwa katika Kata ya Sinza eneo la Sinza E&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-_7nDEouuZFo/Ts0fDSgY1bI/AAAAAAAAAi4/9rvHCL1QuDA/s1600/Sinza%2B3.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-_7nDEouuZFo/Ts0fDSgY1bI/AAAAAAAAAi4/9rvHCL1QuDA/s320/Sinza%2B3.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5678228846551815602" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Prof. Anna Tibaijuka wa pili kutoka kulia akiangalia ramani halisi inayoonyesha maeneo ya wazi wakati alipokagua maeneo ya wazi yaliyovamiwa na wananchi maeneo ya Sinza E wilaya ya Kinondoni, ambapo pia alikuwa akikagua mabango yaliyowekwa kwa ajili ya kuwataarifu wananchi na kuwaelimisha maeneo ambayo ramani inaonyesha yako wazi kwa ajili ya mipango ya maendeleo ya Serikali.&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-e-dZdgEmHoQ/Ts0eBYOgmQI/AAAAAAAAAis/HYVkqrS7pLY/s1600/Sinza%2B4.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-e-dZdgEmHoQ/Ts0eBYOgmQI/AAAAAAAAAis/HYVkqrS7pLY/s320/Sinza%2B4.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5678227714216073474" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;Diwani wa Kata ya Sinza, Renatus Pamba akimwonyesha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Prof. Anna Tibaijuka maeneo ya wazi yaliyovamiwa na wananchi katika maeneo ya Sinza E&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Nashukuru sana blogu ya http://www.hakingowi.com/ kwa kurusha habari hii!&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-5783133801757404883?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/5783133801757404883/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=5783133801757404883' title='4 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5783133801757404883'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5783133801757404883'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/waziri-wa-ardhi-nyumba-na-makazi.html' title='Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Prof.Anna Tibaijuka katika Kata ya Sinza kukagua uuzwaji maeneo ya wazi'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/-KLD4eMnpmJE/Ts0hBH5ZvVI/AAAAAAAAAjQ/oyMit1QK8hw/s72-c/Sinza%2B1.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>4</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-5778660618959789950</id><published>2011-11-15T02:34:00.000-08:00</published><updated>2011-11-15T02:38:05.536-08:00</updated><title type='text'>Sheria ya Manunuzi!</title><content type='html'>&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Sheria ya Ununuzi: Wabunge wapunguza nguvu za Rais&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;Monday, 14 November 2011 21:41&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kizitto Noya, Dodoma &lt;br /&gt;MUSWADA wa Sheria ya Ununuzi wa Umma jana ulipita kwa mbinde baada ya wabunge kuibana Serikali na kuilazimu kuufanyia marekebisho kwenye baadhi ya vipengele, ikiwemo kuondoa kipengele kinachotaka Rais athibitishe ununuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbali na kuibana Serikali kubadili kipengele hicho, wabunge pia walitaka ufafanuzi wa kina kuhusu kifungu cha 104 kinachoelezea adhabu ya mtu anayeisababishia Serikali hasara katika mchakato wa ununuzi pamoja na kifungu cha 66 kinachopendekeza ununuzi wa vifaa vilivyotumika, hatua ambayo ilimfanya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuagiza vipengele hivyo kurudishwa kwenye Kamati ya Sheria Ndogo za Bunge, kwa ajili ya majadiliano zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muswada huo ambao awali ulipangwa kupitishwa jana mchana, ulilazimika kusubiri katika kikao cha jioni baada ya kutokea malumbano makali ya hoja kati ya wabunge waliopinga vipengele hivyo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema ambaye alikuwa akivitetea.Malumbano hayo yalijitokeza wakati Bunge lilipokuwa limekaa kama kamati kwa ajili kupitisha sheria hiyo mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wabunge waliotawala mjadala huo walikuwa John Mnyika wa Ubungo (Chadema), Luhaga Mpina wa Kisesa (CCM) na Godfrey Zambi wa Mbozi Mashariki (CCM).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nyakati tofauti, wabunge hao walipinga adhabu iliyopendekeza mtu anayepatikana na hatia ya kuisababishia Serikali hasara katika mchakato wa ununuzi, kufungwa miaka mitano na kulipa faini ya kuanzia Sh5milioni hadi Sh10 milioni wakisema ni ndogo na inapaswa kuongezwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Mheshimiwa Mwenyekiti mimi naona adhabu hiyo ni ndogo, mtu wa aina hiyo anapaswa kufungwa siyo zaidi ya miaka 30 na baadaye afilisiwe mali zake kulipa hasara aliyoisababishia Serikali,” alisema Mpina na baadaye kuungwa mkono na wabunge wengine watano: Seleman Jafu (Kisarawe), Christina Mughwai (Viti Maalumu), Alphaxard Lugola (Mwibara), Dk Mahmoud Mgimwa (Mufindi Kaskazini) na Mnyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kuunga mkono hoja hiyo, wabunge hao walisema si sahihi wala haki mtu aliyeisababishia Serikali hasara ya mabilioni ya shilingi kufungwa jela kwa kipindi kisichozidi miaka mitano na kulipa faini isiyopungua Sh10 milioni au zaidi wakisisitiza kuwa mtu huyo anapaswa kufungwa miaka isiyopungua 20 na isiyozidi 30 na baadaye afilisiwe mali zake zote kulipa deni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, Werema alipinga mapendekezo hayo ya wabunge kwa maelezo kuwa adhabu hiyo ni kubwa mno kwa watu ambao mfumo, uliwadhamini kuitumikia jamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Waheshimiwa wabunge, katika kutunga sheria tusiwe na hasira kwa sababu hasira ni pango la shetani. Nakubaliana kwamba tatizo hilo linahitaji adhabu kali lakini, adhabu hiyo inapaswa kuwa ya uwiano na kosa lenyewe. Kosa tunalotaka kulifanya tuliwahi kulifanya mwaka 1983 katika Sheria ya Uhujumu Uchumi. Sheria ile tuliitunga kwa hasira, kwa ushauri wangu adhabu hiyo inatosha,” alisema Jaji Werema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kauli hiyo ya Jaji Werema, iliwaamsha wabunge kadhaa na Makinda kumchagua Mpina kuzungumza ambaye alisema: “Ninachoweza kusema hapa ni kwamba Mwanasheria Mkuu hana uzoefu na manunuzi.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Kwa nini tuwe na sheria za upendeleo? Tumetunga sheria kwamba raia akionekana kwenye mbuga za wanyama hata kama hana silaha, akamatwe na watu wanapigwa risasi. Lakini tunapokuja kutunga sheria kwa ajili ya watendaji tunataka ziwe laini, kwa faida ya nani?”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Malumbano hayo yalimfanya Spika Makinda ambaye wakati huo alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge zima, kuifunga hoja hiyo akisema: “Sasa naagiza kifungu hicho kirudishwe kwenye kamati ili kikajadiliwe upya.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hoja nyingine iliyozua mjadala katika kikao hicho ni ile aliyoitoa Mnyika kutaka kanuni zitakazotungwa na waziri kwa ajili ya utekelezaji wa sheria hiyo, zipitiwe upya na Bunge pamoja na kutaka kufutwa kabisa kifungu cha 66 kinachotaka kuruhusiwa ununuzi wa vifaa vilivyotumika. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkulo&lt;br /&gt;Awali, akifunga mjadala huo, Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo alisema Serikali imeridhia mapendekezo ya wabunge kufanyia marekebisho kipengele kinacholihusisha Baraza la Mawaziri kushiriki katika kuidhinisha ununuzi wa umma.&lt;br /&gt;“Tumekubaliana na mapendekezo ya wabunge kwamba Rais asihusishwe kuidhinisha ununuzi, badala yake sasa kazi hiyo itafanywa na Waziri wa Fedha baada ya kushauriwa na kamati maalumu atakayoiunda.”&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri Mkulo aliwaomba wabunge kuondoa hofu ya mwanya wa ufisadi katika sheria hiyo, akisema Serikali imejipanga vya kutosha kukabiliana na hali hiyo kwa kuja na kanuni zitakazodhibiti mianya yote ya rushwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Alitaja baadhi ya kanuni hizo kuwa ni zile zinazotaka wataalamu kukagua mali inayotaka kununuliwa, mmiliki kuwasilisha nyaraka zinazoonyesha kifaa husika kimetengenezwa lini, ulinganifu wa ubora wa vifaa pamoja na taasisi zisizoridhika na mchakato kutoa taarifa (Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupitisha muswada&lt;br /&gt;Kabla ya kupitishwa kwa muswada huo jana jioni, Jaji Werema alifafanua kwamba Serikali imekubaliana na hoja ya Mpina ya kukifanyia marekebisho kifungu cha 104 kinachohusu adhabu kwa watuhumiwa ambacho kinatoa mamlaka ya mtuhumiwa aliyesababishia Serikali hasara katika ununuzi kuhukumiwa adhabu ya miaka zaidi ya saba na kufidia hasara hiyo au kukamatwa na kutaifishwa kwa mali zake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jaji Werema alisema anaamini kwamba adhabu hizo zitaongeza uwajibikaji na umakini katika kusimamia na kutekeleza Sheria ya Ununuzi ili kuliepusha taifa na hasara na kuongeza kwamba Serikali pia ilikubaliana na hoja ya Mnyika aliyeonyesha shaka juu ya mamlaka ya waziri katika utekelezaji wa kanuni ambayo pamoja na mambo mengine, ataweza kuunda timu ya wataalamu ambayo itamshauri katika baadhi ya vitu muhimu vinavyohitaji ununuzi kisha naye kuamua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, baadaye muswada huo ulipitishwa na utakapotiwa saini na Rais, Sheria ya Ununuzi ya mwaka 2011 itachukua nafasi ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2004, inayotumika sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari/49-uchaguzi-mkuu/17501-sheria-ya-ununuzi-wabunge-wapunguza-nguvu-za-rais&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-5778660618959789950?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/5778660618959789950/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=5778660618959789950' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5778660618959789950'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5778660618959789950'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/sheria-ya-manunuzi.html' title='Sheria ya Manunuzi!'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-5637547704082990131</id><published>2011-11-14T22:32:00.000-08:00</published><updated>2011-11-14T22:44:15.616-08:00</updated><title type='text'>MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA KATIBA NA   SHERIA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU (MB.)</title><content type='html'>&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA KATIBA NA &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;SHERIA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU (MB.)KUHUSU&lt;br /&gt;MUSWADA WA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, 2011&lt;br /&gt;(Kanuni ya 86(6) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2007)&lt;br /&gt;UTANGULIZI&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Tarehe 11 Machi 2011, Serikali ilichapisha Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 katika Gazeti la Serikali la tarehe hiyo. Muswada huo ulipelekwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa Hati ya Dharura. Hata hivyo, baada ya upinzani mkubwa dhidi ya Muswada huo kujitokeza karibu nchi nzima, Bunge lililazimika kuondoa Hati ya Dharura na hivyo kufanya Muswada kushughulikiwa kwa mujibu wa utaratibu wa kawaida wa kutunga sheria uliowekwa na kanuni za 80, 83 na 84 za Kanuni za Kudumu za Bunge la Jamhuri ya Muungano, 2007. Katika kufanya hivyo, Bunge – kwa kupitia Spika - liliiagiza Serikali kufanya mambo yafuatayo kwa mujibu wa Taarifa Rasmi ya Majadiliano Katika Bunge (Hansard) ya Kikao cha Nane cha Mkutano wa Tatu cha tarehe 15 Aprili 2011:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(a) “Muda zaidi utolewe kwa Kamati na wananchi kuufikiria Muswada huu. Katika kufanikisha hili, “... iandae Muswada huu kwa lugha ya Kiswahili ili wananchi wenyewe waweze kusoma yaliyomo kwenye Muswada huo badala ya kupewa tafsiri tu na watu wengine;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(b) “Muswada uchapishwe kwenye magazeti na kutangazwa kwenye vyombo mbali mbali vya habari ili kutoa fursa ya kutosha kwa wananchi wengi kuuelewa na kuutolea maoni;&lt;br /&gt;(c) “Utangulizi wa Muswada huu uwekwe vizuri zaidi ili wananchi waelewe madhumuni ya Muswada huu, kwani imeonekana wazi wananchi wengi wanadhani tayari tumeanza kuandika Katiba, kumbe lengo la Muswada huu ni kutunga Sheria ya Kuunda Tume ya Kukusanya Maoni tu.” (uk. 31-32)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Katika kutoa maagizo haya, Bunge lilisitiza kwamba “... Muswada huu uko ndani ya Bunge, hauko serikalini.” (uk. 33) Hii ni kwa sababu, kwa mujibu wa kanuni ya 84(1) ya Kanuni za Bunge, Muswada ulikwishasomwa kwa mara ya kwanza na kupelekwa kwenye Kamati inayohusika kwa ajili ya kuanza kujadiliwa. Aidha, kwa mujibu wa kanuni ya 84(2) Kamati ilikwishaanza kupokea maoni ya wadau “... kwa lengo la kuisaidia katika uchambuzi wa Muswada huo.” Kazi iliyokuwa imebaki kwa Kamati ilikuwa ni kutumia mamlaka yake chini ya kanuni ya 84(3) “... kufanya marekebisho katika Muswada wa Sheria kwa kumshauri Waziri ... anayehusika na Muswada huo kufanya mabadiliko....” Ni baada tu ya kupata ushauri wa Kamati kuhusu mabadiliko ndio Serikali ingeweza kuleta Jedwali la Mabadiliko kwa lengo la kufanya mabadiliko katika hatua hii kabla Muswada haujaletwa Bungeni kwa ajili ya kusomwa mara ya pili na kwa mjadala wa Bunge zima. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Hakuna hata moja ya maagizo haya ya Bunge ambalo limetekelezwa na Serikali. Tafsiri ya Kiswahili ambayo imeletwa Bungeni – pamoja na kuonyesha imesainiwa tarehe 8 Machi 2011 sawa na Muswada wa Zamani uliopigiwa kelele sana na wananchi – ililetwa kwenye Kamati wiki mbili zilizopita, ikiwa ni wiki moja baada ya Kamati kukataa kuujadili Muswada Mpya kwa vile ulifanyiwa mabadiliko na Serikali bila kupata ushauri wa Kamati kama inavyotakiwa na kanuni ya 83(4) ya Kanuni za Bunge. Badala ya kutekeleza maagizo ya Bunge, Serikali imeleta Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 ambao ulichapishwa katika Gazeti la Serikali la tarehe 14 Oktoba 2011. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muswada huu mpya una tofauti kubwa na za kimsingi na Muswada wa Zamani kama nitakavyoonyesha hapa. Kwa maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, mabadiliko makubwa na ya kimsingi yaliyofanywa kwenye Muswada wa Zamani yalihitaji na bado yanahitaji mjadala wa kitaifa wa wananchi kama ambavyo wengi wamedai katika mijadala inayoendelea nchi nzima. Aidha, Bunge hili tukufu lilihitaji, na bado linahitaji, muda zaidi wa kuyatafakari mabadiliko haya makubwa nay a kimsingi katika Muswada wa Zamani. Katika mazingira haya, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini ni busara na ni sound policy kwa Muswada huu Mpya kusomwa mara ya Kwanza ili kuruhusu mjadala unaohitajika kufanyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;TUME YA MABADILIKO YA KATIBA&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Kama ilivyokuwa kwa Muswada wa Zamani, Muswada huu unapendekeza kuundwa kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo, kwa mujibu wa Utangulizi wa Muswada, itawajibika “... kuratibu na kukusanya maoni ya wananchi juu ya Katiba (na) kuainisha na kuchambua maoni ya wananchi....” Kwa mujibu wa ibara ya 5, Tume hii itaundwa na Rais “kwa kushauriana na kukubaliana na Rais wa Zanzibar, na kwa ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar....” Aidha, kwa mujibu wa ibara ya 6(1), Rais atateua wajumbe wa Tume “... kwa kushauriana na kukubaliana na Rais wa Zanzibar....” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ibara ya 6(2) inapendekeza kwamba “... muundo wa Tume utazingatia msingi wa kuwepo kwa uwakilishi ulio sawa kwa kila upande wa Jamhuri ya Muungano.” Pendekezo hili linarudia, kwa njia iliyojificha zaidi, msimamo wa ibara ya 6(2) ya Muswada wa Zamani iliyokuwa imeweka wazi kwamba idadi ya wajumbe wa Tume itakuwa sawa kwa sawa kwa pande zote za Jamhuri ya Muungano! Kama ilivyokuwa kwa Muswada wa Zamani, ibara ya 7(2) ya Muswada inapendekeza kwamba “uteuzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti utafanyika kwa msingi kwamba iwapo Mwenyekiti atatoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, basi Makamu Mwenyekiti atakuwa mtu anayetoka upande mwingine wa Jamhuri ya Muungano.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muundo wa Tume unakamilishwa na Sekretarieti ya Tume itakayoongozwa na Katibu. (ibara ya 13(1) Kwa mujibu wa ibara ya 13(2), Katibu huyo atateuliwa na Rais “baada ya kukubaliana na Rais wa Zanzibar.” Watendaji wengine wa Sekretarieti watateuliwa na Waziri “kwa makubaliano na Waziri mwenye dhamana ya mambo ya Katiba wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muswada unapendekeza kumpa Rais - baada ya makubaliano na Rais wa Zanzibar - mamlaka ya kutoa hadidu za rejea za Tume na muda wa kukamilisha na kuwasilisha ripoti. (ibara ya 8(1) Na kama hali itahitaji kufanya hivyo, Rais – “kwa makubaliano na Rais wa Zanzibar” – anaweza kuongeza muda usiozidi miezi mitatu ili kuwezesha Tume kukamilisha na kuwasilisha ripoti. (ibara ya 8(2) Hadidu za rejea, kwa mujibu wa ibara ya 8(3), “... zitakuwa ni hati ya kisheria ambayo Tume itaizingatia katika utekelezaji wa majukumu na utumiaji wa mamlaka yake kwa mujibu wa Sheria hii.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Ibara ya 9(1) ya Muswada inaelezea kazi za Tume kuwa ni pamoja na:&lt;br /&gt;(a) Kuratibu na kukusanya maoni ya wananchi;&lt;br /&gt;(b) Kupitia na kutafiti usahihi na ulinganifu wa masharti ya kikatiba yanayohusu mamlaka ya watu, mifumo ya kisiasa, demokrasia, utawala wa sheria na utawala bora;&lt;br /&gt;(c) Kutoa mapendekezo kwa kila hadidu ya rejea; na &lt;br /&gt;(d) Kuandaa na kuwasilisha ripoti.&lt;br /&gt;Ijapokuwa haijaanishwa hivyo, ni wazi - kwa mujibu wa wa ibara ya 17(1)(d) na (2) ya Muswada - kwamba moja ya kazi za Tume ni kuandaa Rasimu ya Muswada wa Katiba mpya. Mapendekezo ya Muswada kuhusu Tume ya Mabadiliko ya Katiba ni muhimu na yanazua maswali mengi yanayohitaji mjadala wa kitaifa na maamuzi ya wananchi. Maeneo haya muhimu ni pamoja na nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano katika mchakato mzima wa kutengeneza Katiba Mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;MAMLAKA YA RAIS &lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika,&lt;br /&gt;Kama ambavyo tumepata kusema ndani ya Bunge hili, kwa muda wote wa uhai wetu kama taifa huru, mfumo wetu wa kikatiba na wa kisiasa umejengwa juu ya nguzo kuu ya Urais wa Kifalme (Imperial Presidency). Hii inatokana na ukweli kwamba katika mfumo huu, Rais ana madaraka makubwa sana ya kiutendaji na ya kiutungaji sheria. Vile vile Rais ana kivuli kirefu cha kikatiba juu ya mahakama kwa kutumia mamlaka makubwa aliyonayo katika uteuzi wa viongozi wote wa ngazi za juu za Mahakama. Urais wa Kifalme ndio chanzo kikuu cha kukosekana kwa uwajibikaji katika ngazi zote za serikali na ndio kichocheo kikubwa cha rushwa na ufisadi wa kutisha ambao umefanywa kuwa ni sehemu ya kawaida ya maamuzi ya kiserikali. Sio vibaya, katika kuthibitisha jambo hili, kurudia maneno ya ibara ya 37(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977: “... Rais atakuwa huru na hatalazimika kufuata ushauri atakaopewa na mtu yeyote....” Na kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere kwenye mahojiano ya mwaka 1978 na Shirika la Habari la Uingereza (BBC), kama Rais wa Tanzania alikuwa na mamlaka – kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi yetu – ya kuwa dikteta!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muswada unaendeleza kivuli kirefu cha Urais wa Kifalme katika mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya. Mtu mwenye mamlaka ya kidikteta, kama Rais alivyo kwa mujibu wa Katiba ya sasa, hawezi kusimamia upatikanaji wa katiba ya kidemokrasia. Kwa kutumia mamlaka makubwa ya uteuzi wa Tume yanayopendekezwa na Muswada huu, ni wazi Rais Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama tawala cha CCM, atateua wajumbe anaowataka yeye na Rais Ali Mohamed Shein, Makamu wake na pia Rais wa Zanzibar! Ni wazi vile vile kwamba watu watakaoteuliwa na Marais hawa ni watu wasiokuwa tishio kwa status quo kwa maana ya kupendekeza mabadiliko makubwa katika mfumo wa kikatiba na kiutawala na hivyo kuhatarisha maslahi ya CCM! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Hali ni hiyo hiyo kwa Sekretarieti ya Tume ambayo ndio chombo cha kiutendaji na moyo wa Tume yenyewe. Kama Katibu, ambaye ndiye mtendaji mkuu wa Tume ni mteuliwa wa Rais na ni mtumishi wa Serikali; kama watendaji wengine wa Tume ni watumishi wa serikali walioteuliwa wa Waziri ambaye naye ni mteuliwa wa Rais baada ya kukubaliana na Waziri mwenzake wa Zanzibar; na kama watumishi wengine wa Tume nao ni watumishi wa Serikali kama inavyopendekezwa na ibara ya 13 ya Muswada Mpya, ni wazi, kwa hiyo, kwamba mapendekezo haya yote ya uteuzi wa wajumbe, watendaji na watumishi wengine wa Tume yana lengo moja tu: kuhakikisha kwamba matokeo ya kazi ya Tume hiyo ni yale tu yanayotakiwa na Rais na Serikali yake na chama chake cha CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Badala ya mapendekezo haya ya Muswada Mpya, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza utaratibu wa kidemokrasia zaidi katika uteuzi wa Tume. Kwanza, badala ya Tume hiyo kuwa ‘Tume ya Rais’ kama inavyopendekezwa katika Muswada, tunapendekeza iwe ‘Tume ya Vyama’ (multiparty Commission) kwa maana moja kubwa: wajumbe wa Tume wateuliwe kufuatana na mapendekezo na makubaliano ya vyama vya siasa vyenye uwakilishi Bungeni, vyama vingine vilivyosajiliwa pamoja na mashirika ya kijamii, taasisi za kitaaluma na za kidini. Hii haina maana kwamba wajumbe wa Tume hiyo hawatatakiwa kuwa na sifa zilizoainishwa katika ibara ya 6(3) ya Muswada Mpya. La hasha! Wajumbe wa Tume ya Vyama watatakiwa kuwa na sifa zozote za kitaaluma zinazotakiwa ili kuwawezesha kufanya kazi ya kitaalamu kama inavyopendekezwa na &lt;br /&gt;Muswada Mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, baada ya uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Vyama, inapendekezwa kwamba wajumbe walioteuliwa kwa mashauriano na makubaliano kama tunavyopendekeza watatakiwa wathibitishwe na Bunge la Jamhuri ya Muungano. Pendekezo hili litahakikisha kwamba wajumbe wa Tume wanakuwa vetted na chombo kikuu cha uwakilishi wa wananchi. Hili litajenga kuaminiana baina ya Serikali, vyama vya siasa, mashirika ya kijamii, taasisi za kitaaluma na za kidini na litaipa Tume ya Mabadiliko ya Katiba uhalali mkubwa wa kisiasa, kitu ambacho ni muhimu katika mazingira ya sasa ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Tofauti pekee na muhimu kati ya pendekezo la Muswada Mpya na pendekezo letu kuhusu mamlaka ya uteuzi wa wajumbe wa Tume ni locus ya uwajibikaji wao. Wajumbe wanaoteuliwa na Rais wanakuwa na shinikizo la kutoa matokeo yatakayompendezesha Rais au chama chake. Wajumbe wanaotokana na mapendekezo na makubaliano ya wadau wengi na wanaothibitishwa na chombo cha uwakilishi cha wananchi kama tunavyopendekeza hawawezi kuwa na shinikizo la kutoa matokeo yatakayompendezesha mmojawapo wa wadau hao. Faida kubwa na ya wazi ya Tume ya Vyama ni kwamba matokeo ya kazi yake yana nafasi kubwa zaidi ya kukubaliwa, kuheshimiwa na kutekelezwa na wadau mbali mbali kuliko matokeo ya kazi ya Tume ya Rais. Kwa lugha nyingine, kazi ya Tume ya Vyama itakuwa na uhalali wa kisiasa (political legitimacy) mkubwa zaidi kuliko Tume ya Rais. &lt;br /&gt;Pendekezo hili linawahusu Katibu, watendaji na watumishi wengine wa Tume vile vile. Kutokana na uzoefu uliotokana na historia yetu na mfumo wetu wa kiutawala na kikatiba, watumishi wa serikali wamekuwa hawana uhuru wa kufanya maamuzi kwa kuzingatia utashi wao na uadilifu wa kitaaluma bali hufanya maamuzi kwa kuzingatia matakwa ya mabosi wao wa kisiasa. Hii ni kwa sababu, kisheria na hata kivitendo, watendaji na watumishi karibu wote wa umma hujiona wanawajibika kwa mamlaka zao za uteuzi, yaani Rais na/au Waziri. Aidha, watendaji na watumishi hawa wanawajibika kinidhamu kwa mamlaka zinazoongozwa na watendaji wa Serikali ambao nao ni wateuliwa wa Rais na kwa hiyo wanakuwa na woga wa kufanya maamuzi yanayoweza kuhatarisha maslahi ya kisiasa ya Rais na chama tawala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hizo, ni muhimu kwa watendaji na watumishi wote wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wawe huru dhidi ya mashinikizo yoyote ya kisiasa kutoka kwa Rais na Serikali yake na chama chake. Ili Tume iwe na mamlaka na uhuru unaohitajika kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake na ili isiingiliwe kweli na mtu au mamlaka yoyote kama inavyosema ibara ya 10 ya Muswada, inabidi mamlaka ya uteuzi yaondolewe katika mikono ya Rais na/au Waziri ambaye ni mdau mmojawapo tu wa wadau wengi wa mchakato wa Katiba Mpya. Na namna ya pili ya kuhakikisha uhuru huu unakuwepo ni kuweka utaratibu wa kuwapata watendaji na watumishi hawa nje kabisa ya utumishi wa serikali kwa kuweka masharti ya kuwataka waombe kazi, kufanyiwa usaili na kuteuliwa na jopo la wataalamu walio huru. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Namna ya tatu ya kuhakikisha uhuru wa Tume katika kutekeleza majukumu yake ni kuhakikisha wajumbe wake wanapatiwa ulinzi wa ajira zao (security of tenure) sawa na wanaopatiwa majaji wa Mahakama ya Tanzania ili kuzuia uwezekano wa wajumbe kuondolewa kwa sababu zisizotokana na utendaji wao wa kitaaluma au ukosefu wa maadili. Kwa maana hiyo, mapendekezo ya ibara ya 10 Muswada Mpya juu ya uhuru wa Tume hayatoshelezi hata kidogo. Hii ni kwa sababu ibara ya 12 ya Muswada Mpya, ambayo inazungumzia ukomo wa ujumbe wa Tume, haijaweka utaratibu wowote wa namna ya kushughulikia nidhamu ya wajumbe pale kunapokuwepo tuhuma za ukiukaji wa Kanuni za Maadili zinazopendekezwa katika ibara ya 12(2) na Jedwali la Pili la Muswada. Kutokuweka utaratibu huu kuna hatari kubwa kwani, kisheria, mamlaka ya uteuzi huwa ndio mamlaka ya nidhamu pale ambapo sheria haijaweka utaratibu tofauti wa nidhamu. Hii ina maana kwamba bila kuweka utaratibu wa kisheria wa nidhamu ya wajumbe wa Tume, Rais ndiye atakuwa na uwezo wa kuwaondoa madarakani kwa sababu yeye ndiye aliyewateua! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Pendekezo letu la tatu linahusu hadidu za rejea. Hapa kuna hoja za aina mbili. Kwanza, sambamba na pendekezo la kutompa Rais madaraka ya uteuzi wa wajumbe wa Tume, Rais asipewe mamlaka ya kutoa hadidu za rejea kwa Tume. Pili, kwa vile – kama inavyopendekezwa katika Muswada Mpya – hadidu za rejea ni hati ya kisheria inayotakiwa kuzingatiwa na Tume katika utekelezaji wa majukumu yake, ni muhimu hati hii iwekwe wazi katika sheria yenyewe badala ya kubakia kuwa siri ya Rais. Watanzania lazima wajue Tume inapewa majukumu gani ya kisheria. Aidha, wajumbe wa Tume wenyewe lazima wafahamu wanapewa majukumu gani ya kisheria na wafahamu kwamba wanatakiwa kufuata matakwa ya sheria na sio maelekezo ya mtu mmoja hata kama ni Rais wa Kifalme. Hii itasaidia uwajibikaji wa Tume kwa wananchi kwani itakuwa rahisi kupima matokeo ya kazi ya Tume kwa hadidu za rejea zilizowekwa wazi katika sheria. &lt;br /&gt;Ukweli ni kwamba badala ya kumsubiri Rais kutoa hadidu za rejea, tayari ibara za 9 na 16 za Muswada Mpya zimeshafanya hivyo kwa kuainisha kazi za Tume, mipaka ya Tume katika utekelezaji wa kazi hizo na utaratibu wa namna ya kuzifanya. Kwa ajili hiyo, zaidi ya kutaka kuonyesha kwamba Rais ana mamlaka makubwa katika mchakato mzima wa upatikanaji wa Katiba Mpya, mapendekezo ya ibara ya 8 hayana maana wala sababu yoyote na yanaweza kuondolewa bila kuathiri maudhui ya Muswada. Aidha, kwa kuzingatia mapendekezo ya ibara ya 9, haijulikani Rais atatoa maelekezo gani ya ziada yanayohusu kazi za Tume na namna ya kuzitekeleza. Kwa upande mwingine, mapendekezo ya ibara ya 8 yanaweza kuleta mkanganyiko na mgogoro wa kisiasa na kisheria usiokuwa wa lazima endapo Rais atatoa hadidu za rejea zinazotofautiana na matakwa ya kisheria kama yanavyopendekezwa na ibara 9 ya Muswada Mpya. Pendekezo letu, kwa hiyo, ni kwamba ibara ya 8 ifutwe yote na ibara za 9 na 16 zifafanuliwe vizuri ili kuweka wazi zaidi hadidu za rejea za Tume na namna ya kuzitekeleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Kuna mapendekezo mengine yaliyoko kwenye Muswada yanayoonyesha hatari za Urais wa Kifalme. Kama tulivyoona, Tume inatakiwa kuwasilisha ripoti yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na kwa Rais wa Zanzibar. Baada ya hapo, kwa mujibu wa ibara ya 18(2) ya Muswada, “baada ya mashauriano na makubaliano na Rais wa Zanzibar na baada ya kumalizika kwa taratibu za ndani zinazohusu utungaji wa sera, Rais atamwelekeza Waziri kuwasilisha Muswada wa Katiba katika Bunge la Katiba kwa ajili ya kupitishwa kwa vifungu vya Katiba.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pendekezo hili ni la hatari kubwa. Kwanza, ‘kumalizika kwa taratibu za ndani zinazohusu utungaji wa sera’ maana yake ni baada ya kukamilika kwa utaratibu wa kawaida wa kiserikali unaohusu utungaji sera na sheria. Chini ya utaratibu huu, rasimu ya muswada hupelekwa kwanza kwenye Kamati ya Watalaam ya Baraza la Mawaziri (Inter Ministerial Technical Committee of the Cabinet) kwa ajili ya kufanyiwa marekebisho na Makatibu Wakuu kabla ya kupelekwa kwenye Baraza la Mawaziri kwa maamuzi ya mwisho. Baada ya maamuzi ya mwisho ya Baraza la Mawaziri, rasimu ya muswada hurudishwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili ya kuandikwa upya ndipo upelekwe Bungeni la Katiba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hatua zote hizi, muswada wa sheria huweza kufanyiwa marekebisho makubwa. Kwa maana hiyo, pendekezo la kuuwasilisha Muswada wa Katiba Mpya katika Bunge la Katiba baada ya kuupitisha kwanza kwa Makatibu Wakuu ambao wote ni wateuliwa wa Rais, na kwenye Baraza la Mawaziri ambalo wajumbe wake wote (ukiacha Makamu wa Rais na Rais wa Zanzibar) ni wateuliwa wa Rais ni kutengeneza mazingira ya kisheria yatakayoruhusu uchakachuaji wa Muswada huo kwa lengo la kuhakikisha matokeo yake ya mwisho, yaani Katiba Mpya, yanakidhi maslahi ya Rais na chama chake cha CCM. Kwa vyovyote vile, pendekezo hili halikubaliki kwa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;SIFA ZA WAJUMBE &lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Muswada Mpya unapendekeza sifa zifuatazo wanazotakiwa kuwa nazo wajumbe wa Tume: &lt;br /&gt;(a) Uzoefu katika kufanya mapitio ya katiba na sifa za kitaaluma za wajumbe kwenye mambo ya katiba, sheria, utawala, uchumi, fedha na sayansi ya jamii;&lt;br /&gt;(b) Jiografia na mtawanyiko wa watu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;&lt;br /&gt;(c) Maslahi ya umma;&lt;br /&gt;(d) Umri, jinsia na uwakilishi wa makundi mbali mbali ya kijamii; na &lt;br /&gt;(e) Vigezo vingine ambavyo Rais ataona vinafaa. (ibara ya 6(3)&lt;br /&gt;Zaidi ya sifa zilizotajwa, ibara ya 6(4) inakataza watu wenye sifa zifuatazo kuteuliwa kuwa wajumbe wa Tume:&lt;br /&gt;(a) Wabunge, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, madiwani na viongozi wa vyama vya siasa wa ngazi zote kuanzia Wilaya hadi Taifa;&lt;br /&gt;(b) Watumishi wa vyombo vya usalama;&lt;br /&gt;(c) Watu waliowahi kuhukumiwa kwa kutenda kosa au wanaotuhumiwa mahakamani kwa mashtaka ya kukosa uaminifu au uadilifu;&lt;br /&gt;(d) Watu wasiokuwa raia wa Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo haya yana athari kubwa kwa mchakato mzima wa upatikanaji wa Katiba Mpya. Kwanza, kwa kukataza viongozi wa ngazi za juu na za kati wa vyama vya siasa kuteuliwa wajumbe wa Tume kunaondoa kwenye mchakato wa Katiba Mpya kundi kubwa la watu wenye utaalamu na uzoefu katika masuala mbali mbali ya kisiasa, kikatiba, kisheria, kiuchumi, kiutawala, kifedha na kisayansi jamii. Vile vile, viongozi wa vyama vya siasa wanawakilisha makundi makubwa ya kijamii yenye mtawanyiko wa watu na wa kijiografia katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wanawakilisha watu wa umri na jinsia zote kama inavyopendekezwa katika Muswada Mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, kwa kuwa maneno ‘maslahi ya umma’ hayajafafanuliwa katika Muswada, hakuna anayeweza kudai kwamba viongozi wa ngazi za juu na za kati wa vyama vya siasa vilivyosajiliwa kisheria baada ya kutimiza masharti yote husika ya kisheria, na ambao wanaungwa mkono na mamilioni ya wananchi wa Tanzania kwa kupewa nafasi za uwakilishi katika taasisi za uwakilishi za umma kama Bunge, Baraza la Wawakilishi na Halmashauri za Serikali za Mitaa hawajui wala hawazingatii maslahi ya umma na kwa hiyo hawafai kuwakilishwa katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba! Kama ingekuwa hivyo, Rais – ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM na kwa hiyo kiongozi wa chama cha siasa – naye pia atakuwa hana sifa za kuteua Tume! Na wakati haja ya kutoshirikisha watumishi wa taasisi za ulinzi na usalama katika mchakato wenye ubishani wa kisiasa kama utungaji wa Katiba Mpya inaeleweka, ni matusi kwa watu waliochaguliwa na wananchi kuwa Wabunge, Wawakilishi au Madiwani au viongozi wa vyama vya siasa vilivyowapendekeza watu hao, kuwekwa pamoja na wahalifu na kutamkwa kuwa hawana sifa za kuteuliwa kuwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inaelekea lengo kuu la pendekezo hili ni kuhakikisha kwamba vyama vya upinzani, hasa hasa CHADEMA, vyenye ushawishi mkubwa ndani na nje ya Bunge havipati fursa ya kuamua muundo na maudhui ya Katiba Mpya hasa katika hatua muhimu za uundaji wake. Pili, lengo kuu vile vile ni kuhakikisha kuwa Rais, na kwa hiyo chama chake cha CCM, wanadhibiti mchakato wa Katiba Mpya katika hatua muhimu ya uundaji wake. Endapo watafanikiwa katika hili, Rais na chama chake cha CCM watakuwa na nafasi kubwa ya kuamua aina ya Katiba Mpya itakayotokana na mchakato walioudhibiti kama inavyopendekezwa na Muswada Mpya. Hii ni kwa sababu, kwa kutumia uzoefu wa Tume nyingine zilizopata kuteuliwa miaka ya nyuma, wajumbe wengi huwa ni watumishi au waliopata kuwa watumishi wa Serikali na/au taasisi zake. Wajumbe wa aina hii wamekuwa hawana uthubutu wa kupendekeza mabadiliko makubwa yanayohitajika katika mfumo wa utawala wa nchi yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Badala ya kukataza viongozi wa vyama vya siasa kama inavyopendekezwa na Muswada Mpya, na kwa kuzingatia nafasi ya vyama vya siasa katika historia yetu na mfumo wetu wa utawala, na kwa lengo la kuhakikisha Tume inakuwa na utaalamu, uzoefu na uhalali wa kisiasa unaohitajika, watu wanaostahili kuteuliwa kuwa wajumbe wa Tume wawe ni wale wenye sifa zinazopendekezwa na ibara ya 6(3)(a), (b), (c) na (d) ya Muswada. Kwa sababu hiyo, hakutakiwi kuwa na vigezo vingine visivyojulikana wazi kwa wananchi. Kwa maneno mengine, pendekezo la kuwa na ‘vigezo vingine ambavyo Rais ataona inafaa’ halikubaliki kwani linampa Rais mwanya wa kuteua marafiki zake au watu ambao hawana sifa zinazojulikana. Kwa maoni yetu vile vile, badala ya kuwa sababu ya disqualification, uongozi wa kuchaguliwa na wananchi katika taasisi za uwakilishi au katika vyama vya siasa unatakiwa kuwa an added advantage pale ambapo kiongozi husika ana sifa za kitaaluma zinazotakiwa! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;MISINGI MIKUU YA KITAIFA&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Muswada unapendekeza kuwepo kwa ‘misingi mikuu ya kitaifa’ ambayo Tume inatakiwa kuizingatia kwa lengo la kuihifadhi na kuidumisha. Misingi mikuu inayopendekezwa ni:&lt;br /&gt;(a) Kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano;&lt;br /&gt;(b) Uwepo wa Serikali, Bunge na Mahakama;&lt;br /&gt;(c) Mfumo wa kiutawala wa kijamhuri;&lt;br /&gt;(d) Umoja wa kitaifa, amani na utulivu;&lt;br /&gt;(e) Uchaguzi wa kidemokrasia wa mara kwa mara katika vipindi maalum kwa kuzingatia haki ya watu wote kupiga kura;&lt;br /&gt;(f) Ukuzaji na na uhifadhi wa haki za binadamu;&lt;br /&gt;(g) Utu, usawa mbele ya Sheria na mwenendo wa sheria; na&lt;br /&gt;(h) Uhuru wa kuabudu na uvumilivu wa dini nyingine. (ibara ya 9(2)&lt;br /&gt;Kifungu hiki kimefanyiwa mabadiliko kwa kufuta maneno ‘Tume itahakikisha ... kutokugusika na utakatifu (inviolability and sanctity) wa mambo yafuatayo’ yaliyokuwa katika Muswada wa Zamani, na badala yake yamewekwa maneno mapya ‘... kuhifadhi na kudumisha mambo yafuatayo....’ Mabadiliko haya yamefanywa ili kujaribu kuondoa hofu iliyojitokeza wakati wa mikutano ya kukusanya maoni ya wadau kwamba lengo la pendekezo hilo lilikuwa kuzuia mjadala juu ya masuala ya kikatiba yenye utata mkubwa kama vile suala la Muungano. Hata hivyo, hatari ya kuzuiliwa kwa mjadala juu ya misingi mikuu ya kitaifa bado haijaondolewa kwani, kwa mujibu wa ibara mpya ya 9(3), “... Tume itatoa fursa kwa watu kutoa maoni yao kwa uhuru kwa lengo la kuendeleza na kuboresha masuala hayo.” Tafsiri halisi ya maneno haya ni kwamba mjadala pekee utakaoruhusiwa juu ya ‘misingi mikuu ya kitaifa’ ni ule ambao lengo lake ni ‘kuendeleza na kuboresha masuala hayo.’ &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maoni yetu, lengo kuu la pendekezo linalohusu kuendeleza na kuboresha ‘misingi mikuu ya kitaifa’ ni kuzuia mjadala wenye kuhoji ‘kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano’ ili kuendeleza mfumo wa sasa wa Muungano wenye Serikali mbili. Hii ni kwa sababu katika mambo yote yanayopendekezwa kuwa misingi mikuu ya kitaifa, ni ‘kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano’ yenye Serikali mbili ndio ambayo imekuwa na mgogoro mkubwa kwa muda wote wa maisha ya Jamhuri ya Muungano. Ukiacha ‘ukuzaji na uhifadhi wa haki za binadamu’ ambalo lilikataliwa na Serikali ya Mwalimu Nyerere kwa miaka yote ya utawala wake, mambo mengine yote yanayotajwa kuwa ‘misingi mikuu ya kitaifa’ hayajawahi kubishaniwa kwa miaka yote ya uhai wa Jamhuri ya Muungano. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Pendekezo la ‘misingi mikuu ya kitaifa’ linastaajabisha sana kwani, kwa mujibu wa ibara ya 98(1)(b) ya Katiba ya sasa, ‘kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano, Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, madaraka ya Serikali ya Kamhuri ya Muungano, kuwapo kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano, madaraka ya Serikali ya Zanzibar, Orodha ya Mambo ya Muungano na idadi ya Wabunge kutoka Zanzibar’ ni mambo yanayoweza kubadilishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano ili mradi tu mabadiliko hayo yaungwe mkono na theluthi mbili ya Wabunge wote wa kutoka Tanzania Bara na wa Tanzania Zanzibar. Kwa sababu hiyo, pendekezo la ibara ya 9(3) ya Muswada kwamba ‘misingi mikuu ya kitaifa’ izungumzwe kwa lengo la kuiendeleza na kuidumisha tu halikubaliki kwa sababu linazuia uhuru wa kuhoji na/au kupinga mambo ambayo kwa Katiba ya sasa ni ruhusa kuyahoji, kuyapinga na/au hata kuyabadilisha! Tunapendekeza ibara ya 9(2) na (3) za Muswada zifutwe kabisa ili kuwepo na uhuru kamili wa kujadili, kwa kupinga au kuunga mkono, kila jambo linalohusika na Katiba Mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;NAFASI YA ZANZIBAR&lt;/span&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Pengine mabadiliko makubwa yaliyofanywa katika Muswada ni mapendekezo yanayohusu nafasi ya Zanzibar katika mchakato wa Katiba Mpya. Itakumbukwa kwamba moja ya masuala yaliyozua tafrani kubwa katika mchakato wa kukusanya maoni juu ya Muswada wa Zamani hasa katika kituo cha Zanzibar ni kuwepo hisia kwamba nafasi ya Zanzibar ilikuwa imepuuzwa katika Muswada huo. Muswada sio tu kwamba umetekeleza matakwa yote ya ushirikishwaji wa Zanzibar, bali umekwenda mbali zaidi kwa kuifanya Zanzibar mwamuzi wa mustakbala wote wa kikatiba wa Tanzania. Hii imefanyika kwa njia mbili: kwanza, kwa kumfanya Rais wa Zanzibar kuwa mshirika sawa wa kikatiba wa Rais wa Jamhuri ya Muungano; na pili, kwa kuipa Zanzibar nafasi kubwa ya uwakilishi katika mchakato mzima wa Katiba Mpya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;NAFASI YA RAIS WA ZANZIBAR&lt;/span&gt;&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Muswada unapendekeza kwamba utekelezaji wa mamlaka yote ya Rais, Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano lazima ufanyike kwa ‘mashauriano na makubaliano’ na Rais, Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar. Kwa mfano, ibara ya 5 inayohusu kuundwa kwa Tume inamtaka Rais ‘kushauriana na kukubaliana’ na Rais wa Zanzibar na kupata ushauri wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar. Vile vile, ibara ya 6(1) inayohusu uteuzi wa wajumbe wa Tume; ibara ya 8(1) na (2) inayohusu hadidu za rejea na kuongeza muda wa Tume; na ibara ya 13(2) inayohusu uteuzi wa Katibu wa Tume, zote zinataka kuwepo na makubaliano na Rais wa Zanzibar. Aidha, ibara ya 13(5) inayohusu uteuzi wa watendaji wengine wa Tume inalazimu makubaliano kati ya Waziri na Waziri mwenzake wa Zanzibar ambao nao ni wateuliwa wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar. &lt;br /&gt;Mamlaka ya Rais wa Zanzibar hayaishii tu kwenye uteuzi wa wajumbe na watendaji wa Tume, bali pia yanaingia hata katika uwasilishaji wa ripoti ya Tume. Kwa mujibu wa ibara 18(1) ya Muswada, mara baada ya kumaliza kazi yake, Tume itawasilisha ripoti yake kwa Rais na kwa Rais wa Zanzibar. Aidha, kwa mujibu wa ibara ya 18(2), mara baada ya kupokea ripoti hiyo, Rais, ‘baada ya kushauriana na kukubaliana’ na Rais wa Zanzibar, “... atamuagiza Waziri kuwasilisha Muswada wa Katiba katika Bunge la Katiba.” Kwa mapendekezo haya pia, Rais wa Zanzibar sio tu kwamba ana mamlaka karibu sawa na Rais wa Jamhuri ya Muungano bali pia ana kura ya turufu katika mchakato wa Katiba Mpya. Maana yake ni kwamba Rais wa Zanzibar asipopatiwa nakala ya ripoti ya Tume au asipokubaliana na Rais wa Muungano, basi Muswada wa Katiba hautawasilishwa kwenye Bunge la Katiba! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Mapendekezo haya yanaashiria kuwepo kwa mtazamo ambao chanzo chake ni Makubaliano ya Muungano kati ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika ya tarehe 25 Aprili 1964. Kwa mtazamo huo, Zanzibar ni nchi huru kama ilivyokuwa mwaka 1964 na kwa hiyo ni lazima sio tu ishirikishwe kwa usawa, bali pia lazima ikubaliane na mabadiliko yoyote ya kikatiba yanayopendekezwa na Muswada. Kama Profesa Palamagamba Kabudi wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alivyosema kwenye Semina ya Wabunge Juu ya Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba iliyofanyika tarehe 12 Novemba 2011: ‘Katika kuandika katiba mpya, wabia wa Muungano wanarudi kwa usawa.’ &lt;br /&gt;Hata hivyo, Mheshimiwa Spika, mtazamo huu sio sahihi. Kwanza kabisa, Zanzibar sio nchi huru tena kama ilivyokuwa mwaka 1964, kama ambavyo hakuna tena nchi inayoitwa Tanganyika wala serikali yake. Hii ni kwa sababu tangu kusainiwa kwa Hati za Muungano mwaka 1964, na kwa mujibu wa ibara ya 4(3) ya Katiba ya sasa, masuala yote yanayohusu Muungano kama vile Katiba ya Tanzania yamekasimiwa kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, ambayo pia imekasimiwa mamlaka juu ya masuala ya iliyokuwa Tanganyika. Masuala haya ya Muungano hayawezi kujadiliwa upya na kwa usawa kati ya nchi hizi mbili kwa vile moja kati ya nchi hizo haipo tena na iliyobaki imepoteza sehemu ya uhuru wake kutokana na Muungano huo! Hii ndio kusema hakuwezi tena kuwa na wabia wa Muungano bila kwanza kuirudisha Tanganyika kama nchi na bila kuirudisha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar yenye uhuru na mamlaka kama iliyokuwa nayo kabla ya Muungano!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, kuna dhana kwamba Rais wa Zanzibar hakushirikishwa katika mchakato wa maandalizi ya Muswada wa Zamani. Dhana hii vile vile ni potofu. Kwanza, Rais Ali Mohamed Shein mwenyewe ametamka wazi kwa waandishi wa habari kwamba alishiriki katika hatua zote za maamuzi kwenye Baraza la Mapinduzi. Pili, mujibu wa ibara ya 54(1) ya Katiba ya sasa, Rais wa Zanzibar ni mmoja wa wajumbe wa Baraza la Mawaziri la Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kwa hiyo ni mshiriki wa maamuzi yote ya Serikali hiyo. Kwa maana hiyo, maslahi ya Zanzibar yanawakilishwa ndani ya ‘chombo kikuu cha kumshauri Rais’ katika Jamhuri ya Muungano. (ibara ya 54(3) Hii ni licha ya ukweli kwamba, kwa mlolongo wa madaraka uliopo katika ibara ya 54(2), Rais wa Zanzibar sio mmoja wa wajumbe wanaoweza kuongoza mikutano ya Baraza hilo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, ndani ya Baraza la Mawaziri, Zanzibar inawakilishwa pia na Makamu wa Rais ambaye – kwa mujibu wa ibara ya 47(1) ya Katiba ya sasa – “... ndiye Msaidizi Mkuu wa Rais kuhusu mambo yote ya Jamhuri ya Muungano....” Kwa maana hiyo, mapendekezo ya Muswada yanayomfanya Rais wa Zanzibar kuwa sio tu mshiriki sawa lakini pia mwamuzi wa mustakbala wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano yanaenda kinyume sio tu na Katiba ya sasa bali pia na Hati za Muungano wenyewe. Kwa mapendekezo haya, endapo Rais wa Zanzibar hatakubaliana na uteuzi wowote wa wajumbe wa Tume au Katibu wake au watendaji wake wengine, anaweza kusimamisha mchakato mzima wa kikatiba hata kama unahusu masuala ya Tanzania Bara yasiyo ya Muungano! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;UWAKILISHI WA ZANZIBAR&lt;/span&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Ushawishi mkubwa wa Zanzibar hauishii katika kura ya turufu aliyo nayo Rais wa Zanzibar pekee yake. Zanzibar ina ushawishi mkubwa vile vile kutokana na nafasi kubwa iliyo nayo katika vyombo vya maamuzi vinavyopendekezwa na Muswada. Kwa mfano, kwa mujibu wa ibara ya 6(2), “... muundo wa Tume utazingatia msingi wa kuwepo kwa uwakilishi ulio sawa kwa kila upande wa Jamhuri ya Muungano.” Hii ina maana kwamba wajumbe wa Tume na Sekretarieti yake wanatakiwa wawe sawa kwa sawa kati ya Tanzania Bara na Zanzibar. Ikumbukwe kwamba Tume hii inatengeneza Katiba inayohusu masuala ya Muungano, ambayo ni haki kwa Zanzibar kushirikishwa kwa usawa kabisa, na vile vile masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanzania Bara ambayo Zanzibar haina haki ya kushiriki. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;BUNGE LA KATIBA &lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Eneo la pili ambalo Zanzibar ina ushawishi mkubwa kutokana na uwakilishi wake ni katika Bunge la Katiba linalopendekezwa katika Sehemu ya Tano ya Muswada. Kwa mujibu wa ibara ya 20(2), wajumbe wa Bunge la Katiba watakuwa ni wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano; wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar; mawaziri wa katiba na sheria wa Jamhuri ya Muungano na wa Zanzibar; Wanasheria Wakuu wa Jamhuri ya Muungano na wa Zanzibar; na wajumbe mia moja kumi na sita wakaoteuliwa kutoka asasi zisizokuwa za kiserikali, asasi za kidini, vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu, taasisi za elimu ya juu na makundi yenye mahitaji maalum katika jamii. Inaelekea kwamba, kwa mujibu wa ibara ya 20(4), wajumbe wasiokuwa wabunge ama wawakilishi nao pia watateuliwa na Rais licha ya kutoka nje ya mfumo wa kiserikali!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa ibara ya 66(1)(a) ya Katiba ya sasa ya Muungano, wajumbe wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ni pamoja na wabunge wa majimbo ya uchaguzi. Kwa composition ya sasa ya Bunge, kuna jumla ya majimbo ya uchaguzi 239 ambayo kati yao majimbo ya Zanzibar ni hamsini. Vile vile, kwa mujibu wa ibara ya 66(1)(c) ya Katiba, Baraza la Wawakilishi Zanzibar linawakilishwa na wabunge watano katika Bunge la Jamhuri ya Muungano. Aidha, kama inavyotakiwa na ibara ya 66(1)(b), kuna wabunge wanawake mia moja na mbili wanaojulikana kama ‘wabunge wa viti maalum.’ Kwa mgawanyo wa sasa wa wabunge hawa, idadi ya wanaotoka Zanzibar ni ishirini na tano kwa vyama vyote vyenye uwakilishi bungeni. Na mwisho, kuna wabunge wasiozidi 10 wanaoteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa ibara ya 66(1)(e). Hadi sasa, Rais ameshateua wabunge watatu ambao wote ni wa kutoka Zanzibar. Kwa hiyo, katika Bunge la sasa lenye wabunge 353, wabunge wanaowakilisha Zanzibar ni themanini na tatu au karibu 23.5% ya wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa Sehemu ya Kwanza ya Sura ya Tano ya Katiba ya Zanzibar, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar ni pamoja na wawakilishi wa majimbo hamsini ya uchaguzi, wawakilishi kumi wa kuteuliwa na Rais wa Zanzibar na wawakilishi ishirini wa viti maalum na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa hiyo, jumla ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa sasa ni themanini na moja. Kwa maana nyingine ni kwamba endapo mapendekezo ya ibara ya 20(1)(b), (c) na (d) ya Muswada yatakubaliwa, idadi ya wajumbe wa Bunge la Katiba wanaotoka Zanzibar itaongezeka hadi kufikia mia moja sitini na nne kati ya wajumbe 545 wa Baraza hilo kwa mujibu wa ibara ya 20(2). Idadi hii ni sawa na 30% ya wajumbe wote wa Bunge la Katiba. &lt;br /&gt;Idadi hiyo ya uwakilishi wa Zanzibar bado haitakidhi matakwa ya Muswada kwani ibara ya 20(3) inapendekeza kwamba “... idadi ya wajumbe wa Baraza la Katiba kutoka Tanzania Zanzibar ... haitapungua theluthi moja ya wajumbe wote wa Bunge la Katiba”! Theluthi moja ya wajumbe wa Bunge la Katiba ni wajumbe 182. Kwa hiyo ili kukidhi matakwa ya Muswada kuhusu uwakilishi wa Zanzibar, itabidi wajumbe 18 kati ya 116 waliotajwa na ibara ya 20(2)(e) watoke Zanzibar ili kufikisha idadi ya wajumbe 182 ambayo ndio theluthi moja ya wajumbe wote wa Bunge la Katiba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Kuna maeneo mengine ya Muswada ambayo pia yanazua maswali mengi juu ya nafasi ya Zanzibar katika mchakato wa Katiba Mpya. Kwa mfano, wakati ibara ya 21(1) inapendekeza kwamba Spika na Naibu Spika wa Bunge la Katiba wachaguliwe kutoka miongoni mwa wajumbe wa Bunge hilo, ibara ya 21(2) inapendekeza kwamba endapo Spika atatoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano basi Naibu wake lazima atoke upande mwingine. Sambamba na pendekezo hili, ibara ya 22(1) inapendekeza Makatibu wa sasa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar watakuwa ndio Katibu na Naibu Katibu wa Bunge la Katiba. Aidha, sawa na ibara ya 21(2), ibara ya 22(2) inapendekeza kwamba endapo Spika atatoka upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano, basi Katibu wa Bunge la Katiba lazima atoke upande mwingine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo haya yanaonyesha sio tu nafasi na ushawishi mkubwa wa Zanzibar katika mchakato wa Katiba Mpya, bali pia ni mwendelezo wa dhana potofu kwamba Zanzibar ni mshirika sawa wa Jamhuri ya Muungano. Hii inathibitishwa pia na pendekezo la ibara ya 24(3) ya Muswada inayotaka Katiba Mpya ikubaliwe na theluthi mbili ya wajumbe wa Bunge la Katiba wanaotoka Tanzania Bara na vile vile theluthi mbili ya wajumbe wanaotoka Zanzibar. Ni wazi, kwa hiyo, kwamba iwe ni kwa masuala ya Muungano yanayoihusu Zanzibar pia, au kwa masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanzania Bara ambayo hayaihusu, Zanzibar itakuwa na kura ya turufu kwa mujibu wa mapendekezo ya Muswada huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Uwakilishi mkubwa wa Zanzibar katika Bunge la Jamhuri ya Muungano umetumika kihistoria kwa lengo la kuwatuliza Wazanzibari wakati Serikali ya Mwalimu Nyerere ilipokuwa inamomonyoa uhuru wa Zanzibar kwa kuongeza orodha ya Mambo ya Muungano kwenye Katiba ya Muungano. Katika kitabu chake Pan Africanism or Pragmatism? Lessons of Tanganyika – Zanzibar Union, Profesa Issa Shivji, mwanazuoni mashuhuri wa kikatiba na mwanafunzi wa historia ya Muungano huu amemnukuu aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar wakati wa utawala wa hayati Sheikh Abedi Amani Karume, Bw. Wolfgang Dourado akimnukuu Sheikh Karume juu ya nafasi ya Zanzibar katika Bunge la Jamhuri ya Muungano: “‘Msiwe na wasi wasi, sisi tuna haki ya kuwakilishwa katika Bunge lao lakini wao hawana haki ya kuwakilishwa katika Baraza letu la Mapinduzi’”!&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Sababu nyingine inatokana na kuongezeka kwa ushawishi na nafasi ya Zanzibar katika siasa za ndani ya CCM, hasa hasa katika zama hizi za vyama vingi na vita za makundi mbali mbali ndani ya chama hicho. Katika mazingira haya, mtu yeyote anayetaka kupitishwa kuwa mgombea urais kwa kupitia CCM anakuwa anahitaji kura za CCM Zanzibar ili kushinda katika kinyang’anyiro hicho. Kwa kauli ya Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere mwenyewe katika kitabu chake Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, “sababu moja kubwa iliyofanya viongozi wetu wasitake kuwaudhi ‘Wazanzibari’ ... ni umuhimu wa kura za Zanzibar katika kumteua mwanachama wa CCM kuwa Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano. Kwa kiongozi yeyote anayeliona jambo hilo kuwa ni muhimu kupita mengine yote, kuwaudhi ‘Wazanzibari’ ni dhambi ambayo haina budi iepukwe kwa kila njia.” Kwa maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, hofu hii ya kuwaudhi ‘Wazanzibari’ ndio imepelekea kimya kikuu – ndani ya CCM na ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano - juu ya ukiukwaji mkubwa wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano uliofanywa na Sheria ya Mabadiliko ya Kumi ya Katiba ya Zanzibar, 2010.&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba upendeleo wa Zanzibar unaopendekezwa katika Muswada huu kuhusiana na uwakilishi katika Bunge la Katiba na katika vyombo vingine vya maamuzi juu ya mchakato wa Katiba Mpya sio wa haki na haukubaliki tena. Kwanza, ibara ya 64(2) ya Katiba ya sasa inaweka wazi kwamba Baraza la Wawakilishi Zanzibar lina mamlaka ya kutunga sheria katika Zanzibar ‘... juu ya mambo yote yasiyo mambo ya Muungano....’ Hii pia ndio lugha ya ibara ya 78(1) ya Katiba ya Zanzibar kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka jana. ‘Katiba ya Tanzania’ ni jambo la kwanza katika orodha ya Mambo ya Muungano iliyoko kwenye Nyongeza ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Kwa Muswada Mpya kupendekeza kwamba Baraza la Wawakilishi Zanzibar liwe sehemu ya Bunge la Katiba ni kukiuka wazi wazi matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano na ya Katiba ya Zanzibar. Ni ajabu iliyoje kwamba wale wanaojifanya ni machampioni wa Muungano wanaweza kunyamazia ukiukaji huu wa Katiba!&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Thomas Paine, mwandishi maarufu wa Marekani ya wakati wa Mapinduzi ya mwaka 1776, aliwahi kuandika kijitabu alichokiita Common Sense juu ya uhalali wa Uingereza kutawala Bara la Amerika ya Kaskazini ambako alisema: ‘... [T]here is something very absurd in supposing a continent to be perpetually governed by an island [for] in no instance hath nature made the satellite larger than its primary planet...’! Yaani, ni ujinga kudhani kwamba bara linaweza kutawaliwa milele na kisiwa kwa sababu utaratibu wa asili haujawahi kufanya kitegemezi kuwa kikubwa kuliko sayari yake ya msingi. Hata kama ni kweli kwamba Tanganyika sio bara kama ilivyokuwa Marekani ya Kaskazini, bado tunakubaliana na Tom Paine kwamba ni ujinga kudhani kwamba Visiwa vya Zanzibar vitaendelea kuwa na maamuzi na ushawishi mkubwa katika masuala yasiyokuwa ya Muungano ya Tanganyika kwa sababu utaratibu wa asili haujawahi kufanya maslahi ya Visiwa hivyo kuwa bora zaidi ya maslahi ya Tanganyika! &lt;br /&gt;Kwa maoni yetu, wakati umefika kwa Muungano kuwekwa kwenye msingi wa usawa na imara zaidi. Msingi huo unahitaji kurudishwa tena kwa Serikali ya Tanganyika ambayo ndio ilikuwa – pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar – mbia mkuu wa Muungano wa mwaka 1964. Kurudishwa huko kwa Tanganyika kutaiwezesha Zanzibar kujadiliana nayo kwa usawa juu ya masuala yote yanayohusu Muungano. Haya yote yanawezekana tu endapo Muungano huu utawekwa mbele ya wananchi ili waamue – kwa kura ya maoni - kama wanataka kuendelea nao au la; na kama wanataka kuendelea nao ni muundo gani wa Muungano wanaoutaka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Mapendekezo ya kurudishwa kwa Tanganyika na Serikali yake sio mapya. Miaka ishirini iliyopita, Tume ya Rais ya Mfumo wa Chama Kimoja au Vyama Vingi vya Siasa (Tume ya Nyalali) ilipendekeza hivyo hivyo. Miaka saba baadae, Tume ya Kukusanya Maoni Juu ya Katiba, White Paper Na. 1 ya 1998 (Tume ya Kisanga) nayo ilipendekeza hivyo hivyo. Kuendelea kupuuza mapendekezo haya wakati Zanzibar inavunja Katiba ya sasa ya Muungano; kuendelea kukaa kimya kwa hofu ya kuwaudhi ‘Wazanzibari’ wakati wao wanajitwalia uhuru wa kujiamulia mambo yao wenyewe huku wakiendelea kushiriki katika maamuzi ya mambo ya Tanganyika yasiyokuwa ya Muungano; kuendeleza kile alichokiita Mwalimu Nyerere falsafa ya ‘changu ni changu, chako ni chetu’ katika mahusiano ya Zanzibar na Tanzania Bara, ni kutulazimisha tuipinge dhana nzima ya Muungano kati ya nchi zetu mbili kitu kinachoweza kupelekea kuvunjika kwa Muungano wenyewe. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni isingependa tufike huko lakini ndoa hii ya kulazimishana haiwezi ikadumu muda mrefu kwa taratibu za aina hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;UDHOOFISHAJI WA UPINZANI&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Mapendekezo ya Muswada juu ya uwakilishi katika Bunge la Katiba yana athari nyingine kubwa katika majadiliano na maamuzi ndani ya Bunge la Katiba. Kwa mujibu wa uchambuzi uliofanywa na Profesa Issa G. Shivji kwa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala, endapo mapendekezo ya ibara ya 20(2) ya Muswada yatapitishwa, CCM itakuwa na kati ya wajumbe 350 hadi 400 katika Bunge la Katiba ambalo lina wajumbe 545. Kwa upande mwingine Chama cha Wananchi (CUF) ambacho kina Wawakilishi 29 katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar kitakuwa na wajumbe 65 katika Bunge la Katiba. Kwa maana ya uwakilishi katika Bunge la Katiba, CUF itakuwa ndio chama cha pili kwa nguvu za kisiasa ndani ya Bunge hilo, licha ya kuwa na wabunge wawili tu wa kuchaguliwa kwa upande wa Tanzania Bara na licha ya kupata kura chache sana katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kama inavyojulikana, tangu Muafaka wa Kisiasa Zanzibar kati ya CCM na CUF wa mwaka 2010 na kuzaliwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, upinzani wa kisiasa Zanzibar umekufa na kwa upande wa Tanzania Bara, na hasa Bungeni na kwenye chaguzi ndogo kama ule wa Igunga, CUF imekuwa ikishirikiana na CCM kuipinga CHADEMA. Kwa mapendekezo haya, kambi ya CCM na CUF katika Bunge la Katiba inaweza kufika hata zaidi ya wajumbe 465 katika ya wajumbe 545 wa Bunge hilo! CHADEMA ambayo kwa sasa ndio chama kinachoongoza Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kutokana na matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2010, itabakia na Wabunge wake 48 na vyama vya kibunge vilivyobaki, yaani NCCR-Mageuzi, TLP na UDP vitabaki na jumla ya Wabunge sita. Kwa hiyo, CHADEMA itakuwa chama cha tatu kwa nguvu za kisiasa ndani ya Bunge la Katiba licha ya kuwa ni chama kikuu cha upinzani chenye nguvu na ushawishi mkubwa wa kisiasa nchini! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maana nyingine, iwe ni kwa makusudi au bila ya kujua au kwa kunuia, athari mojawapo kubwa ya mapendekezo ya Muswada kuhusu uwakilishi katika Bunge la Katiba itakuwa ni kuiongezea nguvu zaidi kambi ya CCM/CUF na kupunguza nguvu na ushawishi wa CHADEMA ambayo ndio chama pekee kinachobeba matarajio na matamanio ya Watanzania wengi wanaotaka mabadiliko ya kimsingi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii katika nchi yetu. Haihitaji kuwa na shahada ya uzamivu kujua kwamba Bunge la Katiba lenye uwakilishi wa aina hii litapitisha Katiba Mpya ambayo pengine itatofautiana na Katiba ya sasa kwa jina tu! Na wala haihitaji kisomo kikubwa kujua kwamba Bunge la Katiba la aina hii halitagusa ‘msingi mkuu’ uliobaki wa Jamhuri ya Muungano, yaani Serikali mbili. Hapa pia ni wazi kuwa lengo halisi la mapendekezo haya ni kuhakikisha kwamba mchakato wa Katiba Mpya utazaa matunda yasiyokuwa tofauti sana na ya Katiba ya sasa!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;‘UWAKILISHI’ WA BUNGE LA KATIBA &lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika,&lt;br /&gt;Sio Bunge hili tukufu la Jamhuri ya Muungano wala Baraza la Wawakilishi Zanzibar lenye mamlaka kikatiba na kisiasa ya kutunga Katiba Mpya ya Tanzania. Hii ni kwa sababu sisi wote tulioko humu ndani tulichaguliwa kwa mujibu wa Katiba ya sasa na mamlaka yetu yote yako ndani ya kona nne za Katiba hiyo. Kama ni kweli, kama anavyodai Profesa Kabudi, kwamba kitendo cha kutunga Katiba Mpya vile vile ni kitendo cha kuua Katiba ya Zamani, basi sisi Wabunge na Wawakilishi wa Zanzibar hatuna mamlaka ya kuiua Katiba ya sasa kwa sababu sisi wote tulikula kiapo cha kuilinda, kuihifandhi na kuitetea. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, sisi sote ni Wabunge na Wawakilishi wa vyama vya siasa kwa sababu, kwa mujibu wa Katiba ya sasa sheria zote husika, tumechaguliwa kwa sifa kuu ya kuwa wanachama wa, na tuliopendekezwa na, vyama vya siasa. Kuligeuza Bunge la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Wawakilishi Zanzibar kuwa Bunge la Katiba ni sawa na kusema kwamba wasiokuwa wanachama wa vyama vya siasa hawana haki ya kushiriki katika kutunga Katiba Mpya kwa sababu ya kuwa na kilema cha kisheria kinachowakataza kuchaguliwa kuwa Wabunge na Wawakilishi! Ibara ya 20(4) ya Katiba ya sasa inatamka wazi kwamba “... ni marufuku kwa mtu yeyote kulazimishwa kujiunga na chama chochote....” Sio kosa, kwa hiyo, kwa mamilioni ya Watanzania ambao wameamua kwa hiari zao kutokuwa wanachama wa vyama vya siasa. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haikubaliani, na haiwezi kukubali, ubaguzi wa aina hii dhidi ya Watanzania walioamua kutumia haki zao za kikatiba ya kutokujiunga na chama chochote cha siasa. Aidha, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haitakubali Watanzania hao waadhibiwe kwa kunyimwa kushiriki katika Bunge la Katiba kwa sababu tu ya kutokuwa wanachama wa vyama vya siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, wajumbe 116 wanaopendekezwa kuteuliwa kwenye Bunge la Katiba kwa mujibu wa ibara ya 20(2)(e) na (4) ya Muswada Mpya sio, na hawawezi kuwa, wawakilishi wa wananchi. Kwanza, hawajachaguliwa na mtu yeyote na wala taasisi zao kuwawakilisha katika Bunge la Katiba kwa sababu Muswada Mpya unapendekeza wateuliwe na Rais. Pili, Bunge la Katiba ni chombo cha uwakilishi wa moja kwa moja wa wananchi na kwa mila na desturi zinazokubalika na kutumika kimataifa, wajumbe wa Bunge la Katiba huchaguliwa moja kwa moja na wananchi bila ya kujali vyama vya siasa na huwa na kazi moja tu: kutunga Katiba Mpya. Kwa sababu zote hizi, Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza wajumbe wa Bunge la Katiba wachaguliwe moja kwa moja na wananchi na kusiwe na masharti yoyote kuhusu uanachama wa vyama vya siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;UHALALISHAJI WA KATIBA MPYA&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Muswada una mapendekezo ambayo yanaashiria kuachana na utaratibu wa kihistoria wa utungaji wa Katiba ambao umewaweka wananchi kando katika michakato wa kikatiba tangu miaka ya mwanzo ya uhuru. Kwa mujibu wa ibara ya 27(1), kutakuwa na kura ya maoni kwa lengo la kuihalalisha Katiba Mpya. Kwa mujibu wa ibara ya 30, watu wote walioandikishwa kuwa wapiga kura kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi ya Taifa na Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, watakuwa na haki ya kupiga kura katika kura hiyo ya maoni. Aidha, kufuatana na ibara ya 32(2), matokeo ya kura ya maoni yataamuliwa kwa msingi wa kuungwa mkono kwa zaidi ya 50% ya kura zote zilizopigwa Tanzania Bara na kiasi hicho hicho kwa Zanzibar. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapendekezo ya ushirikishwaji wa wananchi katika kuipa Katiba uhai wa kisheria ni jambo la maana sana na linaonyesha kuwa tumeanza kuachana na urithi wa kikatiba wa kikoloni ulioanza na Katiba ya Uhuru ya mwaka 1961. Hata hivyo, mapendekezo haya yamejaa mitego na vichaka vingi vya hatari. Kwanza, ibara ya 27 inapendekeza kwamba kura ya maoni itaratibiwa na kusimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Tume hizi mbili – kwa mashauriano na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar - ndizo zitakazotengeneza swali litakaloulizwa kwenye kura ya maoni. (ibara ya 28(1) na (2) Aidha, kwa mujibu wa ibara ya 31, utaratibu utakaotumika katika kura ya maoni ni ule unaotumika katika chaguzi za kawaida katika nchi yetu, yaani Sheria ya Uchaguzi wa Taifa, Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292 na Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inarudia kauli yake ndani ya Bunge hili wakati wa kujadili Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria tarehe 24 Agosti, 2011: “Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haina imani, sio tu na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, bali pia na mfumo mzima wa kisheria na kitaasisi unaoendesha chaguzi za nchi yetu. Mfumo huu na watendaji wake wameonyesha wazi kutokuwa huru na kutumiwa na Chama cha Mapinduzi kuchakachua matokeo ya chaguzi mbali mbali hapa nchini. Kwa maana hiyo, Tume ya Uchaguzi ya Taifa, na ile ya Zanzibar, haiwezi kuachiwa jukumu kubwa la kuendesha kura ya maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya. Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba Serikali ilete bungeni muswada wa mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba na ya sheria husika za uchaguzi kwa lengo la kuiunda upya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa lengo la kuhakikisha inasimamia zoezi la kura ya maoni kwa uhuru na bila upendeleo kwa chama tawala.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna maeneo mengine ambayo nayo yanaonyesha kwamba lengo halisi la Muswada huu ni kupata Katiba ambayo haitabadilisha mambo ya msingi ila itakuwa mpya kwa jina tu. Kwanza, ibara ya 26(2) inapendekeza kumpa Rais mamlaka ya “kuliitisha tena Bunge la Katiba lenye wajumbe wale wale siku zijazo kwa ajili ya kutunga masharti ya katiba kabla ya kuizindua Katiba inayopendekezwa kwa lengo la kurekebisha masharti yaliyomo kwenye Katiba iliyopendekezwa.” Maana halisi ya maneno haya ni kwamba Rais atakuwa na mamlaka ya kuita tena Bunge la Katiba ili lifanye marekebisho ya mambo ambayo yeye au serikali yake au chama chake hawayapendi katika Katiba Mpya kabla haijapigiwa kura ya maoni na wananchi! Kama chombo huru cha wananchi, Rais hawezi kujipa madaraka ya kupingana na kauli ya wananchi kupitia Bunge la Katiba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, wakati ibara ya 32(3) inapendekeza kurudiwa kwa kura ya maoni endapo kura za ‘NDIYO’ na ‘HAPANA’ zitalingana, ibara ya 32(4) inaelekeza kwamba “endapo wingi wa kura ya maoni utakuwa ni ‘HAPANA’, Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977, itaendelea kutumika.” Endapo pendekezo hili litapitishwa na kuwa sheria, hii itakuwa ni kualika maasi kwa vile, kwa vyovyote vile, wananchi wa Tanzania – baada ya kupitia mchakato mrefu wa kutengeneza Katiba Mpya – hawatakubali tena kuvishwa minyororo ya Katiba ya sasa. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza kwamba badala ya kurudi kwenye status quo ante kama inavyopendekezwa, mchakato wa Katiba Mpya uanze tena hadi hapo utakapopatikana muafaka wa kitaifa wa katiba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;HITIMISHO&lt;/span&gt; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, &lt;br /&gt;Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, 2011 ni Muswada muhimu kuliko pengine miswada yote ambayo Bunge la Kumi litapata fursa ya kuijadili na kuipitisha. Ni muswada wa kihistoria kwa vile, tangu uhuru wa Tanganyika miaka hamsini iliyopita, na tangu Muungano miaka karibu arobaini na nane iliyopita, Watanzania hatujawahi kupata fursa ya kujadili na kuamua mustakbala wa taifa letu kikatiba kwa utaratibu kama unaopendekezwa katika Muswada huu. Hata hivyo, kwa jinsi ambavyo Muswada huu ulivyoandaliwa na kwa maudhui yake na kwa jinsi ulivyoletwa Bungeni kwa kukiuka makusudi Kanuni za Bunge, ni wazi – kama utapitishwa jinsi ulivyo – Watanzania tutakuwa tumekosa fursa ya kuamua mustakbala wa taifa letu kwa njia ya amani na maridhiano. Bunge hili tukufu lina wajibu mbele ya historia na kwa vizazi vya sasa na vijavyo, kuhakikisha kwamba tunapata muafaka wa kitaifa juu ya Tanzania tunayoitaka. Hukumu ya historia, endapo Bunge hili tukufu litaendekeza ushabiki wa kisiasa na kufanya maamuzi ya mambo makubwa kama haya kwa kupiga kelele au kwa kuzomea au kwa kugonga meza kwa nguvu, itakuwa ni kali sana. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haiwezi kuwa sehemu ya maamuzi makubwa kama yanayopendekezwa na Muswada huu bila kwanza wananchi wa Tanzania na Wabunge wenyewe kupata muda wa kutosha wa kuyatafakari masuala haya yote kwa uzito unaoyastahili na kuyafanyia maamuzi ya busara. &lt;br /&gt;Kwa sababu hizi zote, Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja chini ya kanuni ya 86(3)(b) ya Kanuni za Kudumu za Bunge hili tukufu kwamba Bunge hili likatae Muswada huu Kusomwa Mara ya Pili kwa sababu Serikali imeleta Muswada Mpya na wenye mabadiliko makubwa na ya msingi bila kufuata masharti ya kanuni ya 84(3) ya Kanuni za Kudumu za Bunge; na pia kwa sababu Serikali haijatekeleza maagizo ya Bunge hili tukufu kuhusu kutoa muda zaidi kwa Kamati na wananchi kuufikiria, kuuelewa na kuutolea maoni Muswada huu kinyume na matakwa ya ibara ya 18(a) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano juu ya uhuru wa wananchi kutoa maoni yao; ibara ya 21(1) na (2) juu ya haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wan chi, na haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayowahusu wananchi, maisha yao au yanayolihusu Taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tundu Antiphas Mughwai Lissu (MB)&lt;br /&gt;MSEMAJI, KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI&amp; WAZIRI KIVULI, KATIBA NA SHERIA&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-5637547704082990131?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/5637547704082990131/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=5637547704082990131' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5637547704082990131'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5637547704082990131'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/maoni-ya-msemaji-mkuu-wa-kambi-rasmi-ya.html' title='MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA KATIBA NA   SHERIA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU (MB.)'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-4822288792219852812</id><published>2011-11-12T01:03:00.000-08:00</published><updated>2011-11-12T01:20:06.076-08:00</updated><title type='text'>Matumizi ya nguvu katika mgomo Chuo Kikuu DSM jana, 11.11.11</title><content type='html'>Poleni wanafunzi na jumuiya ya Chuo Kikuu cha DSM (UDSM), ni aibu kwamba mpaka mgomo na mabomu ndio serikali ichukue hatua kwa madai ya mikopo kucheleweshwa na kupewa kwa masharti yenye kuumiza watoto wa watanzania wa kawaida.Kila binadamu anayo haki ya kusoma!Ni moja ya haki ya msingi ktk haki za kibinadamu. Nasikitika siko pamoja nanyi jimboni Ubungo ktk wakati huu mgumu, nitachukua hatua za kibunge huku Dodoma-Bungeni.Kwa Pamoja Tunaweza!!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/-mArojKbL1Ww/Tr44ZWvsamI/AAAAAAAAAic/yrFqF6xNdZM/s1600/UDSM7.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 184px; height: 275px;" src="http://2.bp.blogspot.com/-mArojKbL1Ww/Tr44ZWvsamI/AAAAAAAAAic/yrFqF6xNdZM/s320/UDSM7.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5674034588786911842" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-BKh8fGpVtGU/Tr44ZA7yaHI/AAAAAAAAAiU/r6hxqNkmg40/s1600/UDSM6.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 228px; height: 221px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-BKh8fGpVtGU/Tr44ZA7yaHI/AAAAAAAAAiU/r6hxqNkmg40/s320/UDSM6.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5674034582932056178" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-PiM3mEaBemg/Tr43ECKCQHI/AAAAAAAAAiI/H7rT6Ghhr-4/s1600/UDSM5.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 274px; height: 184px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-PiM3mEaBemg/Tr43ECKCQHI/AAAAAAAAAiI/H7rT6Ghhr-4/s320/UDSM5.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5674033122971369586" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/-1bHeY_Jj8oQ/Tr43DlwpyFI/AAAAAAAAAh8/wmQprjsfuFE/s1600/UDSM4.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 210px; height: 240px;" src="http://4.bp.blogspot.com/-1bHeY_Jj8oQ/Tr43DlwpyFI/AAAAAAAAAh8/wmQprjsfuFE/s320/UDSM4.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5674033115348715602" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/-q8QVGTh41YU/Tr43C28sqeI/AAAAAAAAAhw/20Da-ZwyR4k/s1600/UDSM3.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 194px; height: 259px;" src="http://4.bp.blogspot.com/-q8QVGTh41YU/Tr43C28sqeI/AAAAAAAAAhw/20Da-ZwyR4k/s320/UDSM3.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5674033102782769634" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-A-MtdnY2f7k/Tr43CsF2NFI/AAAAAAAAAhg/3kFX3cqKVf4/s1600/UDSM2.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 274px; height: 184px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-A-MtdnY2f7k/Tr43CsF2NFI/AAAAAAAAAhg/3kFX3cqKVf4/s320/UDSM2.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5674033099868353618" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/-WwD5CbF58N4/Tr43CQ0CxYI/AAAAAAAAAhY/rIkdeIPMXQg/s1600/UDSM1.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://4.bp.blogspot.com/-WwD5CbF58N4/Tr43CQ0CxYI/AAAAAAAAAhY/rIkdeIPMXQg/s320/UDSM1.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5674033092545922434" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-style:italic;"&gt;Shukrani Chanzo za Picha: Mtandao wa JamiiForums&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimehuzunika sana baada ya kuona picha hizi na habari katika vyombo mbalimbali vya habari. Nipo pamoja nanyi!&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-4822288792219852812?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/4822288792219852812/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=4822288792219852812' title='10 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4822288792219852812'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/4822288792219852812'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/matumizi-ya-nguvu-katika-mgomo-chuo.html' title='Matumizi ya nguvu katika mgomo Chuo Kikuu DSM jana, 11.11.11'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://2.bp.blogspot.com/-mArojKbL1Ww/Tr44ZWvsamI/AAAAAAAAAic/yrFqF6xNdZM/s72-c/UDSM7.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>10</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-8443043251251577566</id><published>2011-11-10T06:05:00.000-08:00</published><updated>2011-11-10T06:06:59.551-08:00</updated><title type='text'>Katika kuchochea ukuzwaji wa Michezo!</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-DI3phKcDwQI/TrvaXBV3SDI/AAAAAAAAAhM/CgKzQMG-yTo/s1600/JJ%2Bna%2Bmpira%2B2.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-DI3phKcDwQI/TrvaXBV3SDI/AAAAAAAAAhM/CgKzQMG-yTo/s320/JJ%2Bna%2Bmpira%2B2.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673368244635256882" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/-lS1-s0Wp11c/TrvaW6ThONI/AAAAAAAAAhA/rWPvD8tS5Fw/s1600/JJ%2Bna%2Bmpira.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://2.bp.blogspot.com/-lS1-s0Wp11c/TrvaW6ThONI/AAAAAAAAAhA/rWPvD8tS5Fw/s320/JJ%2Bna%2Bmpira.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673368242746374354" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-8443043251251577566?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/8443043251251577566/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=8443043251251577566' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8443043251251577566'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8443043251251577566'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/katika-kuchochea-ukuzwaji-wa-michezo.html' title='Katika kuchochea ukuzwaji wa Michezo!'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/-DI3phKcDwQI/TrvaXBV3SDI/AAAAAAAAAhM/CgKzQMG-yTo/s72-c/JJ%2Bna%2Bmpira%2B2.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-7136767749642118949</id><published>2011-11-10T05:44:00.000-08:00</published><updated>2011-11-10T05:56:21.726-08:00</updated><title type='text'>05/11/2011: Kituo cha Polisi Mbezi kwa Yusuf-Kufatilia viongozi wa CHADEMA waliokamatwa sambamba na vifaa</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-g1JtnBy_LA0/TrvWbrnxVeI/AAAAAAAAAgw/Rdg5lGOUASs/s1600/IMG00186-20111105-1849.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-g1JtnBy_LA0/TrvWbrnxVeI/AAAAAAAAAgw/Rdg5lGOUASs/s320/IMG00186-20111105-1849.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673363926657619426" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-t_zDGxbka3o/TrvWa-aC46I/AAAAAAAAAgo/9v0-UxNxoxE/s1600/IMG00180-20111105-1848.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-t_zDGxbka3o/TrvWa-aC46I/AAAAAAAAAgo/9v0-UxNxoxE/s320/IMG00180-20111105-1848.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673363914520454050" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-wcwIVowKRvE/TrvWafjeq9I/AAAAAAAAAgY/FvSK9_knnGY/s1600/IMG00188-20111105-1849.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-wcwIVowKRvE/TrvWafjeq9I/AAAAAAAAAgY/FvSK9_knnGY/s320/IMG00188-20111105-1849.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673363906238524370" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/-n8O-Rteq1Wc/TrvWZzyB19I/AAAAAAAAAgM/KwOipY3MMk0/s1600/IMG00175-20111105-1831.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://2.bp.blogspot.com/-n8O-Rteq1Wc/TrvWZzyB19I/AAAAAAAAAgM/KwOipY3MMk0/s320/IMG00175-20111105-1831.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673363894488389586" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/-LPCrYGf37Ng/TrvWZ0rTIvI/AAAAAAAAAgA/_mSaCrBuvsw/s1600/IMG00173-20111105-1719.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://4.bp.blogspot.com/-LPCrYGf37Ng/TrvWZ0rTIvI/AAAAAAAAAgA/_mSaCrBuvsw/s320/IMG00173-20111105-1719.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673363894728598258" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kufanya mkutano eneo la Ubungo mkabala na kituo cha mabasi ya Daladala, niliongozana na wananchi ambao kwa hiari yao wenyewe walipatwa utashi kuungana nami kwenda kituo cha Polisi Mbezi kwa Yusuf kufatilia viongozi, wanachama wa chadema na vifaa mbalimbali Jeshi la Polisi lilivikamata kabla ya kuanza kwa mkutano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya mvutano wa muda mrefu takribani masaa mawili na nusu ndipo Jeshi la Polisi lilikubali kuachia vifaa vyote na viongozi/wanachadema waliokamatwa.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-7136767749642118949?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/7136767749642118949/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=7136767749642118949' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7136767749642118949'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7136767749642118949'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/05112011-kituo-cha-polisi-mbezi-kwa.html' title='05/11/2011: Kituo cha Polisi Mbezi kwa Yusuf-Kufatilia viongozi wa CHADEMA waliokamatwa sambamba na vifaa'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/-g1JtnBy_LA0/TrvWbrnxVeI/AAAAAAAAAgw/Rdg5lGOUASs/s72-c/IMG00186-20111105-1849.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-6434193119570635077</id><published>2011-11-10T05:26:00.000-08:00</published><updated>2011-11-10T05:43:52.912-08:00</updated><title type='text'>Mkutano wa 05/11/2011:Kutoa mrejesho wa utendaji mwaka 1 na kukusanya maoni ya wananchi!</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://1.bp.blogspot.com/-QcYMYLbkx08/TrvST_-8u5I/AAAAAAAAAf0/DswJ7a5aBb8/s1600/IMG00169-20111105-1716.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://1.bp.blogspot.com/-QcYMYLbkx08/TrvST_-8u5I/AAAAAAAAAf0/DswJ7a5aBb8/s320/IMG00169-20111105-1716.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673359396638079890" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/-crQplOskcsA/TrvSTCXNOII/AAAAAAAAAfo/Gj-MkNx5XDc/s1600/IMG00168-20111105-1715.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://3.bp.blogspot.com/-crQplOskcsA/TrvSTCXNOII/AAAAAAAAAfo/Gj-MkNx5XDc/s320/IMG00168-20111105-1715.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673359380096825474" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://4.bp.blogspot.com/-Gq-suFEy624/TrvSS7ubluI/AAAAAAAAAfY/uH4oSW4ObtI/s1600/IMG00167-20111105-1715.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://4.bp.blogspot.com/-Gq-suFEy624/TrvSS7ubluI/AAAAAAAAAfY/uH4oSW4ObtI/s320/IMG00167-20111105-1715.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673359378315187938" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://2.bp.blogspot.com/-gcoqHraY8sM/TrvSSpH2HXI/AAAAAAAAAfQ/mWooYmU0v8A/s1600/IMG00166-20111105-1715.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 240px;" src="http://2.bp.blogspot.com/-gcoqHraY8sM/TrvSSpH2HXI/AAAAAAAAAfQ/mWooYmU0v8A/s320/IMG00166-20111105-1715.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5673359373321510258" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ni mkutano ambao niliufanya katika kata ya Ubungo ndani ya Jimbo la UBUNGO baada ya maombi ya wananchi wengi kuufanyia mkutano huo katika kata hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Licha ya kufuata taratibu zote za kutoa taarifa polisi, Jeshi la Polisi lilitoa amri ndani ya muda mfupi sana kusitisha mkutano huu. Sikurudi nyuma! Niliufanya mkutano huu. Nashukuru sana wananchi ambao walijitokeza kwa wingi sana. Nawashukuru sana wananchi ambao licha ya hofu na vitisho ambavyo Jeshi la Polisi ilivitoa walikuwa mstari wa mbele kuhudhuria mkutano. Nawashukuru pia wananchi walionipa kipaza sauti baada ya vifaa vilivyoandaliwa kwa ajili ya mkutano kukamatwa na Jeshi la Polisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Napenda kuwapa pole viongozi wenzangu wote sambamba, wanachadema na wananchi wote ambao walipata misukosuko ya kukamatwa na Polisi siku ile, Novemba 5, 2011. Daima; Aluta continua!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukumbuke: "SIASA SI UADUI"!&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-6434193119570635077?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/6434193119570635077/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=6434193119570635077' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6434193119570635077'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6434193119570635077'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/mkutano-wa-05112011kutoa-mrejesho-wa.html' title='Mkutano wa 05/11/2011:Kutoa mrejesho wa utendaji mwaka 1 na kukusanya maoni ya wananchi!'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://1.bp.blogspot.com/-QcYMYLbkx08/TrvST_-8u5I/AAAAAAAAAf0/DswJ7a5aBb8/s72-c/IMG00169-20111105-1716.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-8877705058292863830</id><published>2011-11-02T08:40:00.000-07:00</published><updated>2011-11-02T08:42:39.067-07:00</updated><title type='text'>Kumbukumbu ya Loyola-Maslahi ya Umma KWANZA</title><content type='html'>Kwangu tarehe 2 Novemba itaendelea siku ya kuwakumbuka kwa mchango wenu wa hali na mali 2010 wakati wa kutafuta, kupiga na hatimaye kulinda kura vituoni na hatimaye kukesha Loyola. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza nilitokwa machozi hadharani sio kwa furaha ya ushindi bali kwa kuguswa na imani mliyoonyesha kwangu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliwaeleza sina cha kuwalipa isipokuwa kuwatumikia kwa akili, mwili, moyo na roho yangu yote. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Novemba 5 nitakuwa na mkutano kata ya Ubungo kuwaeleza kazi tulizofanya 2011 na kupata tathmini, mawazo na maoni yenu kuhusu mwelekeo kwa 2012 na kuendelea. Maslahi ya Umma Kwanza&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-8877705058292863830?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/8877705058292863830/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=8877705058292863830' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8877705058292863830'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/8877705058292863830'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/11/kumbukumbu-ya-loyola-maslahi-ya-umma.html' title='Kumbukumbu ya Loyola-Maslahi ya Umma KWANZA'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-2770925255673593984</id><published>2011-09-03T22:27:00.000-07:00</published><updated>2011-09-03T22:31:25.595-07:00</updated><title type='text'>Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje; mchango wangu bungeni</title><content type='html'>MKUTANO WA NNE-Kikao cha Thelathini na Moja – Tarehe 22 Julai, 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ina umuhimu wa pekee sana wakati huu dunia iko kwenye mwelekeo wa ubeberu na ubepari, hivyo iongezwe fedha kwenye bajeti yake kwa ajili ya kulinda maslahi ya Taifa Kimataifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza kazi yake, inahitajika kufanyike mabadiliko ya kisheria na kitaasisi ili kuweka mkazo katika diplomasia ya uchumi na usalama. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kitabu cha bajeti, Volume II, Fungu 34; Wizara ieleze sababu za kupanda kwa Kasma 220800 Kifungu 1002, hizi zimepanda kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na mwaka 2010/2011 na 2011/2012. Kifungu 2006 ielezwe hatua zilizochukuliwa kurekebisha ongezeko la matumizi ya zaidi ya 832 milioni nje ya bajeti iliyopitishwa na Bunge (Ubalozi wetu London). Kifungu 2009- hatua za kumaliza masuala ya nyuma yaliyotolewa na CAG ya takribani 451 milioni kuhusu Ubalozi wetu Moscow. Hatua zilizochukuliwa kurekebisha kasoro za mawasiliano na sekta mbalimbali kuwezesha utekelezaji wa miradi inayodhaminiwa na Serikali ya China na Taasisi/Makampuni yake, hii ifanyike kwa kutumia vizuri rasilimali zilizotengwa kwenye Kifungu 2014. Kifungu 2027; hatua zilizochukuliwa kushughulikia kasoro ya milioni 865 kutumiwa bila idhini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Volume IV, Fungu 34, Kifungu 1604, Kasma 6391, kwenye utekelezaji 2009/2010, 2010/2011 na malengo 2011/2012, napenda kujua hatua zilizochukuliwa kwa Ubalozi wetu Kigali kulipa nyumba miezi saba bila kutumika, ukarabati wa Ubalozi wetu Nairobi na ujenzi kwenye kiwanja Upper Hill.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ajili ya kulinda maslahi ya kiuchumi ya nchi yetu,&lt;br /&gt;mkazo uwekwe kwenye Balozi za nchi ambazo tuna maslahi mengi ya kiuchumi kwa 87 kurejea Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano. Aidha, safari za nje za viongozi zipunguzwe ukubwa wa misafara na idadi ili kuweka mkazo kwenye safari zenye tija. Haiwezekani kwa safari zote kati ya 2005-2010 kwa kisingizio cha kutafuta wawekezaji halafu tumeshindwa kuweka mstari wa mbele kuondoa kero ya umeme na upatikanaji wa gesi asilia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ijikite katika kuepusha uongozi wetu kutumiwa&lt;br /&gt;na makuwadi wa kiuchumi bila maslahi ya Taifa na rasilimali zake kulindwa kwa&lt;br /&gt;kiwango cha kutosha hususani kwenye ardhi, madini, gesi n.k Kampuni kama Good Works International zichunguzwe kwa ajili ya maslahi ya umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ishirikiane na Wizara ya Afya, NSSF na balozi wa India kuharakisha ujenzi wa Hospitali ya Apollo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuongeza ushiriki wa Watanzania wanaoishi ughaibuni (Diaspora) kwenye maendeleo; Wizara ishirikiane na mamlaka nyingine&lt;br /&gt;kuhakikisha inafanyika sensa rasmi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, masuala ya kiusalama yapewe kipaumbele katika kazi&lt;br /&gt;za Wizara. Serikali itoe kauli kuhusu malalamiko ya Askari wa Tanzania katika vikosi vya kuleta amani vya UN hususani nchini Lebanon na Sudan (Darfur). Malalamiko hayo yanahusisha kuchelewa kwa mishahara na kupelekewa malipo pungufu ya mikataba. Malalamiko hayo yameshaandikwa kwa Rais na Waziri wa Ulinzi badala ya haki zao kulindwa, wameandikiwa Waraka toka Makao Makuu ya Jeshi wa kuwatishia kuwa watarudishwa na kufukuzwa kazi. Ni muhimu Wizara ya Mambo ya Nje ikaingilia kati ili kuhakikisha masharti yote na stahili zote zilizomo kwenye mikataba ya kulinda amani baina ya Tanzania na Umoja wa Mataifa UN yanatekelezwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, kwa ajili ya kusafisha taswira ya Tanzania Kimataifa, ni vizuri Serikali ikatoa kauli ya hatua ambazo imechukua kuhusu tuhuma za baadhi ya Watanzania kuhusika na biashara ya silaha haramu. Mathalani Ripoti ya Timu ya Wataalamu wa Baraza la Usalama la UN ya tarehe 26 Januari 2006. Pia mkataba wa tarehe 17 Agosti 1997 kati ya Kampuni ya Executive Outcomes Inc. na Tanzania kwenye mradi wa madini kupitia mradi wa Meremeta, suala ambalo limehusishwa na usafirishwaji wa silaha haramu Congo (DRC) kati ya 1997 mpaka 2007.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Kupitia kifungu hiki cha Mshahara wa Waziri, ningeomba kupata ufafanuzi kuhusu jambo moja&lt;br /&gt;la Kisera. Ninaelewa kwamba, jukumu mojawapo la Kisera la Wizara hii ni kujenga taswira pana ya nchi yetu Kimataifa. Sasa kuna suala mahususi ambalo nililiuliza kuhusiana na tuhuma juu ya Watanzania kushiriki kwenye masuala ya uuzaji wa silaha haramu ambazo zinachafua taswira ya nchi yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninaelewa kwamba, Mheshimiwa Membe, analifahamu jambo hili, kwa sababu&lt;br /&gt;mwaka 2000 lilijadiliwa kwenye Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa na mwaka wa 2006 lilijadiliwa vilevile Umoja wa Mataifa. Sasa ningependa kupata kauli ili tusichafuke kama Watanzania, kwa sababu ya matendo ya watu binafsi kuhusiana na tuhuma hizi hususan tuhuma zinazoihusu Kampuni ya Meremeta, kwa sababu wengi wamezoea kufikiria kwamba, ilikuwa ni kashfa sijui ya utoroshaji wa madini peke yake na ufisadi wa pesa za Watanzania shilingi bilioni 100, lakini kuna tuhuma nzito vilevile za kuhusiana na utoroshaji wa silaha. Kwa hiyo, ninaomba ufafanuzi kuhusu hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA:&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, ni sahihi kabisa kusema kwamba, Watanzania na hasa Wizara yetu, wanayo haja ya kujua nini kinachoendelea na kuthibitisha madai mbalimbali yanayotolewa kama hili ambalo limetolewa na Mheshimiwa Mnyika.&lt;br /&gt;Mheshimiwa Mwenyekiti, suala alilolisema Mheshimiwa John Mnyika ni zito,&lt;br /&gt;linastahili kutoa majibu ya uhakika na nilivyojiandaa leo katika shughuli hizi, suala la silaha na suala la Meremeta, halikuwepo kwenye vocabulary yangu. Tunaomba suala hili tulitafutie muda ili tuweze pengine kulitolea majibu, sitaweza kutoa majibu ya haraka haraka kwa swali zito.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MWENYEKITI: Ahsante&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-2770925255673593984?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/2770925255673593984/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=2770925255673593984' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2770925255673593984'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2770925255673593984'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/09/bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje.html' title='Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje; mchango wangu bungeni'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-409201046305417830</id><published>2011-09-02T00:41:00.000-07:00</published><updated>2011-09-02T00:44:11.500-07:00</updated><title type='text'>Kuhusu kukatwa maji Goba</title><content type='html'>Taarifa kuhusu kukatwa maji kata ya Goba na tuhuma za kamati ‘kutafuna’ m 18&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naomba kutoa taarifa ya awali kuhusu ufuatiliaji ambao nimeufanya na hatua ambazo nakusudia kuzichukua kuhusu maji kukatwa katika kata ya Goba na tuhuma juu ya kamati ya maji Goba ‘kutafuna’ kiasi cha shilingi milioni 18 zilizotolewa tarehe 28 Agosti 2011 na hivyo kulimbikiza deni la kiwango hicho DAWASCO.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara baada ya kuingia ofisini tarehe 29 na 30 Agosti 2011  nimefuatilia na kubaini kwamba maji yamekatwa kwenye kata ya Goba kutokana na DAWASCO kuidai kamati ya mradi wa maji shilingi 18,108,478.  Aidha, katika kufuatilia deni hilo nimepata taarifa za Kamati ya Maji kuwasilisha malalamiko DAWASCO ya kutokukubaliana na kiwango hicho cha deni na pia kwa Manispaa ya Kinondoni kuhusu matatizo ya kiutendaji na kifedha katika mradi huo wa maji ikiwemo ya upotevu wa fedha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naomba kutoa taarifa kwamba katika ufuatiliaji wangu nimebaini kwamba Matatizo ya Maji katika Kata ya Goba kama ilivyo katika kata zingine katika Jimbo la Ubungo na Mkoa wa Dar es salaam kwa ujumla yanatokana na matatizo ya kimfumo, kiuongozi, kifedha na kiutendaji yanayosababishwa na Kamati ya mradi wa Maji Goba, DAWASCO, DAWASA, Halmashauri za Jiji la Dar es salaam na Wizara ya Maji ambayo nimekuwa nikiipa taarifa na kutaka iingilie kati kwa nyakati mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba tarehe 31 Januari 2011 niliitisha Kongamano la Maji katika Jimbo la Ubungo na kuwaweka pamoja wananchi pamoja na wadau wa msingi ili kuunganisha nguvu ya pamoja kukabiliana na matatizo mbalimbali ikiwemo la maji katika kata ya Goba ambalo mgogoro katika kamati ya mradi umedumu kwa zaidi ya miaka mitano. Pamoja na kuwasilisha ripoti ya kongamano husika wa DAWASCO, DAWASA, Manispaa ya Kinondoni na Wizara ya Maji hatua muhimu kuhusu matatizo katika mradi wa maji Goba na maeneo mengine hazikuchuliwa kwa wakati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili kuweza kuzisukuma mamlaka husika kutimiza wajibu tarehe 27 Februari 2011 nilifanya mkutano na wananchi ambapo risala ya wananchi pamoja na ripoti ya ukaguzi wa mradi wa mradi wa maji Goba ya mwaka 2007 zilizosomwa ambazo zilieleza bayana matatizo yaliyokuwepo kwenye kamati ya maji pamoja na mradi kwa ujumla ikiwemo yaliyohusu upotevu wa fedha.  Maazimio mbalimbali yalifikiwa ikiwemo ya kuitishwa kwa mkutano wa watumiaji wa maji kwa ajili ya kuvunja kamati iliyokuwepo na kuunda kamati mpya. Tarehe 6 Machi 2011 nilishiriki mkutano wa watumiaji Goba ulioitishwa na diwani na mtendaji wa kata ambao wananchi walifikia uamuzi wa kuvunja kamati ya awali na kuunda kamati mpya. Pamoja na kuundwa kwa kamati hiyo nilibaini matatizo ya mradi yaliyoendelea hivyo tarehe 21 Machi 2011 nilimuandikia Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni  barua yenye kumb.na. OMU/MJ/005/2011 kumtaarifu kuchukua hatua za haraka kuhusu mradi wa maji Goba ikiwemo kukutana na kamati husika. Hata hivyo, toka wakati huo Manispaa ya Kinondoni ambayo ndiyo yenye mradi kwa mujibu wa sheria haikuchukua hatua zinazostahili. Hivyo; tarehe 2 Septemba 2011 nitachukua hatua za ziada za kukutana na meya, mkurugenzi na uongozi mwingine wa manispaa ili kuweza kuchukua hatua za haraka kuhusu tuhuma zilizotolewa, kuhakikisha madeni yanalipwa kwa wakati na huduma ya maji inarejeshwa kwa wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tarehe 1 Juni 2011 niliandika barua kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASCO)  yenye kumbu. Na. OMU/MJ/007/2011 ya kutaka kupatiwa maelezo kuhusu  hatua ambazo zimechukuliwa kushughulikia upatikanaji wa maji katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo toka Kongamano la Maji na toka niwasilishe taarifa kwa mamlaka husika tarehe 15 Machi 2011.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika barua hiyo nilitaka hatua pia kuhusiana na mradi wa maji Goba kwa kuwa pamoja na kuwa mradi kuwa chini ya Manispaa ya Kinondoni na Kamati ya wananchi  kutokana na malalamiko ya muda mrefu ambayo yamehusisha pia tuhuma dhidi ya watendaji wa DAWASCO kuhusu uharibifu wa mita na ufisadi uliofanyika kati ya mwaka 2005 mpaka 2010. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika barua hiyo nilitaka pia DAWASCO na DAWASA wafanyie kazi pendekezo la eneo husika kuhudumiwa moja kwa moja na DAWASCO kutokana na ongezeko kubwa la watu na pia mradi wa sasa kununua maji toka DAWASCO na kuwauzia maji wananchi kwa bei kubwa zaidi. Hivyo, iwapo DAWASCO isipotoa majibu ifikapo tarehe 3 Septemba 2011 ikiwemo kuhusu malalamiko juu ya deni la maji katika kata ya Goba nitawaongoza wananchi wa kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo kwenda makao makuu ya DAWASCO wiki ijayo ili kuunganisha nguvu ya umma hatua za haraka zaidi ziweze kuchukuliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni muhimu mamlaka husika zikazingatia kwamba  Kamati ya Maji Goba haikuridhika na kiwango cha deni hilo kwa kuwa tarehe 9 Agosti 2011 iliwasilisha malalamiko kwa Meneja wa DAWASCO Kawe kutokana na mabadiliko ya ghafla ya kupanda kwa Ankara za Maji kutoka Tshs. 1,761,967 ya kipindi cha Februari 2011 kufikia 18,108,478 mwezi Julai. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika Barua hiyo Kamati ya Maji Goba ilimtaka meneja au wataalamu wake kufanya ukaguzi wa mwenendo wa mita ili kuweza kupunguza kiwango hicho cha deni. Kamati ya Maji Goba imetoa maelezo kwamba tarehe 8 Machi 2011 kamati mpya ilipoanza kazi mita hiyo namba 090080215 ilisoma Qm 8210 (kwa miezi tisa) lakini ghafla toka Machi mpaka Juni 2011 ikasoma Qm 11,954 (kwa miezi minne) na  Juni mpaka Julai Qm 12,212 (mwezi mmoja). Pia, kamati ya Maji Goba iliileza DAWASCO kuwa katika siku 154 ambazo kamati imefanya kazi haikuweza kupeleka maji kwa wananchi katika siku zote kutokana na kupasuka kwa mara kwa mara kwa bomba kuu la DAWASCO, mgawo wa kitaifa wa umeme na kukatwa mara kwa mara kwa umeme katika eneo la Tanki Bovu kutokana na kuhamishwa mtandao wa umeme kupisha ujenzi wa Barabara Kuu ya Bagamoyo. Hivyo, katika kipindi husika wametoa maji kwa takribani siku 70 kwa wastani wa saa 7 mpaka 9 kwa siku hali ambayo inajenga mashaka ya ziada ya kamati kwamba kiwango hicho cha deni la milioni 18 hakilingani na matumizi halisi ya maji ambayo mradi umeyatumia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuwa upande mwingine, nyaraka za kiofisi zinaonyesha kwamba Kamati ya Maji Goba iliwahi kuandika barua kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni tarehe 22 Mei 2011 ambayo haikufanyiwa kazi yenye kueleza matatizo katika uendeshaji wa mradi ambayo yalihitaji Halmashauri kuingilia kati kwa kuwa kimsingi eneo hilo la Goba linahudumiwa na mradi ulio chini ya Manispaa pamoja na kupata maji kutoka DAWASCO. &lt;br /&gt;Kamati ya Maji Goba ililalamika kutokupata ushirikiano toka kwa uongozi wa kata hususani Diwani na Afisa Mtendaji na kueleza mgogoro uliokuwepo miongoni mwa baadhi wajumbe wa kamati. Mgogoro huo ni pamoja na mvutano kuhusu utaratibu wa ukusanyaji na matumizi ya fedha za mradi kati ya mweka hazina wa kamati na viongozi wengine katika kamati husika. Kutokana na hali hiyo Mhandisi wa Maji wa Manispaa kwa niaba ya Mkurugenzi alimsimamisha katika nafasi hiyo mweka hazina na kaimu mweka hazina akateuliwa lakini Afisa Mtendaji akakataa hali ambayo ilifanya mradi kuwa na watunza fedha wawili hali ambayo inaelezwa kusababisha upotevu wa fedha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia hali hiyo Kamati ya Maendeleo ya Kata (WDC) ilimuita mkaguzi wa ndani ya manispaa kufanya ukaguzi ambao mpaka sasa taarifa yake haijatolewa. Aidha, WDC pia uliunda kamati ya kufuatilia mfumo mzima wa uendeshaji wa mradi iliyoanza tarehe 2 Juni 2011 lakini mpaka sasa taarifa yake haijatolewa. Kamati ya Maji Goba iliandika barua kwa mtendaji wa kata kuomba kikao cha wananchi tarehe 12 Juni 2011 ili kuweza kutoa taarifa ya mapato na matumizi kwa mujibu wa muongozo hata hivyo  kamati ilizuiwa kufanya mkutano wa wananchi mpaka kwanza uchunguzi uweze kukamilika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakumbukwa kwamba Gazeti la Tanzania Daima toleo la tarehe 29 Agosti 2011 lilikuwa na habari yenye kueleza kwamba Kamati ya Maji kata ya Goba katika Manispaa ya Kinondoni inatuhumiwa ‘kutafuna’ kiasi cha shilingi milioni 18. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Habari hiyo imeeleza kwamba kukosekana kwa kiwango hicho cha fedha kumesababisha Ankara ya maji ya mradi wa maji Goba inayodaiwa na Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASCO) kufikia deni la shilingi milioni 18 na hivyo DAWASCO kuwakatia maji wananchi wa kata ya Goba na maeneo jirani yanayohudumiwa na mradi huo wa maji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Habari hiyo imenukuu kauli yangu niliyohojiwa kwa simu nikiwa njiani kutoka bungeni Dodoma kuwa nitafuatilia chanzo cha matatizo hayo na nitachukua hatua pindi nikifika Dar es salaam; taarifa hii ya awali ni sehemu ya kutimiza wajibu huo na nitatoa taarifa ya ziada baada ya kuchukua hatua zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Dar es salaam-01/09/2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-409201046305417830?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/409201046305417830/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=409201046305417830' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/409201046305417830'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/409201046305417830'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/09/kuhusu-kukatwa-maji-goba.html' title='Kuhusu kukatwa maji Goba'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-7357837057546256801</id><published>2011-08-31T04:23:00.000-07:00</published><updated>2011-08-31T04:24:37.074-07:00</updated><title type='text'>Salaam za Eid al-Fitr</title><content type='html'>Nawatakia heri waislamu wote wa jimbo la Ubungo na watanzania kwa ujumla katika kusherehekea sikukuu ya Eid al Fitri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha nawapongeza waislamu wote ambao waliweka mstari wa mbele usafi wa kweli katika mawazo na matendo katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa Ramadan.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawashukuru viongozi wote wa kislamu tulioshirikiana katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadan kwa namna mbalimbali katika kuhamasisha maendeleo ya kiimani na ya jamii kwa ujumla hususani kwa michango katika kufanikisha mashindano ya kuhifadhi Qur’an kwa wanawake kata ya Manzese, ununuzi wa jenereta na ujenzi wa msikiti katika kata ya Saranga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawaomba tuendelee kushirikiana katika kipindi chote cha mwaka kwa kuwa taasisi za dini zina mchango mkubwa katika kudumisha maadili miongoni mwa wananchi na kuchangia katika maendeleo ya nchi kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wote kumbukeni Aya 185 Sura 2 (Al Baqara) na maneno mengine matukufu ili kuweka mbele swala, sadaka, uvumilivu na unyenyekevu katika matendo na maisha yetu ya kila siku.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenyezi Mungu abariki umoja na mshikamano wa wananchi kwa ustawi na amani ya taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-7357837057546256801?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/7357837057546256801/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=7357837057546256801' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7357837057546256801'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7357837057546256801'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/08/salaam-za-eid-al-fitr.html' title='Salaam za Eid al-Fitr'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-7794298279193208243</id><published>2011-08-28T13:14:00.000-07:00</published><updated>2011-08-28T13:22:24.095-07:00</updated><title type='text'>"Jairo", ufisadi wa kitaasisi na ombwe Ikulu</title><content type='html'>Toka mjadala almaarufu kama wa “Jairo” uanze nimekuwa kimya bila kutoa maoni yoyote hadharani. Nilikuwa kimya kwa sababu kubwa mbili; mosi, kwa kuwa Mkutano wa Bunge ulikuwa ukiendelea kama mbunge na waziri kivuli niliona nitumie fursa ya uwakilishi bungeni kuishauri na kuisimamia serikali katika suala hili na mengine. Pili, nilikuwa mmoja wa watu ambao walihojiwa na ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu suala hili; hivyo niliona busara nisiseme chochote hadharani mpaka pale taarifa ya uchunguzi husika itakapotolewa &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kuwa hivi karibuni Katibu Mkuu kiongozi na CAG wametoa baadhi ya mambo ndani ya taarifa hiyo na kwa kuwa jana mkutano wa nne wa bunge umeahirishwa nimeona nichangie mawazo machache katika mjadala huu; katika muktadha wa majibu niliyopewa jana na Waziri wa Fedha Bungeni kufuatia maelezo niliyoomba kuhusu hatua ambazo amechukua kuhusu suala hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika kikao cha jana cha bunge wakati bunge lilipokaa kama kamati ya kupitia bajeti ya Wizara ya Fedha nilishika mshahara wa Waziri na kutaka kauli yake kwa kuwa Mlipaji Mkuu wa Serikali, Mhasibu Mkuu wako chini yake na pia jana ndio tulikuwa tunapitia pia Mafungu ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi,  Hazina na taasisi nyingine za Wizara ya Fedha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, Waziri wa Fedha akakwepa kuwajibika katika suala ambalo liko kwenye mamlaka yake kwa mujibu wa sheria kwa kisingizio kwamba anasubiria kamati teule ya bunge iundwe kuhusu suala hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwenye mkutano huu wa bunge kuanzia vikao vya mwanzo kabisa, nimesisitiza mara kwa mara kwamba matatizo mengi katika serikali kwa sasa yanatamalaki kutokana na ombwe la uongozi katika Ofisi ya Rais na Ikulu; hali inayohitaji Rais Jakaya Kikwete kutumia kwa uthabiti na umakini mamlaka makubwa aliyonayo kwa mujibu kwa katiba na sheria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sakata hili la “Jairo” ni moja ya matokeo tu ya hali hiyo ambayo kama isipodhibitiwa mapema mengine zaidi yataibuka  kutokana na kuyumba kwa serikali. Ikiwa Rais anachelea kutumia ipasavyo mamlaka makubwa ya urais aliyonayo; njia mbadala ya kuongeza uthabiti na udhibiti wa serikali inaweza kuwa ni kuvunja baraza la mawaziri na kulisuka upya ili kuongeza uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazolikumba taifa kwa sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mjadala huu unaoendelea hivi sasa ungekuwa na tija ya kutosha kama tungepata nakala kamili ya taarifa ya CAG kuhusu suala hili badala ya maelezo mafupi tu yaliyotolewa na Luhanjo na Utouh mbele ya wanahabari. Binafsi nakusudia kuwaandikia kuomba taarifa husika iwekwe hadharani ili watanzania wenye kutaka kutoa mchango wao kwa kamati teule ya bunge wafanye hivyo wakiwa pia na taarifa ya awali iliyofanywa tayari kwa gharama za walipa kodi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maoni yangu sakata la “Jairo” lisichukuliwe kama ‘tukio pweke” (isolated event) bali litazamwe kuwa ni kiashiria cha matatizo makubwa zaidi katika mifumo ya matumizi ya fedha za umma ndani ya Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali. Hata hivyo, nilishangazwa zaidi na kauli ya katibu mkuu kiongozi- hata kwa maelezo tu aliyoyatoa mwenyewe kwenye vyombo vya habari amedhihirisha kwamba kuna ukiukaji wa sheria za fedha, ubadhirifu na ufisadi wa kitaasisi katika Wizara ya Nishati na Madini. Lakini inashangaza hatimaye akatoa kauli ya kuhitimisha kuwa  ni utamaduni wa kawaida katika serikali na kwamba Jairo hana hatia yoyote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msingi wa kutoa hitimisho hili ulianzia naamini ulianza kutokana na udhaifu wa hadidu rejea ambazo wachunguzi wa ofisi ya CAG walikuwa nazo- kwa kipindi kifupi nilichokuwa karibu na Wizara hii nafahamu idadi ya idara, vitengo, wakala, mashirika na taasisi zilizoko chini yake.Ndio maana nikatahadharisha kwamba lazima uchunguzi uhusishe mfumo mzima ikiwemo maagizo ya barua ya Jairo na matokeo badala ya kujikita kwenye kauli za Shellukindo bungeni pekee. Na nilieleza matendo yanayoshabihiana na ya Jairo yaliyofanywa pia na Wizara nyingine kuanzia wakati wa kamati za Bunge Dar es salaam mpaka katika Mkutano huu wa bunge la bajeti katika kile kinachoitwa ‘kufanikisha kupitishwa kwa bajeti’. Kwa ujumla kuna mianya katika mifumo ya fedha ambayo imewezesha ubadhirifu na ufisadi wa kitaasisi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na kauli ya Waziri Mkuu kiongozi kuwa matendo kama aliyoyafanya Jairo ni ya kawaida katika Serikali; Waziri wa Fedha anapaswa kuwajibika kuchukua hatua badala ya kusubiri mpaka kamati teule imalize kazi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ni kwa sababu kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Umma (Public Finnance Act no 6 of 2001); wajibu na mamlaka ya Waziri wa Fedha na Hazina kwa majibu wa 5(1) (i) ni kusimamia na kufuatilia masuala yote ya fedha za umma, 5(3) kudhibiti na kutoa muongozo kwa masuala yote ya kifedha ya serikali. Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha kama Mlipaji Mkuu ndiye anayesimamia udhibiti na utoaji fedha kwa Wizara na Idara mbalimbali za serikali nzima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jairo anaingia katika picha kwa Wizara yake kwa kuwa sheria hiyo kifungu 8(1) kimetoa mamlaka kwa Wizara ya Fedha kuteua Afisa Masuhuli (Accounting Officer) kwa Fungu husika ambapo kwa Wizara ya Nishati na Madini ni yeye kama katibu mkuu. Hivyo, kama katibu mkuu kiongozi Luhanjo amesema kwamba matendo hayo ni ya kawaida katika serikali nilitegemea kauli nzito toka kwa ama Waziri wa Fedha au Mlipaji Mkuu au Mhasibu Mkuu wa Serikali  kukanusha ama kuunga mkono.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi, kwa Wizara ya Nishati na Madini anayepaswa kuwajibika kiutendaji ni Jairo; ingawa Waziri na Naibu nao hawawezi kukwepa kuwajibika kisiasa kutokana na kadhia hiyo hasa baada ya kutoa kauli tata na tete mara baada ya Luhanjo ‘kumsafisha’ Jairo hali inayoaishiria kwamba ‘baraka’ zao zilikuwepo kwenye barua ya Jairo na matumizi yaliyofuatia. Aidha, pamoja na kukingwa na kifungu 8(2); Watendaji wa wakala, mashirika na taasisi yaliyohusika nao wana nafasi yao ya kuwajibika katika sakata nzima. Katika muktadha huo, mnyororo huu unaelekea kuwa mrefu lakini ni muhimu hatua za msingi zikachukuliwa ili kudhibiti hali hii ambayo imeelekea kuwa ni utamaduni wa ubadhirifu na ufisadi wa kitaasisi unaoitwa ‘wa kawaida’ kwenye serikali kwa muda mrefu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Utetezi wa Luhanjo ambao unaelekea kuungwa mkono na baadhi ya watu ndani na nje ya serikali ni kwamba ‘CAG amekagua na kukuta hakuna fedha ambazo wabunge wamepewa rushwa ili kupitisha bajeti’. (Hili la Wabunge kupewa rushwa kupitisha bajeti, naomba nisilitoleee maoni hadharani katika hatua ya sasa kwa kuwa yapo masuala ambayo niyaeleza nilipohojiwa ambayo naamini ofisi ya CAG na mamlaka zingine naamini zinaendelea kuyafanyia kazi).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tuchukue vigezo vya kimaamuma pekee na tutumie tu maelezo ambayo yametolewa na Katibu Mkuu Kiongozi na Mkaguzi Mkuu kwa waandishi wa habari halafu tuyalinganishe na misingi ya kisheria na kikanuni inayosimamia fedha za umma na utendaji wa kazi katika serikali. Kwa hayo tu, utabaini kwamba mamlaka hizi za kiserikali zimepuuzia ubadhirifu na ufisadi wa kitaasisi unaodhihirika katika Wizara ya Nishati na Madini.&lt;br /&gt;Sheria ya Ukaguzi (Public Audit Act no. 11 of 2008) kifungu cha 10(1) kinampa jukumu CAG kufanya ukaguzi wa fedha za umma kwa niaba ya bunge (Hapa unaweza kujiuliza; kwa kuwa suala lilianzia bungeni na kwa kuwa CAG hufanya ukaguzi kwa niaba ya bunge- pamoja na kuwa katika suala la Jairo aliombwa na mamlaka za kiserikali, kwa nini haikuonekana haja ya bunge kupewa taarifa ya haraka kabla ya kwenda kwenye vyombo vya habari kusafishana?).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu cha 10 (2) (c) kinaelekeza matumizi yote ya umma yawe yameadhinishwa kwa kufuata utaratibu na yatumike kwa madhumuni kwayo yalipitishwa kwa mujibu wa sheria na maelekezo (appropriation laws and directives). (d) matumizi hayo lazima yafanyike kwa kuzingatia ufanisi na tija (economy, efficiency and effectiveness). Je, ni kwa kiwango gani matumizi hayo tuliyoelekezwa yamezingatia vigezo hivyo viwili vya msingi ambavyo CAG alipaswa kuvitumia katika ukaguzi wake?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kifungu cha 12 kimempa mamlaka CAG kutoa mapendekezo ya kuzuia au kupunguza matumizi yasiyokuwa na tija ya fedha za umma (tujiulize, ni kwanini Luhanjo kama CAG alitoa mapendekezo ya namna hiyo au la?). Aidha kifungu hicho hicho kinatoa mwanya wa kutolewa mapendekezo ya kudhibiti uzembe, ukosefu wa uaminifu, ufisadi nk.&lt;br /&gt;Naelewa kwamba ukaguzi uliofanyika sio wa kawaida, hivyo wengine wametumia sababu hiyo kujenga hoja kwamba halikuwa suala la bunge katika hatua ya sasa bali la mamlaka iliyoomba ukaguzi ufanyike.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni vyema tukarejea tena kwenye sheria husika kifungu cha 26 (2) ambayo inaelekeza kwamba CAG anaweza kufanya ukaguzi maalum kwa maombi ya mtu au taasisi; ukiondoa ukaguzi wa kawaida unaofanywa kwa mujibu wa sheria ama kwa azimio la bunge au kamati zake za usimamizi wa fedha za umma. Hata hivyo, izingatiwe kwamba Kifungu cha 36 (1) cha Sheria hiyo hiyo kinaeleza kwamba CAG anaweza akiona kwamba kuna jambo lolote la ukaguzi wowote lina maslahi ya umma na angependa kulitaarifu bunge sheria inaelekeza kwamba anaandaa ripoti maalum anamkabidhi Rais kwa mujibu wa sheria Rais anawajibika kuipeleka ripoti husika  bungeni. Kwa kuwa suala hili la Jairo lilihusu tuhuma za Bunge, likatolewa kauli na Waziri Mkuu ambayo ndiye kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni kwamba analipeleka kwa Rais, Rais badala ya kutoa maagizo mwenyewe akaikabidhi mamlaka ya nidhamu ambayo ni Katibu Mkuu Kiongozi (Hapa Rais alipaswa kutambua kwamba suala hili halikuhusu Nidhamu tu ya Jairo, lilihusu masuala ya kimfumo na kifedha ya Wizara ambayo kwa mujibu wa katiba muhusika mkuu ni yeye au watendaji aliowateua kufanya kazi kwa niaba yake mf. Waziri Mkuu, Waziri wa Fedha, Mlipaji Mkuu nk).  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kwamba ukaguzi huu maalum haukupaswa tu kuwa wa kawaida, CAG alipaswa kutumia vizuri pia kifungu cha 28 kwa kuingiza masuala ya kukagua ufanisi (economy, efficiency, effectiveness) katika hadidu rejea (a) kuhusiana na matumizi ya fedha na rasilimali (b) kuhusu utendaji wa maafisa masuhuli husika (Accounting officer), wakuu wa idara na watendaji wakuu wa wakala, taasisi na mashirika yaliyohusika. Ukaguzi wa namna hii ungeweza kuibua masuala ambayo yangehitaji sasa kufanyika ukaguzi wa kiuchunguzi (Forensic Audit) kwa ajili ya hatua za ziada. Kamati teule ya Bunge inaweza kupanua wigo zaidi kutoka pale CAG alipoishia ili kuwezesha bunge kutimiza wajibu wa kikatiba wa kuisamia serikali kuondokana na mfumo wa ubadhirifu na ufisadi wa kitaasisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JJ&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-7794298279193208243?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/7794298279193208243/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=7794298279193208243' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7794298279193208243'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7794298279193208243'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/08/jairo-ufisadi-wa-kitaasisi-na-ombwe.html' title='&quot;Jairo&quot;, ufisadi wa kitaasisi na ombwe Ikulu'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-6181223783811089213</id><published>2011-08-11T07:56:00.000-07:00</published><updated>2011-08-11T07:58:20.103-07:00</updated><title type='text'>Muongozo kuhusu hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu</title><content type='html'>Leo tarehe 11 Agosti 2011 katika kikao cha 48 cha Mkutano wa Nne wa Bunge la Kumi nilitaka kuomba muongozo wa Spika kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la 2007 ) kifungu cha 68 (7) kuhusu maswali na majibu ya Waziri Mkuu na nikarejea pia kanuni ya 133 (1).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, kabla hata ya kutoa maelezo kamili ya kuomba muongozo wa Spika nilizuiwa na Naibu Spika Mheshimiwa Job Ndugai (Mb) bila hata ya kusikilizwa muongozo ambao nilitaka kuomba kinyume na kanuni ya 5 (1) inayotaka Spika kuongoza Bunge kwa kuzingatia kanuni na pale ambapo kanuni hazijatoa muongozo Spika anapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia katiba, sheria nyingine za nchi, kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali na desturi za kibunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naomba kutoa taarifa kwa umma kwamba sijaridhika na uamuzi uliofanywa na Naibu Spika Mheshimiwa Job Ndugai hivyo nawajulisha kwamba ninakusudia kuwasilisha malalamiko kwa mujibu wa kanuni za Bunge kifungu 5 (4) na 7 (3) mara baada ya kupata nakala ya kumbukumbu rasmi ya Bunge (Hansard) ya kikao husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara baada ya kunukuu kanuni husika nilipoanza tu kuzungumza kwamba katika kipindi cha Maswali na Majibu kwa Waziri Mkuu, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amekuwa akitoa majibu yenye upotoshaji yasiyokuwa ya kweli; baada ya kauli hiyo kabla hata ya kumaliza maelezo niweze kuomba muongozo kwa Spika; Naibu Spika alinikatisha na kuninyima fursa ya kuomba muongozo kinyume na kifungu 68 (7) na 5 (1).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naomba umma uelewe kwamba nilikuwa naelewa kwa kina mahitaji ya kanuni za bunge kifungu cha 133 na vipengele vyake kuanzia cha kwanza mpaka cha sita; ndio maana katika kuanza kuomba muongozo nikasoma kifungu cha 133(1).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Napenda umma ufahamu kwamba muongozo ambao nilitaka kuomba kwa Spika ni kwamba kumekuwa na kawaida ya Waziri Mkuu wakati akijibu maswali ya papo kwa papo kutoa maelezo yasiyokuwa ya kweli yenye upotoshaji ambayo ni kinyume cha katiba ya nchi, sheria mbalimbali pamoja na kanuni ikiwemo kanuni za bunge hivyo nilitaka Spika atoe muongozo wenye kumpa nafasi nyingine Waziri Mkuu kutoa ufafanuzi wa kweli kuhusu masuala husika ili kuepusha uwezekano wa wabunge kupoteza imani na Waziri Mkuu kwa mujibu wa kanuni za bunge kifungu cha 133. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika maelezo yangu ya kuomba muongozo huo nilikusudia kutaja mifano miwili mikubwa ya majibu ya Waziri Mkuu kwenye maswali ya papo kwa papo yasiyokuwa ya kweli yenye upotoshaji kuhusu kashfa ya Meremeta na kuhusu mgogoro katika Manispaa ya Arusha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba tarehe 14 Aprili 2011 wakati wa kikao cha saba cha mkutano wa tatu wa Bunge la Tanzania wakati wa maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, nilimuuliza Mheshimiwa Mizengo Pinda kuwa “Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye vile vile ni Mwenyekiti wa CCM amenukuliwa akizungumzia kuhusu haja ya Chama kinachotawala kujivua gamba. Kati ya mambo aliyoyazungumza ni pamoja na kuondokana na watuhumiwa wa ufisadi.   Mheshimiwa Mkuu uliwahi kulieleza  Bunge hili tukufu kwamba usingetaka kabisa kuzungumzia masuala ya Meremeta kwa sababu ni siri za Jeshi. Baada ya kauli hii ya Rais na dhamira hii ya kujivua gamba kuhusiana na masuala ya ufisadi. Je, uko tayari Mheshimiwa Waziri Mkuu kutaja wahusika wa Kampuni ya Meremeta na kuelekeza Serikali kuchukua hatua zinazostahili kuhusiana na tuhuma hizo? . Waziri Mkuu katika majibu yake Mheshimiwa Mizengo Pinda hakuitumia nafasi hiyo kurekebisha kauli zake zisizokuwa za kweli zenye upotoshaji alizozitoa kwa nyakati mbalimbali katika Bunge la Tisa kuhusu kashfa ya Meremeta.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe pia kwamba tarehe 10 Februari 2011 katika kikao cha tatu cha mkutano wa pili wa Bunge la kumi Waziri Mkuu Mizengo Pinda akijibu maswali ya papo kwa papo ya Mheshimiwa Freeman Mbowe (Mb) kuhusu matukio yaliyojitokeza Arusha wakati na baada ya uchaguzi batili wa Meya wa Halmashauri ya Jiji la Arusha.  Tarehe 11 Agosti 2011 katika kipindi cha Maswali ya papo kwa papo ya Waziri Mkuu kuliulizwa maswali kuhusu maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA ya tarehe 6 na 7 Agosti 2011 kwa kurejea pia mazungumzo baina ya Waziri Mkuu na viongozi wa taifa CHADEMA kuhusu muafaka batili juu ya mgogoro katika Halmashauri ya Jiji la Arusha na uamuzi wa kuwafukuza uanachama madiwani watano kutokana na kukiuka maagizo ya kamati kuu. Badala ya Waziri Mkuu kuitumia nafasi hiyo kutoa majibu yenye kulenga kutoa ufafanuzi wa kurekebisha upotoshaji uliofanyika awali Waziri Mkuu Mizengo Pinda akatoa majibu mengine yasiyokuwa ya kweli kuhusu mazungumzo yake na viongozi wa CHADEMA pamoja na uamuzi wa chama wa kuwafukuza uanachama madiwani waliokiuka maamuzi ya kamati kuu ya chama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Majibu ya Waziri Mkuu kuhusu ufisadi wa Meremeta, matukio katika halmashauri ya Jiji la Arusha na masuala mengine ya kitaifa katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo yenye uhusiano na utekelezaji wa majukumu ya Waziri Mkuu yaliyoanishwa katika ibara ya 52 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yana mwelekeo wa kuvunja sheria ya maadili ya viongozi wa umma, sheria nyingine za nchi yetu pamoja na misingi muhimu ya utawala bora kama ambavyo nitafafanua katika hatua zinazofuata. Naomba umma upuuze upotoshaji uliofanywa na Naibu Spika Job Ndugai kuhusu muongozo nilioomba mpaka pale maamuzi yatakapofanywa na Kamati ya Kanuni za Bunge kwa mujibu wa kifungu 5(5) na Bunge kujulishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Bungeni-Dodoma&lt;br /&gt;11/08/2011&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-6181223783811089213?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/6181223783811089213/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=6181223783811089213' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6181223783811089213'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6181223783811089213'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/08/muongozo-kuhusu-hoja-ya-kutokuwa-na.html' title='Muongozo kuhusu hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-93456193183011140</id><published>2011-08-10T05:58:00.000-07:00</published><updated>2011-08-10T06:00:44.041-07:00</updated><title type='text'>Hatma ya Bajeti ya Nishati na Madini</title><content type='html'>&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;LEO TAREHE 10 AGOSTI 2011 NILIOMBA MUONGOZO WA SPIKA BUNGENI KWA MUJIBU WA KANUNI 68(7) KUTAKA SERIKALI ITOE MAELEZO KWANINI AHADI YA WAZIRI MKUU YA KUZISHIRIKISHA KAMATI ZA BUNGE KATIKA KUANDAA MPANGO WA DHARURA WA UMEME NA MAELEZO KUHUSU NISHATI NA MADINI HAIJATEKELEZWA NA KUTAKA MUONGOZO KUHUSU UTARATIBU GANI UTATUMIKA KUENDELEZA MJADALA TAREHE 13 AGOSTI. UKIREJEA MAJIBU YALIYOTOLEWA UTABAINI KWAMBA SERIKALI INAKUSUDIA ‘KUFUNIKA KOMBE MWANAHARAMU APITE’ KUHUSU BAJETI YA NISHATI NA MADINI; REJEA HAPA CHINI TAMKO LANGU LA TAREHE 8/8 TUSHIKIRIANE KUISIMAMIA SERIKALI KUTIMIZA WAJIBU&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakumbukwa kwamba tarehe 18 Julai 2011 Waziri Mkuu Mizengo Pinda alitoa hoja bungeni ya kuahirisha mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2011/2012 kwa mujibu wa kanuni za kudumu za bunge(toleo la 2007) kanuni ya 55 (3) (b) na 69 (1).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri Mkuu alilieleza bunge kuwa serikali imetoa hoja ya kuahirisha mjadala wa bajeti ya Wizara husika ili kupata muda usiozidi wiki tatu wa kutoa maelezo kuhusu michango ya wabunge hususani kwa kuwasilisha mpango wa dharura wa kuondoa mgawo wa umeme kwa kuzishirikisha kamati za bunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, ikiwa imesalia chini ya wiki moja kufikia tarehe ya kuendelea kwa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini tarehe 13 Agosti 2011 serikali bado haijazishirikisha kikamilifu kamati za bunge hususani ya nishati na madini pamoja na fedha na uchumi kama ilivyoahidi. Hatua za haraka zisipochukuliwa na uongozi wa bunge, kamati husika na wadau wengine serikali italeta maelezo yake yakiwa yamechelewa na hivyo kukosekana kwa muda wa marekebisho ya msingi kufanyika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, natoa mwito kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa kuwa ndiye mwenye dhamana ya Shughuli zote za Serikali Bungeni kwa mujibu wa katiba ibara ya 52 (2) hivyo anapaswa kuwajibika kutoa maelezo bungeni kuhusu sababu za kutozihusisha kamati za bunge mpaka hivi na kutimiza wajibu wa serikali kuwasilisha mpango wa dharura pamoja na marekebisho mengine ya kibajeti kwa kamati zinazohusika mapema iwezekanavyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, kwa umma una matarajio makubwa kuwa serikali itafanya marekebisho ya msingi katika bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ni muhimu kwa Spika wa Bunge Anna Makinda kutoa fursa ya mjadala kuendelea mara baada ya serikali kutoa maelezo na mpango wa dharura kwa kamati zitakazohusika za bunge pamoja na kambi rasmi ya upinzani kutoa maoni kabla ya mtoa hoja kupewa nafasi ya kujibu wa mujibu wa kanuni ya 99 (9). Hii italiwezesha bunge kutekeleza kwa ukamilifu wajibu wa kikatiba uliotajwa kwenye ibara ya 63 (3) (b) na (c).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mpango wa dharura na maelezo yatayotolewa natarajia Serikali itazingatia mapendekezo tuliyotoa kambi rasmi ya upinzani kupitia Bajeti Mbadala ya Nishati na Madini na kuongeza kiwango cha bajeti kwa kiwango kisichopungua bilioni 977 kwa bajeti ya maendeleo pekee kwa kutumia vyanzo vya nyongeza vya mapato tulivyovitaja. (tofauti na ile ambayo serikali ilitenga awali Sh. Bilioni 452 kwa maendeleo ya nishati na Madini-Fungu 58 na 50).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya vyanzo hivyo ni kupunguza misamaha ya Kodi ikiwemo kuondoa msamaha wa ushuru wa mafuta Kampuni za Madini peke yake kutaongeza mapato ya shilingi bilioni 59. Kutoka Vyanzo vipya vya mapato tulivyovianisha; kwa upande wa sekta ya madini kwa Kurekebisha Kodi Sekta ya Madini peke yake tunaweza kukusanya shilingi bilioni 240 katika mwaka wa fedha 2011/2012. Kupunguza fedha kwenye Wizara zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida yasiyokuwa ya lazima na kuelekeza fedha katika miradi ya maendeleo hususani ya umeme na gesi. Wizara ya Nishati na Madini peke yake imepanga kutumia Sh. Bilioni 7.9 kulipana posho ambazo zinaweza kupunguzwa  na kuongezwa kwenye ujenzi wa miundombinu wa Chuo Cha Madini Dodoma na na kuongeza kiwango cha fedha katika mfuko wa wachimbaji wadogo wa madini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama sehemu ya vyanzo vya mapato tunatarajia kwamba serikali itatoa maelezo ya kukamilisha majadiliano ya ubia ama mikopo toka Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na washirika wengine isiyopungua bilioni 400 kwa ajili ya miradi ya umeme na gesi asilia.  Pia, serikali itaeleza namna itavyoharakisha ufilisi wa IPTL ili kupata takribani bilioni 200 zilizohifadhiwa katika katika akaunti maalum (escrow account) na kuzielekeza kwenye kuliwezesha Shirika la Umeme (TANESCO) kuwekeza katika umeme na kukamilisha utekelezaji wa mpango maalum wa kurekebisha hali ya kifedha ya shirika.  Aidha, zaidi ya bilioni 100 zingine zinaweza kuongezwa katika ujenzi wa miundombinu ya umeme kutoka kwenye fungu 98 kasma 4168 ya fedha za bajeti ambazo zimepitishwa bila kupangiwa matumizi halisi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunaamini kwamba ongezeko hilo la bajeti litawezesha vipaumbele vifuatavyo kuzingatiwa kwa uzito unaostahili kwa kurejea mwelekeo wa matumizi ambao tuliuwasilisha kwenye bajeti mbadala ya Nishati na Madini tarehe 15 Julai 2011: Kuwekeza fedha za kutosha kwenye mpango wa dharura wa  sekta ya umeme na Gesi ili kumaliza kabisa tatizo la nishati ya Umeme na kupunguza gharama za maisha. Hatua hizo ziambatane kuwekeza katika Bomba la Gesi kutoka Mtwara, pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant) ili kuwezesha gesi kutumika kwenye magari, viwandani na majumbani.  Kuhakikisha tunazalisha 360MW za umeme katika mwaka wa fedha 2011/2012 ili kufikia malengo ya Mpango wa Maendeleo wa miaka Mitano na kumaliza tatizo la mgawo wa umeme. Pamoja na ununuzi wa mitambo mingine kipaumbele kiwekwe pia kuanza kutekeleza miradi ya Kiwira, Stiggler Gorge, Ngaka na Mchuchuma Kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya usafirishaji na usambazaji wa umeme vijijini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi vijijini kama tulivyoshauri katika bajeti mbadala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha kufuatia Kamati Kuu ya CCM kutoa agizo  lenye kukubaliana na maoni tuliyotoa kwenye Bajeti Mbadala ya Nishati na Madini tarehe 15 Julai 2011 kuhusu ongezeko la kodi katika mafuta ya taa; serikali ipaswa kuwasilisha muswada wa marekebisho ya sheria ya fedha katika mkutano wa bunge unaoendelea ili kupunguza gharama za maisha kwa wananchi kwa kuondoa ongezeko kubwa lililofanywa kwenye kodi ya mafuta ya taa na pia kupunguza kodi zaidi kwenye dizeli na petrol kama tulivyoshauri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande wa sekta ya madini, pamoja na kushughulikia masuala ya mapato kama tulivyoyaeleza natarajia kwambaWaziri wa Nishati na Madini William Ngeleja  atatoa maelezo na mpango wa kushughulikia masuala yote ya ufisadi na migogoro tuliyoyaeleza kwenye hotuba ya kambi ya upinzani tarehe 15 Julai 2011.  Mathalani kuhusu mauzo na mabadilishano ya umiliki yaliyofanyika baina ya kampuni ya Australia (Mantra Resources) na Kampuni ya Urusi ya ARMZ Uranium Holding kampuni tanzu ya Rosato. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mauzo hayo ambayo yanaelezwa kimataifa kuwa yamefanyika kwa bei ya dola 1.16 bilioni ambayo ni zaidi ya shilingi trilioni 2. Mauzo hayo yamehusisha kuhamishiana umiliki wa maeneo ya Tanzania Mkuju River (Namtumbo) na Bahi Kaskazini (Dodoma) bila serikali kupata mapato yanayostahili wala wananchi wa maeneo husika kunufaika. &lt;br /&gt;Pia Serikali itoe maelezo kuhusu kutokutekelezwa kikamilifu kwa ahadi ya kumaliza migogoro katika sekta ya madini baina ya wachimbaji wakubwa na wachimbaji wadogo pamoja na kuepusha migogoro ya leseni mathalani mgogoro wa wachimbaji wadogo eneo la Winza wilaya ya Mpwapwa ambao serikali iliahidi bungeni tarehe 9 Julai 2010 kuumaliza ambapo mpaka hivi sasa wanaendelea kuhamishwa kwa nguvu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kadhalika Serikali itoa maelezo juu ya shughuli za New Alamasi Ltd iliyochimba almasi katika eneo la Luhumbo bila leseni stahiki, kiasi cha almasi iliyochimbwa kinyemela kwa kipindi chote tokea tarehe 1 Juni 1965 hadi tarehe 8 Mei 2000 (kwa miaka 35); zilizokoenda fedha zilizotokana na mauzo haramu ya almasi na hatua zilizochukuliwa kwa wahusika na ikiukaji wa sheria. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Waziri Kivuli wa Nishati na Madini&lt;br /&gt;Bungeni, Dodoma-08/08/2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-93456193183011140?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/93456193183011140/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=93456193183011140' title='3 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/93456193183011140'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/93456193183011140'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/08/hatma-ya-bajeti-ya-nishati-na-madini.html' title='Hatma ya Bajeti ya Nishati na Madini'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>3</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-5702864107721651378</id><published>2011-08-03T03:46:00.000-07:00</published><updated>2011-08-03T03:50:32.180-07:00</updated><title type='text'>Kuhusu maamuzi dhaifu ya CC ya CCM juu ya nishati na madini</title><content type='html'>Maamuzi yaliyofanywa na kamati kuu ya CCM katika kikao chake cha tarehe 31 Agosti 2011 kuhusu masuala mbalimbali yanayolikabili taifa hususani kuhusu nishati na madini imethibitisha ulegelege na kupoteza mwelekeo kwa serikali na chama hicho kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha maagizo hayo bado ni legelege na hayawezi kutoa muongozo thabiti kwa serikali katika kukabiliana na changamoto za msingi zinazolikabili taifa kwa sasa katika sekta za nishati na madini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nyakati mbalimbali kuanzia mwaka 2005 nimekuwa nikitoa kauli za kueleza kwamba CCM na serikali yake ni legelege kiuongozi na kimaadili hali ambayo inaathiri maisha ya wananchi na mustakabali wa nchi kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatimaye mwezi Februari mwaka 2007 wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya CCM Mwenyekiti wa chama hicho Rais Jakaya Kikwete akatambua hali hiyo na kurejea kauli ya Mwalimu Julius Nyerere kwamba “chama legelege huzaa serikali legelege’ na kueleza dhamira ya kuondoa ulegelege huo kuanzia kwenye chama na hatimaye katika serikali.&lt;br /&gt;Hata hivyo, maagizo yaliyotolewa na kamati kuu katika kikao chake cha tarehe 31 Agosti 2011 kuhusu bei ya mafuta ya taa, matatizo ya umeme na masuala ya madini yamedhihirisha kwamba CCM na serikali yake bado hawajaondokana na ulegelege ambao kama usipodhibitiwa ni hatari kwa hatma ya nchi kisiasa, kiuchumi na kijamii.&lt;br /&gt;Ni muhimu watanzania wakatambua kwamba Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete ambaye ndiye aliyeongoza kikao cha kamati kuu kilichotoa maagizo kuhusu bei ya mafuta ya taa, matatizo ya umeme na migogoro migodini ndiye kiongozi mkuu wa shughuli za serikali na mwenyekiti wa baraza la mawaziri ambalo vikao vyake vimejadili masuala hayo hayo na kupitisha maamuzi mabovu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha umma ukumbuke kwamba kabla ya Mkutano wa Nne wa Bunge hili la bajeti palifanyika vikao vya vyombo vya maamuzi vya CCM hususani sekretariati, kamati kuu na halmashauri kuu ambavyo vilijadili pamoja na ajenda nyingine hali ya siasa ikiwemo maandalizi ya bajeti na kushindwa kutoa maagizo muafaka kwa serikali hali ambayo imelitumbukiza taifa katika matatizo ya sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, maagizo yaliyotolewa kwa serikali na Kamati Kuu ya chama hicho ni ya kisiasa yenye kulenga kumkosha Rais Kikwete na CCM  kufuatia malalamiko ya wananchi juu ya ugumu wa maisha na tishio la maandamano ya CHADEMA kuhusu maamuzi mabovu yaliyofanywa na serikali yaliyopitishwa kwa kura za wabunge walio wengi wa CCM bila kuzingatia maslahi ya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikiwa maagizo hayo yametolewa kwa dhamira ya kweli ya chama kuisimamia serikali yanapaswa kuambatana na hatua ya Rais Kikwete kuvua magamba kwa kuvunja baraza la mawaziri kwa kushindwa kumshauri vizuri katika kuiongoza serikali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Agizo la kamati kuu ya CCM la kuitaka serikali ‘kutafuta njia ya kushusha bei ya mafuta ya taa’ ni dhaifu kwa kuwa sababu ya kupanda kwa bei ya mafuta hayo inajulikana wazi kuwa ni kupandishwa kwa kodi kulikofanywa tarehe 22 Juni 2011 hivyo; Kamati Kuu ya CCM ilipaswa kutoa agizo la kukubaliana na maoni tuliyotoa kwenye Bajeti Mbadala ya Nishati na Madini tarehe 15 Julai 2011 na kuiagiza serikali kuwasilisha muswada wa marekebisho ya sheria ya fedha katika mkutano wa bunge unaoendelea ili kupunguza gharama za maisha kwa wananchi kwa kuondoa ongezeko kubwa lililofanywa kwenye kodi ya mafuta ya taa na pia kupunguza kodi zaidi kwenye dizeli na petroli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Azimio la kamati kuu kueleza kusikitishwa na tatizo la umeme halionyeshi CCM kuwaomba radhi watanzania kutokana na kuliingiza taifa katika hali hiyo kutokana na uzembe, ufisadi na udhaifu wa kiuongozi. Aidha,  azimio hilo halionyeshi kamati kuu kutambua uzito wa tatizo hilo kwa kulitangaza kuwa janga la taifa au hali ya dharura yenye kuhitaji uwajibikaji wa pamoja ikiwemo wa Rais Kikwete badala yake imelichukulia kuwa ni suala la kurekebisha bajeti ya nishati na madini kwa kuambatanisha mpango wa dharura. Kamati Kuu ya CCM ingetambua tatizo la ukosefu wa nishati linavyoathiri uchumi wa nchi na maisha ya wananchi kuwa ni janga la taifa ingetoa maagizo ya kukabiliana na maoni tuliyotoa kwenye bajeti mbadala ya nishati na madini tarehe 15 Julai 2011 ya kutaka sio tu kufanya marekebisho ya bajeti ya nishati na madini bali pia kwa Wizara ya Fedha kuwasilisha bajeti ya nyongeza (supplementary budget) ili kurekebisha kasoro zilizotokana na kupitishwa kwa bajeti finyu tarehe 21 Juni 2011. Aidha, kamati kuu ya CCM ingetambua kwamba taifa lipo kwenye hali ya dharura lingemtaka Rais Kikwete ambaye pia na mwenyekiti wa chama hicho kuwajibika kutumia mamlaka yake ya kikatiba ikiwemo ya hali ya dharura kuwezesha hatua za haraka kuchukuliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taarifa ya kwamba kamati kuu ya CCM imejadili masuala mengine kama ‘migogoro migodini’ na ‘kuagiza serikali kuyashughulikia kwani yanatatulika’ inaonyesha ulegelege na udhaifu wa chama hicho katika kuishauri na kuisimamia serikali. Kamati Kuu ya CCM ilipaswa kutoa maelekezo mahususi ya maeneo ya migogoro migodini kwa kuzingatia maoni tuliyoyatoa kwenye bajeti mbadala ya nishati na madini tarehe 15 Julai 2011. Aidha, Kamati Kuu ya CCM imejikita katika kutoa agizo la ujumla kuhusu migogoro migodini bila kutoa maagizo kuhusu suala muhimu zaidi kuhusu mapato katika madini na ufisadi katika sekta hiyo pamoja na gesi asilia. Kamati Kuu ya CCM ilipaswa kukubaliana na maoni tuliyotoa kwenye bajeti mbadala ya nishati na madini na kuiagiza serikali kuwasilisha muswada wa marekebisho ya kitabu cha mapato na sheria ya fedha  ili kuongeza wigo wa mapato kwenye sekta ya madini na pia kuchukua hatua za kushughulikia ufisadi pamoja na kupanua uwekezaji katika gesi asilia ikiwemo ujenzi wa bomba la gesi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania warejee hotuba ya bajeti mbadala ya nishati na madini ya kambi rasmi ya upinzani bungeni ambapo tulieleza bayana vyanzo vya matatizo kwenye sekta za nishati na madini ikiwemo suala la bei ya mafuta ya taa, tatizo la umeme, migogoro migodini na changamoto zingine na kueleza kwamba matatizo yamezidi kuongezeka baada ya kupitishwa kwa bajeti mbovu tarehe 21 Juni 2011 kwa kura za ndio za wabunge wa CCM bila kutanguliza mbele maslahi ya umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umma ufahamu kwamba bajeti iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha Mustapha Mkullo tarehe 8 Juni 2011 ilishindwa kutenga fedha za kutosha za kushughulia matatizo ya umeme pamoja na upungufu wa gesi asilia ilipitia katika baraza la mawaziri chini ya uenyekiti wa Rais Kikwete. Hata baada ya kambi rasmi ya upinzani kuwasilisha bajeti mbadala na  serikali haikukubali kuzingatia maoni yaliyotolewa kwa uzito unaostahili.&lt;br /&gt;Aidha muswada wa sheria ya fedha na marekebisho yake yaliyowasilishwa tarehe 22 Juni 2011 ambao uliongeza kodi kubwa katika mafuta ya taa na kuongeza misamaha ya kodi katika madini badala ya kupanua wigo wa mapato ulitokana na serikali inayoongozwa na CCM. Ikumbukwe kwamba wakati wa kujadiliwa sheria husika niliwasilisha marekebisho kwenye muswada yenye lengo la kupunguza kiwango cha kodi ambacho serikali ya CCM ilidhamiria kuongeza kwenye mafuta ya taa lakini yalikataliwa na serikali pamoja na wabunge wa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bajeti ya Serikali pamoja na Sheria ya Fedha vyote vilipitishwa kwa kura ya ndio na wabunge wa CCM kwa kufuata kilichoelezwa kuwa ni msimamo wa chama uliofikiwa katika kikao cha kamati ya wabunge wa chama hicho (party caucus) kwa maelezo kwamba ni utekelezaji wa sera na ilani za chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sehemu kubwa ya Kamati Kuu ya CCM ni wabunge ambao tayari walishapiga kura bungeni kupitisha bajeti na sheria bila kuzingatia mahitaji ya nishati na madini kwa kuongeza gharama za maisha kwa wananchi kupitia kupandisha bei ya mafuta ya taa, kupitisha bajeti isiyokidhi mahitaji ya kukabiliana na matatizo ya umeme na kushindwa kupanua wigo wa mapato katika madini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, ni muhimu Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM akaliomba radhi taifa kutokana na hali hiyo na pia CCM ikawaagize wabunge wake kuwaomba radhi wananchi wa majimbo yao na watanzania kwa kupiga kura ya ndio kwa kutanguliza mbele maslahi ya chama badala ya maslahi ya umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha natoa mwito kwa kamati kuu za vyama vingine vyenye uwakilishi bungeni ikiwemo CHADEMA inayoongoza kambi rasmi ya upinzani bungeni kuitisha vikao vya dharura kabla ya mkutano wa bunge unaoendelea hivi sasa kumalizika kujadili hali ya siasa ili kutoa ushauri kwa wabunge wake na serikali kwa ujumla kwa ajili ya kulinusuru taifa kwa kuwa nchi ipo katika hali tete. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Izingatiwe kuwa Kwa sehemu kubwa matatizo katika sekta za nishati na madini yamechangiwa na sababu za kibinadamu za kutowajibika ipasavyo kisera, kimaamuzi, kiusimamizi na kiutendaji kwa viongozi wa kiserikali kuanzia kwa viongozi wakuu wa nchi, wizara na watendaji wengine na hivyo kusababisha ugumu wa maisha kwa wananchi na kuathiri uchumi wa nchi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uwajibikaji unahitajika ukiambatana na hatua za haraka za kusimamia sera sahihi, uongozi makini na taasisi thabiti zenye kuelewa kwamba sekta ya nishati ni moyo wa taifa na sekta ya madini ni mtaji wetu kwa sasa na kuchukua hatua kali dhidi ya ufisadi uliofanyika katika sekta husika, kufanya mapitio ya mikataba, kuharakisha utekelezaji wa mipango kwa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Waziri Kivuli wa Nishati na Madini&lt;br /&gt;Bungeni, Dodoma-02/08/2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-5702864107721651378?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/5702864107721651378/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=5702864107721651378' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5702864107721651378'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/5702864107721651378'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/08/kuhusu-maamuzi-dhaifu-ya-cc-ya-ccm-juu.html' title='Kuhusu maamuzi dhaifu ya CC ya CCM juu ya nishati na madini'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-6069163530517414944</id><published>2011-08-02T04:28:00.000-07:00</published><updated>2011-08-02T04:31:08.217-07:00</updated><title type='text'>Kauli yangu kuhusu uuzwaji batili wa hisa na mali za UDA</title><content type='html'>Tarehe 27 Julai 2011 vyombo mbalimbali vya habari vimemnukuu Meya Wa Jiji la Dar es salaam Dkt. Didas Masaburi akieleza kilichoitwa maamuzi ya Baraza la Madiwani wa Jiji kuhusu kuvunja uongozi wa Shirika la Usafiri Dar es salaam (UDA) na kuunda kamati ya kuchunguza matatizo katika shirika hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tarehe 28 Julai 2011 vyombo mbalimbali vya habari vimemnukuu Meneja wa UDA, Victor Milanzi akimjibu Meya Masaburi kwa pamoja na mambo mengine kugoma kuondoka katika nafasi hiyo na kukanusha tuhuma zilizoelekezwa juu yake kuhusu ubadhirifu wa fedha za mauzo ya hisa za shirika hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa nafasi yangu ya ubunge ni mjumbe katika Baraza la Madiwani wa Jiji la Dar es salaam ambalo lina hisa 51% katika Shirika hilo na pia nawajibika kushiriki kuisimamia serikali kuu ambayo ina hisa 49% katika kampuni hivyo inanibidi kutoa kauli kuhusu upotoshaji unaondelea kufanywa na Meya Masaburi pamoja Meneja Milanzi kuhusu kashfa hii kupitia vyombo vya habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naomba wakazi wa Dar es salaam na wananchi watanzania kwa ujumla wafahamu kwamba Meya Masaburi na Meneja Milanzi wote wawili ni sehemu ya matatizo ya UDA kwa kushiriki kwa kiwango kikubwa katika kukiuka sheria, kanuni na taratibu kwenye uendeshaji wa shirika bila kuzingatia kwa ukamilifu maslahi ya wasafiri na walipa kodi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Meya Masaburi na Meneja Milanzi wote kwa nyakati mbalimbali wameshiriki katika kuachia maamuzi ya kifisadi ya kuuzwa kwa bei chee kwa hisa za kampuni ya UDA bila ya kuzingatiwa kwa sheria, kanuni na taratibu. Meneja Milanzi ameshiriki kuanzia hatua za mwanzo za mkataba kati ya UDA na Kampuni ya Simon Group mwaka 2009 wakati Meya Masaburi ameshiriki  katika kubariki utekelezaji wa mkataba huo wa kifisadi mwaka 2011 bila kuzingatia sheria, kanuni na maslahi ya wananchi wa Dar es salaam. &lt;br /&gt;Meneja Milanzi na bodi ya Wakurugenzi chini ya uenyekiti wa Iddi Simba wameshiriki katika kuingia mkataba mbovu na wa kifisadi wa mauzo ya kampuni hiyo huku sehemu ya fedha za malipo zikiingizwa kwenye akaunti za watu binafsi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Meya Masaburi ametekeleza mkataba huo kinyume cha sheria, kanuni na maslahi ya umma kwa yeye binafsi kuhamisha umiliki wa kampuni ya UDA kwa Simon Group baada ya malipo ya milioni 285 tu sawa na asilimia 12.5 ya mauzo ya hisa hizo kupitia maamuzi yake ya tarehe 10 Juni 2011 wakati UDA ina mali zenye thamani ya zaidi ya bilioni 12.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kufanya maamuzi hayo kinyume cha sheria, kanuni na maslahi ya wananchi Meya Masaburi amejaribu kujikosha kwa maamuzi batili ya vikao haramu vya kamati ya fedha na uongozi cha tarehe 29 Juni 2011 na Baraza la Madiwani la tarehe 20 Julai 2011.&lt;br /&gt;Kwa nafasi yangu ya ubunge ni mjumbe wa kamati ya fedha na uongozi na pia ni mjumbe wa baraza la Madiwani na tarehe 20 Julai 2011 nilieleza mbele ya waandishi wa habari kwamba vikao hivyo vyote viwili vilikuwa batili kwa kuwa viliitishwa bila kuzingatia sheria na kanuni pia vilifanya maamuzi haramu ambayo hayakuzingatia sheria, kanuni na maslahi ya wananchi wa Dar es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama nilivyoelekeza kusudio siku hiyo, nitatoa waraka kwa wananchi wa Dar es salaam na mamlaka husika wenye kueleza msingi wa kupiga kura ya HAPANA siku hiyo kwa maamuzi yote haramu yaliyofanywa na vikao hivyo batili na kueleza kwa kina vifungu vya sheria, kanuni, mkataba na taratibu zilizokiukwa pamoja na kuwataja wa majina wahusika na kiwango cha fedha kilichotolewa. Hata hivyo, kabla ya kutoa waraka huo nimeona nitoe taarifa hii kwa umma ili mamlaka zote zinazohusika ziingilie kati na kuchukua hatua za haraka kunusuru mali na mwelekeo wa shirika la UDA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri Mkuu Mizengo Pinda anapaswa kuingilia kwa kuchukua hatua stahiki za kuingoza serikali kupitia upya mkataba ulioingiwa na kutekelezwa kinyume cha sheria, kanuni na maslahi ya wananchi kati ya Jiji, UDA na Simon Group Limited. Maamuzi yaliyofanywa na Meya Masaburi na vikao vyake haramu vya jiji na vya UDA yanapaswa kubatilishwa. Aidha maamuzi ya bodi ya UDA chini ya uenyekiti wa Iddi Simba kwa miaka kadhaa yanapaswa kupitiwa upya kwa kuzingatia sheria, kanuni na maslahi ya umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waziri wa Fedha Mustapha Mkullo anapaswa kuingilia kati kupitia Msajili wa Hazina na CHC ili kunusuru hisa za serikali kuu katika UDA pamoja na mali za shirika kwa ujumla wake. Izingatiwe kwamba tarehe 28 Februari 2011 ofisi ya Waziri Mkuu iliandika barua yenye kumbukumbu namba CAB. 185/295/01/27 ambayo Katibu Mkuu Hazina anayo nakala yake yenye kueleza bayana kwamba uuzwaji wa hisa ambazo hazijagawiwa (unallocated shares) uliokuwa ukifanywa na UDA haukuzingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma na kuagiza mchakato huo usitishwe na CHC kushirikishwa. Izingatiwe kwamba katika maamuzi haramu yaliyofanywa na Meya Masaburi tarehe 10 Juni 2011 Wizara ya Fedha (hazina) na  CHC wote hawakushiriki kwenye kikao kilichoitwa cha wana hisa wa UDA wakati serikali kuu imekuwa na hisa 49%.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kamati husika za Bunge hususani ya Miundo mbinu na ya Hesabu za Mashirika ya Umma ziingilie kati kwa haraka kwa kushirikiana na ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Mamlaka ya Kudhibiti Manunuzi ya Umma(PPRA) na wabunge wa mkoa wa Dar es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua hizo za haraka zitaokoa mali za umma, kuweka msingi wa kuboresha usafiri katika mkoa wa Dar es salaam na kuwezesha hatua za kisheria na kinidhamu kuchukuliwa kwa wahusika wote waliofikisha jiji na taifa katika hali hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba masuala ya Mashirika na Makampuni yaliyo chini ya jiji la Dar es salaam nilianza kuyahoji katika vikao hususani vya kamati ya fedha na uongozi mara baada ya kuingia katika utumishi wa umma kwenye Halmashauri ya Jiji kupitia mikutano ya mwezi Machi na Mei 2011.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, badala ya Mstahiki Meya Masaburi kuchukua hatua stahiki kama ilivyoazimiwa katika vikao hivyo akaenda kufanya maamuzi binafsi ambayo yameongeza ukubwa wa matatizo badala ya kuyapunguza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na hali hiyo mwezi Juni nikaamua kutumia fursa za kibunge katika kushughulikia hatma ya UDA na usafiri mkoani Dar es salaam kwa ujumla wake. &lt;br /&gt;Hivyo, wakati wa mjadala wa Azimio la kuliongezea muda Shirika Hodhi la Mali za Mashirika ya Umma (CHC) tarehe 23 Juni 2011 nilihoji kwa maandishi kuhusu mauzo ya hisa na mali za kampuni ya UDA na kutaka hatua za haraka kuchukuliwa kwa kurejea pia ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) . Hata hivyo, Waziri wa Fedha Mustapha Mkullo kwenye majumuisho yake hakutoa kauli wala kuchukua hatua za haraka pamoja na kuwa hatma ya hisa 51% za shirika hilo zinahusu Wizara yake kupitia Msajili wa Hazina.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nikarudia tena kuhoji kwa maandishi wakati wa mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu iliyowasilishwa tarehe 23 Juni 2011 nikipinga uuzwaji wa hisa za UDA bila maslahi ya usafiri wa wananchi wa Dar es salaam kuzingatiwa na kutaka kuwe na uhusiano baina ya  hatma ya UDA na Mradi wa Mabasi yaendayo kwa Haraka (DART) ambao unaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu. Nilihoji suala hilo kama sehemu ya hitaji la kuwa na mfumo thabiti wa Usafiri wa Halaiki wa Umma (Mass Public Transit) ambao utachangia kwa kiwango kikubwa kupunguza adha ya usafiri katika jiji la Dar es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatahivyo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika majumuisho ya bajeti yake tarehe 1 Julai 2011 hakutoa kauli wala kuchukua hatua za haraka za kunusuru hali ya mambo pamoja na kuwa yeye ndiye mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) hivyo ana wajibu wa kufuatilia masuala ya kisheria, kinanuni na kimikataba ya Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kama ilivyo kwa halmashauri zingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya hapo ndipo kashfa ya UDA ikaanza kujitokeza kwenye vyombo vya habari tarehe 11 Julai 2011  ikiwa katika sura ya mzozo baina ya Meneja Milanzi na Mkurugenzi Kisena wa Simon Group Limited katika hatua za kulazimishana kuondoka ofisini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia hali hiyo tarehe 15 Julai 2011 baada ya majibu ya swali la msingi nililouliza Ofisi ya Waziri Mkuu kuhusu ukaguzi maalum wa mahesabu na ufisadi katika kituo cha Mabasi cha Ubungo (UBT) niliuliza swali la nyongeza kuhusu kashfa ya kampuni ya UDA kutokana na uhusiano wake na mradi wa DART ambapo maeneo ya UBT na UDA yatahusika. Katika swali langu nilitaka hatua za haraka kuchukuliwa na serikali kutokana na mauzo hayo kuendelea bila kuzingatia sheria, kanuni na maslahi ya wananchi hata hivyo Naibu Waziri Aggrey Mwanri hakutoa majibu ya kuridhisha wala kuchukua hatua zinazostahili kufuatia suala hilo hali ambayo ilitoa mwanya kwa Meya Masaburi kuendelea na mchakato haramu. Katika muktadha huo nitaendelea kushirikiana na madiwani wenzangu wenye kutanguliza mbele maslahi ya umma  ikiwemo wabunge wa mkoa wa Dar es salaam ambao mimi ni katibu wao pamoja na mamlaka zingine za kiserikali na kibunge katika kushughulikia suala hili. Natoa mwito kwa wananchi wa Dar es salaam kutuunga mkono katika kulifuatilia kwa karibu suala hili na kuchukua hatua zinazostahili kila mmoja kwa nafasi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenu katika utumishi wa umma,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;Bungeni-Dodoma&lt;br /&gt;31 Julai 2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-6069163530517414944?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/6069163530517414944/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=6069163530517414944' title='4 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6069163530517414944'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/6069163530517414944'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/08/kauli-yangu-kuhusu-uuzwaji-batili-wa.html' title='Kauli yangu kuhusu uuzwaji batili wa hisa na mali za UDA'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>4</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-2886068089736885816</id><published>2011-07-31T06:58:00.000-07:00</published><updated>2011-07-31T07:00:33.975-07:00</updated><title type='text'>Ufisadi Kituo cha Ubungo(UBT) na Usafiri DSM (UDA)-Majibu Bungeni</title><content type='html'>Ripoti ya Uchunguzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi ya Ubungo (Swali la Nyongeza kuhusu Ufisadi kwenye Shirika la Usafiri Dar es salaam –UDA)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MKUTANO WA NNE: Kikao cha Ishirini na Sita – Tarehe 15 Julai, 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MHE. JOHN J. MNYIKA aliuliza:-&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tarehe 15 Machi, 2009 Serikali kupitia Waziri Mkuu iliagiza ufanywe uchunguzi&lt;br /&gt;maalum kuhusu makusanyo ya kituo cha Mabasi cha Ubungo ili kuboresha mapato ya Jiji&lt;br /&gt;la Dar es Salaam. Tarehe 28 Julai, 2009, Serikali ilikabidhi ripoti ya uchunguzi huo kwa&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CAG ambayo pamoja na mambo mengine ilieleza kasoro za ukusanyaji na tuhuma za&lt;br /&gt;ubadhirifu wa mapato ya kituo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mosi; Je, ni lini Serikali itaweka wazi taarifa hiyo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili; Je, Serikali imechukua hatua gani juu ya kasoro zilizobainishwa kuhusu&lt;br /&gt;mikataba ya kampuni ya Smart Holdings, Rick Hill Hotel, Abood Bus Services, Clear&lt;br /&gt;Channel, Globe Accounting Services na Scandinavian Express Services, ambayo&lt;br /&gt;imesababisha hasara na upotevu wa mapato?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu; Je, Serikali iko tayari kufuatilia na kuchukua hatua za haraka juu ya&lt;br /&gt;malalamiko yanayotolewa na ukusanyaji wa mapato unaofanywa sasa ili kunufaisha&lt;br /&gt;umma kikamilifu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NAQ&lt;br /&gt;SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:-&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la&lt;br /&gt;Mheshimiwa John John Mnyika, Mbunge wa Ubungo, lenye (a) (b) na (c) kama&lt;br /&gt;ifuatavyo:-&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mosi; Mheshimiwa Naibu Spika, Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali&lt;br /&gt;(CAG) alifanya uchunguzi maalum katika kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo na&lt;br /&gt;kubaini kasoro mbalimbali. Aidha, hoja zilizojitokeza katika taarifa ya Uchunguzi ya&lt;br /&gt;CAG katika kituo hicho zimejitokeza pia katika taarifa ya mwaka ya ukaguzi ya CAG ya&lt;br /&gt;mwaka 2009/2010 ambayo iliwasilishwa hapa Bungeni na hoja hizo zimeaza kufanyiwa&lt;br /&gt;kazi na Halmashauri ya Jiji.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili; Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuondoa kasoro zilizojitokeza katika Kituo&lt;br /&gt;hicho, Serikali inapitia upya mikataba ya makampuni na kuhuisha viwango&lt;br /&gt;vinavyotakiwa kukusanywa kulingana na sheria ndogo ya Halmashauri ya Jiji la Dar es&lt;br /&gt;Salaam inayosimamia ushuru huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Marekebisho ya viwango hivyo yatasaidia kuongeza mapato yanayokusanywa&lt;br /&gt;katika kituo hicho na kuondoa kasoro zilizokuwepo za ukusanyaji wa mapato.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukusanyaji wa ushuru katika kituo hicho kwa sasa unafanywa na Halmashauri ya Jiji la&lt;br /&gt;Dar es Salaam kupitia kwa Wakala aitwae KONSAD INVESTMENT LIMITED ambaye&lt;br /&gt;anakusanya ushuru huo kwa wastani wa shilingi milioni 4 hadi milioni 5.7 kwa mwezi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu; Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingaia malalamiko yaliyopo, Serikali&lt;br /&gt;tayari imebadilisha Menejimenti ya kituo na itaendelea kuboresha miundombinu yake.&lt;br /&gt;Aidha, katika Bajeti ya mwaka 2011/2012, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam&lt;br /&gt;imetenga kiasi cha shilingi milioni 85 kwa ajili ya kufanya matengenezo katika eneo a&lt;br /&gt;maegesho ya magari. Mpango wa muda mrefu wa Serikali ni kukijenga upya kituo cha&lt;br /&gt;Mabasi kama ilivyoainishwa katika mpango wa biashara wa mwaka 2007.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na majibu&lt;br /&gt;yaliyotolewa, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu Naibu Waziri ameeleza kwamba&lt;br /&gt;mkandarasi KONSAD Investment anakusanya milioni Nne hadi milioni Tano kwa&lt;br /&gt;mwezi, lakini kwa mujibu wa taarifa zilizopo ni kwamba toka Mkandarasi aingie&lt;br /&gt;mkataba mwezi Oktoba mwaka 2010, kwa mujibu wa Mkataba alipaswa kukusanya&lt;br /&gt;shilingi milioni 5.6 lakini alifanya hivyo kwa siku mbili tu (mara mbili tu) baada ya hapo&lt;br /&gt;toka wakati huo Oktoba 2010 mpaka leo amekuwa hatekelezi mkataba na ameandika&lt;br /&gt;barua Ofisi ya Waziri Mkuu na inaelekea anakingiwa kifua kuutekeleza huu mkataba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mosi; Ningependa kupata kauli kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na ninajua inafahamu&lt;br /&gt;hili jambo kwa undani, Je, iko tayari sasa kuiruhusu Jiji la Dar es Salaam liweze kuvunja&lt;br /&gt;huu mkataba ambao haunufaishi wananchi wa Dar Es Salaam?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili; Suala la udhaifu wa kimikataba wa kituo cha mabasi ya Ubungo ambayo&lt;br /&gt;yanahusisha vile vile sehemu ya eneo litakalohusiana na mradi wa mabasi yaendayo kasi&lt;br /&gt;ambayo linahusiana na Kampuni ya UDA yamefikia kiwango cha juu sana, ninaelewa&lt;br /&gt;kwamba ofisi ya Waziri Mkuu iliandika barua ya kusitisha taratibu za uuzwaji wa hisa za&lt;br /&gt;kampuni ya UDA ambazo zimeuzwa na upotevu wa mali nyingi; ninaomba kauli ya Ofisi&lt;br /&gt;ya Waziri Mkuu kuhusiana na ufisadi uliopo kwenye kampuni ya UDA unaoendelea hivi&lt;br /&gt;sasa, na iko tayari kutoa maelekezo kwa Jiji la Dar es Salaam kuweza kusitisha taratibu&lt;br /&gt;zinazoendelea?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA&lt;br /&gt;NAQ SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, nataka&lt;br /&gt;niseme hapa kwamba, Waziri Mkuu alikwenda akamwelekeza CAG aende katika kituo&lt;br /&gt;hiki cha mabasi, akamtaka afanye uchunguzi pale. Walipokwenda pale kwa mara ya&lt;br /&gt;kwanza walikuwa wanakusanya milioni 1.5 kwa siku.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CAG alipofanya marekebisho yale wakafanya na mahesabu na wakamaliza&lt;br /&gt;wakaweka na Menejimenti nyingine pale, ikapanda mpaka milioni 5.7&lt;br /&gt;ninazozizungumza, siyo kwa mwezi ni kwa siku, na kama alivyosema Mbunge kwamba&lt;br /&gt;kampuni ilikusanya kwa siku ya kwanza na siku ya pili na baadaye kukawa na matatizo&lt;br /&gt;hawakukusanya kiasi hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mnyika analifahamu jambo hilo kuliko&lt;br /&gt;sisi sote hapa, tunachojua ni kwamba kuna kampuni nyingine mpya ambayo imekwenda&lt;br /&gt;pale inafanya kazi na hivi tunavyozungumza hapa wanao huu mgogoro anaozungumza na&lt;br /&gt;wameanza kupelekana mpaka mahakamani, kuna mambo ambayo wakati anakwenda kuoperate&lt;br /&gt;ameona kwamba yanakwenda kinyume na jinsi walivyokuwa wamekubaliana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Naibu Spika, hivi ninavyozungumza hapa sasa hivi, tumemwita&lt;br /&gt;Mkurugenzi Mtendaji Kingopi hapa Dodoma tukamuuliza hili analolizungumza hapa,&lt;br /&gt;wameniambia kwamba hili wameliona na wanalifanyia kazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo Mheshimiwa Mnyika ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri hii&lt;br /&gt;tunayoizungumza yaani (DCC) avute subira katika jambo hili. Hili jambo jingine jipya&lt;br /&gt;sasa linaanza kwa sababu huyu ni mpya ambaye tumesema kwa taratibu hizi mpya akaye&lt;br /&gt;pale, kama ikiwezekana tukubaliane leo tukitoka hapa nimwuite Kingobi na wenzake&lt;br /&gt;tukae na tuseme ni nini kilichotokea kwamba kiasi hiki sasa hakiendelei kukusanywa&lt;br /&gt;kama ilivyokuwa siku ya kwanza na siku ya pili kama anavyosema Mbunge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la DART analolizungumza hapa, huu ni&lt;br /&gt;mpango mwingine unaokuja, DART tunasimamia sisi Ofisi ya Waziri Mkuu na ujenzi ule&lt;br /&gt;utafanywa chini ya Wizara ya Ujenzi, na hili suala la UDA analolizungumza hapa kwa&lt;br /&gt;pamoja mimi ningemuomba tukutane kwa sababu linahitaji details zaidi ili tuliangalie&lt;br /&gt;pamoja na lile ambalo tumelizungumzia.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-2886068089736885816?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/2886068089736885816/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=2886068089736885816' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2886068089736885816'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/2886068089736885816'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/07/ufisadi-kituo-cha-ubungoubt-na-usafiri.html' title='Ufisadi Kituo cha Ubungo(UBT) na Usafiri DSM (UDA)-Majibu Bungeni'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-7652175012296909297</id><published>2011-07-30T12:50:00.000-07:00</published><updated>2011-07-30T12:51:31.928-07:00</updated><title type='text'>Salam za Mshikamano kwa Mdahalo wa Katiba</title><content type='html'>Nikiwa bungeni Dodoma nimefuatilia kupitia vyombo vya habari mdahalo wa katiba ambao umefanyika Ubungo Plaza. Natoa salamu za mshikamano na pongezi kwa waandaaji, watoa mada na washiriki wa mdahalo huu wenye kuchangia katika mjadala wa katiba mpya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kupitia kongamano hilo maoni mbalimbali ya maudhui hususani masuala ya muafaka wa kitaifa, ardhi na rasilimali za nchi, jinsia, muungano, haki za binadamu ikiwemo za makundi mbalimbali katika jamii, mgombea binafsi, bunge, mahakama,  wananchi kuwa na mamlaka juu ya dola, maadili ya taifa nk &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kongamano pia limejadili masuala mbalimbali kuhusu mchakato wa katiba ikiwemo kasoro katika muswada wa kuandikwa kwa katiba mpya, muundo wa vyombo vitavyoratibu mchakato wa katiba mpya, haja ya kuwa na mkutano mkuu wa katiba, nafasi ya bunge katika mchakato wa katiba na umuhimu wa kupunguza mamlaka ya Rais katika mchakato wa katiba nk.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo, imezungumzwa katika mdahalo kuwa muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba utawasilishwa katika mkutano wa nne wa bunge unaoendelea hivi sasa. Natoa tahadhari kwa wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla kuzingatia kuwa muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba umeondolewa kinyemela katika ratiba ya mkutano wa nne wa bunge, kilichobakishwa kwenye ratiba ni semina tu ya wabunge kuhusu muswada husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, pamoja na kujadili kuhusu maudhui ni vizuri katika hatua ya sasa mkazo ukawekwa katika kujadili mchakato wa katiba mpya hususani kuhusu hatma ya muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba. Hii ni kwa sababu maoni kuhusu maudhui hayatazingatiwa kikamilifu ikiwa sheria ya kusimamia mchakato wa katiba mpya itacheleweshwa na itatungwa sheria mbovu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ikumbukwe kwamba hati ya dharura kuhusu sheria ya mabadiliko ya katiba ilipoondolewa katika mkutano tatu wa Bunge mwezi Aprili serikali iliahidi muswada huo utajadiliwa katika mkutano wa nne wa Bunge unaoendelea hivi sasa baada ya kupata maoni ya wananchi. Serikali haikutimiza ahadi ya kuwashirikisha wananchi kwa upana na uwazi kuhusu muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba wala ahadi ya muswada huo kujadiliwa katika mkutano wa nne wa Bunge kama ilivyotolewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha wakati wa mkutano wa nne wa Bunge unaoendelea hivi sasa Waziri wa Katiba na Sheria Celina Kombani akijibu maswali alieleza kwamba serikali imeshawasilisha kwa bunge marekebisho ya muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba na Spika wa Bunge Anne Makinda akaongezea majibu kuwa sasa muswada huo uko kwa bunge ambalo ndilo litakaloamua hatma ya muswada husika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Marekebisho ambayo serikali imeyawasilisha mpaka hivi sasa pamoja na kuyatafsiri kwa lugha ya Kiswahili (sio kuutunga upya) hayajazingatia hoja za msingi zilizotolewa na wananchi na wadau mbalimbali wakati walipoukataa  muswada wa awali wa sheria ya mabadiliko ya katiba wa mwaka 2011 (The Constitutional Review Act 2011) uliochapwa katika gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11 Machi 2011 na kuwasilishwa bungeni mwezi Aprili 2011.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Natoa mwito wa Kituo Cha Sheria za Haki za Binadamu (LHRC), Jukwaa la Katiba, wadau mbalimbali na wananchi kwa ujumla kuelekeza nguvu katika hatua ya sasa kutaka muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba ulioandikwa upya kuwekwa hadharani hivi sasa. Pia kuitaka Serikali na Bunge kuzingatia kwa ukamilifu hatua zinazohusika kwa mujibu vifungu vya 80, 83 na 84 vya Kanuni za Kudumu za Bunge baada ya kuondolewa kwa hati ya dharura ikiwemo kutoa ufafanuzi kuhusu utata uliopo hivi sasa kuhusu muswada husika. Muswada mbovu wa sheria ya mabadiliko ya katiba utatuletea katiba bomu isiyo na uhalali wa kukubaliwa na umma na kuongeza mpasuko katika nchi badala ya kuwa na muafaka wa kitaifa na misingi muhimu ya uwajibikaji kwa ustawi wa wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika (Mb)&lt;br /&gt;29/07/2011&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/7405076116754779487-7652175012296909297?l=mnyika.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://mnyika.blogspot.com/feeds/7652175012296909297/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=7405076116754779487&amp;postID=7652175012296909297' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7652175012296909297'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/7405076116754779487/posts/default/7652175012296909297'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://mnyika.blogspot.com/2011/07/salam-za-mshikamano-kwa-mdahalo-wa.html' title='Salam za Mshikamano kwa Mdahalo wa Katiba'/><author><name>John Mnyika</name><uri>http://www.blogger.com/profile/06318351914677487946</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-7405076116754779487.post-1812929349432896352</id><published>2011-07-15T03:56:00.000-07:00</published><updated>2011-07-15T03:57:34.475-07:00</updated><title type='text'>Hotuba Mbadala Wizara ya Nishati na Madini</title><content type='html'>HOTUBA YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI WIZARA YA NISHATI NA MADINI MHE. JOHN JOHN MNYIKA (MB) KUHUSU MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA 2010/2011 NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012 UTANGULIZI &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuwasilisha maoni haya ya kambi rasmi ya upinzani kuhusu makadirio ya matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2011/2012 kwa mujibu wa kanuni za Bunge (Toleo la mwaka 2007) kifungu cha 99 (7) ikiwa ni sehemu ya kuchangia katika wajibu wa bunge wa kuishauri na kuisimamia serikali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Nawashukuru wananchi wenzangu wa jimbo la Ubungo kwa kuniamini bila kujali tofauti zingine na kunituma kuwawakilisha kwa kunitunuku heshima ya kuwa mtumishi wa umma. Nawashukuru pia kwa kunipa madiwani wa kufanya nao kazi. Asanteni wazee kwa busara zenu, wanawake kwa sala zenu na vijana wenzangu tuliokuwa pamoja kipindi cha kampeni na kukesha wote Loyola katika kulinda ushindi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumeandika historia kwamba hakuna hujuma inayoweza kudhibiti nguvu ya umma (people’s power) mabadiliko yameanza kuonekana na kwa pamoja tuendelee kutimiza wajibu kwa kurejea dira yetu: A.M.U.A; Maslahi ya Umma Kwanza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Nawashukuru wanafamilia yetu ya Dalali; wazazi wangu na ndugu zangu kwa upendo wenu ambao umechangia katika furaha yangu na motisha ya kuendeleza ujasiri na uadilifu katika kusimamia ukweli, haki na ustawi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Natambua kwa shukrani mchango wa viongozi wenzangu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) makao makuu, Mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum Dar e salaam, Jimbo la Ubungo na wa kambi rasmi ya upinzani bungeni katika hatua ambayo tumefikia; mahitaji na matumaini ya watanzania yanatutaka tuendelee kuongoza kwa umoja, umakini na uwajibikaji mpaka kieleweke dhidi ya ubinafsi, uzembe na ufisadi ambao unazidi kushamiri katika taifa letu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Nawashukuru wote katika mamlaka ambao mmenipa ushirikiano kwenye serikali kuu, manispaa ya Kinondoni, katika kamati ya nishati na madini na wabunge wengine kwa ujumla katika kutekeleza majukumu ya kibunge kwa manufaa ya taifa letu na watu wote. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Wizara ya Nishati na Madini ambayo tunatolea maoni bajeti yake leo ni wizara nyeti sana katika taifa letu nyakati za sasa na kwa vizazi vijavyo. Sekta ya nishati ni moyo wa taifa wakati madini ni mtaji wa nchi yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania imejaliwa rasilimali nyingi watu, ardhi yenye rutuba , maji (bahari, mito na maziwa), kuwa katika eneo la kimkakati la kijiografia kwa biashara, mali asili ikiwemo za utalii na madini. Hata hivyo, tunaelekea kuwa na laana ya rasilimali hali ambayo inafanya wananchi walio wengi kuendelea kuwa katika lindi la umasikini na wakiendelea kusukumwa pembezoni nje ya urithi ambao taifa linao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Tishio la usalama na amani katika taifa letu kwa sasa sio migomo wala maandamano bali ni migogoro inayoendelea ya kirasilimali maeneo mbalimbali ya nchi ambayo ni bomu la wakati litakalolipuka iwapo kasi ya ukuaji wa uchumi wenye kutoa fursa kwa wengi haitaongezwa. Sekta ya nishati ni moyo wa kurekebisha hali hii na sekta ya madini ni mtaji wa kufanikisha dhamira hiyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; tunakutana leo ikiwa ni miezi michache kuelekea kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru taifa likiwa gizani kutokana na mgawo wa umeme unaoendelea, idadi ndogo ya watanzania waliounganishwa kwenye gridi ya taifa na matatizo ya sekta ya nishati kwa ujumla. Tunakutana wakati ambao urithi wetu mkuu ambao mababu zetu waliupigania wakati wa kudai uhuru; ardhi na rasilimali zake ikiwemo madini ukiwa mashakani kutwaliwa na kutawaliwa kwa ubeberu mamboleo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Mnamo tarehe 21 Juni 2011 Bunge lilipitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012 ambapo wabunge wa Kambi Rasmi ya Upinzani tulipiga kura ya HAPANA; lakini ikapita kutokana na uwingi wa wabunge wa upande wa pili bila kuzingatia maslahi ya umma. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tulipiga Kura ya HAPANA kwa kuwa ilikuwa ni bajeti yenye maneno matupu bila matendo katika mipango na utekelezaji; athari za bajeti hiyo zimeshaanza kudhihirika kwenye uchumi wa nchi na maisha ya wananchi wa kawaida. Bajeti ya mwaka 2011/12 ilielezwa kwa maneno matupu kuwa imeweka nishati kuwa ni kipaumbele cha kwanza. Hata hivyo vitabu vya Bajeti ya Serikali iliyopitishwa vinadhibitisha ukweli mchungu kwamba jumla ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya nishati na madini ni bilioni 539.3 tu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa Vitabu vya Bajeti ya Serikali 2011/2012 iliyopitishwa, Wizara ya Nishati na Madini imetengewa jumla ya shilingi 402.4 bilioni kwenye Fungu 58. Fedha hizo zimegawanywa katika mafungu ya Matumizi shilingi 76,953,934,000 na bajeti ya Maendeleo zimetengwa shilingi 325,448,137,000 tu. Fedha nyingine kidogo za maendeleo bilioni 126.6 zipo kwenye Fungu la 50 miradi ya MCC kwa kutegemea wahisani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo; bajeti hii haijaichukulia kwa uzito unaostahili sekta za nishati na madini hususani umeme hali ambayo inaibua maswali iwapo serikali ina dhamira ya dhati ya kukabiliana na changamoto za msingi zinazolikabili taifa hivi sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kambi rasmi ya upinzani imepitia kitabu cha pili cha matumizi ya kawaida ya Wizara ya Nishati na Madini ( Volume II Supply Votes) Fungu la 58 vifungu 1001-1009, 2001-2012 na 3001 na kubaini kwamba hii ni bajeti ya mgawo mkubwa wa posho na ufujaji. Mathalani Idara ya Kitengo cha Mawasiliano katika kulipana posho zitatumika Sh. Milioni 405.62 sawa na asilimia 63% ya fedha yote iliyotengwa Sh. Milioni 641.99 kwa idara hii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Idara ya fedha na uhasibu itatumia Sh milioni 598.49 sawa na asilimia 42% ya fedha yote iliyotengwa. Kanda ya Ziwa – Mwanza kulipana posho inatumia Sh. milioni 389.68 sawa na asilimia 40% ya fedha yote iliyotengwa. Kuna posho kuwanunulia mavazi wafanyakzi wanao safiri nje ya nchi, sherehe na maonesho, chakula na vinywaji, huduma kwa wageni, posho za kukaimu nafasi na posho nyingine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ujumla Wizara ya Nishati na Madini inakadiriwa kutumia Sh. Bilioni 7.9 kulipana posho na matumizi mengine ya kawaida ya anasa. Kwani jumla hii ni nje ya posho za msingi kama vile; posho za uhamisho, posho za mafunzo, nyumba, maji na umeme. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani inataka serikali ifanye marekebisho kwenye bajeti ili fedha hizi zipunguzwe ziweze kuongezwa kwenye kuongeza ujenzi wa miundombinu wa Chuo Cha Madini Dodoma na na kuongeza kiwango cha fedha katika mfuko wa wachimbaji wadogo wa madini. Aidha yako matumizi mengine ya ujenzi wa maofisi na gharama kubwa za kisheria ambayo yanapaswa kuhamishiwa katika miradi muhimu ya maendeleo ikiwemo ya umeme vijijini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Ikumbukwe kwamba tarehe 15 Juni 2011 Kambi ya upinzani iliwasilisha bajeti mbadala ambayo ilitenga fedha za kutosha katika kukabiliana na changamoto za sekta za nishati na madini. Bajeti mbadala ilitenga fedha za maendeleo Sh. Bilioni 977 kwa ajili ya Wizara ya Nishati na Madini ukilinganisha na ile serikali iliyotenga Sh. Bilioni 452 kwa maendeleo (Fungu 58 na 50); ambayo ni sawa na ongezeko la zaidi ya asilimia 100 (100 %). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi rasmi ya upinzani inataka kiwango cha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuongezwa ili vipaumbele vifuatavyo viweze kuzingatiwa kwa uzito unaostahili: · Kuwekeza fedha za kutosha kwenye sekta ya umeme na Gesi ili kumaliza kabisa tatizo la nishati ya Umeme na kupunguza gharama za maisha. Hatua hizo ziambatane kuwekeza katika Bomba la Gesi kutoka Mtwara, pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant) ili kuwezesha gesi kutumika kwenye magari, viwandani na majumbani. ·&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuhakikisha tunazalisha 360MW za umeme kila mwaka ili kufikia malengo ya Mpango wa Maendeleo wa miaka Mitano na kumaliza tatizo la mgawo wa umeme. Kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya usafirishaji na usambazaji wa umeme vijijini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi vijijini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Tunatambua kwamba wakati wote serikali imekuwa ikitoa visingizio kuwa kiasi cha fedha kilichopo ni kidogo na hivyo kutegemea zaidi fedha za wahisani. Hivyo, kambi rasmi ya upinzani imewasilisha vyanzo vya mapato ambavyo vinaweza kutumika kuongeza kiwango cha bajeti kwa ajili ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini. Baadhi ya misingi muhimu ya mapato ambayo tumeiwasilisha ni pamoja na: · Kupunguza misamaha ya Kodi ikiwemo kuondoa msamaha wa ushuru wa mafuta Kampuni za Madini peke yake kutaongeza mapato ya shilingi bilioni 59. ·&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutoka Vyanzo vipya vya mapato tulivyovianisha; kwa upande wa sekta ya madini kwa Kurekebisha Kodi Sekta ya Madini peke yake tunaweza kukusanya shilingi bilioni 240 katika mwaka wa fedha 2011/2012. · Kupunguza fedha kwenye Wizara zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida yasiyokuwa ya lazima na kuelekeza fedha katika miradi ya maendeleo hususani ya umeme na gesi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; katika muktadha huo pamoja na kifungu cha 106 cha Kanuni za Bunge kutenguliwa kuruhusu sheria ya fedha 2011 kupitishwa tarehe 22 Juni 2011; ni muhimu mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini uhusishe pia kupitia kitabu cha kwanza cha mapato (Volume 1- Revenue Estimates) ili kuongeza wigo wa mapato. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kuzingatia maoni na mapendekezo yanayoendelea kutolewa na kuwasilisha marekebisho (amendments) ya sheria ya fedha ili kuongeza wigo wa mapato. Aidha, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka kuwasilisha bajeti ya Nyongeza (Supplimentary budget) kwa ajili ya Wizara ya Nishati na Madini ili kuwa na makadirio ya nyongeza ya matumizi kwa mujibu wa kanuni 107 kwa ajili ya miradi ya umeme na gesi asilia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umeme Mheshimiwa Spika; Tatizo sugu la mgawo wa umeme ambalo sasa limekomaa na kuwa janga la taifa limetokana na ufisadi na udhaifu wa kiuongozi na kiutendaji ambao umeikabili sekta ya nishati nchini kuanzia awamu ya pili, likaongezeka katika awamu ya tatu na kukomaa katika awamu ya nne ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ufisadi na udhaifu huo wa kiutendaji unajidhihirisha zaidi katika maamuzi mbalimbali yaliyofanyika awamu ya pili hususani 1990 mpaka 1995; awamu ya tatu hususani 1996 mpaka 2004 na awamu ya hususani 2006 mpaka 2011 kwenye maamuzi na mikataba mbalimbali mathalani kashfa ya IPTL, hasara ya mchakato wa ubinafsishaji wa TANESCO, uzembe wa Net Group Solution, ufisadi wa Kiwira, kashfa ya Alstorm Power Rentals, sakata la Songas/Pan African Energy, ufisadi wa Richmond, madhara ya Dowans (ambayo sasa mitambo yake iko chini ya Symbions bila serikali kutoa kauli, kashfa kuhusu mitambo hiyo zimekwisha baada ya umiliki kuhamia kwa kampuni ya Marekani na iwapo taratibu za zabuni zilifuatwa) ambapo mkazo haukuwekwa katika mipango ya muda mrefu ya kuondokana na tatizo la mgawo wa umeme nchini ambayo imetajwa bayana katika nyaraka mbalimbali za mipango ya kiserikali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Pamoja na maamuzi ya Bunge la tisa ya kuhusu masuala hayo bado kambi ya upinzani inataka hatua kamili kuchukuliwa kwa wahusika wa kashfa hizo kama walivyotajwa kwenye orodha ya mafisadi ili kujenga msingi wa kuepusha hali kama hiyo kujirudia katika uwekezaji unaondelea hivi sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika,athari za upungufu wa umeme kwenye uchumi wa nchi na maisha ya wananchi ni makubwa sana. Taarifa za Serikali zinaonyesha kwamba Mamlaka ya Mapato inapoteza mapato ya Bilioni 840 kwa mwaka kutokana na mgawo wa umeme na ripoti za wadau wengine zimeeleza bayana upungufu wa ajira unaosababishwa na mgawo wa umeme. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Ikumbukwe kwamba katika mkutano wa pili wa Bunge kikao cha sita tarehe 15 Februari 2011 Waziri wa Nishati na Madini alitoa kauli bungeni kuhusu mipango ya dharura ya serikali kupunguza tatizo la mgawo wa umeme. Kati ya hatua ambazo zilielezwa ni ukodishaji wa mitambo ya dharura ya MW 260 na kuongeza matumizi katika mitambo ya IPTL.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi rasmi ya upinzani imefadhaishwa na taarifa iliyotolewa kwa umma na TANESCO wakati wa kuanza kwa mgawo wa umeme unaoendelea hivi sasa kuwa umechangiwa na mitambo ya IPTL kuzalisha chini ya kiwango kutokana na upungufu wa mafuta mazito (HFO) suala ambalo linatosha kwa serikali kuwajibika kutokana na uzembe wenye kulitia hasara taifa kwa sababu suala hili lilikuwa likijulikana kwa miezi mingi bila hatua stahili kuchukuliwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Tarehe 1 Aprili 2011 Rais Jakaya Kikwete alitoa ahadi kupitia hotuba yake kwa taifa kwamba mitambo ya MW 260 ingekodishwa na kuanza kufanya kazi mwezi Julai kukabiliana na mgawo wa umeme. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi ya Upinzani haijaridhika na visingizio ambavyo vimekuwa vikitolewa na serikali kwa kutumia sababu za matatizo ya nje ya nchi kuelezea uzembe wa kiutendaji wa kushindwa kusimamia maamuzi ya ndani na inaitaka Wizara ya Nishati na Madini ieleze kwa uwazi na ukweli sababu za kuchelewa kwa mpango huo na hivyo kuongeza kwa kiwango kikubwa muda na kiwango cha mgawo wa umeme unaoendelea hivi sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kwa upande mwingine mgawo wa umeme unaoendelea hivi sasa ni matokeo ya serikali kushindwa kutekeleza kwa wakati mpango wa kuweka mitambo ya MW 100 Ubungo (Dar es salaam) na MW 60 Nyakato (Mwanza) ambayo iliwekwa kwenye mpango wa umeme wa mwaka 2009 ambao ulicheleweshwa na hatimaye wakati wa Bajeti ya mwaka fedha 2010/2011 Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati na Madini wote waliahidi kukamilisha uwekaji wa mitambo hiyo mapema mwaka 2011. Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali ieleze sababu za kuchelewa kutekelezwa kwa mpango huo na hatua za uwajibikaji zilizochukuliwa kutokana na udhaifu huo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Ni aibu kwa taifa kuendelea kutegemea vyanzo ambavyo vilianzishwa na Serikali ya Awamu ya Kwanza iliyoongozwa na Hayati Mwalimu Nyerere na awamu zilizofuata sio tu kushindwa kuongeza kasi ya kuzalisha umeme bali pia kushindwa kukarabati mitambo hiyo na hivyo kuzalisha chini ya kiwango. Taarifa ya Hali ya Uchumi ya mwaka 2010 inaonyesha kuwa vituo vyetu vya umeme vinazalisha 3694.74 jigawati kwa saa yaani MW 421.8 sawa na asilimia 53.5 ya uwezo wa vituo hivyo MW 788.68. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;(Rejea Kielelezo cha Pili). Sababu zinazotolewa za uzalishaji kidogo ni uchakavu wa mitambo na ukame unaoliathiri taifa. Kambi ya Upinzani inaishauri serikali kuacha kuwalaghai wananchi kwa sababu zisizo za msingi kwani ikumbukwe kwamba zipo nchi zilizo katika hali ya jangwa lakini vituo vya kuzalisha umeme vina uwezo wa kuzalisha umeme wa wastani wa zaidi ya asilimia 90. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Mwaka 2010 Serikali ilieleza kupitia taarifa ya hali ya uchumi kwamba mahitaji ya umeme yalifikia MW 791 na Waziri wa Nishati na Madini akatoa matumaini hewa kwa wananchi kupitia bajeti ya mwaka 2010/2011 kuelekea uchaguzi kwa kutaja miradi ambayo jumla yake iliahidi uzalishaji wa MW 2,960; hata hivyo serikali haikutenga fedha za kutosha kufanikisha mipango husika au walau kuweka mazingira wezeshi kwa taasisi zingine na sekta binafsi kwa ujumla kufanikisha utekelezaji hali ambayo imejirudia tena katika bajeti ya mwaka wa fedha 2011/2012. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Kutokana na hali hiyo ya mgawo wa umeme unaoendelea na kasi ndogo ya usambazaji wa umeme vijijini na majibu yaliyotolewa na Serikali kupitia kwa maswali ya papo kwa papo ya Waziri Mkuu tarehe 14 Julai 2011 yameonyesha kwamba serikali halichukulii tatizo la umeme kwa udharura na uzito unaostahili. Hivyo, kambi rasmi ya upinzani inatoa hoja kwa bunge kupitisha azimio la kutangaza kwamba ukosefu wa nishati ni janga la taifa na kupitisha maamuzi ya hatua za haraka ambazo serikali inapaswa kuzichukua kwa uwajibikaji wa pamoja. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bunge lichukue nafasi yake kwa niaba ya wananchi kwa mujibu wa katiba ibara ya 63 (2) (3) ili kuisimamia serikali kuondoa janga hili la taifa; maazimio ya bunge yatawezesha taarifa za mara kwa mara kutolewa bungeni kuhusu hatua za utekelezaji na adhabu kutolewa kwa mawaziri wa serikali watakaozembea katika kuchukua hatua za haraka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Mpango wa Taifa wa miaka mitano (2011/2012-2015/2016) umelenga kuongeza uzalishaji wa umeme mpaka kufikia MW 2780 kwa kuongeza MW 1788 kwa mujibu wa miradi iliyotajwa kwenye mpango. Lengo hili ni dogo ukilinganisha na rasilimali ambazo zipo katika taifa letu; hivyo Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kufanya mapitio ya mpango huo na kuongeza miradi mingine mikubwa ukiwemo wa Stiggler Gorge ambao una uwezo wa kuzalisha MW 2100 na kuingiza pia makadirio ya ujumla ya MW zinazotokana na miradi midogo midogo itakayoanzishwa katika maeneo mbalimbali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Kambi Rasmi ya Upinzani imebaini kwamba hata lengo hili dogo la MW 1788, ambalo ni sawa na ongezeko la wastani wa MW 360 kila mwaka; halijaanza kutekelezwa kwa ukamilifu. Hii ni kwa sababu katika mwaka wa fedha 2011/2012 serikali imepanga katika bajeti kuongeza MW 160 ambazo kimsingi zilipaswa ziwe zimekamilika mwaka wa fedha 2010/2011. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kueleza mradi mwingine wa MW 200 ambao unapaswa kukamilika katika mwaka huu wa fedha na rasilimali zilizotengwa kwa ajili ya kufanikisha mradi husika. Kambi Rasmi ya Upinzani inasisitiza kwamba mradi wa Kiwira wa MW 200 awamu ya kwanza upewe kipaumbele maalum katika mwaka huu wa fedha ili kuweza kuziba pengo lililopo. Kambi rasmi ya Upinzani inataka kauli ya serikali kuhusu pendekezo letu la kutenga fedha za ndani kutekeleza mradi wa njia za kusafirisha umeme huo kutoka Kiwira mpaka Mbeya katika mwaka wa fedha 2011/2012 . &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza miradi iliyosalia kwa wakati Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Wizara ya Nishati na Madini kueleza mazingira wezeshi ambayo yanakusudiwa kuandaliwa ili miradi ifuatayo iweze kupata rasilimali kwa wakati na makubaliano kukamilishwa mapema: Dar es salaam-Kinyerezi (Gesi Asilia MW 240), Iringa-Mchuchuma na Ngaka (Makaa ya Mawe-300), Mtwara – Somanga Fungu (Gesi Asilia-MW 300) na Morogoro/Iringa- Ruhudji (Maji- MW 358). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Uchambuzi wa Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu Taarifa ya Utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2010/2012 na makadirio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2011/2012 unaonyesha uwezo mdogo na kasi ndogo ya kufikisha umeme vijijini. Mathalani katika bajeti yake ya mwaka huu Wizara imetenga Sh Bilioni 1.1 kupeleka umeme katika vijijini 4 tu ( Kijiji cha Magindi, kijiji cha Mbwewe, Kijiji cha Mgwashi, kijiji cha Kiwanga) kati ya vijiji 12,176 vilivyosajiliwa kutokana na taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hali hiyo itachukua karibu miaka elfu mia mbili sawa na karne mbili kufikisha umeme katika vijiji vyote; kama ambavyo tumetumia miaka 50 ya uhuru kuunganisha umeme kwa 14% tu kwenye gridi ya taifa. Kasi ndogo ya kusambaza umeme inadhihirishwa na idadi kubwa ya maombi ya wananchi wanaotaka kufungiwa umeme huku Shirika la Umeme (TANESCO) likiwajibu kuwa halina uwezo kwa sasa mpaka lipate miradi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2010/2011 Serikali iliahidi kutekeleza Mradi wa MCC (Millenium Challenge Cooperation) wa kuvipatia umeme vijiji 289 katika mikoa 6. Mwanza (42), Tanga (129), Dodoma (45), Mbeya (18), Iringa (17) na Morogoro (38). Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kutoa taarifa ya kina ya utekelezaji kutokana na malalamiko ya kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi kwa kulinganisha na kiwango cha fedha kilichotumika. Aidha tathmini ifanyike kuhusu utekelezaji wa mradi husika ili kuwezesha umeme kuweza kufika vijijini kwa wakati. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani tulieleza kwenye bajeti mbadala 2011/2012 kwamba Kipaumbele chetu cha muhimu ni Kuwezesha Ukuaji wa Sekta za Uzalishaji na hasa ukuaji wa uchumi vijijini ili kuboresha kilimo, kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya kuongeza thamani za bidhaa, kuongeza ajira na kupunguza umasikini kwa wananchi walio wengi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mkakati huu ambao utapunguza vijana wengi kukimbilia mijini na kuliokoa Tanzania kuwa taifa la wachuuzi unahitaji uwekezaji wa kutosha kwenye miundombinu ya vijijini ikiwemo ya umeme. Mheshimiwa Spika; Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kutenga bilioni 150 kwa ajili ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya kwa ajili ya uzalishaji wa umeme toka vyanzo vidogo vya maeneo mbalimbali pamoja na usambazaji wa umeme katika maeneo ya vijijini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chanzo cha nyongeza ikiwa ni fedha ambazo zinaendelea kutozwa hivi sasa kutokana na ongezeko katika kodi ya mafuta ya taa ambayo ikiendelea kwa mwaka mzima serikali kukusanya kiasi kisichopungua bilioni 70. Mheshimiwa Spika; tunatambua kwamba utekelezaji wa mradi kabambe wa kusambaza umeme katika mikoa 16 unasuasua kutokana na serikali kutokupeleka fedha kwa REA kwa mujibu wa bajeti zinazopitishwa na serikali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mpaka mwezi Mei mwaka 2011 serikali ilikuwa imepeleka bilioni 23.3 tu kwa ajili ya malipo ya wakandarasi wakati ambapo fedha zinazohitajika ni shilingi bilioni 78.3. Kwa mwaka wa fedha 2008/2009 fedha ambazo hazikutolewa na hazina ni bilioni 25.3 huku mwaka wa fedha 2010/2011 mpaka mwezi Mei zikiwa zimetolewa bilioni 13.6 tu ambazo ni sawa na chini ya robo (23%) ya bajeti iliyopangwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha kambi ya upinzani inashauri mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG) afanye ukaguzi wa ufanisi wa miradi inayoendelea kutekelezwa ili hatua stahili ziweze kuchukuliwa mapema kuwezesha wananchi wa vijijini kupata umeme. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kambi rasmi ya upinzani hairidhiki na kasi ya kuboresha utendaji wa Shirika la Umeme (TANESCO) na tunataka serikali ieleze hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mpango maalum wa kurekebisha hali ya kifedha ya shirika (2006-2010). Kambi rasmi ya upinzani inaitaka serikali iwaeleze watanzania ni lini mapitio ya mikataba ambayo inaipa mzigo mkubwa wa kifedha TANESCO na kusababisha bei ya umeme kupanda itafanyiwa mapitio. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, serikali imekuwa ikiidhamini TANESCO kupata mikopo ambayo kwa sehemu kubwa imekuwa ikitumika kwenye kukodi mitambo ya dharura; hivyo kambi rasmi ya upinzani inashauri kuwe na udhibiti wa kutosha ili mikopo hiyo isigeuke kuwa mzigo kwa taifa baadaye. Kwa upande mwingine, TANESCO imekuwa ikizidai wizara, idara na taasisi za serikali Ankara za umeme zinazofikia bilioni 76; hivyo serikali inapaswa ionyeshe mfano kwa kufanya malipo kwa wakati. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Pia pamekuwepo malalamiko mbalimbali kuhusu mazingira ya kupitishwa kwa zabuni za ununuzi wa nguzo, transforma na nyaya za umeme kwa kiwango kikubwa toka nje ya nchi huku viwanda vya ndani mathalani TANALEC ABB, East African Cables (hususani kampuni tanzu ya Tanzania Cables) na vingine vikididimia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii imesababisha pia kukwama kwa utekelezwaji wa miradi mbalimbali ya kusambaza umeme kutokana kwa kile kinachoelezwa kuwa ni vifaa kutokupatikana kwa wakati toka nje ya nchi. Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali kuandaa mkakati wa kupunguza gharama za manunuzi na pia kupunguza kiwango cha uagizaji wa nguzo na vifaa vingine kutoka nje ili kutumia rasilimali za ndani ili kuchangia katika kukuza uzalishaji na uchumi wetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kambi rasmi ya upinzani hairidhiki na hatua ambazo serikali inachukua katika kupunguza gharama wanazotozwa wananchi za kuunganishiwa huduma ya umeme suala ambalo linapunguza kasi ya uunganishwaji wa umeme. Tumepokea malalamiko toka kwa wananchi wanaotakiwa na TANESCO kulipia nguzo na gharama nyingine za kuunganishwa umeme kwa kiasi kinachozidi milioni moja ambacho ni vigumu kwa wananchi wa kawaida kumudu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, serikali itoe kauli ya hatua inazopanga kuchukua ikiwemo za kubadili mfumo wa Ankara ili kuruhusu kuingiza kwa mteja gharama hizo kidogo kidogo katika kipindi hiki cha mpito. Aidha, TANESCO inahimizwa kutangaza kwa umma Kanuni za Sheria ya Umeme zilizotolewa kwenye gazeti la Serikali tarehe 4 Februari 2011 (GN 63) ambazo kifungu cha nne kinaeleza namna mteja atakavyofidiwa na kampuni ya usambazaji pale ambapo mteja anajigharamia mwenyewe kuvutiwa umeme ili fursa hiyo iweze kutumika ipasavyo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kutokana na kasi ndogo ya usambazaji wa umeme, pamoja na kuondoa kodi katika vifaa vya umeme wa jua; serikali ieleze hatua ilizochukua katika kuweka mazingira wezeshi kwa vifaa vya umeme wa dharura kuweza kupatikana kwa urahisi mathalani vifaa vya kuhifadhia umeme (invetors). Aidha, serikali iongeze kasi ya kutekeleza miradi ya kuhamasisha nishati mbadala hususani vijijini kwa kufanya marekebisho ya msingi katika sheria ya fedha na sheria ya umeme. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Gesi Asilia Mheshimiwa Spika, Nchi yetu imejaliwa utajiri wa gesi asilia katikati ya lindi la umasikini wa wananchi. Gesi asili iligunduliwa nchini mwaka 1974, ikaanza kutumika kuzalisha umeme viwandani 2004 mpaka sasa inatumika kuzalisha MW 440 sawa na 60% ya matumizi yote ya umeme kila siku na inatumiwa na takribani viwanda 25 kwa uzalishaji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mujibu wa tafiti tuna zaidi ya 12 tr cf za gesi na uko uwezekano wa kugundua zaidi kutokana na utafutaji unaoendelea. Taifa letu lina fursa ya kuwa nchi kiongozi katika gesi Afrika na kushindana kimataifa ikiwa tutaweka mstari wa mbele upeo, umakini na uadilifu katika sekta ya nishati kuepusha laana ya rasilimali. Hata hivyo kwa mwelekeo wa ufisadi na udhaifu wa kiuongozi unaoendelea hivi sasa rasilimali hii inaweza kuwa chanzo cha migogoro na kuhatarisha pia usalama wa nchi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba mradi wa Bomba la Gesi kutoka Mtwara kupitia Dar es salaam mpaka Tanga uwekwe kipaumbele katika Bajeti ya nyongeza ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2011/2012. Hivyo, serikali itenge bilioni 200 kwa ajili ya kuchangia kwenye mradi wa Bomba la Gesi na kuchangia katika ujenzi wa Kiwanda cha Gesi kama sehemu ya mkakati wa kushughulikia upungufu wa nishati kama janga la taifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha usiri katika majadiliano ya mradi wa bomba la gesi ni muhimu ukaondolewa kwa wakati nyaraka rasmi za kiserikali zinaonyesha majadiliano yanayoendelea kati ya Tanzania na China kuhusu mradi husika; kambi rasmi ya upinzani inayo mawasiliano baina ya watendaji wakuu wa kampuni ya Orca Exploration Limited na baadhi ya maofisa wa ikulu kutaka kupatiwa mradi husika; wakati kampuni yao tanzu ya Pan African Energy Tanzania (PAT) imekuwa ikilalamikiwa kuhusu mradi mwingine wa gesi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kambi ya rasmi ya upinzani inasisitiza mradi kwa kujenga kiwanda cha kujaza gesi kwenye mitungi (LPG) na mradi wa usambazaji wa gesi Dar es salaam pamoja na mradi matumizi ya gesi kwenye magari inayotekelezwa na Shirika la Petroli Nchini (TPDC) inapaswa kuongezewa rasilimali katika mwaka wa fedha 2011/2012. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua hii itapunguza pia matumizi ya umeme katika maeneo yenye kuweza kutumia gesi na kubakiza umeme mwingine utakaoweza kutumika kwenye maeneo ikiwemo ya viwandani yenye upungufu wa nishati mbadala. Uamuzi huu utawezesha pia kupunguza gharama za uzalishaji na za maisha zinazotokana na kupanda kwa bei ya mafuta ambayo pamoja na mizigo ya kodi na gharama zinazotokana na mfumo mbovu wa uingizaji inasababishwa pia na kupanda kwa bei katika soko la dunia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha ili kuongeza mapato kwa serikali na TPDC kambi rasmi ya upinzani inataka mrabaha wa asilimia 12 kwenye gesi uanze kutozwa kwa mujibu wa sheria na isitishe mara moja utaratibu wa baadhi kuachiwa kutokulipa malipo husika kwa mujibu wa wa sheria. Mapitio ya kitabu cha mapato yameonyesha kwamba wakati kwenye kifungu cha 2001 cha madini kuna mrabaha hakuna kasma hiyo kwenye kifungu 3001 kinachohusika na gesi na mafuta. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; ili kujiandaa kitaaalumu kama taifa kwa mipango kabambe ya gesi, kambi rasmi ya upinzani itekeleze mkakati wa kuwaambatanisha wataalamu wazawa na makampuni makubwa yenye uzoefu wa sekta husika. Aidha, kambi rasmi ya upinzani inataka Wizara ya Nishati na Madini iharakishe kukamilisha mtaala wa uhandisi wa gesi na mafuta ili fani hizo ziweze kutolewa kwenye Chuo Cha Madini Dodoma. Aidha, kwa kuwa serikali wakati wa kuhitimisha mjadala wa mpango wa mpango wa taifa wa miaka mitano; serikali ilikubali pendekezo la kuanzisha Chuo Kikuu cha Mtwara. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi rasmi ya upinzani inaitaka Wizara ya Nishati na Madini kueleza maandalizi ambayo inakusudia kuyafanya kwa kushirikiana na mamlaka zingine husika ili kuwezesha uanzishwaji wa chuo kikuu hicho muhimu ambacho kitatoa mchango mkubwa kwa taifa katika masuala ya gesi na bidhaa zitokanazo na gesi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kwa muda mrefu sasa taifa letu limekuwa likitegemea mradi mkubwa wa Songo Songo kwa shughuli za uendelezaji, uzalishaji, usafishaji na usafirishaji ambao uko chini ya Kampuni ya Songas. Hata hivyo, kampuni ya Songos imeiajiri Kampuni ya PanAfrican Energy Tanzania (PAT), ambayo ni mshirika wa TPDC katika uzalishaji, usambazaji na ugavi wa gesi asili. PAT imepewa pia Mradi wa Kusambaza Gesi Asili (Ring Main and CNG Project) jijini Dar es Salaam. Taarifa mbalimbali zinaonyesha kuwa Kampuni ya PAT ililipwa kiasi kikubwa cha fedha zaidi gharama ilizoingia wakati wa kujenga mtandao wa usambazaji wa gesi asili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa spika, Aidha upo mwenendo usioridhisha wa kampuni hii ambao unapelekea upungufu wa gesi unaosababisha mgawo wa umeme, mfumo wa bei kubwa unaoongeza mzigo wa watumiaji na pia upotevu wa mapato ya serikali. Hivi karibuni kampuni hii ilipewa na TPDC mabilioni ya fedha kinyume cha taratibu mpaka sasa serikali inadai; ni muhimu serikali ikawaeleza watanzania ni viongozi gani walinufaika na malipo hayo na kiasi gani mpaka sasa hakijarejeswa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na uzito wa tuhuma na usiri katika mikataba; Kambi Rasmi ya Upinzani inashauri kuundwe kamati teule ya bunge itayofanya mapitio ya mikataba, sheria, kanuni pamoja na tuhuma za upungufu wa mgawo wa mapato na ufisadi kutokana na mauzo ya gesi kuanzia mwaka 2004 mpaka 2010. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mafuta Mheshimiwa Spika; Taarifa za Hali ya Uchumi nchini zinaeleza kuwa mfumuko wa bei unaombatana na kupanda kwa gharama za maisha unazidi kuongezeka katika taifa letu kutoka asilimia 4.2% Oktoba mpaka 6.4% Aprili, na kama utaendelea kupanda hivi kwa ari, nguvu na kasi zaidi kwa miezi michache ijayo utakuwa zaidi ya tarakimu moja. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi rasmi ya upinzani inatambua kwamba ukiondoa kupanda kwa bei ya chakula kunakutokana na kushuka kwa uzalishaji, chanzo kikuu cha hali hii ni ongezeko la bei ya nishati hususani mafuta, umeme na gesi hali ambayo isipodhibitiwa kwa mikakati makini ni tishio kwa utulivu wa taifa kiuchumi, kijamii na kisiasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, tarehe 15 Juni 2011 kambi rasmi ya upinzani iliishukuru serikali kwa kutoa kauli ya kukubali matakwa ya umma na pendekezo la kambi rasmi ya upinzani la kupunguza kodi na tozo kwenye bidhaa za mafuta ili kupunguza bei na mzigo mkubwa wa gharama za wananchi na kuonyesha mashaka kuhusu kiwango ambacho kitaondolewa na serikali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Mashaka hayo yalidhihirisha kwenye kupitishwa kwa muswada wa sheria ya fedha tarehe 22 Juni 2011 ambapo serikali haikuonyesha kivitendo dhamira ya kupunguza kodi kwenye mafuta kwa kiwango cha kuwapunguzia ugumu wa maisha badala yake ikajikita kwenye kupunguza tatizo la uchakachuaji pekee ambalo limedumu kwa sababu ya serikali kushindwa kusimamia utawala wa sheria. Ushahidi ni kwamba katika marekebisho ya kodi; serikali haikupunguza hata senti moja katika mzigo wa kodi kwenye petrol. Aidha, serikali ilipunguza kodi ya dizeli kwa shilingi 99 tu huku ikiongeza kodi ya mafuta ya taa kwa shilingi 358. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; kambi rasmi ya upinzani ilikuwa na dhamira ya kuwianisha bei ya mafuta ya taa na dizeli ili kupunguza tatizo la uchakachuaji; lakini si kwa kuongeza kwa kiwango kikubwa kodi ya mafuta kama ilivyofanya serikali. Matokeo ya uamuzi huu ni kwamba wakati bei ya petroli na dizeli zikibaki bila kupungua au zikipanda katika maeneo mengi ya nchi; bei ya mafuta ya taa imepanda kwa ari, nguvu na kasi zaidi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuleta marekebisho ya sheria ya fedha ili kurekebisha hali hiyo na kueleza mkakati wa kweli wa kupunguza gharama za maisha kwa wananchi. Aidha, serikali ijieleze bungeni kutokana na udhaifu ulionyeswa na taasisi zake ikiwemo Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) katika kusimamia bei elekezi na kupunguza bei za mafuta ambazo serikali iliahidi bungeni kuwa zingepungua kuanzia Julai 2011. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha kama sehemu ya mchakato wa kupunguza gharama za mafuta kufuatilia mabadiliko ya kodi, tozo na mfumo wa uingizaji wa mafuta serikali ifanye mapitio ya mkataba baina ya EWURA na kampuni ya Global Fluids International (T) Ltd kuhusu ufanisi na gharama za kuweka vinasaba na kuleta vifaa maalum vya kupima ubora (XRF). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, ukiondoa kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na ukubwa wa kodi zinazotozwa na serikali bei ya mafuta inakuwa juu kutokana na mfumo mzima wa uagizaji, usafirishaji, uingizaji na usambazaji. Mfumo uliopo sasa unanufaisha makampuni makubwa mengi yakiwa ya kigeni na wafanyabiashara wachache wa ndani pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali wasiokuwa waadilifu kwa kulinyonya taifa na kuongeza gharama za maisha kwa watanzania walio wengi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Hali hii ndiyo iliyokwamisha kwa muda mrefu kuanza kwa mfumo wa uagizaji na uingizaji wa mafuta ya pamoja (Bulk Procurement System) ili kupunguza gharama; suala ambalo Julai 2010 serikali ilisema liko katika hatua za mwisho na Julai 2011 mwaka mmoja baadaye bado serikali bado inatumia lugha ile ile. Aidha Serikali iwajibike kwa kutoanzisha hifadhi ya mafuta mpaka hivi sasa wakati mwaka 2010 ilitoa kauli ya kufufua kampuni ya taifa ya mafuta (COPEC); kwa ujumla kupanda kwa gharama ya mafuta kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na udhaifu wa serikali wa kutochukua hatua zinazostahili kwa wakati. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama imeshindwa kufufua kampuni ya taifa ya mafuta itekeleze pendekezo lililotolewa na kambi rasmi ya upinzani la kuchukua hisa 100% katika kampuni ya BP ambayo serikali ina hisa na kuigeuza kuwa chombo cha kutimiza azma husika. Aidha Wizara ya Nishati na Madini ieleze hatua mahususi za kulinda maslahi ya nchi katika kampuni ya TIPER ambayo serikali ina hisa 50% katika hatua za uingizaji na uhifadhi wa mafuta. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Ili kuongeza tija na ufanisi wa TPDC, kambi rasmi ya upinzani inaitaka Serikali itoe maelezo kuhusu hatua iliyofikiwa katika kutekeleza ushauri wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma wa kulifanyia marekebisho shirika hilo ili kuwa na mamlaka itakayohusika na kutoa vibali kwenye leseni na kusimamia uchimbaji wa mafuta na gesi na kampuni itakayoshiriki katika biashara ya mafuta na gesi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upizani Bungeni inaendelea kusikitishwa na uamuzi uliofanywa wa tarehe 22 Juni 2011 wa kuondoa msamaha wa kodi ya mafuta kwa kampuni za utafutaji ya mafuta na Gesi. Uzoefu kutokana na misamaha ambayo imekuwa ikitolewa kwa makampuni ya madini unadhihirisha kwamba makampuni mengi yanatumia mwanya huo kuleta mafuta yasiyo na kodi na kuyaingiza kwenye soko la ndani la reja reja. Mathalani takwimimu zimedhihirisha kuwa kupitia misamaha iliyotolewa kwa makampuni matano tu ya madini ni karibu robo ya mafuta yote ya Dizeli yaliyoingia nchini na kampuni hizi zililipa dola laki mbili tu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Misamaha hii haina maslahi ya taifa na ni mianya mingine ya uhujumu uchumi; hivyo Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kufikiria upya uamuzi huo na kuleta marekebisho ya sheria ya fedha ili kuufuta msamaha hiyo kwa kuwa kampuni za utafutaji mafuta na gesi zinayofursa kwa mujibu wa mikataba (PSA) kurejeshewa gharama zao mara baada ya mafuta kupatikana. Aidha, uamuzi huu uhusishe pia kampuni za madini bila kujali mikataba (MDA) kwa kuwa imethibitika kampuni hizi zote hutengeneza faida nono bila kulipa kodi inavyostahili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Madini &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa sekta ya madini mwaka 2010/2011 kumekuwa na ongezeko la uzalishaji huku mauzo ya nje ya madini yakiwa yameongezeka; dhahabu pekee ikifikia thamani ya dola 1,516.6. Hata hivyo mchango kwenye mauzo ya nje umeendelea kuwa ule ule wa asilimia 3.3 wa mwaka 2009/2010 na mchango kwenye pato la taifa ni asilimia 7.1 tu licha ya maelezo matamu ya serikali kuwa mapato yameongezeka kutokana na kutungwa kwa sheria mpya ya madini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Nyaraka ambazo kambi rasmi ya upinzani inazo toka vyanzo vya kiserikali yanaonyesha kwamba sehemu kubwa ya makampuni yenye mikataba yamekataa kukubaliana na serikali. Hatua za haraka zinahitajika kulinusuru taifa na hali hii ambapo utajiri wetu unaendelea kuondoka huku watanzania wakiendelea kuwa masikini; hatua ambazo zitahusisha mwingiliano baina ya sekta ya madini na sekta nyingine. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Ukirejea kitabu cha kwanza cha mapato ya serikali kwa mwaka 2011/2012, nchi yetu itakusanya bilioni 99.5 tu; hii ni aibu ya taifa ukilinganisha na mauzo ambayo sekta hii inauza nje hasa kwa kuzingatia sehemu kubwa ya kampuni hizo hazilipi kodi inavyostahili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi ya Rasmi ya Upinzani inaishauri Wizara ya Nishati na Madini kuwasiliana na Wizara ya Fedha ili kuboresha mfumo wa utoaji wa taarifa za malipo ya kodi kwa kampuni za madini ili malipo ya kila kampuni na mchangunuo wake yafahamike kwa umma badala ya mfumo wa sasa ambapo hurundikwa pamoja katika takwimu za idara ya walipa kodi wakubwa. Aidha, Wakala wa Madini (TMAA) ufanye ufuatiliaji maalum wa madini ya Tanzanite; ambapo bei katika soko iko kati ya dola 250-400 na zaidi kwa kwa karati wakati viwango vinavyotumiwa na mamlaka husika kukadirani vidogo hali inayosababisha upotevu wa mapato. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Ili kuongeza kiwango cha mapato ikiwemo ya kodi kutokana na uchimbaji wa madini; kambi rasmi ya upinzani inaitaka serikali kutekeleza mikakati ya kupenya kuta za umiliki na mitaji (capital and ownership structures) zilizojengwa kwa muda mrefu na makampuni ya kimataifa kwa kutumia mianya ya udhaifu wa kisheria na ushawishi wa kifisadi uliosababisha mikataba mibovu katika sekta ya madini nchini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kueleza bayana hatua ambazo imechukua kufuatia ripoti ya tume/kamati mbalimbali ambazo ziliundwa na serikali kwa nyakati mbalimbali kwa kutumia fedha nyingi za walipa kodi lakini mapendekezo yake bado hayajatekelezwa kwa ukamilifu wake. Mathalani ripoti za karibuni za Kamati ya Masha na ile ya Bomani (2008) zilieleza bayana namna ambavyo makampuni makubwa ya madini yamekuwa yakitumia sehemu kubwa ya uwekazaji wao kama mkopo (debt financing). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani, inatambua kwamba makampuni hayo yamekuwa yakitumia mianya hiyo ya kisheria na kimikataba kuwezesha wamiliki na wanahisa kupata faida mapema kuliko kuweka mtaji kwa kuwa riba ya mikopo huondolewa katika kukokotoa kodi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani inataka serikali iwaeleze watanzania ni trilioni ngapi za mapato tumezikosa kati ya mwaka 1995 mpaka 2010 katika kipindi cha miaka 15 ya kuachia mianya ya upotevu wa mapato kwa kuruhusu asilimia kubwa ya mikopo kuwa mitaji. Aidha, ni hatua gani zimechukuliwa kwa waliohusika kuliingiza taifa katika mikataba mibovu iliyoruhusu makampuni hayo kujitangazia hasara kila mwaka huku yakipata faida kubwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; ukipitia kitabu cha mapato serikali imeweka malengo madogo ya mapato kwa upande wa Wizara ya Nishati na Madini hali ambayo inadhihirisha kwamba inakusudia kuendelea kutoza mrabaha wa asilimia 3; tofauti na mapendekezo ya Kamati ya Bomani ya asilimia 5 na Sheria ya Madini ya mwaka 2010 ambayo inaitaka serikali kutoza asilimia 4. Kwa upande mwingine bado serikali inaachia mianya kwa makampuni ya madini kutotoa mrabaha baada ya kuondoa gharama za usafiri (net back value) badala ya kutoa kwenye mahesabu ya ujumla (gross); Hatua hizi zikichukuliwa zinaweza kuongeza mapato ya serikali kufikia zaidi ya bilioni 200. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, ili kudhibiti hali hii ya ukwepaji kodi na kuongeza mapato ya serikali katika mwaka wa fedha 2011/2012 kambi Rasmi ya Upinzaniinaitaka Wizara ya Nishati na Madini ieleze hatua mahususi ambazo itazichukua kutekeleza mapendekezo yafuatayo yaliyotolewa kwenye bajeti mbadala: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutunga Sheria ya kuhakikisha kwamba mikopo kwenye makampuni ya uwekezaji wa madini katika mahesabu ya kodi isizidi 70% ya mtaji; Kutunga Sheria kuhakikisha kwamba riba ya mikopo kwenye makampuni yanayohusiana haitaondolewa kwenye mahesabu ya kodi; Kufanya marekebisho ya sheria kuhakikisha kwamba kodi ya mtaji (capital gains) inatozwa katika mauziano ya makampuni yote ya madini ambayo mali zake au uwekezaji wake uko nchini hata kama mauziano hayo yamefanyika nje ya nchi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, kutokana na kuendelea kuporomoka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania; kambi rasmi ya upinzani inaishauri Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Fedha katika kuweka mikakati na usimamizi wa kuhusisha sekta ya madini katika kuimarisha fedha yetu. Kwa kuwa mauzo ya madini yetu yanaongezeka huku shilingi ikishuka; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani, inaitaka Wizara ieleze hatua ilizochukua za kushirikiana na Wizara ya Fedha katika kuwezesha Benki kuu kutunza sehemu ya hifadhi yetu ya fedha za kigeni katika mfumo wa madini ya dhahabu. Wizara ya Nishati na Madini ishirikiane na benki kuu kuweka mfumo wa kununua dhahabu kwa wachimbaji wadogo na pia kutoza sehemu ya mrabaha wa dhahabu kwa ajili ya uhifadhi kama ilivyoshauriwa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma. Taratibu hizi ziende sambamba na kusimamia mfumo wa kuhakikisha kwamba makampuni hayo yanatunza sehemu kubwa ya fedha za nje (walau 60%) kwenye benki za ndani ili kusaidia kudhibiti kuporomoka kwa shilingi ya Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; Sheria ya Madini ya mwaka 2010 imeipa majukumu muhimu STAMICO ya kuwa mwakilishi na msimamizi wa rasilimali za madini nchini kwa niaba ya serikali. Kambi Rasmi ya Upinzani hairidhishwi na kasi ya kuliwezesha shirika hili muhimu kutekeleza wajibu wake. Mwaka mmoja umepita bila ya serikali kukamilisha mchakato wa marekebisho ya STAMICO kuweza kukidhi haja. Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali ieleze ni kwa nini marekebisho ya sheria ndogo iliyoanzisha STAMICO (Establishment order) katika mwaka wa fedha 2010/2011 kama ilivyoahidiwa na kurejesha fedha za nyumba nne za STAMICO ambazo ziliuzwa na wakala wa majengo Tanzania (TBA)? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Mkakati wa Msingi katika sekta ya madini ni kuhakikisha watanzania wanaumiliki katika miradi mikubwa ya madini ama kupitia hisa za makampuni hayo kuwekwa katika soko la ndani (DSE) au kwa kampuni ya umma kushikilia sehemu kubwa ya uwekezaji hasa katika madini nyeti ikiwemo urani. Hivyo, ni lazima mtaji wa STAMICO uongezwe haraka kwa kurekebisha sheria na kanuni lakini pia kuongeza mtaji wa shirika. Ukiondoa albaki ya bilioni 5.25 bilioni Serikali ieleze hatua ambazo inakusudia kuongeza mtaji wa STAMICO katika mwaka wa fedha 2011/2012. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; tunatambua kwamba Wakala Jiolojia (GST) anaendelea na utekelaji wa mradi wa kutambua maeneo ya madini. Kambi ya upinzani inataka mradi huu uende sambamba na kufanya tathmini ya kina (mineral appraisal) ya madini yetu na kupendekeza mabadiliko ya kisheria na kimikataba ambayo yatawezesha utajiri wa madini yetu kutumika kama mtaji na dhamana katika hatua ya kuhakikisha taifa letu linanufaika na rasilimali zake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia; ili kuongeza uwezo wa GST kutimiza wajibu wake malipo yote yanayopaswa kutolewa kwa mujibu wa sheria ndogo iliyounda wakala husika (Establishment Order) yafanyike kwa mujibu wa taratibu kuanzia mwaka wa fedha 2011/2012. Aidha; ramani na ripoti zinazotokana na utafiti na uchunguzi huo zitolewe kwa uangalifu ili kuhakikisha maslahi ya taifa yanalindwa katika hatua zote. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; tunasikitishwa na maamuzi ya serikali ya kuendelea na hatua za mbele katika utafutaji na uchimbaji wa madini ya urani bila kukamilisha maandalizi ya kisera, kisheria, kikanuni na kitaasisi yanayohitajika suala ambalo litaachia mianya ya upotevu wa mapato kwa taifa kama ilivyokuwa kwenye madini mengine na pia itahatarisha usalama. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi ya Rasmi ya Upinzani inataka maelezo ya kina kuhusu mauzo na mabadilishano ya umiliki yaliyofanyika baina ya kampuni ya Australia (Mantra Resources) na Kampuni ya Urusi ya ARMZ Uranium Holding kampuni tanzu ya Rosato. Mauzo hayo ambayo yanaelezwa kimataifa kuwa yamefanyika kwa bei ya dola 1.16 bilioni ambayo ni zaidi ya shilingi trilioni 2. Mauzo hayo yamehusisha kuhamishiana umiliki wa maeneo ya Tanzania Mkuju River (Namtumbo) na Bahi Kaskazini (Dodoma). &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Iwapo tungepata asilimia 30 tu ya mauzo hayo kama kodi taifa letu lingepata 600 bilioni ambayo ni fedha nyingi kuliko bajeti nzima ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka. Izingatiwe kwamba eneo husika lina madini ya urani takribani paundi 108 milioni sawa na asilimia 77 ya uchimbaji wote wa urani kwa mwaka jana. Hii ni aibu kwa taifa linalokwenda nje kuomba huku ikiachia bwerere fursa za rasilimali za ndani na kufikia hatua hata ya mbuga za wanyama kuvamiwa kwa uchimbaji usio kuwa na tija ya moja kwa moja kwa watanzania walio wengi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kusimamisha kwa muda taratibu zinazoendelea za uchimbaji wa urani mpaka maandalizi ya msingi yafanyike yatakayohakikisha umiliki, manufaa na usalama. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika; pamoja na ahadi ya serikali kumaliza migogoro katika sekta ya madini baina ya wachimbaji wakubwa na wachimbaji wadogo pamoja na kuepusha migogoro ya leseni mathalani mgogoro wa wachimbaji wadogo eneo la Winza wilaya ya Mpwapwa ambao serikali iliahidi bungeni tarehe 9 Julai 2010 kuumaliza. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi Rasmi ya Upinzani inataka kauli ya serikali kuhusu mgogoro huo kwa kuwa tayari wachimbaji wadogo wameanza kuhamishwa kwa nguvu toka maeneo yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, pia migogoro ya wafanyakazi katika makampuni ya madini. Wizara ya Nishati na Madini ilieleze taifa hatua ilizochukua kushirikiana na Wizara nyingine husika kutatua malalamiko ya wafanyakazi wa Tanzanite kuhusu ongezeko la wafanyakazi wageni; Wafanyakazi walioachishwa katika kampuni ya Bulyankulu; kampuni ya Caspiani katika mgodi wa Mwadui Shinyanga ambayo yapo Wizarani kwa muda mrefu bila hatua za msingi kuchukuliwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Mnamo tarehe 25 Mei 1946 kampuni iitwayo Alamasi Limited ilipewa leseni ya kuchimba madini ya almasi kaskazini ya kijiji cha Luhumbo katika eneo la Mwadui, Wilaya ya Shinyanga. Leseni hiyo ijulikanayo kama Hati ya Uchimbaji (Mining Lease) Na. 224 ilitolewa chini ya Sheria ya Madini ya mwaka 1929 iliyokuwa inatumika wakati huo na ilihusu eneo la ukubwa wa ekari 3007. Ili kuchimba almasi katika eneo hilo, Alamasi Ltd. ilipewa Hati Milki ya ardhi Na. 5954. Muda wa leseni hiyo ulikuwa miaka ishirini na moja kuanzia tarehe 14 Juni 1944 na ulitakiwa kwisha tarehe 31 Mei 1965. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa leseni hiyo, Alamasi Limited ilitakiwa kulipa kodi ya ardhi ya senti hamsini kwa ekari moja kwa nusu ya mwaka 1944 iliyokuwa imebakia, na baadae kodi ilitakiwa kupanda hadi shilingi moja kwa ekari kwa mwaka 1945; shilingi moja na thumni kwa mwaka 1946; shilingi mbili kwa mwaka 1947 na baada ya hapo kodi ilitakiwa kuwa shilingi mbili na thumni kwa ekari kwa kila mwaka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Ilipofika Januari Mosi 1963, Alamasi Ltd. ilihamisha umiliki wa leseni hiyo kwa muda uliobakia kwa kampuni mpya iitwayo New Alamasi (1963) Limited. Uhamisho wa milki hiyo ulithibitishwa na Msajili wa Hati Msaidizi mnamo tarehe 23 Mei 1963 baada ya taratibu zote za kisheria za uhamisho kukamilika. Kwa mujibu wa taarifa ya Msajili wa Hati Mkuu Msaidizi Mary J. Mziray iliyotolewa tarehe 30 Januari 2006, milki ya leseni ya New Alamasi (1963) Ltd. ilikwisha muda wake tarehe 31 Mei 1965, na eneo la leseni hiyo lilirudishwa katika milki ya Rais. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa sababu hiyo, kwa mujibu wa barua ya Kamishna wa Madini ya tarehe 27 Machi 2006, Leseni Na. 224 Hati Milki Na. 5954 ilifutwa katika rejesta ya leseni za madini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Licha ya muda wa leseni Na. 224 kwisha na leseni yenyewe kufutwa katika rejesta ya leseni za madini, New Alamasi (1963) Ltd. iliendelea kuchimba madini ya almasi katika eneo hilo na kuyauza nchi za nje bila ya kuwa na leseni yoyote ile kwa miaka thelathini na tano! Aidha, kwa kipindi chote hicho, hakuna takwimu zozote zinazoonyesha kiasi cha almasi iliyochimbwa kinyume cha sheria na wala fedha zilizopatikana kutokana na mauzo ya almasi hiyo na zilikoenda fedha hizo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, tunaitaka Serikali itoe kauli rasmi juu ya shughuli za New Alamasi Ltd., uhalali wa shughuli zake za uchimbaji almasi katika eneo la Luhumbo, kiasi cha almasi iliyochimbwa kwa kipindi chote tokea tarehe 1 Juni 1965 hadi tarehe 8 Mei 2000 na zilizokoenda fedha zilizotokana na mauzo ya almasi hiyo! Aidha, Serikali ieleze ni kwa nini kampuni iliruhusiwa au iliachwa kuendesha shughuli za uchimbaji haramu wa almasi kwa miaka thelathini na tano na hatua ambazo zimechukuliwa au zinatarajiwa kuchukuliwa dhidi ya wale wote waliohusika na ukiukaji huu mkubwa wa sheria za Tanzania. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Mnamo tarehe 9 Mei 2000, Waziri wa Nishati na Madini wakati huo Mh. Dr. Abdallah Omari Kigoda aliipatia New Alamasi (1963) Ltd. leseni Na. ML. 71/2000 kwa ajili ya kuchimba almasi katika eneo hilo hilo kwa kipindi cha miaka ishirini na tano. Kwa mujibu wa Kamishna wa Madini kwa barua yake ya tarehe 21 Machi 2006, tarehe 25 Mei 2005, “eneo lililokuwa na leseni hiyo liliunganishwa pamoja na maeneo mengine na kuwa leseni ya uchimbaji Na. SML 216/2005 ya Williamson Diamond Ltd. kwa maombi ya wamiliki wa leseni hiyo ya awali.” &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ina maana kwamba wamiliki wa New Alamasi (1963) Ltd. waliomba leseni yao iunganishwe na maeneo mengine na leseni hiyo mpya kukabidhiwa kampuni ya Williamson Diamond Ltd. ambayo imekuwa ikichimba almasi katika eneo la Mwadui kwa zaidi ya miaka sitini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Kuna shaka kubwa na ya kimsingi juu ya uhalali wa milki hii mpya ya leseni ya uchimbaji almasi katika eneo la Luhumbo. Kwanza, kwa mujibu wa kifungu cha Sheria ya Madini ya mwaka 1998 iliyokuwa inatumika wakati huo, leseni pekee inayoweza kutolewa kisheria kwa ajili ya uchimbaji almasi ni Leseni ya Uchimbaji wa Mawe ya Vito (Gemstone Mining Licence). Leseni ya Uchimbaji (Mining Licence) hutolewa tu kwa madini yasiyokuwa mawe ya vito au dhahabu. Hii ndio kusema kwamba ML. 71/2000 isingeweza kuwa leseni halali kwa uchimbaji wa almasi katika eneo la Luhumbo au eneo lingine lolote nchini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa barua ya Kamishna wa Madini ya tarehe 27 Machi, 2006, ML. 71/2000 iligeuzwa na kuwa Leseni Maalum ya Uchimbaji (Special Mining Licence) Na. 216/2005 mnamo tarehe 25 Mei 2005. Hii ndio inayosemekana kuwa leseni ya Williamson Diamond Ltd. na ina ukubwa wa kilometa za mraba 29.73. Hata hivyo, kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya 1998, madini ya almasi hayawezi kuchimbwa kihalali kwa kutumia Leseni Maalum ya Uchimbaji kwani leseni ya aina hii hutumika tu kwa uchimbaji wa madini ya vyuma (metals) kama vile dhahabu na sio kwa mawe ya vito. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, madai yaliyotolewa kwa maandishi na Kamishna wa Madini kwamba ML. 71/2000 iliunganishwa na leseni nyingine na kugeuzwa kuwa SML. 216/2005 yanaelekea kutokuwa na ukweli wowote. Hii ni kwa sababu, kwa mujibu wa barua ya Kamishna wa Madini ya tarehe 19Aprili 2008, leseni pekee ambayo Williamson Diamond Ltd. wanayo katika eneo la Mwadui ni Leseni ya Uchimbaji namba ML 02/92 iliyotolewa tarehe 20 Mei 1992 na aliyekuwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eneo la leseni hiyo ni kilometa za mraba 12.33. Kwa mujibu wa barua nyingine ya Kamishna wa Madini ya tarehe 21 Aprili 2008, ML 02/92 bado ‘iko hai’ na “haijaunganishwa na eneo au maeneo ya mining licence nyingine”!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mheshimiwa Spika, Miezi mitatu baadae, Kamishna wa Madini alipigilia msumari wa mwisho katika madai haya alipoandika ifuatavyo mnamo tarehe 24 Julai 2008: “Hapakuwa na leseni ya uchimbaji madini ya Williamson Diamond Limited iliyotumika kuunganishwa na leseni namba ML 71/2000 na kuwa moja Special Mining Licence SML 216/2005”! Ni wazi, kwa nyaraka hizi za Serikali, kwamba kuna jambo ambalo limefichwa kuhusiana na shughuli za uchimbaji almasi za New Alamasi (1963) Ltd. na uhalali wa shughuli hizo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kambi ya Upinzani ,Tunaitaka Serikali itoe kauli rasmi ya kufafanua mustakabali wa sasa wa eneo la iliyokuwa Hati ya Madini Na. 224. Tunaitaka Serikali ifafanue utaratibu wa kisheria ambao umeiruhusu Williamson Diamond Ltd. kuendelea kuch
